Search This Blog

Sunday, April 1, 2012

HIGUAIN AFUATA NYAYO ZA RONALDO - AFIKISHA MAGOLI 101 AKIWA NA REAL MADRID

 
Gonzalo Higuain amekuwa moja kati ya wachezaji wa Real Madrid ambao wamefikisha magoli 100 katika klabu hivi karibuni, baada ya kufunga goli lake la kwanza dhidi ya Osasuna jana Jumamosi.

Mshambuliaji huyu aliwasili Santiago Bernabeu in 2007 kutoka River Plate na tangu wakati huo ameshacheza mechi 210 katika mashindano yote. Pia yupo katika harakati ya kuwa na msimu wake bora kabisa katika in Spain, akiwa tayari ameshafunga jumla ya magoli 24, na goli lake la pili jana usiku lilimaanisha sasa ana magoli 101 tangu aanze kuitumikia Los Blancos.

Pia amekuwa mchezaji namba 18 kuweza kuifungia magoli 100 au zaidi Real Madrid, akiwafuatia Raul, Di Stefano, Fernando Hierro, Cristiano Ronaldo, Santillana, Hugo Sanchez, Ferenc Puskas, Emilio Butragueno, Pirri, Amancio Amaro, Francisco Gento, Pahino, Juanito, Michel, Luis Molowny, Ivan Zamorano na Ronaldo De Lima.

No comments:

Post a Comment