Taarifa zisizo rasmi nilizozipata hivi punde klabu ya Yanga ipo kwenye mazungumzo na aliyekua kocha wa Taifa Stars Mbrazil Marcio Maximo.
Kama mazungumzo hayo yatafanikiwa basi Maximo atarejea kwa mara nyingine tena hapa nchini kuja kuifundisha Yanga.
Search This Blog
Thursday, June 7, 2012
UFARANSA: HAIJASHINDA MECHI YOYOTE KWENYE EURO WALA WORLD CUP TANGU 2006: ITAFANYA NINI KWENYE EURO 2012.
Laurent Blanc anaichukua Ufaransa kwenda nayo kwenye Euro 2012 huku akiiongoza timu hiyo kutofungwa katika michezo 20, ambayo inahusisha ushindi dhidi ya Ujerumani, England na Brazil. Lakini kocha huyo wa timu ya taifa ya Ufaransa bado haipi nafasi kubwa timu. Ufaransa haijashinda mechi yoyote ya mwisho ya michuano mikubwa yenyewe tangu mechi ya nusu fainali ya World Cup 2006 (haikushinda mechi yoyote kwenye Euro 2008 na WOZA 2010), huku wakishika nafasi ya 16, nafasi tisa nyuma ya wapinzani wao England wanaoshika nafasi ya saba kwenye ubora wa viwango wa FIFA.
Blanc bado na maumivu ya kichwa kuhusu upangaji wa kikosi hasa kwenye nafasi ya beki wa kushoto, ambapo Gael Clichy ameonyesha kiwango kizuri kwenye mchi dhidi ya Serbia siku chache baada ya Evra kucheza chini kiwango dhidi ya Iceland. Kiungo mkabaji Yann M'Vila pia ana majeruhi ya enka ambayo yatamfanya asicheze mchezo wa kwanza na Alou Diarra anategemewa kumbadili.
Lakini hiki ni kikosi tofauti sana na kile kilichoenda kwenye kombe la dunia 2010 chini Raymond Domenech nchini South Africa. Golikipa Hugo Lloris sasa ni nahodha, lakini Phillipe Mexes, M'Vila na Karim Benzema ambaye yupo kwenye form sasa hivi, wote waliikosa michuano ya WOZA 2010 hivyo hawakuwemo kwenye aibu iliyopita. Lakini hili haliwezi kusemwa linapojitokeza jina la Frank Ribery, ambaye kwa sasa yupo desparate kuweza kurudisa imani na upendo wa wafaransa. Baada ya miaka 3 bila kufunga bao, Ribery alifunga mara mbili katika mechi 2 za kirafiki zilizopita. Ikiwa ataanza japo kuileta nusu ya uwezo anaonyesha Bayern Munich akiwa kwenye jezi za Blue, then Les Bleus wanaweza kuwashangaza wengi.
WACHEZAJI MUHIMU
Karim Benzema
Tumaini kubwa la soka la Ufaransa lilikuwa na mwanzo mmbaya kwenye career yake ndani ya timu ya taifa ya Ufaransa kwenye michuano ya Euro 2008, pale alipotuhumiwa kwa pamaja na Samir Nasri kwa kutokuwa na heshima kwa wachezaji wakubwa na kwa kutompasia mipra mingi Thierry Henry. Akaachwa kwenye kombe la dunia 2010, lakini amekuwa ndio mfungaji bora wa Ufaransa chini ya Blanc, akifunga mabao matano katika mechi 17, likiwemo goli la ushindi dhidi ya Brazil. Huku akiwa amemaliza msimu wa mafanikio na Real Madrid akifunga mabao 32, huku akitamba kwamba amekuwa mchezaji mzuri zaidichini Jose Mourinho. Na kama hayo maneno yataonekana kwenye vitendo basii Ufaransa itaifadika sana.
Samir Nasri
Mpaka aliposhinda kombe la premier league na Manchester City mwezi uliopita, Nasri alikuwa ameshinda kombe moja tu kwenye maisha yake ya soka la kulipwa: alipofunga goli la ushindi kwenye fainali ya Euro 2004 kwa timu ya vijana wa miaka 17. Nasri ni moja ya sehemu ya kundi 'Kizai cha 87' kinachowahusisha wachezaji waliozaliwa mwaka 1987 na kwa sasa wakiwa ndio wanaelekea kwenye vilele vya viwango vyao wakiwa kwenye timu ya taifa ya wakubwa. Kundi hilo lilikuwa linawahusisha Benzema, Hatem Ben Arfa, Jelemu Menez na Blaise Matuidi - wote walicheza kwenye Euro 2004, na sasa wapo kwenye Euro 2012 ya wakubwa. Kama kiungo mchezeshaji Nasri anayo nafasi ya kuifanya timu ikacheza soka zuri la kushambulia na ahatimaye kuiletea timu ushindi. Ni jukumu ambalo amekuwa alilitumikia siku nyingi, sasa hivi anayo nafasi ya kuonyesha kama kweli anastahili.
Yann M'Vila
Kiungo mkabaji anatarajiwa kuuzwa kwa mapesa mengi mara baada ya michuano hii, na klabu yake. Rennes, inaweza ikataka kuongeza beikama atacheza vizuri kwenye Euro.M'Vila alikuwa na bahati kuikosa world cup, alitoswa na Domenech lakinii chini ya Blanc amejihakikishia nafasi ya kudumu. Akiwa na miaka 21, amekuja kuwa mchezaji muhimu wa Ufaransana kwa jinsi inavyocheza, kuvunja mashambulizi ya wapinzani na kushambulia kutokea kwenye kiungo huku akiwa na uwezo mkubwa wa kupiga pasi. Ameshajulikana kwamba ataikosa mechi yake ya kwanza ya Euro dhidi ya England na anategemewa kurudi dimbani kwenye mechi ya Ukraine.
Blanc bado na maumivu ya kichwa kuhusu upangaji wa kikosi hasa kwenye nafasi ya beki wa kushoto, ambapo Gael Clichy ameonyesha kiwango kizuri kwenye mchi dhidi ya Serbia siku chache baada ya Evra kucheza chini kiwango dhidi ya Iceland. Kiungo mkabaji Yann M'Vila pia ana majeruhi ya enka ambayo yatamfanya asicheze mchezo wa kwanza na Alou Diarra anategemewa kumbadili.
Lakini hiki ni kikosi tofauti sana na kile kilichoenda kwenye kombe la dunia 2010 chini Raymond Domenech nchini South Africa. Golikipa Hugo Lloris sasa ni nahodha, lakini Phillipe Mexes, M'Vila na Karim Benzema ambaye yupo kwenye form sasa hivi, wote waliikosa michuano ya WOZA 2010 hivyo hawakuwemo kwenye aibu iliyopita. Lakini hili haliwezi kusemwa linapojitokeza jina la Frank Ribery, ambaye kwa sasa yupo desparate kuweza kurudisa imani na upendo wa wafaransa. Baada ya miaka 3 bila kufunga bao, Ribery alifunga mara mbili katika mechi 2 za kirafiki zilizopita. Ikiwa ataanza japo kuileta nusu ya uwezo anaonyesha Bayern Munich akiwa kwenye jezi za Blue, then Les Bleus wanaweza kuwashangaza wengi.
WACHEZAJI MUHIMU
Karim Benzema
Tumaini kubwa la soka la Ufaransa lilikuwa na mwanzo mmbaya kwenye career yake ndani ya timu ya taifa ya Ufaransa kwenye michuano ya Euro 2008, pale alipotuhumiwa kwa pamaja na Samir Nasri kwa kutokuwa na heshima kwa wachezaji wakubwa na kwa kutompasia mipra mingi Thierry Henry. Akaachwa kwenye kombe la dunia 2010, lakini amekuwa ndio mfungaji bora wa Ufaransa chini ya Blanc, akifunga mabao matano katika mechi 17, likiwemo goli la ushindi dhidi ya Brazil. Huku akiwa amemaliza msimu wa mafanikio na Real Madrid akifunga mabao 32, huku akitamba kwamba amekuwa mchezaji mzuri zaidichini Jose Mourinho. Na kama hayo maneno yataonekana kwenye vitendo basii Ufaransa itaifadika sana.
