Search This Blog

Friday, March 9, 2012

Hili ndo sakata la ubingwa wa CDA huko Mkoani Dodoma !

Mwanzoni kabisa wakati ligi inaanza kulizuka tetesi kwenye wilaya, kwamba mwaka huu timu ya CDA, itapandishwa daraja.

Baada ya tetesi hizo, watu wakatulia wakisubiri kuona ukweli wa tetesi hizo.

Mara ligi ilipoanza , hapa sasa ndio ukweli ulipojidhihrisha. Ligi ikachezwa kwa makundi. Ikaja hatua ya tisa bora na wakazigawa timu katika makundi matatu.

Hap kilichotakiwa ni kila kundi inapita timu moja  na kuunda tatu bora, kisha bingwa wa wilaya.

Katika kundi la timu ya CDA, kulikuwa na timu nyingine ( GANAZ FC, na ……….)

Katika mechi yao ya mwisho dhidi ya GANAZ FC ya Jeshi, CDA, walishinda 2-1 huku CDA, wakiwa wamewatumia wachezaji watatu ambao walikuwa wachezaji wa timu za Under 20 ya polisi Tanzania, na golikipa wa Yanga ambao walicheza mashindano ya UHAI.

Tatizo likaanzia hapa…..



GANAZ ikakata rufaa chama cha wilaya kupinga wachezaji hao huku ikiwa na vielelezo vyote.
( mmoja kati ya wachezaji hao ni Yule aliyepata nafasi ya kwenda kwenye academy Senegal)
Matokeo ya rufaa hiyo yalikwenda vizuri, na Ganaz wakaonekana wako sahihi, wakapewa ushindi na chama cha wilaya wakaambiwa wajiandae na 3 bora na punde kidogo ratiba ikatoka ikiijumuisha ganaz, Polisi na AREA A, kugombania ubingwa wa Wilaya.

Mechi ya kwanza ikachezwa ya kwanza siku ya Juma tano POLISI  na AREA A, na ijumaa ikachezwa mechi kati ya GANAZ na AREA A.
Kwa mshangao wa wengi alhamis kukawa na kikao cha chama cha mkoa DOREFA, wakaipoka tena ushindi GANAZ, na ikaiagiza CDA, ijiandae kesho yake kwa mechi.
Asubuhi Ganaz fc inapokea barua kutaarifiwa maamuzi ya rufaa kwamba CDA walikata rufaa chama cha mkoa hivyo chama kimeona maamuzi yaliyoamriwa na DOREFA zile kamati za kuamua rufaa zilikaa kwa pamoja kwamba kamati ya rufaa na ya nidham na ilitakiwa kila moja ikae kivyake na itoe maamuzi.
Tukahoji inakuaje sasa isikilizwe upya wakasema haiwezekani tena hivyo kama tunataka tukate rufaa TFF taifa kumbuka saa 4 hiyo tunaambiwa hivyo na ilikuwa ijumaa na jioni tuna mechi.
Uongozi wa GANAZ ukaona isiwe tabu kwa kuwa mazingira yalikuwa yapo wazi na wao ndo wameshika mpini.

Kilichotokea sasa wakacheza CDA ile hatua ya 3 bora na DRFA wakasimamia mpaka wakapata ule ubingwa wa wilaya.
Wakati huo huo zile timu 3 zinatakiwa zisonge mbele kwenye hatua ya mkoa yani kutafuta bingwa wa mkoa kwa mujibu wa sheria ambapo ni timu 3.
Ganaz ikahoji gharama za kuiandaa timu kwa kipindi kile walipwe cha ajabu wakaambiwa watulie watapatiwa nafasi na wao ziwe timu 4 kutoka wilaya ya dodoma mjini hapo inaonyesha zahiri katiba imevunjwa maana miaka yote ni timu 3 iweje ziwe 4?
Sababu zikatolewa na kweli kwakuwa nafasi ilikuwa inahitajika ganaz ikatulia.
zikagawanywa timu kituo cha kongwa na dodoma mjini, GANAZ ikapelekwa kongwa na CDA ikabakishwa mjini na timu zingine za wilayani.
kituo cha kongwa kikaenda vizuri bingwa halali akapatikana GANAZ kimbembe kikawa town...
kila timu ya wilayani inapocheza na CDA kesho yake inatangaza kujitoa inarudi kwao kwa kuwa waliona wanapoteza muda bure na garama za bura, zikajitoa karibu timu 4 matokeo yake kati ya timu 8 ikapita CDA na point 4, polisi jamii na magereza mpwapwa wakapita na point moja moja wote maajabu haya.
Ikaja hatua ya 6 bora sasa 3 kutoka kongwa na 3 kituo cha town ambazo zilikuwa ni cda,polisi jamii,magereza mpwapwa,ganaz,magereza isanga na maskani.
Mechi zikaanza gemu ya kwanza CDA ikatoa droo ya 0-0,na maskani gemu ya 2 ikaifunga magereza isanga goli 7-0 yani style ikawa ni ile ile saidia ishinde, kesho yake magereza isanga ikatangaza kujito kwa kutiridhishwa na mwenendo wa ligi hivo cda ikafutiwa point zote 3 mechi ya 3 ikaifunga polisi jamii 2-0 ikawa na point 4 mechi ya 4 ikacheza na magereza mpwapwa ikatoa droo ya 1-1 na hapo ulikuwa sio mpira zaidi ya mbereko ya kufa mtu maana dakika za mwisho cda ilifungwa goli la wazi kabisa likakataliwa hivo wakawa na point 5,maskani point 5,polisi jamii point 4,ganaz 3.hapo sasa ndo pakawa patamu....
ila kabla ya yote ile gemu ya cda na polisi jamii cda walishinda 2-0 polisi wakawakatia tena cda rufaa kama ya ganaz kupinga kuwatumia wachezaji wawili na kwa kuwa hii ni polisi ndogo vile vigezo viliboreshwa zaidi kwa kuwa walikuwa wachezaji wao cha ajabu ile rufaa ikaanza kupigwa danadana ilipelekwa kwa kamati ya rufaa wakaambiwa wapeleke kwenye ya kamati ya nidham wakasema basi tunahitaji majibu haraka kabla ya gemu inayofuata.
viongozi wakaifumbia macho kana kwamba hakuna kitu na ligi ikawa inaendelea kama kawaida...!! basi mechi ya mwisho cda na ganaz halafu kesho yake polisi jamii na maskani...kwa zengwe lile lileganaz ikafungwa goli 2-0 ingawa magoli yalikuwa halali ila mazingira ya mechi kuhusu maamuzi hayakuridhisha kabisa hapo hapo wakajitangaza mabingwa kwa kuwa na point 8 na magoli ma4 ya kufunga wakati kuna mechi nyingine ya mwisho




