Search This Blog

Thursday, February 16, 2012

CHRISTIAN ERIKSEN NILICHAGUA KUJIUNGA NA AJAX NA KUKATAA OFA ZA TIMU ZA ENGLAND.



In action: EriksenBig challenge ahead: Eriksen in training

Unapokuwa na miaka 20 matumaini mazuri uanyoweza kuwa nayo hasa unapokuwa mwanasoka na kuweza kuiangamiza  timu aina ya Manchester United, inasaidia katika kuwa na uzoefu zaidi katika maisha yako ya kucheza kandanda.

Kwa bahati nzuri kiungo mshambuliaji wa Ajax Christian anayo nafasi hiyo leo hii katika mechi ya Europa league dhidi ya mabingwa wa Uingereza Manchester United.
Eriksen pia leo hii atapata uzoefu japo kidogo kuhusu soka la kiingereza.

Anakumbuka: “Nilienda Chelsea mara 2 nilipokuwa na miaka 14 na 15. Nilikuwa nacheza katika klabu ya Odense kipindi hicho na tulienda Chlesea kufanya majaribio tukacheza mechi moja dhidi ya Milwall na West Ham za watoto.

“Nilishangazwa na aina ya mchezo waliokuwa wanacheza. Nilijua aina ya mchezo wa kiingereza kwamba ni tough, wenye kutumia nguvu kwa kiasi kikubwa. Ni mchezo tofauti sana na Denmark. Wanacheza kwa nguvu sana na kufanya tackles za hatari lakini nashukuru mungu sikuumia mpaka niliporudi Denmark.”

Eriksen alifanya vizuri kiasi cha kumvutia Jose Mourinho lakini kinda hilo liliamua England hapakuwa mahali sahihi hivyo akaamua kujiunga na academy ya Ajax.
Kinda ambalo liliitwa katika timu ya taifa ya DENMARK iliyoshiriki World Cup 2010 na ndio alikuwa mchezaji mwenye umri mdogo kuliko wote katika mashindano hayo.

Uwezo wa kutisha aliounyesha dhidi ya England mwaka mmoja uliopita uliwafanya maskauti wa vilabu vya premier league kuuanza kumtafuta, huku Manchester United na Liverpool wakiungana na Chelsea, AC Milan na Bayern Munich wakimgombea kinda hili kidanish.

“Siku zote nimekuwa nikiamini mahala pazuri kwa kuanzia career yangu ni Holland, especially kwa sababu na upinzani ninaokutana nao na soka linalochezwa huku, anasema Eriksen ambaye ni mwembamba kiasi kwamba ni vigumu kuamini kama ni mwanasoka.

“Ajax wana utamaduni mzuri wa soka zuri na wanacheza mfumo wa 4-3-3,  ambao unanifaa sana mie. Pia wanatumia pesa nyingi katika kutafuta na kukuza vipaji vya wanasoka wachanga ambao hukuzwa hadi kuwa kiwango kizuri.

“Timu kubwa nchini England wana ulazima wa kucheza Champions league kila mwaka hivyo hawawezi kumnunua mcheza mwenye miaka 17 na kumuweka katika kikosi cha kwanza moja kwa moja. Wanawanunua wachezaji wanaoweza kuwatumia sasa. Unaweza ukakosa kucheza mpaka unatakpokuwa na miaka 21. Hivyo kwanini uende kule?”

No comments:

Post a Comment