Search This Blog

Wednesday, June 15, 2011

INTER YATHIBITISHA KUONDOKA KWA LEONARDO-YAMTAKA MARCELO BIESLA



INTER MILAN wamethibitisha kuondoka kwa kocha wao Leonardo na wanamuwania Marcelo Biesla kama mbadala wa mchezaji huyo wa zamani wa Brazil na AC milan.
Leonardo ambaye alikuwa mbadala wa Rafa Benitez ndani ya Inter ameisadia timu hiyo kushika nafasi ya pili kwenye Serie A na pia ameipa timu hiyo ubingwa wa kombe la Italia, lakini Leonardo jana alithibitisha kuwa yupo katika mipango ya kuhamia Paris Saint Germain ya Ufaransa baada ya kufanya mazungumzo na wamiliki wapya wa timu hiyo Qatar Sports Investments.

Inter president Massimo Moratti ambaye mwanzo alikanusha kuondoka kwa Leo" ameandika katika website ya Inter kuwa kocha huyo anaweza kuondoka Guisseppe De Meazza.
"Leonardo ameifundisha timu yetu kwa mapenzi makubwa lakini anaweza asiwe na sisi msimu ujao, ni kitu kizuri ametuambia mapema na sisi tumeanza kujiandaa kutafuta kocha mpya.Anaweza akawa Leonardo kama akiamua kubadilisha mawazo.Hata hivyo tayari tumeshafanya mawasiliano na Biesla kumshawishi ajiunge nasi msimu ujao.


Wakati huo huo taarifa kutoka Italia zinasema kuwa Raisi huyo wa Inter amewaambia Real Madrid wanaweza kumpata Douglas Maicon ikiwa watawapa Sergio Ramos.


Corriere dello Sport limesema kuwa kocha Jose Mourinho yupo tayari kumtoa Marcelo katika dili hilo lakini Morrati amesisitiza kumtaka Ramos.

No comments:

Post a Comment