kesho yake.... kwa mtaji huo maskani peke yake ndo akawa anauwezo wa kuwa bingwa kwakuwa na point 5 dhidi ya polisi j ina 4, na kwakuwa cda iliitesa kila timu kwa fitina zake

mechi ikachezwa na hapo maskani ikawa inahitaji magoli ma 4 ili imzidi cda kwa goli 1 ndo iwe bingwa ha haaa hadi dk ya 6 zikawa zimeshapatikana hizo zinazohitajika mpira ukawa unachezwa sasa hadi halftime ikawa 4-0 na hadi mwisho maskani ikaifunga polisi jamii 5-0 basi kimahesabu ikawa maskani ndio bingwa lakini hakuna chombo chochote cha habari kilichotangaza na hata DOREFAwakaondoka uwanjani...!! ila mji mzima ukawa unajua maskani ndio bingwa....

likaanza zengwe lingine wakati mechi inaendelea ile na cda wakaona hamna namna wakaanza kusema wanakata rufaa kwa kuwa hiyo maskani ilinunua jina wilayani na sheria inasema lazima kuwe na wachezaji 10 kutoka hiyo timu kitu ambacho maskani walikuwa hawana...lakini tokea inashiriki kituo cha kongwa hiyo maskani ilikuwa inatumia wachezaji wake ambao wameidhinishwa na hao hao dorefa[halafu sorry nilikuwa natumia DOREFA sasa iweje leo mwisho wa siku wajifanye kuwakatia rufaa....zengwe hilo..!!.....

Walikuwa na rufaa hao hao cda dhidi na mechi yao na magereza mpwapwa ile waliotoka 1-1 kwamba golikipa namba 2 wa magereza jezi yake haikwenda kwenye pre match hivo ilitumika kimakosa uwanjani wakawa wanadai wapewe ushindi...zengwe hilo sheria ya wapi hiyo...na hapo makosa si yanakuwa ya waamuzi..?....

basi ndo wakatoka na hiyo mpya ya kwamba hiyo gemu ya maskani na polisi eti matokeo yalipangwa wakakata rufaa na siku wanapeleka hiyo rufaa naona huku wanashangilia kana kwamba matokeo ya hiyo rufaa wanayajua... maana hata hiyo gemu ya maskani na polisi walitaka iwe droo au polisi ashinde matokeo yake waamuzi ndo wakawa mabeki wa polisi lakini pia ikashindikana....

na hao wanaosema wasimamizimwa mechi kwa nini wasimamie gemu moja ya mwisho kwa nini wasisimamie gemu zote kama wapo makini...? hivo kwa kauli moja na kwa mujibu wa timu zote shiriki wanapinga cda kupewa ubingwa sio halali hata kidogo na ndo wanaofanya hata polisi tanzania haifanyi vizuri ligi kuu gemu za polisi hazipewi promo yoyote na chama,wala hawawapi ushirikiano wowote kwakuwa wanaona ile ni timu ya taasisi hivyo wanataka ishuke waipandishe cda ili wapate maslahi ndio maana hata gemu za polisi tanzania ligi kuu sio ajabu ukasikia mapato sh 25,000/= timu ikapata 1250 ni kitu cha kawaida hapa...!!!!
Mimi ni mchezaji wa GANAZ na nimejionea ukiritimba wa hii michuano na mwaka jana ndo tuliofanya tukawanyima mji mpwapwa ubingwa kwa style hii hii kutaka fulani apande kwanini? kwakuwa yeye ndo kalipa ada ya ushiriki peke yake basi tukatoa droo na hao mji na gemu ya mwisho kwakuwa hatukuwa na nafasi tena tukawaachia majengo wakatufunga 2-0 wakawa mabigwa mji akazidiwa point akaula wa chuya..!!
Nahiyo rufaa cda waliyokatiwa na ganaz kuhusu hao wachezaji kwa style hiyo hiyo mji mpwapwa nao kuna baadhi ya wachezaji waliwatumia huko mpwapwa wa u20 ya polisi tanzania wakakatiwa rufaa wakapokonywa point 9 matokeo yake hawaakwenda kokote sasa kwa nini kwa cda iwe tofauti? na ni mwaka huu huu?
Ni hayo tu bro shaffih na kama una la kuniuliza 0717982800 sina pa kutolea dukuduku langu zaidi ya sports xtra kwa kuwa ni member na nyie mnasaidia sana sio siri kufichua na angalau hata kukuza soka letu ambalo linaporomoka balaa kwa uhuni wa watu wachache kama hawa maana wasingepanga fulani awe bingwa mbona mpira ungechezwa kwa raha tu
ni hayo tu bro usiku mwema....ggmu

No comments:

Post a Comment