Search This Blog

Wednesday, October 5, 2011

MKOSI WA MECHI 50 KWA JURGEN KLOPP NA UBINGWA WA DORTMUND







Kama vile mambo hayajaharibika vya kutosha kwa muda huu, Jurgen Klopp atakutana na mbaya @ Coface – Arena jumamosi jioni: Stephan Mai.



Mai sio mchezaji wala kocha ila ni TV reporter anayefanya kazi katika channel ya kusini magharibi mwa Ujerumani.Kutokana na gazeti la Ujerumani la “WAZ”, Mai ameudhuria michezo 50 ambayo imemuhusisha Klopp aidha kama mchezaji au kocha (akiwa na Mainz na Dortmund) tangu mwaka 1993 na cha ajabu Klopp hajawahi kushinda hata mchezo mmoja kati ya 50 aliyoudhuria mwandishi huyo wa habari.







The 43-year old manager anafahamu sana juu ya mksi huu na Stephen Mai.Wakati timu yake ya Borussia iliporudishiwa goli la kusawazisha mwishoni mwa mchezo dhidi ya Kaiserslautern mwezi February, Klopp kwa hasira alikataa kufanya interview na Mai baada ya mechi hiyo, akimwita Stephen “Ndege mwenye ugonjwa mbaya wa kuambukiza”.





Mai hakutaka kujibizana nae, badala yake bila majivuno alihaidi kutokwenda tena katika mchezo wa ugenini wowote wa Borussia msimu ule.Lakini kwa bahati mbaya kwa kocha kocha huyo wa Dortmund, repota Mai anategemea kuhudhuria mchezo wa ugenini wa mabingwa watetezi wa Bundesliga @Mainz wikiendi hii, mchezo ambao Dortmund wanahitaji sana kushinda ili kuondoa fikra mbaya juu yao.





Point saba kutoka katika michezo 6 ya ufunguzi inaashiria mwanzo mbovu wa kwa mabingwa watetezi wa Bundesliga.Borussia wapo katika nafasi ya 11 kwenye msimamo wa ligi.Wanaongoza ligi Bayern Munich wapo 8 mbele lakini hiyo sio mbaya sana, Dortmund sasa tayari wameshapoteza michezo mingi (mechi 3).”Presha sasa ipo juu” alisema Klopp baada ya kufungwa 2-1 na Hannover, mechi ambayo walianza kufunga na ku-dominate mchezo kabla ya kufungwa mabao mawili katika dk 4 za mwisho na kurudi nyumbani mikono mitupu.





Recently historia inaonyesha kwamba matokeo mabovu ya Black n Yellow Team hayaji kama surprise.Stuttgart (Mabingwa wa 2007) na Wolfsburg (mabingwa wa 2009), ambao wote walishinda ligi bila kutegemea, wote walihangaika sana msimu uliofuatia, wakati michezo ya champions league ilipowaongezea mzigo na changamoto mpya.So far mchezo bora kwa Dortmund, ukiondoa wa ushindi wao wa 3-1 dhidi ya timu ambayo haipo kwenye kiwango kabisa Hamburger SV katika siku ya ufunguzi, ulikuwa mchezo dhidi ya Arsenal waliopata matokeo ya 1-1.Dortmund wamecheza vizuri mara chache san asana, lakini ni sawa kusema kwamaba vijana wa Klopp wame-struggle to kufikia levo yao yenye ubora iliyowafanya wachukue ubingwa msimu wa 2010/2011.





NINI TATIZO?



