Search This Blog

Wednesday, August 3, 2011

RAISI WA MATEJA LANGA SHABIKI WA BARCELONA


Msanii maarufu wa muziki wa bongo flava aliyekuwa akiunda kundi la Cocacola Pop Star kwa pamoja na Shaa na Witness, Langa a.k.a Raisi wa Mateja amesema kama kama asingekuwa mwanamuziki basi angechagua soka kama kazi yake.

Langa ambaye recently alijitangaza kuwa ameathirika na matumizi ya madawa ya kulevya baada ya kutumia kwa zaidi ya miaka 5, amesema kabla hajawa mwanamuziki alikuwa anapiga soka vibaya mno katika timu ya mtaani kwao ya Regent Football club lakini kutokana na muziki kuonyesha mwelekeo zaidi wa kimafanikio zaidi ya soka akaamua kuachana na soka na kujikita katika music business.

“Kiukweli nina mapenzi makubwa sana na mchezo wa soka, na kama nisingekuwa rapper basi now ningekuwa dimbani nazungusha tu.Kwa sasa nimebaki kama mshabiki na timu ninazozishabikia ni Barcelona kwa Spain, Juventus in Serie A na Liverpool in England.”-Langa.

No comments:

Post a Comment