Samir Nasri
Mpaka aliposhinda kombe la premier league na Manchester City mwezi uliopita, Nasri alikuwa ameshinda kombe moja tu kwenye maisha yake ya soka la kulipwa: alipofunga goli la ushindi kwenye fainali ya Euro 2004 kwa timu ya vijana wa miaka 17. Nasri ni moja ya sehemu ya kundi 'Kizai cha 87' kinachowahusisha wachezaji waliozaliwa mwaka 1987 na kwa sasa wakiwa ndio wanaelekea kwenye vilele vya viwango vyao wakiwa kwenye timu ya taifa ya wakubwa. Kundi hilo lilikuwa linawahusisha Benzema, Hatem Ben Arfa, Jelemu Menez na Blaise Matuidi - wote walicheza kwenye Euro 2004, na sasa wapo kwenye Euro 2012 ya wakubwa. Kama kiungo mchezeshaji Nasri anayo nafasi ya kuifanya timu ikacheza soka zuri la kushambulia na ahatimaye kuiletea timu ushindi. Ni jukumu ambalo amekuwa alilitumikia siku nyingi, sasa hivi anayo nafasi ya kuonyesha kama kweli anastahili.
Yann M'Vila
Kiungo mkabaji anatarajiwa kuuzwa kwa mapesa mengi mara baada ya michuano hii, na klabu yake. Rennes, inaweza ikataka kuongeza beikama atacheza vizuri kwenye Euro.M'Vila alikuwa na bahati kuikosa world cup, alitoswa na Domenech lakinii chini ya Blanc amejihakikishia nafasi ya kudumu. Akiwa na miaka 21, amekuja kuwa mchezaji muhimu wa Ufaransana kwa jinsi inavyocheza, kuvunja mashambulizi ya wapinzani na kushambulia kutokea kwenye kiungo huku akiwa na uwezo mkubwa wa kupiga pasi. Ameshajulikana kwamba ataikosa mechi yake ya kwanza ya Euro dhidi ya England na anategemewa kurudi dimbani kwenye mechi ya Ukraine.
EXCLUSIVE: SIMBA YAKAMILISHA USAJILI WA SALUM KINJE WA AFC LEOPARDS
![]() |
| Salum Kinje |
Taarifa rasmi za uhakika kutoka ndani ya uongozi na kamati ya ufundi ya klabu ya Simba ni kwamba timu hiyo imefanikiwa kukamilisha usajili wa mchezaji bora wa nafasi ya kiungo kwenye ligi kuu ya soka nchini Kenya, Salum Kinje ambaye anaichezea AFC Leopards.
![]() |
| Nikiwa na Salum Kinje nilipotembelea Kenya mwezi uliopita. |
Kinje ambaye ni mtanzania amesajiliwa na Simba kwa kiasi cha fedha ambacho hakijawekwa wazi na pande zote mbili, lakini amesaini mkataba wa kuitumikia Simba kwa miaka 2 na siku chache zijazo ataanza mazoezi na timu yake mpya inayojiandaa kushiriki michuano ya Kagame Cup inayotarajiwa kuanza hivi karibuni.
Wednesday, June 6, 2012
SAKATA LA KELVIN YONDANI: YANGA YATOA USHAHIDI WA PICHA
KWANINI MANJI ANAUTAKA UONGOZI WA YANGA?
*NI KWELI ANATAKA KUIMILIKI YANGA?
*NA KAMA AKIFANIKIWA KUWA MMILIKI ATAIFANYIA NINI YANGA?
*KWANINI BAADHI YA WANACHAMA HAWAMTAKI?
Katika hali ya kushtusha siku ya jumatatu mfanyabiashara na mdhamini wa klabu hiyo, Manji akachukua fomu ya kugombea uenyekiti wa klabu hiyo yenye maskani yake mitaa ya jangwani,huku akimchukulia mmoja wa wajumbe wa kamati ya usajili Abdallah Ahmed Bin Kleb fomu ya kugombea ujumbe wa kamati ya utendaji, na hatimaye leo Manji alikuwa mmoja ya wanachama 29 wa Yanga waliorudisha fomu za kugombea nafasi za uongozi mbalimbali ndani ya Yanga.
Wakati wakili Iman Madega anataka kuingia Yanga alikuwa akipigwa tafu kubwa sana na bwana Manji mpaka akafanikiwa kuutwa uongozi wa klabu hiyo. Lakini baada ya muda kupita kukatokea kutokuelewana baina ya watu hao wawili. Hii ilikuwa ni baada ya Manji kuleta wazo la kutaka Yanga iendeshwe na kampuni. Kwa maana ingeanzishwa kampuni ambayo ingenunua asilimia 51 za Yanga, na asilimia 49 zinazobakia zingekuwa zinamilikiwa na wanachama ambao wangekopeshwa kiasi cha billioni 3 na Manji kwa mkopo wa mwaka mmoja tu, huku akiwawekea sharti kwamba kama wangeshinda kuzilipa billioni 3 zake alizowakopesha ndani ya kipindi walichokubaliana kulipwa na mkopo huo , basi Manji ndio angekuwa mtu wa kwanza kuuziwa hisa zile zile ambazo walishindwa kuzilipia.
KIVIPI?
Kiuhalisia tu shilingi billioni 3 ni fedha nyingi sana kwa wanachama wa kawaida wa Yanga ambao ndio wapo wengi kuweza kumudu kuzilipa ndani ya kipindi mwaka mmoja. Hata kama wangemudu kuzilipa basi isingekuwa rahisi unless kuwe kuna mkono wa mtu nyuma yao, na kama wangeumudu kwa uwezo wao basi ni wachache sana wangeweza kufanya hivyo, hivyo mwisho wa siku hisa nyingi sana zingerudi mikononi mwa Manji.
*NA KAMA AKIFANIKIWA KUWA MMILIKI ATAIFANYIA NINI YANGA?
*KWANINI BAADHI YA WANACHAMA HAWAMTAKI?
Kwa kipindi kirefu sasa tangu mfanyabiashara maarufu Bwana Manji ajiingize katika kuifadhili klabu ya Dar Young Africans kumekuwepo na mgawanyiko mkubwa wa kifikra miongoni mwa wanamichezo, wanachama na wapenzi wa Yanga, juu ya madhumuni hasa kabisa ya mfanyabiashara huyo kuisadia Yanga.
Huku baadhi ya watu wakisema Manji ana nia ya dhati kabisa ya kuisadia Yanga na kuifanya kuwa klabu ya kisasa kabisa,huku wengine wakibaki kusema kwamba mmiliki huyo wa Quality Group of Companies anataka kuitumia Yanga kibiashara na kujinufaisha binafsi kwa kutumia brand ya Yanga.
Katika kipindi cha awamu mbili za uongozi tofauti pale Yanga, kuanzia kwa Wakili Iman Madega mpaka uongozi huu uliopinduliwa wa mwanasheria Lloyd Nchunga, Yusuph Manji amekuwa akitajwa kuhusika na migogoro mikubwa iliyojitokeza ndani ya klabu hiyo.
Hivi karibuni baada ya baadhi ya wanachama wa klabu ya Yanga hasa wakiongozwa na wazee wa klabu hiyo, waliongoza mapinduzi ya kuuondoa uongozi halali wa bwana Lloyd Nchunga, ambaye mara ya kwanza alijaribu kutuna lakini mwishowe akaachia ngazi mwenyewe baada ya kuandamwa sana kiasi cha kuanza kupokea vitisho na kufanyiwa vurugu. Wazee wakachukua timu huku wakitamba wana zaidi ya millioni 750 za kufanya usajili, lakini TFF ikairudisha timu chini ya uongozi wa katibu mkuu Celestine Mwesiga huku wakiagiza ufanyike uchaguzi kama katiba ya klabu inavyosema.
Uchaguzi ukaitishwa kwa mujibu wa kanuni, na kamati ya uchaguzi ikaanza kutoa fomu za nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya Yanga.
Katika hali ya kushtusha siku ya jumatatu mfanyabiashara na mdhamini wa klabu hiyo, Manji akachukua fomu ya kugombea uenyekiti wa klabu hiyo yenye maskani yake mitaa ya jangwani,huku akimchukulia mmoja wa wajumbe wa kamati ya usajili Abdallah Ahmed Bin Kleb fomu ya kugombea ujumbe wa kamati ya utendaji, na hatimaye leo Manji alikuwa mmoja ya wanachama 29 wa Yanga waliorudisha fomu za kugombea nafasi za uongozi mbalimbali ndani ya Yanga.
