Search This Blog

Wednesday, December 21, 2011

Debate: LIGI GANI BORA ULIMWENGUNI: EPL au La Liga?





Tangu msimu wa 1992-93 nimekuwa nikiifatilia ligi kuu ya England lakini kwa mtazamo wangu nadhani LA LIGA ndio ligi bora Ulimwenguni. Je wewe unasemaje ?

20 comments:

  1. Kwangu EPL ni bora mara 100 ya LA LIGA

    ReplyDelete
  2. Ligi ya spain (la liga) ina timu kubwa mbili na hakuna timu yoyote inayoweza kushindana na hizo timu. Ligi ya England (epl) ina ushindani mkubwa kwa timu zote. Kwa mfano timu inayoongoza ligi inafungwa na timu ambayo inashuka daraja. Mtazamo wangu, spain ubingwa ni wa timu mbili lkn England ni ubingwa wa timu 6 yaani yoyote kati ya hizo inaweza kuwa bingwa

    ReplyDelete
  3. EPL ina msisimko mkubwa sana kwetu bongo, labda kwa sababu tunaiona kwa muda wa hapa nyumbani ambao hautusumbui kuifuatilia kama LIGA ambayo kwa timings zake inakuwa siyo rahisi sana kufuatilia labda kwa gemu kubwa kubwa tu.

    So huenda LA LIGA ni bora zaidi ya EPL, lakini kwa kuwa swali umeuliza katika sample population ambayo inaangalia sana EPL, then jibu utakalopewa lipo wazi kabisa.

    Nakutakia kazi njema Shaffih.

    ReplyDelete
  4. LIGI BORA NI LA LIGA , PRIMERA DIVISION ligi ya ENGLAND ni Ligi maarufu tu na huwezi kushangaaa kuona Manchester Utd kuwa na mashabiki wengi Ulimwengu kiasi cha milioni 92 pekee wanapatikana Asia kati ya milioni 333 lakini kwa maana ya mpira hakuna ubora hapo. kmf angalia kwenye timu ya taifa Hispania mchango wa nyota wao wanaochezea soka vilabu vya nchini humo ni mkubwa sana kuliko England ambayo kwa kiasi kikubwa imejazwa wengi kutoka nje ya nchi yao na timu ya taifa inavurunda sana. Levante ni miongoni mwa klabu zenye ubishi mkubwa sana ikiwa uwanjani yaani hata rythm ya mpira unaweza kuipata, Deportivo la Coruna licha ya kwamba sasa ipo daraja la kwanza lakini unaweza kuona ni kwa kiasi gani watu wanacheza mpira, pia England ni ligi yao inataka nyota wenye spidi sana. sababu nyingine ni kwamba mtanzania wa kawaida ukimwambia kuwa EPL ipo chini atakukatalia kwa maana ndio mpira anao anagalia kila siku lakini kama hauoni atakubishia tu Shafii. Ndio maana kumekuwa na ugomvi mkubwa sana kati ya England na Hispania katika Shirikisho la Soka Ulimwenguni (FIFA) kuhusu viwango hata vya ubora vaya kila mwezi inaonekana kura nyingi inachukua Hispania lakini England ikibakia kulia tu.

    Ndimi Johnson Jabir, Mbeya
    www.jaizmelaleo.blogspot.com

    ReplyDelete
  5. ligi ya england ni nzuri sana spain hakuna ushindani england ndipo maana ya ligi inapopatikana na si spain ambako kuna advertisers wa football ya spain na si ligi kwa maana ya ligi(barca na madrid)

    ReplyDelete
  6. mzazi natumia criteria zifuatazo kufanya tathmini
    1.ushindani baina ya timu-EPL ushindani ni mkubwa kuliko laliga ambako kuna only 2giants ambao ni barca na madrid wakat EPL ziko timu zaidi ya 6 ambazo kila zinapokutana huwezi kua na uhakika nani anashinda na ndo maana hata top 4 haiko stable tena wakati Laliga wale wengine wanashindania 3 na 4.
    2.Marketing-EPL wamejaribu sana kumarket brand yao na kuhakikisha inakua na market share kubwa sana than laliga ndo maana hata fixtures zao zinapigwa kwanzia sa6 mchana kwao ili kuwezesha sehemu nyingine kutazama mpira.
    3.Ubora wa wachezaji-Laliga kuna timu mbili tu za barca na madrid zenye uwezo wa kusajili wachezaji wakubwa tofauti na EPL ambapo ,Manutd,city,Chelsea,liva,Totenahm,Arsenal wote wanaweza kusajili wachezaji wakubwa na kuleta ushindani.

