Search This Blog

Monday, June 27, 2011

LEO KATIKA USAJILI BARANI ULAYA


FABREGAS YUPO TAYARI KUKOSA £5 MIL. KWA AJILI YA BARCA

Cesc Fabregas yupo radhi kukosa paundi million 5 katika gawio la uhamisho wake ili aweze kupunguza bei ya Arsenala wanayoitaka kutoka Barcelona.
Arsenal wiki iliyopita waliripotiwa kukataa ofa ya paundi million 27 kutoka kwa Barca kwa ajili kumsaini Fabregas.
Katika mkataba wa kiungo huyo wa Spain kuna kipengele kinasema kuwa Arsenal wakimuuza Fabregas kwa timu yoyote itabidi wampe gawio la asilimia 15 la fedha ya uhamisho, hivyo kupitia kipengele hicho Cesc anatarajiwa kuwaambia Arsenal wasimpe kiasi cha £5 milion kutoka katika katika ofa ya £ 33 million, kiasi ambacho Barcelona wanajipanga kueleka kwa Gunners kwa ajili yake ili aweze kurahisha uhamisho kutoka Emirates kuelekea Nou Camp.

MAN UNITED NA ALCANTARA + NASRI

Klabu bingwa la ligi kuu ya England wanaripotiwa kupeleka ofa ya paundi millioni 15 kwa ajili ya kupata saini ya kiungo wa Spain na Barcelona Thiago Alcantara.

Thiago amekuwa akitumika na Barca katika harakati za kutaka kumrudisha Cesc Fabregas Nou Camp kwa

kumtoa kwa mkopo au kumuuza kwa Arsenal kwa mkataba utakaokuwa na kipengele cha kuwawezesha wao(Barca) kumnunua watakapomhitaji tena, sasa amekuwa gumzo katika dirisha la usajili barani ulaya akifuatilwa na timu kama Chelsea na Bolton.

United wanamuona Alcantara kama moja ya viungo wanaoweza kuziba pengo la Paul Scholes hivyo kumfanya Sir Alex Ferguson kufungua pochi kwa ajili ya kinda huyo aliifungia timu yake ya Spain bao la ushindi katika fainali ya EURO under 21, weekend iliyopita.

Wakati huo huo taarifa za ndani kutoka kutoka ndani ya klabu hiyo ya Mashetani Wekundu zinasema kuwa Mnager wa United anatarajiwa kupeleka ofa nzuri ya paundi million 20 kwa Arsenal kwa ajili ya kiungo kifaransa Samir Nasri.

Man United ambao wakuwa wakihusishwa na kuhitaji huduma za Nasri tangu mchezaji huyo alipokataa kusaini mkataba mpya na klabu yake kutokana na masuala ya mshahara anaotaka sasa wanaonekana kuwa serious na kukamilisha uhamisho wa mchezaji huyo kabla ya kuanza kwa mataarisho ya ligi ya msimu ujao.


No comments:

Post a Comment