Kitendo cha Manji kuutaka ubosi wa klabu ya Yanga umeibua hofu na maswali mengi juu ya nia hasa ya mfanyabiashara huyo dhidi ya Yanga, baadhi ya wanachama wa klabu hiyo ambao siku zote wamekuwa wakimpinga Manji kwa namna moja au nyingine wakidai hana nia nzuri ya klabu yao, wameongea exclusively na shaffihdauda.com na kutoa hoja nyingi sana zinazojaribu kuelezea kwanini hawana imani na mpango wa Manji kuwa mwenyekiti wa klabu yao.
1:MANJI VS IMANI MADEGA NA LLOYD NCHUNGA
Wakati wakili Iman Madega anataka kuingia Yanga alikuwa akipigwa tafu kubwa sana na bwana Manji mpaka akafanikiwa kuutwa uongozi wa klabu hiyo. Lakini baada ya muda kupita kukatokea kutokuelewana baina ya watu hao wawili. Hii ilikuwa ni baada ya Manji kuleta wazo la kutaka Yanga iendeshwe na kampuni. Kwa maana ingeanzishwa kampuni ambayo ingenunua asilimia 51 za Yanga, na asilimia 49 zinazobakia zingekuwa zinamilikiwa na wanachama ambao wangekopeshwa kiasi cha billioni 3 na Manji kwa mkopo wa mwaka mmoja tu, huku akiwawekea sharti kwamba kama wangeshinda kuzilipa billioni 3 zake alizowakopesha ndani ya kipindi walichokubaliana kulipwa na mkopo huo , basi Manji ndio angekuwa mtu wa kwanza kuuziwa hisa zile zile ambazo walishindwa kuzilipia.
Pia katika zile hisa asilimia 51, hakukuwa na sheria zozote za kumkataza mtu yoyote kununua hisa hizo, uwe mwanachama au la ungeweza kununua hisa, hata Manji mwenyewe kama angejisikia kufanya hivyo pia alikuwa na uhuru wa kununua.
Baada ya kuupitia vizuri mpango huo Iman Madega hakuweza kukubaliana na mpango huo kwa hofu, kwamba ule ni mpango ambayo ungeidhuru Yanga.
Baada ya kumshindwa Madega ambaye alifanikiwa kumaliza kipindi chake cha Uongozi, klabu hiyo ikafanya uchaguzi na kupata uongozi mpya chini ya Lloyd Nchunga ambaye naye alipoletewa mpango wa kuanzishwa kwa kampuni na Manji akakataa na matokeo yake timu ikahujumiwa kitu kilichopelekea migomo ya wachezaji, na hivyo timu kufanya vibaya kwenye ligi. Inasemekana baada ya Nchunga kuvimba na kukataa kujiuzulu baada ya kipigo cha 5-0 kutoka watani wao Simba, ndipo bosi Manji alipoanza kutoa mkwanja kwa baadhi ya viongozi na kuwaambia wajiuzulu huku akiwatumia wazee kumtia mshikemshike Nchunga ambaye mwishowe akaamua kujiuzulu na kupelekea kuitishwa kwa uchaguzi mpya.
KIVIPI?
Kiuhalisia tu shilingi billioni 3 ni fedha nyingi sana kwa wanachama wa kawaida wa Yanga ambao ndio wapo wengi kuweza kumudu kuzilipa ndani ya kipindi mwaka mmoja. Hata kama wangemudu kuzilipa basi isingekuwa rahisi unless kuwe kuna mkono wa mtu nyuma yao, na kama wangeumudu kwa uwezo wao basi ni wachache sana wangeweza kufanya hivyo, hivyo mwisho wa siku hisa nyingi sana zingerudi mikononi mwa Manji.
Huku pia kwenye asilimia 51 za kampuni Manji alikuwa na uhuru wa kununua hisa, hivyo kama Manji akazipata labda asilimia 40 ya hisa alizowalipia wanachama kwa mkopo na wakashindwa kuzilipa na huku kwenye kampuni akanunua japo asilimia 15 tu, kwa maana hiyo angekuwa ndio majority shareholder hivyo kumfanya kuwa mmiliki wa Yanga SC.
2: KWANINI HAWATAKI MANJI AIMILIKI YANGA?
Anti-Manji wanasema hawana imani kabisa na Manji kwamba anaitaka Yanga ili kuisadia iwe klabu na yenye mafanikio, bali ni kwa maslahi yake binafsi.
Kwanza wanajenga hoja kwamba Manji hakuingia Yanga kwa mapenzi binafsi bali alisukumwa na sababu za kisiasa kwa kuifanya klabu hiyo inayosadikika kuwa na wapenzi wengi zaidi nchini kuwa kichaka cha kujifunikia madhambi yake baada ya kukumbwa na kashfa ya EPA.
Wanasema Manji tofauti na wadhamini wengine waliowahi kuidhamini na kuisadia Yanga kama akina Gulamali na Mohamed Vilani, ambao walikuwa wakitoa fedha nyingi kuisadia timu yao bila kuidai chochote, lakini Yusuf Manji siku zote amekuwa akiwasainisha kwenye vitabu vya kumbukumbu viongozi kwa niaba ya Yanga kila anapotoa fedha labda ya usajili au kuisadia pale timu inapokwama kiuchumi, na hilo limeshathibitishwa na Manji mwenyewe pale alipokaririwa mara kadhaa akisema anaidai Yanga fedha nyingi bila kuweka wazi ni kiasi gani. Kwa hiyo hawajui ni lini atawadai fedha anazoidai klabu hiyo na kama watashindwa kulipa je atafanya nini?
Anti-Manji wanaendelea kujenga hoja zao kwa kusema kuwa wanahisi kwamba Manji ambaye pia ni mfanyabiashara ambaye anamiliki majengo mengi ya kibiashara hapa nchini anachokihitaji kutoka Yanga kwanza ni kujilipa fedha zote alizotumia kuisaidia klabu hiyo pamoja na zile ambazo zipo nje ya vitabu alizotumia kupata wafuasi waliochini ya himaya yake ndani ya klabu hiyo.
Wanasema wasiwasi wao ni kwamba ikiwa Manji atakuwa mmiliki wa Yanga, ataitumia brand ya klabu hiyo pamoja na assets zake ili kujilimbikizia fedha nyingi kwa kipindi labda cha miaka 3 mpaka mitano na baadae ataliuza tu jina la Yanga ikiwemo timu, na yeye kubaki na assets za Yanga yakiwemo majengo mawili ambayo yote yapo kwenye eneo la kibiashara la kariakoo pamoja na eneo kubwa wanalolimiliki Yanga la Jangwani makao makuu ambapo imegundulika Yanga inahodhi eneo kubwa sana ambalo kwa sasa limevamiwa na baadhi ya majirani wanaoishi karibu na makao makuu ya Yanga-Jangwani.
Endapo Manji ataliuza jina la Yanga na kubaki na assets za klabu hiyo kisha kuzitumia kwa matumizi mengine, klabu hiyo itapoteza sehemu ya historia yake kubwa iliyojijengea.
3: ANTI-MANJI WALIVYOPOKEA TAARIFA ZA MANJI KURUDISHA FOMU BILA TEGEMEO LAO IDD KIPINGU KUSHINDWA KUCHUKUA FOMU.
Baada ya Manji kuchukua fomu za kugombea uenyekiti wa Yanga, kundi la wanachama wanaompinga Manji kwa sababu zao waliamua kutafuta njia za kuweza kupambana nae. Inasemekana wakajaribu kumtumia mtoto wa kigogo wa nchi ambaye nae ana nguvu na ufuasi mkubwa ndani ya klabu hiyo, ili aweze kumshawishi Kanali Iddi Kipingu agombee nafasi hiyo, lakini baada ya Kipingu kushindwa kuhakikishiwa kupewa sapoti ya asilimia 100 ya kuweza kupambana na tajiri Manji akaona bora asijiingize kwenye vita mabayo itaweza kumshushia heshima yake kubwa aliyojijengea kwenye tasnia ya michezo nchini kwa kuangushwa vibaya na Sheikh Mansour wa Tanzania.
