Search This Blog

Saturday, March 17, 2012

SIMBA NAO WAPO MANUNGU KUPAMBANA NA WATEJA WAO MTIBWA.

Kikosi cha Simba
Viongozi wa ligi kuu ya Tanzania bara Simba Sports Club, kesho inatarajiwa kuendeleza harakati zake za kuipokonya Yanga ubingwa wa Yanga, itakapokuwa mgeni wa Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Wanamsimbazi ambao wanaongoza ligi hiyo kwa pointi zao 44, wakifuatiwa na Azam yenye pointi 41, wakati Yanga, mabingwa watetezi wana pointi 10, mara ya mwisho ilifungwa na Mtibwa, Machi 22, mwaka 2009, bao la Omar Matuta lakini tangu hapo wamekuwa wakishinda mfululizo.

Simba inayonolewa na Mserbia Milovan Cirkovic, pamoja na kutarajiwa kulinda rekodi yake mbele ya Mtibwa inayofundishwa na Mkenya, Thom Olaba lakini pia inahitaji kuendeleza wimbi la ushindi katika mechi za ugenini, ikitoka kuifunga Polisi mjini Dodoma 1-0.

Kesho, wachezaji wa kigeni wanatarajiwa kuendelea kuonyesha umuhimu ndani ya Simba kwa kuifungia timu hiyo mabao.
Hadi sasa mabao ya Simba katika Ligi Kuu zaidi yamefungwa na Mnyarwanda Patrick Mutesas Mafisango na Mganda Emmanuel Okwi.     

REKODI YA SIMBA NA MTIBWA TANGU 2005:
                        P      W     D     L      Gf    Ga   Pts
Simba SC        12    8      3      1      19    6      27
Mtibwa Sugar 12    1      3      8      6      19    6
Septemba 25, 2011
Simba 1-0 Mtibwa Sugar
Feb 27, 2011
Simba 4-1 Mtibwa Sugar
Sept 29, 2010
Mtibwa Sugar 0-1 Simba              
Machi 22, 2009
Mtibwa Sugar    1-0 Simba  
Sep 28, 2008
Simba 1-0 Mtibwa Sugar  
Apr 21, 2010    
Mtibwa Sugar    0-4 Simba  
Nov 15, 2009
Simba 3-1 Mtibwa Sugar 
Feb 20, 2008
Simba 1-1 Mtibwa Sugar 
Okt 7, 2007
Mtibwa Sugar    1-3 Simba
2007: Hazikukutana kwenye Ligi ndogo
Sept 10, 2006
Mtibwa Sugar       1-1 Simba
Apr 9, 2006
Simba 1-1 Mtibwa Sugar
Okt 5, 2005
Simba 2-1 Mtibwa Sugar
Mei 22, 2005
Mtibwa Sugar 0-1 Simba  

No comments:

Post a Comment