Klopp anasema kuwa tatizo ni saikolojia. “Tunakosa consistency na tama ya mafanikio,” alisema baada ya mchezo dhidi ya Hannover.Beki wa kushoto Marcel Schmelzer anakubaliana na hili, “Inaonekana kama hutukuupigania vizuri mpaka mwisho.Kila mtu alikuwa ana matumaini hakuna kitakachotokea.Wote tunahitaji kugundua kwamba tunatakiwa kuweka 100% kwa dakika 95.” Hii inaonyesha kwa timu nzima ilikuwa kama wamechoka, lakini data rasmi zinaonyesha Dortmund hawana tofauti sana na msimu uliopita.Labda shida kubwa ni kuweka ukali ule ule ukicheza mchezo mgumu unaohitaji nguvu kwa kipindi kirefu cha muda. “Staili yetu ni ‘very demanding’,” anakiri beki wa kati Mats Hummels. “Lakini hali hiyo unaiona wakati mambo yanapokuendea kombo.Unapofanikiwa, huioni hali hiyo kwa sana.”



Kukosekana kwa umakini ni jambo lingine, kama ushahisi unavyoonesha namba ya magoli ya magoli waliyofungwa kutokana na mipira iliyokufa.Mara tatu Dortmund wamefungwa kwa aina ya mipira hii. “Hii haikubaliki” alisema Klopp. “Tunatakiwa kuwaweka watu warefu ambao wataweza kuondoa mipira ya adhabu pembeni mwa goli letu.” Suala pia ilnaweza kufananishwa kuhusu uwezo wa wao kufunga magoli msimu pia.





Takwimu za wastani wa kumiliki mpira kwa Dortmund ni asilimia 56, ni Bayern pekee ambao wameweza kumiliki vizuri kiasi hicho.Timu imetengeneza nafasi za wazi 34 za kufunga mabao, takwimu inayoonyesha ni timu 5 pekee kwenye ligi waliyoizidi rekodi hii, lakini kiwango chao cha ufunguji ni kidogo mno, aslimia 20, wastani mbaya kuliko wote katika timu 18 za top flight. “Tunakosa kujiamini”, alisema tena Hummels.Inawezekana mchezo wa kutumia nguvu na kasi unachosa akili za wachezaji lakini hawakuwa na tatizo hili msimu uliopita.Tofauti kubwa pekee inawezekana kutokuwepo kwa mshambuliaji wa ki-paraguay Lucas Barrios, ambaye alifunga mabao 16 na akatoa assists 6 msimu uliopita, Dortmund wanamtegemea Polish forward Robert Lewandowski. The 23 year-old Lewandowski ni mchezaji mzuri sana lakini anaonekana kutokuwa sawa kuongoza mashambulizi mwenyewe kama ilivyokuwa kwa Barrios.Hafichi mipira na matokeo yake, Dortmund inabidi wahangaike sana kuingia ndani ya box.







Watu wengine wenye uzoefu nchini Ujerumani wanasema tatizo ni mabadiliko katika kiungo cha kati. Nahodha wa Dortmund Nuri Sahin amehamia Real Madrid kipindi cha kiangazi na mbadala wake Ilkay Gundogan, bado anahitaji uzoefu wa kuichezea timu kubwa.Anajua na ni mchezaji mzuri lakini hana ‘strategic vision’ kama ya Nuri Sahin.Dortmund wamepoteza ya silaha zake katikati mwa kiwanja.





Kama utaangalia mchezaji muhimu Mari Gotze amesimamishwa na si Shiji Kagawa wala Kevin Großkreutz ambaye ameweza kurejesha fomu waliyokuwa nayo msimu uliopita, hivyo haishangazi kuona kuna ukame wa magoli.



Habari nzuri ni kwamba Barrios amerudi kwenye mazoezi baada ya kuwa nje kwa maumivu ya misuli lakini si rahisi kumuona tena uwanjani mpaka baada ya mapumziko ya kupisha mechi za kimataifa kuisha.Mshambuliaji wa Egypt Mohamed Zidan hayupo hata katika kikosi cha kwanza.



Ni muda pekee pekee ndio utakaotoa majibu kwamba Dortmund wanaweza ku-regroup na kuzichaji upya betri zao katika kipindi hiki muhimu.Kama watashindwa, tegemea kuona sera ya uhamisho ya klabu kubadilika sana.





No comments:

Post a Comment