NB: HUU SIO MTAZAMO WANGU BALI NI MTAZAMO WA WANACHAMA WA YANGA WANAOMPINGA MANJI. NIMEWASILISHA. BY SHAFFIH DAUDA.
NB: HUU SIO MTAZAMO WANGU BALI NI MTAZAMO WA WANACHAMA WA YANGA WANAOMPINGA MANJI. NIMEWASILISHA. BY SHAFFIH DAUDA.
YANGA YATANGAZA KUMSAJILI KEVIN YONDAN HUKU SIMBA IKIMUONGEZEA MKATABA KELVIN YONDANI.
Leo hii klabu ya Yanga imetangaza kumsajili kinda raia wa Tanzania Kevin Patrick Yondan mwenye umri wa miaka 17,Yondan ambaye anacheza nafasi ya beki wa kati hajajulikana ametokea Klabu gani alizaliwa 9/10/1994.Mkataba wa Yanga na kinda huyo ni wa miaka miwili na unataraji kumalizika msimu wa 2013/2014.
hapa chini ni sehemu ya mkataba wa beki huyo na klabu ya Yanga yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani.
hapa chini ni sehemu ya mkataba wa beki huyo na klabu ya Yanga yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani.
Wakati huo huo Simba Sc imetangaza kumuongezea mkataba wa miaka miwili beki wake wa kati Kelvin Patrick Yondani, mkataba huo mpya ulisainiwa tangia mnamo 23/12/2011 ikiwa ni maboresho ya mkataba wa awali uliokua unafika kikomo mwishoni mwa mwezi uliopita yaani 31/05/2012. Yondani mwenye umri wa miaka 27 pia ni beki wa kimataifa wa Tanzania.
Kelvin Patrick Yondani
|
Baadhi ya michezo ambayo Kelvin Patrick Yondani ameichezea timu ya Taifa ya Tanzania.
| Tarehe | Nyumbani | matokeo | Ugenini | ||
|---|---|---|---|---|---|
| 2012-06-02 | Côte d'Ivoire |
2 - 0
| Tanzania | ||
| 2012-05-26 | Tanzania |
0 - 0
| Malawi | ||
| 2012-02-23 | Tanzania |
0 - 0
| Congo DR | ||
| 2011-11-15 | Tanzania |
0 - 1
| Chad | ||
| 2011-11-11 | Chad |
1 - 2
| Tanzania | ||
| 2010-06-07 | Tanzania |
1 - 5
| Brazil | ||
| 2010-01-04 | Tanzania |
0 - 1
| Côte d'Ivoire |
BIN KLEB ARUDISHA FOMU YAKE NA MANJI JANGWANI
![]() |
| Anaondoka |
Source: Binzubeiry
TANZANIA YAPANDA VIWANGO VYA FIFA
KIINGILIO MECHI YA TAIFA STARS, GAMBIA 3,000/-
Kiingilio cha chini ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Gambia (The Scorpions) itakayochezwa Jumapili (Juni 10 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 3,000.
Watazamaji watakaolipa kiingilio hicho ni watakaokaa kwenye viti vya rangi ya bluu na kijani ambavyo ni 36,693 kati ya jumla ya viti 57,558 vilivyopo katika uwanja huo wa kisasa. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ni sh. 5,000.
Kwa upande wa VIP C watalipa sh. 10,000 wakati VIP B ni sh. 20,000. Kiingilio kwa jukwaa la VIP A ambalo linachukua watazamaji 748 tu ni sh. 30,000 kwa mechi hiyo itakayoanza saa 10 kamili jioni.
Tiketi zitaanza kuuzwa Jumamosi (Juni 9 mwaka huu) kuanzia saa 2 asubuhi kwenye vituo vya Mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Soko Kuu la Kariakoo na Uwanja wa Taifa. Siku ya mechi pia mauzo yatafanyika katika vituo hivyo na baadaye kuhamia Uwanja wa Taifa.
GAMBIA YATARAJIA KUINGIA LEO DAR ES SALAAM
Timu ya Taifa ya Gambia (The Scorpions) inatarajia kuwasili nchini wakati wowote kuanzia leo (Juni 6 mwaka huu) tayari kwa ajili ya mechi dhidi ya Taifa Stars.
Kamati ya Maridhiano inayoendesha Chama cha Soka Gambia (GFA) hadi leo mchana ilikuwa haijatuma taarifa rasmi kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) juu ya ujio wake.
Lakini vyombo vya habari vya Gambia vimeripoti kuwa timu hiyo ikiwa na wachezaji 23 na viongozi tisa ilitarajiwa kuondoka huko leo kuja Dar es Salaam tayari kwa ajili ya mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu na washabiki wengi nchini.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa GFA aliyekaririwa na vyombo vya habari vya nchi hiyo, Bakary Balder, msafara wa timu hiyo utaongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana na Michezo, Malang Jassey. .
Mbali ya Jassey, viongozi wengine katika msafara huo ni Ofisa Utawala wa timu Modou Sowe, Kocha Luciano Machini, makocha wasaidizi Peter Bonu Johnson na Lamin Sambou, Kocha wa makipa Alhagie Marong, mtaalamu wa tiba mbadala (physiotherapist) Pa Matarr Ndow, Mtunza vifaa Sanna Bojang na Daktari wa timu Kalifa Manneh.
Wachezaji ni Musa Camara, Abdou Jammeh, Momodou Futty Danso, Lamin Basmen Samateh, Ousman Koli, Pa Saikou Kujabi, Mustapha Kebba Jarju, Yankuba Mal Ceesay, Demba Savage, Saihou Gassama, Alieu Darboe, Momodou Ceesay, Pa Modou Jagne, Tijan Jaiteh, Bubacarr Sanyang, Christopher Allen, Musa Yaffa, Sulayman Marr, Mamut Saine, Hamsa Barry, Ali Sowe, Omar Colley na Saloum Faal.
TANZANIA YAPANDA VIWANGO VYA FIFA
Tanzania imepanda kwa nafasi sita kwenye orodha ya viwango ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) iliyotolewa leo (Juni 6 mwaka huu) na shirikisho hilo.
Kwa viwango vya Mei mwaka huu, Tanzania ambayo timu yake ya Taifa (Taifa Stars) inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ilikuwa namba 145 hivi sasa imefika nafasi ya 139 ikiwa na pointi 214.
Mei 26 mwaka huu Taifa Stars ilicheza mechi ya kirafiki na Malawi na kutoka suluhu. Malawi yenye pointi 324 imeporomoka kwa nafasi tano kutoka ya 102 hadi 107.
Ivory Coast ambayo katika mechi yake ya mwisho Juni 2 mwaka huu iliifunga Taifa Stars mabao 2-0 imeporomoka kwa nafasi moja kutoka ya 15 hadi 16 ikiwa na pointi 943. Hata hivyo ndiyo inayoongoza kwa upande wan chi za Afrika katika viwango hivyo.
PROGRAMU YA TAIFA STARS KWA MECHI YA GAMBIA
JUMATANO JUNI 6
01.00 asubuhi Mazoezi- Uwanja wa Karume
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa
ALHAMISI JUNI 7
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa
IJUMAA JUNI 8
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa
JUMAMOSI JUNI 9
04.00 asubuhi Mkutano na Waandishi wa Habari- Ukumbi wa TFF
11.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
EXCLUSIVE: ALLY MAYAY ABADILI MAWAZO -ACHUKUA FOMU YA UMAKAMU WA MWENYEKITI
Mchezaji wa zamani na mmoja ya wajumbe wa kamati ya utendaji ya Yanga ya uongozi uliopita, Ally Mayay amebadili juu ya kutaka kugombea tena ujumbe wa kamati ya utendaji.
Kwaa taarifa nilizonazo kutoka kwake ni kwamba Ally Mayay sasa ameamua kwenda kuchukua fomu za kugombea umakamu uenyekiti wa klabu hiyo aliyoichezea kwa mafanikio miaka kadhaa iliyopita.
