Search This Blog

Saturday, March 31, 2012

SIKU 10 MUHIMU AMBAZO ZITAAMUA HATMA YA UBINGWA WA LA LIGA KATI YA REAL MADRID NA BARCELONA.

Wiki zilizopita, watu wengi walikuwa wameshaanza kusema nani atakuwa bingwa wa La liga msimu huu huku wakihitimisha mbio za ubingwa huo, taji ya ligi likiwa limeanza kuondolewa Nou Camp kwenda Cibeles, wakati Real Madridwakiongoza kwa 10 na kuwapita kabisa Barcelona tangu mwanzoni kabisa mwa mwezi wa pili.

Lakini ndani ya siku nne za kati kati mwa mwezi wa tatu, ile advantage waliyokuwa nayo Madrid, ambayo ilionekana ni vigumu kuifikia imepunguzwa mpaka kufikia nusu.Ilikuwa haitegemewi kuwa hivi sio kwasababu Barca walikuwa hawana uwezo wa kuwafikia mahasimu wao, bali Madrid walikuwa na consistency ya kupata matokeo mazuri kila wiki, hata kufikia hatua Pep Guardiola na Johan Cruyff walishaanza kukata tamaa juu ya Barca kuwakuta Los Blancos.

Lakini bila kutegemea Madrid wameteleza mara mbili, kwanza wakiwa nyumbani walitoka sare ya 1-1 dhidi ya Malaga na baadae katika dimba el madrigal dhidi ya Villareal. Katika mechi zote mbili, vijana wa Jose Mourinho walianza kufunga lakini wakaruhusu nyavu kuguswa kupitia mipira ya set pieces.

Sasa zimebakia points sita kama pengo lilopo kati yao, lakini hizi siku 10 zijazo ambazo zitahusisha mechi tatu kabla ya El Classico ndio zitaamua mbio za ubingwa. Ukiangalia kwenye karatasi unaweza ukaona kwamba Barca wana mechi nyepesi ukilinganisha na Madrid.

Usiku wa leo hii, mahasimu hawa wawili watakutana na timu mbili ngumu kuliko kutoka kaskazini mwa Spain. Real Madrdi watacheza na Osasuna huko Pamplona wakati Barca wataikaribisha Athletic Bilbao pale Nou Camp.

Los Blancos Madrid hawajawahi kushinda katika dimba la Reyno de Navarra katika mechi zao tatu zilizopita, mbili kati ya hizo waliishia kufungwa na nyingine ikiisha kwa suluhu. Pia ulikuwa uwanja huu huu ambao mwezi uliopita Barcelona waliishia kutandikwa 3-2, kipigo ambacho kilipelekea Madrid kuongoza kwa points 10. Pia itaendelea kushangaza ikiwa Osasuna hawa hawa watapunguza pengo la pointi waliloliongeza mwezi uliopita.
THE TITLE RACE: REAL MADRID & BARCELONA'S
LEAGUE FIXTURES KABLA YA THE CLASICO
  REAL MADRID H/A   BARCELONA H/A
Osasuna A Athletic Bilbao H
Valencia H Zaragoza A
Atletico Madrid A Getafe H
Sporting Gijon H Levante A
BARCELONA A REAL MADRID H


Athletic Bilbao siku zote ndio wamekuwa wapinzani ambao wanawapa shida sana The Blaugurana Barca dimbani, lakini wakatalunya kwa kiasi siku zote wamekuwa wakijitahidi mno kupata matokeo mazuri. Bilbao hawajamfunga Barca katika michezo 16 katika mechi zote za ligi za nyumbani, na mara ya mwisho wameshinda ilikuwa waliposhinda pale Nou Camp in 2001.

Kikosi cha Marcelo Biesla kinaweza kikawa katika form nzuri barani ulaya lakini kwenye La liga wamekuwa hawapo vizuri. Wamefungwa mechi tatu na kutoa suluhu katika mechi zao nne za mwisho hivyo kupelekea kushukahadi nafasi ya 11 katika msimamo wa ligi japokuwa walikuwa nafasi ya tano mwanzoni mwa mwezi huu.

Baada ya mechi za weekend hii, mambo yatazidi kuwa magumu zaidi kwa Madrid. Watawakaribisha Valencia kabla ya kucheza derby na Atletico Madrid, wakati Barca watasafiri kwenda kucheza na Zaragoza na baadae watawakaribisha Getafe.

Real Madrid chini ya Mourinho wana matokeo mazuri kwa asilimia 100 dhidi ya Valencia na Atletico, lakini hilo linaweza lisiwe na maana kutokana na kila siku zinavyozidi kwenda ndivyo presha inapozidi kuongezeka kwa Los Blancos.

Kumekuwepo na matatizo ya kisaikolojia kwa Madrid chini mreno huyu, kwa ushahidi ulionekana mwsihoni mwa msimu uliopita presha ilipokuwa kubwa Madrid wakapoteza mechi 2 muhimu dhidi ya Sporting Gijon na Zaragoza.
THE TITLE RACE: REAL MADRID & BARCELONA'S
LEAGUE FIXTURES BAADA YA THE CLASICO
  REAL MADRID H/A   BARCELONA H/A
Sevilla H Rayo Vallecano A
Athletic Bilbao A Malaga H
Granada A Espanyol H
Mallorca H Real Betis A


Kwa Barca, Getafe inaweza ikawa chungu kwa Catalan giant, ikiwa wao ndio moja ya timu pekee zilizoifunga Barca msimu . Lakini Nou Camp uwanja ambao klabu hiyo inayotoka mji wa Madrid hawajawahi kuibuka na ushindi na ni mara mbili tu wameweza kuondoka na droo,hivyo kuifunga Barca sio rahisi kihivyo.

Ikiwa Madrid watapoteza mjini Pamplona weekend  na wakafungwa pia mjini Catalunya tarehe 22 ya mwezi wa nne, na vijana wa Guardiola wakashinda mechi zao zote kuelekea El Classico, mapambano ya kugombea siku hiyo yatakuwa makubwa mno. Barcelona watakuwa wamekata pengo lote la pointi sita na watakuwa wao watakaokuwa juu ya msimamo kuelekea katika michezo minne ya mwisho wa La Liga.

Japokuwa, ikiwa Los Blancos watawanyoosha Osasuna na kuongeza wigo wa pointi kwa kuwafunga Vancia na Atletico, basi kutokea hapo Madrid watakuwa wana nafasi kubwa ya kubeba ndoo hata ya El Classico. Nani angeweza kufikiri Osasuna atacheza part  kubwa katika kuamua ubingwa uende wapi msimu huu.

No comments:

Post a Comment