Search This Blog

Monday, September 5, 2011

GUINESS FOOTBALL CHALLENGE YAZINDULIWA DAR


Wapenzi wa kinywaji mahiri cha Guinness na mashabiki wakubwa wa mpira wa miguu nchini Tanzania, kwa mara ya kwanza leo wamekusanyika katika viwanja vya Leaders kwa ajili ya kushiriki katika GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ ambayo imezinduliwa leo katika viwanja hivyo.

Washiriki wengi wamejitokeza ili kujisajiri na kuonyesha maajabu ya mpira wa miguu katika kipindi hiki kabambe cha Televisheni ambacho kinaangaliwa na kuwavutia watu wengi barani Afrika,Shindano hili litawapatia mashabiki nchini Tanzania nafasi ya kujitokeza na kuonyesha mapenzi yao ya dhati katika mpira wa miguu na kushindana na mashabiki wakubwa wa mpira wa miguu kutoka Kenya na Uganda huku kujishindia mamilioni ya fedha.

Katika picha juu kushoto ni Meneja wa kinywaji cha Guinness Moris Njowoka akumuelekeza jambo Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Serengeti Breweriers Ephraim Mafuru wakati wa shindano hilo leo.

Baada ya kupatika na timu nane zitakazokuwa na watu wawiliwawili , timu hizo zikishiriki katika shindano hilo kupitia Luninga (Television) likirushwa mara moja kila wiki Televisheni kwa muda wa wiki nane, na kila wiki atapatikana mshindi mmoja atakayejishindia Dolla za Kimarekani 50,000.


HAPA NIKIWA NA MKURUGENZI WA MASOKO WA SERENGETI BREWERIERS EPHRAIM MAFURU PAMOJA NA MENEJA WA KINYWAJI CHA GUINESS MORIS NJOWOKA.
WALIODHURIA PIA WALIBURUDIKA NA VINYWAJI KUTOKA GUINESS

No comments:

Post a Comment