Bakari Malima ‘Jembe Ulaya’- EPISODE 5
*Atua mahakamani, Yanga wamuokoa asipande karandinga
*Akubali kusaini Jangwani bila kuuliza hata mshahara wake
*Akubali kusaini Jangwani bila kuuliza hata mshahara wake
Na Saleh Ally
WIKI ILIYOPITA, Malima alikuwa anawasili katika mahakama ya Kisutu akiwa mshitakiwa wa madawa ya kulevya. Kwa kuwa taarifa kuhusiana na suala hilo zilikuwa zimeripotiwa kwenye vyombo vya habari, watu walikuwa wengi sana, hali iliyomfanya awe mwoga. Nini kitafuatia? Endelea.
TULITEREMKA pale mahakamani huku idadi kubwa ya watu ikiwa inatusubiri, niliwaona baadhi ya watu niliokuwa nawajua wakiwemo mashabiki wa Yanga. Wengi waliniangalia kwa jicho la huruma.
Suala hilo kwa kiasi kikubwa lilinichanganya sana, niliona kama ni mtu ninayeonewa lakini ilikuwa vigumu kuwaeleza watu kilichokuwa kinaendelea ili wanielewe.
Ukichana na hivyo, nisingeweza kupata nafasi ya kuwaeleza namna mambo yangu yalivyokwenda vibaya. Nilichofanya ni kuangalia chini ili kupunguza uchungu kwa kuwa nilihisi huenda ningemwaga machozi.
Baadhi ya watu wa Yanga walikuwa pale wakipiga kelele kunipa moyo kuwa nisijali kwani kila kitu kitaisha. Walinipa moyo kiasi cha kunifanya niamini kweli Yanga ni nyumbani kwangu, hilo ninaliamini hadi leo.
Tuliingia mahakamani na tukaanza kusomewa mashitaka, hatukutakiwa kuzungumza lolote na baada ya hapo tukaombewa dhamana. Lakini tukaelezwa tusingeruhusiwa kupewa dhamana kutokana na uzito wa jambo lenyewe.
Hali hiyo ilinichanganya zaidi, niliona mambo yanazidi kuwa mabaya. Nilikanganyikiwa hasa baada ya kukosa hata nafasi ya kuwaona ndugu zangu. Nikajua ndiyo mwisho wangu.
Yule dada aliendelea kulia, hali hiyo ilinitia huruma sana kwa kuwa niliona kama mimi ndiyo chanzo cha tatizo. Lakini sikuwa na sababu ya kujilaumu maana sikujua lolote kuhusiana na litakalofuatia na wala sikuwa na nia mbaya kwake.
Wakati tukiwa tunajiandaa kupanda karandinga kwenda Segerea, tuliijiwa na kuambiwa dhamana ilikuwa imepatikana. Sikuamini, pia sikujua nani aliyetusaidia kiasi hicho.
Baada ya kutoka, nikagundua walioniwekea dhamana mimi na yule dada ni viongozi wa Yanga ambao tayari walishaanza kushughulikia suala la wanasheria kwa ajili ya kutusaidia kuendesha kesi yetu kitaalam zaidi.
Nilifanikiwa kutoka, ingawa kwa dhamana angalau niliona kama nilikuwa huru kwa kiasi fulani maana siku hiyo ningelala nyumbani. Kikubwa nilitakiwa kukutana na viongozi wa Yanga kujadili kuhusiana na suala hilo.
Hakika sikuwa na ubishi kwa sababu ya mambo mawili makubwa, moja Yanga ipo kwenye damu yangu na hupaswi kuuliza hata chembe. Pili, nilikuwa kwenye matatizo ambayo yananifanya niwe msikivu kupindukia.
Nilipokutana na viongozi wa Yanga, walinieleza namna ninavyoweza kusalimika, kwamba ni kuacha sheria ifuate mkondo wake. Lakini niwe mkweli kwa wanasheria watakaoniwekea.
Wakanipa sharti moja kuwa wao watanipigania hadi mwisho lakini nilitakiwa kufanya kitu kimoja, kuachana kabisa na mambo ya Afrika Kusini, niisahau timu yangu ya Vaal na kusaini Jangwani.
Wakati huo Yanga ilikuwa imefanikiwa kuvuka na kuingia kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, hivyo ilihitaji mtu ambaye ni imara kwa ajili ya sehemu ya ulinzi wa kati. Jembe Ulaya likawa chaguo lao.
Sikuwa na sababu ya kubisha, nilikubali haraka sana na nikawaahidi nitafanya mawasiliano na Afrika Kusini na kuwaeleza hali halisi ilivyo ili wasinione ni mbabaishaji.
Unajua wakati ule tumekwenda na Nonda, yeye akasajiliwa na mimi nikakosa kibali, nilikuwa ninawasiliana na mmiliki wa timu hivyo sikupenda kumuangusha maana alifanya juhudi na kunisajili.
Nikakubali kusaini Yanga kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa, kutokana na namna mambo yangu yalivyokuwa mabaya, sikuthubutu kuomba hata senti moja wala kuulizia mshahara wangu utakuwa ni kiasi gani.
Siku ya kusaini, nilizirukia karatasi fasta, nikasaini kwa ajili ya kuichezea Yanga katika michuano hiyo mikubwa huku nikiendelea kupambana na sakata langu ambalo liliendelea kusikika kila sehemu.
Wakati nilipoanza mazoezi Yanga, kila mmoja alitaka kuniona. Mashabiki walijitokeza kwa wingi kutaka kuniona na walikuwa wakinishangaa sana, lakini nilijikausha na kuendelea na shughuli zangu. Nilifanya mazoezi kwa nguvu sana.
Wakati yote yanaendelea, nilijiuliza mara kadhaa ninavyoweza kuzungumza na Wasauz na kuwaeleza kuwa sitarudi kwa kuwa nilishikwa na madawa ya kulevya. Ilinichanganya sana lakini nikaamua kupiga na kuzungumza nao.
MALIMA ameamua kuzungumza na timu yake kuhusiana na kilichomtokea. Je, viongozi wa timu hiyo watamuelewa? Watachukua uamuzi gani wakati yeye tayari ameshasaini kuichezea Yanga huku akiwa na mkataba nao? ITAENDELEA.....
MARADONA; MIMI NI MTU NILIYEKUFA KWA DAKIKA NNE,SASA NAJUA
MAISHA NI NINI
Umaarufu wake katika soka ulianzia katika timu ya Argentina Juniors na taratibu baada ya hapo alizichezea timu za Boca Junior,FC BarcelonaNapoli,Sevilla na Newll's Boys .Amewahi kutwaa tuzo mbalimbali katika maisha yake ya soka na mwaka 2000 alipewa tuzo ya mwanasoka bora wa Karne sambamba na Pele wa Brazili heshima waliyopewa na Fifa.Msomaji wa number10 unajua namna Diego Maradona alivyoishi maisha yakr ya utotoni? Vipi kuhusu uwezo wa familia yake? msikilize Diego mwenyewe katika maala hii ya maswali na majibu.
Swali: Ilikuwaje wakati unajifunza soka?
Maradona; Unajua nilijifunza soka nyuma ya nyumba yetu,kuikuwa na uwanja naotumiwa na timu moja ya daraja la nne,niicheza pale kila siku wakati watoto wengine walipokwenda makwao mimi niliendelea kucheza kwa saa mbili zaid giza likiwa tayari limeshaingia.Nilikuwa sioni kitu gizani ,nilikuwa napiga tu mpira nilichokuwa nazingatia ni miti miwili (magoli).Miaka 10 baadae niliposaini mkataba wangu wa kwanza na Argentina Juniors ndipo nilipobaini uamuzi ule wa kucheza gizani ulikuwa sahihi.
Swali: Wewe ulizaliwa Favel Fiorito,eneo linalosifika kwa umasikini katika jiji la Buenos Aires nini hasa ulichokuwa ukifikiria wakati huo,kwa sababu hujasahau watu wa kule na bado unaendelea kuwa nao karibu?