    3Mapato ya vilabu-klabu za EPL ziko vizuri kiuchumi kuiko za Laliga na ndo maana walikua na mgomo muda mrefu kudai haki zao kitu kinachoashiria hali mbay ya fedha vilabuni.

    Chela wa dom

    ReplyDelete
  7. EPL ndio ligi ngumu zaidi duniani

    ReplyDelete
  8. Nashukuru sana kijana Jabir kutoka mbeya.swali ulililoulizwa ujalijibu katika kiwango kinachotakiwa I mean hujatoa vigezo vya msingi wa ligi bora.2kianza kuangalia vilabu vinavyocheza katika hizi ligi ni 20 kila ligi.Pili 2angalie ushiriki wa hizi timu katika ligi.2anzie La Liga,Ushiriki wa timu ktk ligi hii c mzuri sana kwani timu ndogo hazina upinzani hata kidogo katika timu kubwa zile mbili,na kingine La Liga haina big match zaidi ya mbili katika mcmu 1,uwekezaji ktk ligi;Matajiri wengi wanapenda faida na faida wataipataje pacpo ligi kuwa bora ndo maana hata matajiri wanaokwenda La Liga ni kwaajili ya timu 2 2.Ingawa a2iangalii sana lakini siku izi hii ligi inachezwa mapema sana ila haina mvuto ndo maana hata huitaji kuiangalia.2rudi EPL hii ligi ingawa inasifika kwa wachezaji wake ku2mia nguvu sana lakini ndo ligi yenye mvuto sana kwa vigezo vifuatavyo:-
    1. EPL inatimu sita katika kuwania ubingwa tofauti na La Liga.
    2. ushindani wa timu ndogo ni mkubwa sana ktk ligi.na nyingine nyingi 2 ambazo hata ww mwenyewe unazifahamu.

    UEFA yenyewe ukiwauliza ni ligi gani bora watakuambia.La Liga kwa sasa inazidiwa hata na Selia A kuna upinzani wakutosha kabisa.

    ReplyDelete
  9. kuzungumzia ushindani tangu mwaka 92 ni timu nne tu zimewah kushnd epl...lakn tangu wakati huo..athletico madrid,valencia,diportivo,bara,madrid ,sevilla,real betis,athletc bilbao...duh bado hamjajua tu...ipi lgi bora...damian joseph hapa

    ReplyDelete
  10. kwa vigezo vya uefa epl ni bora kuliko ligi yoyote ulaya kwa miaka mitano iliyopita

    ReplyDelete
  11. kaka tunapenda sana uchambuzi wako,lakini badirisha rangi ya maandishi tuweze kusoma poa.

    ReplyDelete
  12. Kwa mtazamo wa timu mojamoja EPL ina timu sita zenye ushindani wa kusaka ubingwa wa ligi wakati Spain ina timu mbili zenye ushindani wa kusaka ubingwa wa ligi pia ktk mtazamo huohuo wa timu mojamoja EPL karibia timu zote kwenye ligi zina ushindani wakati Spain ni timu mbili tu ndo zenye ushindani wafungana ila timu mbili za juu kutoka Spain ni timu bora kuliko timu zote za EPL kwa maneno haya mtazamo wangu EPL ndo ligi bora kwa ushindani na yenye msisimuko hata ktk kuangalia ukilinganisha na Laliga lakini Spain wana timu bora zaidi kama utalinganisha ktk peformance ya mabingwa wawili wa juu kutoka ktk ligi hizi

