Search This Blog

Thursday, August 4, 2011

ARSENAL KUWEKA USAJILI WA FABREGAS BARCA SHAKANI


Arsenal wanaweza kuuweka hatarini usajili wa Cesc Fabregas kwenda Barcelona kwa kutaka kumchezesha nahodha wao katika Champions League play offs.

Mabingwa wa ulaya ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakimtaka Fabregas lakini wamekuwa wakishindwana na Arsenal katika ada ya uhamisho, na sasa mambo yanaonekana kuzidi kuwa magumu baada ya Arsenal kuanza kufikiria kumtumia Cesc katika hatua za mwanzo za ligi ya mabingwa, hatua ambayo itamuweka Fabregas nje ya michuano hiyo ikiwa atajiunga na Barcelona kutokana na sheria ya kukataza kuchezea timu mbili tofauti katika msimu mmoja wa Champions League.

Gunners watafahamu ni wachezaji gani watakaoshiriki katika play offs kesho ijumaa, huku Samir Nasri, mchezaji mwingine anayetaka kuondoka Emirates na Robin Van Persie wakiwa wamesimamishwa na UEFA.

No comments:

Post a Comment