Maradona; Watu masikini hawawezi kamwe kukuahau au kukulaghai,wengi wao ni marafiki zangu na mmoja wao ni kocha wangu,Coppola,huyu alikuwa akiniibia fedha zangu,watu wa Fiorito wapo katika hali ya umasikini.Leo hii kunaweza kuwa na mambo yanayotoa picha ya maendeleo lakini umasikini bado ni ule ule tangu wakati nikiishi pale,lakini wanasiasa na watu walio karibu na serikali wameendelea kuwa matajiri zaidi na zaidi.Niliwahi kuwa na nafasi ya kuwa kama wao lakini nilikataa kwa sababu ningewaibia masikini,kuna wakati nilizungumza na watu wa Argentina waliojiingiza katika maisha ya sisa na niliwaambia kila kitu ambacho hawakutaka kukisikia.
Swali: Katika maisha hayo ya umasikini,unazungumziaje namna baba yako alivyokuwa akiangaikia familia?
Maradona;Nakumbuka hali ilivyokuwa mara ya baba kurudi kutoka kazini,hakuweza kuwa na chakula cha kutulisha watoto wote sisi nane.Watu walioshiba hawawezi kulijua hilo kamwe,hususani wale ambao hawakuwahi kuwa na njaa,dada yangu alilazimika kula chakula pungufu ili tu chakula kibaki kwa ajili yangu wakati wa jioni kwa mazingira kama hayo unalazimika kuwa na huruma na mwenye kujali wasio na chakula.Historia yangu ya utotoni kamwe siwezi kuisahau hivi hivi,Mama yangu alilazimika kudanganya anaumwa tumbo ili tu aweze kupata chakula kwa ajili ya watoto wake na wakati wote alikuwa akiangalia kwenye mabakuli kuhakikisha kama kuna chakula kwa watu wote.Huo ndiyo umasikini,mama yako analazimika kudanganya,mtu unaweza kuuita uongo wa kisayansi,lakini hiyo ndiyo hali halisi ya maisha ilivyokuwa,nakwambia ukweli.
Swali: Huo ni umasikini kama unavyosema lakini kuna watu wanasahau mapema hali hiyo,wewe vipi unaendelea kuwa na fikra za maisha ya utotoni?
Maradona; Nisingeweza kusahau,sisahau umasikini ni wazamani kuliko utajiri,baba yangu alikuwa akifanya kazi Kvantaca ( eneo la sokoni) na wakati wote alikuwa akibeba mifuko mizito hata wakati ambao umri wake ulikuwa mkubwa.Baada ya kurudi nyumbani Mama alikuwa akimuwekea bonge la barafu shingoni ili kupunguza maumivu na sisi watoto wake wakati huo tulikuwa pembeni,huo ulikuwa kama utamaduni ambao hauwezi kuondoka katika fikra zangu
Swali: Tuzungumzie mambo yaliyozoeleka kwa watu masikini nini hasa unachokumbuka zaidi ukiwa mtoto?
Maradona; Heshima,lakini pia hatukuwa na vitu kama sherehe za kuzaliwa,hatukuwa na fedha kwa mambo hayo,marafiki familia na binamu walikuwa wakikubusu na hiyo ilikuwa zawadi kubwa tu.Hali ni tofauti kwa wale ambao ni matajiri,sina shaka kwamba kuna watu wanaofanya makubaliano na wanasiasa na wanasiasa wanatumia pale wanapohitaji kufanya mambo hayo.Kama wewe hukubali katika utaratibu huo unaonekana kichaa,ndiyo mimi kichaa ni bora niwe kichaa kuliko kukubali nitoe kitu ambacho walitakiwa kunihudumia mimi.Unajua mimi ni kama mtu aliyekufa kwa dakika nne na sasa najua maisha ni nini.
Swali: Kuna walijituma kupunguza umasikini mfano ni mwanamuziki,Bono amezunguka dunia nzima kuwashawishi marais wa nchi tajiri kupunguza madeni kwa nchi masikini na ameweza hata kula chakula cha mchana na aliyekuwa Rais wa Marekani,George W Bush
Maradona; Najua jambo moja ambalo sitoweza kulifanya kamwe ni kupata ujasiri wa kula chakula na Bush,sitaona nimefanya jambo jema kwa kula chakula na muuaji wa halaiki.
Swali: Nini hasa unadhani kifanyike kuleta mabadiliko?
Maradona; Nini cha kufanya?Ni vigumu kubadili mambo,lakini muhimu tuyazungumze matatizo kwanza,bahati mbaya Papa (baba mtakatifu) hataki kuzungumzia matatizo na hata anapofanya hivyo anachofikiria ni kitu kimoja,namna ya kuitunza Vatican kama ilivyo kwa Wamarekani.Vatican ni tajiri sana,dola yao ina ngvu.Papa John Paul II hakuwahi kulifahamu kwa undani kuhusu Afrka,hakwenda pale kubusu ardhi na kuwapa chakula watoto masikini na pia hakuwahi kuijua Argentina.Lakin i ni yeye anayechukua dola million 150 inayotokana na matangazo ya kondomu,asasi inatoa fedha hizo kwa ajili ya kampeni ya matangazo ya biahara,lakini yeye Papa hakuwahi kujua lolote kuhusu kondomu,alikuwa anachukua tu fedha.Leo hii hakuna anayezungumza namna Papa alivyoitupa Afrika na watu masikini wameongezeka tangu kuangushwa kwa ukuta wa Berlin.
Swali: Wewe ni rafiki mkubwa wa rais wab Cuba Fidel Castro,mmekutana vipi na mtu huyu?
Maradona; Mwaka 1987 nilipewa tuzo mbili moja na Cuba nyingine na Marekani,niliwaambia Wamarekani wakae na tuzo yao na moja kwa moja nikaenda Cuba.Nilikutana na Fidel na tukazungumza kwa saa tano kuhusu Che Guevara (mwanamapinduzi wa zamani wa Argentina) .Nikweli nilisoma siku nyingi habar za mapinduzi,busara za Che na Fidel na nikajikuta navutiwa na Fidel na kwa mtazamo wangu yeye ni sawa na Simba anayepigania eneo lake,ni mwanasiasa pekee ambaye hana mtazamo wa kuwaibia masikini.
Swali: Umewaji kusema vita kubwa uliyowahi kupamana nayo ni kuachana na matumizi ya madawa?
Maradona; Ndiyo,ni vita kubwa,lakini ilibidi nipambane nayo kwa bidii na niliamini kuwa ilikuwa vita ngumu,ni kama uko katika mechi ambayo umeshindwa na unataka kushinda kwa namna yoyote ile lakini hakuna msaada wa kupata ushindi nje ya kutimiza majukumu yako.
Swali: Wakati ukichezea Napoli mwaka 1991 ulifungiwa kwa kosa la kutumia dawa za kuongeza nguvu,lakini baadaye ulisema kwamba kufungiwa kwako ni kulipiza kisasi baada ya Argentina kuitoa Italia katika kombe la Dunia mwaka 1990.
Maradona; Naamini hivyo,naamini wale Mafia walikuwa na fedha nyingi sana na walikuwa na hasira na mimi.
Swali: Ilikuwaje hadi ukafungiwa kucheza soka?
Maradona; Walikuta Cocaine kidogo na kunifungia kwa muda wa zaidi ya mwaka mmoja kucheza soka.Hiyo yote naamini ilikuwa sababu ya kunitoa nje ya soka kwa maisha yangu ya soka,walidhani wagenimaliza na kuniacha nimekufa mtaani.
Swali: Uliwaambia nini wachezaji wenzako kabla ya mechi yako ya mwisho ukiwa kama mchezaji mwaka 1997,nasikia wengi walilia!!
Maradona; Ndiyo,wote tulilia nilizungumza na mchezaji mmoja mmoja niliwaaga katika soka na nilifahamu kwamba sitovaa tena jezi nikiwa mchezaji.
EXCLUSIVE: IDDI KIPINGU KUPAMBANA NA MANJI KUWANIA UENYEKITI YANGA
Taarifa zisizo rasmi na za kutoka ndani kabisa ya kamati ya uchaguzi wa Yanga, zinasema aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la michezo nchini (BMT) Kanali Iddi Kipingu anatarajia kuchukua fomu ya kugombea uenyekiti wa klabu ya Yanga muda wowote kutoka sasa.
Kipingu ambaye ni mdau mkubwa michezo nchini, akiwa ni mmoja ya watu waliochangia upatikanaji wa vipaji vya wachezaji wengi kama Juma Kaseja, Boniface Pawasa na wengine wengi wakati akiwa mkuu wa wa shule ya Makongo, anatarajiwa kuchukua fomu ndani ya kipindi cha masaa 72 kutoka kutoka sasa.
