Search This Blog

Saturday, April 28, 2012

JOSEPH SHIKOKOTI - DIET MBOVU CHANZO CHA WAGENI WENGI KUTOKUFANYA VIZURI KATIKA LIGI YA TANZANIA

Unamkumbuka Joseph Shikokoti?
Beki wa kati Ngongoti kimataifa wa Kenya aliyewahi kuja Tanzania kuitumikia klabu bingwa ya Afrika mashariki na kati Dar Young African na akaichezea mechi takribani 6 kabla ya kuondoka na kwenda kucheza Tusker ya Kenya kwa mkopo mpaka mkataba wake ulipoisha.

Nikiwa hapa Kenya nimekutana nae na kupata nafasi ya kuongea nae juu ya kwanini alicheza kwa muda mfupi sana katika ligi kuu ya Tanzania huku akiwa kiwango cha chini.

"Kiukweli nilikuwa napenda sana kucheza soka Tanzania lakini kuna vitu kadhaa vilipelekea uwepo wangu Bongo uwe mfupi. Kwanza nilipata uzito mkubwa nilipokuwa Yanga ndani ya muda mfupi niliokuwepo pale, kitu ambacho kilichangia kushuka kwa kiwango changu. Uzito huu ulichangiwa na mlo ambao nilikuwa nalishwa pale Yanga - yaani diet haikuwa katika mpangilio kabisa. Utakuta asubuhi mnakula manyama na vyakula vyenye wanga mwingi, mchana labda wali nyama na usiku wali kuku. Yaani haikuwa diet iliyopangiliwa kabisa mwisho wa siku nilijikuta naongezeka kilo katika hali isiyokuwa ya kawaida na kiwango kushuka kwa kasi sana."

Hili ni tatizo ambalo limewakumba wachezaji wenzangu kama Mike Baraza, Jerry Santo, Ambani na baadhi ya wachezaji wengine ambao wanatoka nje kwenda kucheza soka Tanzania." - Alisema Shikokoti ambaye hivi karibuni alienda kujaribu kutafuta timu ya kucheza nje ya nchi lakini akakwama na kurudi Tusker.

1 comment:

  1. Huko alikoenda kujaribu nje nako alikwama na kurudi Tusker sababu ya diet!? silly excuses :-(

    ReplyDelete