Search This Blog

Saturday, March 31, 2012

BREAKING NEWS: KOCHA WA MORO UNITED AJIUZULU

Baada ya mfululizo wa matokeo mabaya katika Vodacom premier league, kocha mkuu wa Moro United Hassan Banyai ameamua kujiuzulu kuifundisha timu.

Akiongea na mtandao huu Banyai alisema ameamua kufanya hivyo baada ya kukaa chini na kuongea na viongozi wake na kuamua kukaa pembeni kumpisha mwalimu mwingine aje kuokoa jahazi linalozama la Moro United.

"Mimi nina mapenzi makubwa na Moro United, hii timu yangu na naipenda sana, hivyo siwezi kuweka maslahi yangu mbele huku kalbu yangu ikiwa inafanya vibaya. Nimeamua kukaa pembeni na kujiuzulu ili kuweza kumpisha mwalimu mwingine ambaye ataweza kushikilia pale niliposhindwa na kuweza kuikoa timu yetu isishuke daraja msimu.

"Nwashukuru viongozi wa Moro na wachezaji pia kwa yote waliyonitendea na ushirikiano walionipa tukiwa tupo pamoja katika kuhikikisha timu inafanya vizuri katika michuano mbalimbali. Naipenda sana Moro na nina imani tutapata kocha mwingine ambaye ataweza kuikoa timu yetu kutoka kushuka daraja."

No comments:

Post a Comment