Kwa maana hiyo sasa Kipingu atakuwa akichuana na mfanyabiashara maarufu ambaye ameshaidhamini Yanga Yusuph Manji ambaye nae tayari ameshachukua fomu rasmi ya kugombea ubosi wa klabu bingwa ya afrika mashariki na kati.
Kipingu ambaye ni mdau mkubwa michezo nchini, akiwa ni mmoja ya watu waliochangia upatikanaji wa vipaji vya wachezaji wengi kama Juma Kaseja, Boniface Pawasa na wengine wengi wakati akiwa mkuu wa wa shule ya Makongo, anatarajiwa kuchukua fomu ndani ya kipindi cha masaa 72 kutoka kutoka sasa.
Kwa maana hiyo sasa Kipingu atakuwa akichuana na mfanyabiashara maarufu ambaye ameshaidhamini Yanga Yusuph Manji ambaye nae tayari ameshachukua fomu rasmi ya kugombea ubosi wa klabu bingwa ya afrika mashariki na kati.
Tuesday, June 5, 2012
EURO 2012: KATIKA WACHEZAJI 368 KWENYE EURO. UNAMJUA NANI ANA UMRI MDOGO ZAIDI, MREFU, NA YUPI ANATISHA ZAIDI KUCHEKA NYAVU?
Vikosi vya UEFA EURO 2012 vimeshatajwa, lakini nini unajua kuhusu wachezaji 368 watakaokuwepo kwenye Euro? Nani mrefu? Nani mdogo zaidi? shaffihdauda.com inakupa majibu yote haya.
UREFU
Ujerumani wanaweza kuwa hatari zaidi kwenye mipira ya juu . . . . . . . isipokuwa labda watakapocheza na Croatia. Timu zote mbili zina wastani mzuri wa wachezaji warefu wa sentimita 185, wakati huo mchezaji mrefu zaidi akiwa ni kipa wa Sweden Andreas Isaksson mwenye urefu wa sentimita 199.
MAGOLI
Uholanzi ndio timu iliyofunga mabao mengi zaidi kwenye kufuzu, mabao 37, wakati Ugiriki wakiwa wamefunga mabao 14, huku sita kati ya hayo yakiwa yamefungwa na mabeki.
Klaas Jan Huntelaar, ndio mfungaji mwenye njaa zaidi akiwa amefunga mabao 12, huku Miroslave Klose akiwa wa pili kwa kufunga mabao 9.
UMRI
Italy, Russia, Jamhuri ya Ireland na Sweden ndio watakuwa na wachezaji wakongwe zaidi kwenye michuano hii, wakiwa na wastani wa umri wa miaka 28, huku Ujerumani wakiwa ndio timu yenye wachezaji wadogo zaidi kwenye michuano.
Akiwa na miaka 37, golikipa wa Ugiriki Kostas Chalkias ndio mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi, huku beki wa Uholanzi Jetro Willems akiwa ndio mdogo zaidi akiwa na miaka 18 na ikiwa atapata nafasi ya kucheza atakuwa ndio mchezaji mdogo zaidi kuwahi kucheza kwenye michuano hii.
UREFU
Ujerumani wanaweza kuwa hatari zaidi kwenye mipira ya juu . . . . . . . isipokuwa labda watakapocheza na Croatia. Timu zote mbili zina wastani mzuri wa wachezaji warefu wa sentimita 185, wakati huo mchezaji mrefu zaidi akiwa ni kipa wa Sweden Andreas Isaksson mwenye urefu wa sentimita 199.
MAGOLI
Uholanzi ndio timu iliyofunga mabao mengi zaidi kwenye kufuzu, mabao 37, wakati Ugiriki wakiwa wamefunga mabao 14, huku sita kati ya hayo yakiwa yamefungwa na mabeki.
Klaas Jan Huntelaar, ndio mfungaji mwenye njaa zaidi akiwa amefunga mabao 12, huku Miroslave Klose akiwa wa pili kwa kufunga mabao 9.
UMRI
Italy, Russia, Jamhuri ya Ireland na Sweden ndio watakuwa na wachezaji wakongwe zaidi kwenye michuano hii, wakiwa na wastani wa umri wa miaka 28, huku Ujerumani wakiwa ndio timu yenye wachezaji wadogo zaidi kwenye michuano.
Akiwa na miaka 37, golikipa wa Ugiriki Kostas Chalkias ndio mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi, huku beki wa Uholanzi Jetro Willems akiwa ndio mdogo zaidi akiwa na miaka 18 na ikiwa atapata nafasi ya kucheza atakuwa ndio mchezaji mdogo zaidi kuwahi kucheza kwenye michuano hii.
EURO 2012: UZOEFU NI HAZINA MUHIMU: WAJUE WACHEZAJI 12 WALIOCHEZA MECHI NYINGI ZAIDI WALIOPO KWENYE EURO 2012
Uzoefu mara nyingi ni muhimu sana katika michuano mikubwa na UEFA EURO 2012 kutakuwepo na wachezaji wasiopungua 12 ambao wameshacheza mechi zaidi ya 100 - huku kukiwa kuna wengine wakiwa wanakaribia kufikia idadi hiyo ya mechi.
Wakati kukiwa na mengi ya kuzungumza kuhusu vipaji vya wachezaji wachanga, uzoefu unaweza ukawa na umuhimu katika michuano mikubwa. Wachezaji ambao wameshajifunza vitu vingi na kukabiliana na presha ya mechi kubwa kwa mara nyingi zaidi wana uthamani mkubwa kwa timu yoyote, na watakuwepo wachezaji namna hiyo wengi wakiuleta uzoefu wao kwenye michuano ya Euro 2012.
Wanaume 12 watasafiri kwenda Poland na Ukraine huku wakiwa na uzoefu wa kucheza mechi zaidi ya 100, in fact, huku Spain's goalkeeper Iker Casillas akiwa anaongoza listi hiyo kwa kucheza mechi 130 akiwa na mabingwa wa ulaya na dunia. Kipa wa Real Madrid alicheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Sweden miaka 12 iliyopita na akaweka rekodi mpya Jumatano iliyopita aliposherehekea ushindi wake wa 95 kwenye mechi za kimataifa wakiwafunga 4-1 Korea ya kusini. Akiwa na miaka 31 'Saint Iker' mtakatifu Iker sasa atakuwa kiomba kuisadia Spain kushinda kombe la tatu kubwa mfululizo - huku mchezaji mwenzake Xavi Hernandez ambaye tayari amecheza mechi 108 tangu acheze mchezo wake wa kwanza miaka 12 iliyopita.
Sweden, Jamhuri ya Ireland na Ukraine nazo zimetoa wachezaji waliocheza mechi zaidi ya 100 katika vikosi vyao, Anders Svensson akiwa anamfuatia Casillas kwa kuichezea Sweden mechi 126, akaifuatiwa na mchezaji mwenzie wa timu taifa Olof Melberg akiwa amecheza mechi 113. Shay Given Given wa Ireland akiwa amecheza mechi 121, Robbie Keane amecheza mechi 116, huku wachezaji wawili wa Ukraine Anatoliy Tymoshchuk akicheza mechi 112, na Andrey Shevchenko 107.
Listi ya wachezaji wazoefu zaidi kwenye UEFA EURO 2012:
Iker Casillas (Spain, 130 caps)
Anders Svensson (Sweden, 126)
Shay Given (Republic of Ireland, 121)
Giorgos Karagounis (Greece, 117)
Miroslav Klose (Germany, 116)
Robbie Keane (Ireland, 116)
Anatoliy Tymoshchuk (Ukraine, 116)
Dennis Rommedahl (Denmark, 116)
Gianluigi Buffon (Italy, 114)
Olof Mellberg (Sweden, 113)
Xavi Hernández (Spain, 108)
Andriy Shevchenko (Ukraine, 107)
Lukas Podolski (Germany, 97)
Damien Duff (Ireland, 96)
Rafael van der Vaart (Netherlands, 96)
Xabi Alonso (Spain, 95)
Josip Šimunić (Croatia, 95)
Ashley Cole (England, 94).
