Search This Blog

Saturday, April 21, 2012

GIGGS AMESABABISHA PENATI 5 KATIKA MIAKA 20 - ASHLEY YOUNG NDANI YA MISIMU MIWILI ANAZO 9. YOUNG INABIDI AFUATE MFANO WA RONALDO.

Muingereza huyu amefanikiwa kupewa penati nyingi kuliko mchezaji yoyote katika ligi kuu ya England katika kipindi cha misimu miwili iliyopita - pia kwa idadi ya ya penati 9 alizopewa amemfunika Ryan Giggs ambaye katika miaka 20 aliyocheza soka amefanikiwa kusababisha penati 5 tu.

Wakati wa mkutano wa waandishi wa habari jana Ijumaa, Sir Alex Ferguson alitoa ofa ya takwimu ambayo wengi hatukuwa tunaijua: Ryan Giggs amefanikiwa kupia United penati 5 tu tangu aanze kuichezea klabu hiyo miaka 20 iliyopita.

Ukiangalia namna winga huyo alivyokuwa na kasi na uwezo wa kuuchezea mpira tena huku akiwa na mbinu nyingi za kuwatoka mabeki , bila kusahau namna timu nzima ya United isivyochoka kupeleka mashambulizi katika goli la wapinzani - unaweza ukaanza kujiuliza labda Giggs hakuwa akichezewa sana faulo katika eneo la penati.

Lakini Ferguson alisema veteran Giggs anajua sana ku-ubalance mwili wake, kwa makusudi au vinginevyo kuonyesha utofauti kati ya Giggs na winga mpya wa United, Ashley Young.

Young lazima atakuwa mwangwi wa malalamiko dhidi yake baada ya kulalamikiwa kwenda chini kirahisi sana katika wikiendi mbili mfululizo - dhidi ya QPR na baadae dhidi ya Aston Villa - na kuwasaidia viongozi wa ligi kupata penati muhimu.

Katika mtandao wa Twiiter watu tofauti wamekuwa wakimfananisha na Olympic diver Tom Daley, wakati Young pia amekuwa akionywa na legend wa United Bryan Robson kwamba anajitengenezea sifa mbaya ambayo hahitajiki na amabyo inaweza ikaigharimu klabu yake maamuzi makubwa katika mechi tano za mwisho za msimu.

Alipoulizwa kuhusu mchezaji huyo mwanye miaka 26, Ferguson alikiri kwamba: "Nimeongea na Ashley", na kwa hakika sijamwambia maneno ya "Endelea vizuri mwanangu."

Huku bosi huyo wa United akiendeleza utamaduni wa kuweka maongezi ya ndani ya klabu siri, Jarida lenye nguvu la msahabiki wa United, Fanzine Red Issue lilimshambulia winga huyo na kumuita "mjirushaji anaetia aibu". Pia jarida hilo lilikariri maneno ya legend boss wa United Matt Busby likisema: "Kama kuna kitu chochote kinapatikana kutoka kwenye soka, basi inabidi kipatikane kwa kushinda au kutoshinda na heshima."

Young kwa hakika itabidi ajirekebishe baada ya manager wake na mashabiki wa klabu yake kujitokeza kukemea na kumshawishi aache tabia yake, ambayo imetafsiriwa kama kitendo cha aibu kabisa.

Tangu kuanza kwa msimu wa 2010-11, Young tayari ameshapata penati 9, mara mbili zaidi ya mchezaji yoyote katika Premier league na 4  zaidi ya alizopata Giggs katika maisha yake yote pale OT.






THE YOUNG ONE
 YOUNG'S DEBUT SEASON SO FAR
GAMES PLAYED
AS SUBSTITUTE
GOALS
ASSISTS
26
5
7
8


Makocha wa timu pinzani lazima sasa watakuwa wanachukua hatua muhimu na kuwaonya mabeki wao wachukue tahadhari kubwa dhidi ya mchezaji huyo ambaye hana tatizo la kujirusha na kwenda chini kirahisi pale anapohisi ameguswa japo kidogo.

Lakini kama historia inaweza ikafanya kitu, then Young atajifunza. Tena kwa haraka sana kwamba kujirusha hakukubariki Old Trafford.

Wote Cristiano Ronaldo na Nani, waliotolewa Ureno, walikuwa na tabia ya kujirusha  mwanzoni mwa carrer zao pale OT na kwa haraka zaidi walifanikiwa kupewa jina la wadanganyifu.

Lakini haikuwachukua muda mrefu kwa wili hao kugundua kwamba kujirusha hakukuwa kunakubalika katika ligi kuu ya England, hasa Ronaldo.

Mreno huyo baada ya kupewa lecture na Ferguson, aliacha tabia ya kujirusha, na kuanza kukaza, kupambana na changamoto za kimchezo, na kuwa mchezaji aliyekamilika zaidi. Aligundua kwambani bora badala ya kujidodondosha, angeweza kujikaza nakwenda mbele kufunga na kutenengeneza magoli.

Young inabidi afuate  mfano wa Ronaldo, kuhakikisha anakumbukwa kwa soka lake na sio matukio yake ya utata, ambayo yanaishia kuharibu msimju wake wa kwanza na United.
                                                                                                                                                                                                                                          

No comments:

Post a Comment