Search This Blog

Wednesday, July 6, 2011

BREAKING NEWS: GERVINHO AWASILI LONDON KUFANYIWA VIPIMO NA ARSENAL


Baada ya juzi kumpoteza beki wake mahiri Gael Clichy aliyetimkia Manchester City, klabu ya soka Arsenal leo wanatarajiwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji kutoka Cote d'ivoire Gervinho aliyekuwa anacheza katika klabu ya Lille ya Ufaransa.

Gervinho ambaye aliwasili leo jijini kwa sasa anafanyiwa vipimo na anategemea kutangazwa rasmi kuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Arsenal msimu huu baadae.

Ili kupata huduma za Gervinho, inasemakana Gunners kulipa kiasi cha paundi million 10 kwa klabu ya Lille.


Karibu Emirates - Gervinho

No comments:

Post a Comment