Search This Blog

Tuesday, July 26, 2011

BATISTA AFUKUZWA KAZI ARGENTINA


Chama cha soka la nchini Argentina (AFA) kimetangaza kusistisha ajira ya kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo Sergio Batista baada ya timu hiyo kutolewa katika robo fainali ya Copa America.

Batista ambaye aliongoza Argentina katika michuano ya Copa America akichukua nafasi ya Diego Maradona na kuwa kocha wa nne ndani ya miaka 5.

“Batista ameachishwa kazi ya ukocha mkuu wa timu ya taifa” Ernesto Cherquis Bialo, msemaji wa chama cha soka cha Argentina alisema, jana Jumatatu.

Mpaka sasa kocha wa zamani wa Argentine Club Estudiantes Alejandro Sabella, na kocha wa Paraguay Gerardo Martino ndio wanaopewa nafasi kubwa ya kumrithi Batista.

Msemaji wa AFA, Cherquis Bialo amesema kocha mpya atatangazwa ndani ya wiki moja.

Heshima ya soka Argentina imeshuka kutokana matatizo ya makocha wanaoshindwa kuunda muunganiko mzuri wa timu yenye kama wengi, kitu kilichowafanya kukosa kushinda kombe lolote kubwa ndani ya miaka 18, sasa ni miaka 25 tangu Argentina wachukue kombe la dunia.

No comments:

Post a Comment