Search This Blog

Tuesday, July 26, 2011

TOP 10 YA WACHEZAJI WANAOLIPWA ZAIDI KWENYE KLABU YA SEATTLE SOUNDERS.

FREDY MONTERO ( kulia,mwenye namba 17 ) kushoto kabisa ni Mtanzania anayeishi marekani Mr Mudrick Majaliwa.

Mara nyingi ukifanya kazi kwa juhudi mwisho wa siku matunda huonekana,
Juhudi za mshambuliaji Fredy Montero raia wa Colombia zimemfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi kwenye klabu ya SEATTLE SOUNDERS ya nchini Marekani, SOUNDERS ndiyo timu anayotarajia kuichezea Mtanzania, Mrisho Ngassa,
Montero amepata ongezeko la kiasi cha $ 500,000 kwa mwaka katika mshahara wake na kumfanya sasa kupata kiasi cha $ 636,000 (zidisha mara 1,500 ili upate ni kiasi gani kwa pesa za kitanzania).

hapo awali Montero alikuwa anapata mshahara wa $ 136,000 kwa mwaka kiasi ambacho ni kama $11,333 kwa mwezi,
lakini juhudi zake ndani na nje ya uwanja sasa zinamfanya aweke kibindoni kiasi cha $ 53,000 kwa mwezi sawa na milioni 79.5 za kitanzania.
kutokana na SOUNDERS kuendelea kufanya vizuri kwenye ligi kuu ya soka nchini Marekani (MLS ) ambayo inaendelea,imepelekea kila mchezaji apate ongezeko la mshahara kutokana na namna alivyotoa mchango wake katika timu.


HUU NDIYO MSIMAMO KAMILI WA WACHEZAJI WA SOUNDERS WANAOLIPWA MSHAHARA MKUBWA ( KUANZIA KUSHOTO NI ONGEZEKO NA KULIA NI JUMLA ).

1. Montero Fredy $500,000.00 $636,000.00

2. Fernandez Alvaro $300,000.00 $366,666.67

3. Keller Kasey $250,000.00 $250,000.00

4. Jaqua Nate $200,000.00 $211,000.00

5. Zakuani Steve $90,000.00 $188,000.00

6. White O'Brian $100,000.00 $147,500.00

7. Evans Brad $126,500.00 $140,250.00

8. Alonso Osvaldo $140,000.00 $140,000.00

9. Parke Jeff $136,500.00 $136,500.00

10.Hurtado John Kennedy $135,000.00 $136,000.00

HAYA WACHEZAJI WA KITANZANIA MNATAKIWA KUJITOLEA MUHANGA KATIKA MAANDALIZI YENU KAMA KWELI MNATAKA KUJA KUCHEZA SOKA LA KULIPWA KWENYE MLS MAANA KILA MWAKA KUNA NAFASI 3 KWA AJILI YENU ZA KUJA KUJIUNGA NA TIMU HII.



No comments:

Post a Comment