Search This Blog

Saturday, March 3, 2012

VILLAS-BOAS: LAMPARD SIO MKE WANGU SIHITAJI KUPATANISHWA NAE.


Bosi wa Chelsea Andre-Villas Boas amesisitiza hakuna haja kupatana na Frank Lampard huku akitania “Hatujaoana.”
Lampard wiki iliyopita alikiri kwa mara ya kwanza kwamba mahusiano yake na AVB sio mazuri, lakini AVB amesema haoni umuhimu wa yeye kukaa na chini na Lampard kumaliza tofauti zao, huku akisisitiza bado wanazungumza wanapokuwa mazoezini.
“Mwisho wa siku ni mahusiano kati ya kocha na mchezaji, maneno ya Frank ni ya kweli kutokana na mahusiano yetu yalivyo.
“Kwangu mimi nakubaliana na aliyoyasema, sina tatizo lolote.”
Lampard ameweka wazi kwamba hana furaha na idadi ndogo ya michezo aliyopewa msimu huu lakini AVB alisema: “Inanibidi kuchagua timu – kuchagua timu iliyo bora kwa kila mechi.
“Frank amekuwa hapati sana nafasi lakini haimanishi kwamba nina matatizo nae binafsi.”

2 comments: