Search This Blog

Thursday, September 29, 2011

AFRIKA KUSINI KUANDAA AFRICA CUP OF NATIONS 2013

MOJA YA VIWANJA VITAKAVYOTUMIKA KWENYE AFCON 2013

AFRIKA Kusini watakuwa wenyeji wa Kombe la Mataifa ya Afrika 2013 kuchukua nafasi ya Libya, ilitangaza Shirikisho la Soka la Afrika (Caf).Libya imekubali kuachia wenyeji kwa sababu ya machafuko ya kisiasa yanayoendelea nchini humo.
Hivyo wamategemewa kuwa wenyeji wa fainali za 2017, zilizokuwa zikitegemea kufanyika Afrika Kusini. Kubadilishana huko kwa nchi hizo mbili kulipata baraka za CAF.Afrika Kusini pia watachukua fainali za 2014 za Mataifa ya Afrika wa Wachezaji wa Ndani CHAN zilizokuwa zifanyike Libya.

Mapema mwaka huu waandaji wa Fainali za Mataifa ya Afrika kwa vijana U-20 yaliyokuwa yafanyike Libya waliyaondoa mashindano hayo.

Caf pia walitangaza wenyeji wengine wa mashindano yao makubwa.Namibia watakuwa wenyeji wa fainali za Mataifa ya Afrika 2014 kwa wanawake na Niger watakuwa wenyeji wa U-17 mwaka 2015.
Madagascar watakuwa wenyeji wa U17 mwaka 2017 na mwaka 2015 mashindano ya vijana U20 yatafanyika Senegal.

No comments:

Post a Comment