    ReplyDelete
  13. Nimevutiwa sana na mawazo ya wadau mbalimbali kuhususiana na mada husika kwa kweli kwani wameeleza ukweli wa mambo, huwezi kuwa na ligi ya timu mbili bora kila mwaka zina badilishana ubingwa ukasema una ligi bora, ligi ya Laliga haina ushindani ule tunaouona kwenye ligi ya EPL, huyo mdau aliyesema kwamba watu hawaangalii ligi ya Laliga kisa ni huwa inaonyeshwa late hours kwa saa za Tanzania naomba nimwambie kwamba yeye ndiye amabe huwa haangalii ila watu tunaangalia hata kama ni saa tisa ya usiku halafu si lazima uangalie usiku kuna marudio kama una kingamuzi kwa hiyo hicho sio kigezo.Angalia ligi ya EPL timu 5 za mwanzo huwa zinapossibility ya kuchukua ubingwa na hata hizo zilizobaki sio vibonde unashinda kwa jasho jingi,ni ukweli usio pingika kwamba Barcelona na Madrid ni timu bora kabisa duniani lakini hiyo haiifanyi ligi ya Laliga kuwa ligi bora, suala la umaarufu wa ligi haliji tu ila linaletwa na upenzi wa mashabiki, nikuambie hata hapa ujerumani watu wanaizimia ligi ya EPL ila ukiwauliza Hispania vp jibu ni Barca na Madrid hawasemi ligi ya Laliga, ila kwa Engand tunazungumzia EPL:

    ReplyDelete
  14. Kwa mtazamo wangu LA LIGA ni bora ya EPL. Hata record za mcezaji bora wa UEFA na FIFA wengi wanatoka katika LA LIGA, angalia akina RIVALDO, ZIDANE,FIGO,RONALDO DE LIMA,GAUCHO na sasa MESI. Pia angalia nafasi zote TATU za mchezaji bora zinazoshindaniwa wote wanacheza LA LIGA MESSI,VAVI na C.RONALDO. Mabingwa wa Dunia na Europe ni SPAIN.Vilab vya Spain vinacheza soka ya hali ya juu sana kulinganisha na England. EPL ni maarufuu tu na si ligi bora.

    ReplyDelete
  15. hata ukimuuliza kichaa hili sawli basi sina shaka atakwambia epl ndo league bora duniani!!, ushindan wa team 2 tu kama tanzania wa simba na yanga? alaf kina atletico madrid kila mwaka nazo zikijitahd bla mafanikio kama kina mtibwa na jkt ruvu za tanzania......kufikia ubora wa epl,inahtaji kujipanga kila sector,advertisment yao tu hawa jamaa inaitupilia mbali la liga......je 2kiangalia mambo mengine? usiangalie kisa messi na ronaldo wapo la liga then ndo uipe sifa ambazo hazina! league gan yakuangaliwa team mbili bana,,zikicheza nyingine MNALALAAA. nadhan jibu ushalipata dauda

    ReplyDelete
  16. Kwa mtizamo wangu la liga ni bora sana kuliko epl. tatizo wabongo tunaangalia sana ligi ya mkoloni wetu.
    Vigezo: chukua toka mwaka 1998 wakati mapinduzi ya TV bongo yalianza kushamiri. real madrid ilichukua champion ligi mara tatu, kuna wakati ilikuwa fainali ya spain tupu. zilikuwa wapi timu za epl.
    Nakumbuka tu Liverpool ilichukua uefa dhidi ya alaves ya moreno. baadae sevila ikachukua uefa kwa mido, atletiko madrid ikachukua mwaka jana kwa fulham. ikaja barcelona na champion ligi tena mara 2 ndani ya miaka mitatu ya karibuni. Na england ukiangalia ni liverpool na manchester zimechukua hili kombe mara tatu kwa pamoja. na ukiangalia mwaka bingwa ni kati ya barcelona na madrid ya champion ligi.
    kwa hiyo tuangalie ufanisi wa timu za ligi hizi mbili kwenye uefa na champion ligi. Alwaya Laliga ni bora

    ReplyDelete
  17. Hakuna kitu kama hicho EPL ni bora kuliko la liga

    ReplyDelete
  18. Reginald Mwemezi a.ka. Man united.December 24, 2011 at 12:18 PM

    Listen Shaffih...............Ligi ya England(EPL) ni ya timu moja 2 kwa sasa yaani Manchester united a.k.a The RED DEVILS.......timu kama Chelsea na Arsenal hubahatisha zaidi....
    Kwa upande wa Spain. Pia kule Ligi Ni ya timu moja 2 nayo nia BARCELONA also known as Maajabu ya dunia....Madrid+Others huonekana kubahatisha 2...so kwa ufupi Ligi zote mbili zinazidiwa ubora na BUNDESLIGA...Bingwa mpya kila siku....Mwisho mavi ya zamani hayanuki...kwa sasa EPL na LA LIGA hakuna ubora....zaidi ya ujiko na promo 2...

    ReplyDelete