Search This Blog

Friday, October 14, 2011

MTANZANIA AOMBEWA ITC KUCHEZA UJERUMANI


MCHEZAJI Costancia Maringa wa Tanzania ameombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) ili aweze kucheza mpira wa miguu wa wanawake nchini Ujerumani.
Chama cha Mpira wa Miguu cha Ujerumani (DFB) kimetuma maombi hayo Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ili kumwezesha mchezaji huyo kuichezea timu ya FC 1919 Marnheim ya nchini humo.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa DFB, Helmut Sandrock, Maringa mwenye umri wa miaka 12 ameombewa ITC na chama hicho kama mchezaji wa ridhaa. TFF inafanyia kazi maombi hayo na hati hiyo itatolewa mara baada ya taratibu husika kukamilika.

No comments:

Post a Comment