Search This Blog

Sunday, April 8, 2012

ASHLEY YOUNG NDIO AMEPEWA PENATI NYINGI KULIKO MCHEZAJI YEYOTE KATIKA EPL NDANI YA MISIMU MIWILI - PREMIER LEAGUE KWENYE NUMBER

2 -  Anton Ferdinand amejifunga magoli mawili katika mechi zake mbili za mwisho pale Old Trafford - kabla ya mechi ya leo.

3 - Magoli matatu kati ya matano  ya mwisho waliyofungwa Manchester City katika premier league, yametoka nje ya box la penati.

4 - Magoli manne ya mwisho ya kutoka nje ya box ya Paul Scholes katika Premier League, ameyafunga dhidi ya timu za London -Fulham 2, West Ham United 1 - QPR 1.

5 - Ni QPR pekee wenye kadi 7 nyekundu ndio wamewazidi Man City wenye kadi 5 kwa kuwa na nidhamu mbaya katika premier league.

7 - Tangu mwanzoni mwa msimu wa 2010-11, Ashley Young amepewa penati nyingi kuliko mchezaji yeyote katika EPL - Luis akimfuatia akiwa na penati 5.

8 - Ushindi wa nane mfululizo wa Manchester United katika premier league, umeweka rekodi ya kuwa ndio mfululizo mrefu zaidi katika epl tangu Manchester United walipofanya hivyo mwezi march 2009.

157 -  Micheal Carrick alipiga pasi 81 na Paul Scholes alipiga 76 ambazo kwa pamoja ni 157  katika kipindi cha kwanza dhidi ya QPR leo, idadi hiyo ni 39  zaidi ya pasi zote walizopiga timu nzima ya QPR katika first half.

1 comment:

  1. Shaffih hebu zungumzia kwa nini offside haikionekana na kibendera alikuwa yuko on position ila faulo imeonekana!!!!

    ReplyDelete