Search This Blog

Saturday, April 21, 2012

Mbeya kushuhudia Ligi kuu kwa mara nyingine

Jiji la Mbeya litashuhudia tena ligi kuu ya vodacom msimu ujao wa 2012/13 baada maafande wa magereza Tanzania Prisons kufanikiwa kurejea ligi kuu hii leo.

Prison leo wamewalaza goli 2-0 timu ya Rhino Ranger ya Tabora katika mchezo wa hatua ya 9 bora ligi daraja la kwanza uliochezwa katika uwanja wa Jamhuri Morogoro.

Prisons ilihesabu goli lake la kwanza katika dakika ya 35 kwa mkwaju wa penati uliopigwa na Peter Michael na dakika ya 65 waliandika goli la pili kwa shuti kali lililopigwa na Jeremia Juma na kupelekea mchezo kumalizika kwa Prison kuibuka kidedea kwa goli 2-0.

Kwa matokeo hayo Prison imeitimisha idadi ya timu tatu zitakazo panda ligi kuu ya Vodacom, ambazo ni Mgambo Shooting ya Tanga, Polisi Moro ya Morogoro na Tanzania Prinson.

Katika mchezo mwingine uliochezwa leo kwenye uwanja huo ulio wakutanisha Trans Camp ya Dar es salaam dhidi ya Polisi Tabora na kumalizika kwa sare ya 1-1.

Source:tp://aboodmsuni.blogspot.com

No comments:

Post a Comment