Wakati kukiwa na mengi ya kuzungumza kuhusu vipaji vya wachezaji wachanga, uzoefu unaweza ukawa na umuhimu katika michuano mikubwa. Wachezaji ambao wameshajifunza vitu vingi na kukabiliana na presha ya mechi kubwa kwa mara nyingi zaidi wana uthamani mkubwa kwa timu yoyote, na watakuwepo wachezaji namna hiyo wengi wakiuleta uzoefu wao kwenye michuano ya Euro 2012.
Wanaume 12 watasafiri kwenda Poland na Ukraine huku wakiwa na uzoefu wa kucheza mechi zaidi ya 100, in fact, huku Spain's goalkeeper Iker Casillas akiwa anaongoza listi hiyo kwa kucheza mechi 130 akiwa na mabingwa wa ulaya na dunia. Kipa wa Real Madrid alicheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Sweden miaka 12 iliyopita na akaweka rekodi mpya Jumatano iliyopita aliposherehekea ushindi wake wa 95 kwenye mechi za kimataifa wakiwafunga 4-1 Korea ya kusini. Akiwa na miaka 31 'Saint Iker' mtakatifu Iker sasa atakuwa kiomba kuisadia Spain kushinda kombe la tatu kubwa mfululizo - huku mchezaji mwenzake Xavi Hernandez ambaye tayari amecheza mechi 108 tangu acheze mchezo wake wa kwanza miaka 12 iliyopita.
Sweden, Jamhuri ya Ireland na Ukraine nazo zimetoa wachezaji waliocheza mechi zaidi ya 100 katika vikosi vyao, Anders Svensson akiwa anamfuatia Casillas kwa kuichezea Sweden mechi 126, akaifuatiwa na mchezaji mwenzie wa timu taifa Olof Melberg akiwa amecheza mechi 113. Shay Given Given wa Ireland akiwa amecheza mechi 121, Robbie Keane amecheza mechi 116, huku wachezaji wawili wa Ukraine Anatoliy Tymoshchuk akicheza mechi 112, na Andrey Shevchenko 107.
Listi ya wachezaji wazoefu zaidi kwenye UEFA EURO 2012:
Iker Casillas (Spain, 130 caps)
Anders Svensson (Sweden, 126)
Shay Given (Republic of Ireland, 121)
Giorgos Karagounis (Greece, 117)
Miroslav Klose (Germany, 116)
Robbie Keane (Ireland, 116)
Anatoliy Tymoshchuk (Ukraine, 116)
Dennis Rommedahl (Denmark, 116)
Gianluigi Buffon (Italy, 114)
Olof Mellberg (Sweden, 113)
Xavi Hernández (Spain, 108)
Andriy Shevchenko (Ukraine, 107)
Lukas Podolski (Germany, 97)
Damien Duff (Ireland, 96)
Rafael van der Vaart (Netherlands, 96)
Xabi Alonso (Spain, 95)
Josip Šimunić (Croatia, 95)
Ashley Cole (England, 94).
EURO 2012: URENO - CRISTIANO RONALDO NDIO FUNGUO YA USHINDI
Michuano ya ulaya bila uwepo wa mchezaji bora wa bara hilo ni jambo ambalo lilianza kuonekana linawezekana baada ya Ureno kutoa suluhu 4-4 na Cyprus kwenye mchezo wao wa kwanza kufuzu, kabla ya kufungwa 1-0 na Norway. Baadae Shirikisho la soka la Ureno likamtimua kazi Carlos Queiroz na kumpa ajira Paulo Bento.
Ingawa ndio kocha mwenye umri mdogo zaidi kwenye Euro akiwa na miaka 42, Bento ameonyesha kwamba hana uoga katika kufanya maamuzi makubwa: ameshamtimua kwenye timu ya taifa Ricardo Carvalho na Jose Bosingwa, huku akipunguza presha kwa Cristiano Ronaldo kwa kumfanya acheze huru kama mshambuliaji kivuli. Jambo hilo liliisaidia Ureno sana kwenye mchezo wa play off dhidi ya Bosnia and Herzegovina.
Bento na Ronaldo walikuwa ni wachezaji wa timu moja pale Sporting Lisbon, na sapoti kubwa aliyoionyesha Ronaldo kwa Bento wakati wa sakata la Carvalho, limeukomaza uhusiano wa wawili hao.
Bento amekuwa na mahusiano mazuri na sana na wachezaji kuliko ilivyokuwa kwa Carlos Queiroz, na ushindi wa 4-0 dhidi ya Spain mwezi November 2010 uliongeza kujiamini ndani ya kikosi. Hilo linadhihirishwa na mfumo wa ongezeko la bonasi wachezaji wa Ureno walivyokubaliana na shirikisho: hawatopata kiasi chochote cha fedha kama watashindwa kuvuka kwenye hatua ya makundi, na kiasi cha kwanza watakipata ikiwa tu watafanikiwa kufika hatua ya robo fainali.
Huku wakiwa na timu mojawapo inayopewa nafasi ya juu kubeba taji Ujerumani, wakipewa nafasi ya kuongoza kundi lao, labda itabidi Ureno wawafunge Denmark na Uholanzi kuweza kufika kwenye hatua ya robo fainali. Ikiwa Ronaldo atacheza kwa mafanikio japo nnusu kama ilivyo kwa Real Madrid basi lolote linawezekana.
WACHEZAJI MUHIMU
Cristiano Ronaldo
Hakuna ubishi wala swali kama Ronaldo ni mchezaji bora wa bara la ulaya, lakini siku zote imekuwa ni vigumu kwake kuileta form yake ya kwenye klabu katika timu ya taifa. Wakati Bento alipopewa ukocha alimrudisha kucheza nafasi yake kutoka pembeni, na kumuondolea mzigo wa kuwa kufunga magoli. Lakini ukiangalia rekodi yake ya kutupia nyavuni katika msimu na Real Madrid, michuano hii ndio nafasi nyingine ya Ronaldo kuweza kuirudisha tuzo ya mchezaji bora wa dunia inayomilikiwa na Lionel Messi.
Luis Nani
Atakuwa na jukumu muhimu katika kikosi cha Ureno: winga mwenye kila sifa ambaye sifa yake kubwa ni pale anapokutana na vita ya one against one na mabeki huku akiweza kufunga kwa mashuti ya mbali tena akipiga kwa miguu yote miwili. Hii itakuwa ni advantage kwake kwamba attention yote itakuwa kwa Ronaldo jambo litakalomfanya acheze bila presha. Baada ya kukosa kombe la dunia kutokana na majeruhi wakati wa mazoezi, Nani sasa yupo na hamu ya kuonyesha kwamba yeye ni mchezaji bora pia.
Pepe
Katika hali ya kutokuwepo kwa Carvalho, safu ya ulinzi ya Ureno inaonekana itakuwa na taabu kidogo, hasa ukizingatia Pepe na patna wake Bruno Alves wamekuwa wakijikuta wakipata kadi za mara kwa mara hata pale ambapo wanaweza kuziepuka. Pepe ndio kiongozi mpya wa safu ya ulinzi, na form yake itakuwa muhimu katika kuhakikisha nyavu za Ureno haziguswi na wapinzani wao wenye washambuliaji hatari.
MASWALI
Je Bento anaweza akaleta mshtuko?
Kocha huyu atayari anajua watu gani wa kuwapanga kwenye safu ya ulinzi na ushambuliaji, lakini nafasi pekee ambayo inamtia mawazo ni kiungo cha ulinzi. Joao Moutinho na Raul Meireles tayari wana nafasi kubwa ya kuanza, lakini Bento na uamuzi wa kufanya kwa kiungo anayecheza chini zaidi. Miguel Veloso amecheza kidogo sana akiwa na Genoa msimu huu huku kiungo aliye kwenye form wa Braga Custodio, hajawahi kuichezea timu ya taifa ingawa yupo kwenye kikosi kwa sasa. Kiungo halisi mkabaji atakayebaki nyuma na kuwaruhusu Moutinho na Meireles wacheze kwa mtindo wa box to box.
Lini Nelson Oliveira atapata nafasi?
Mshambuliaji wa Benfica anaweza akawa na miaka 20 na kucheza mechi moja tu, lakini Oliveira ndio jina kwenye mdomo wa kila mtu. Alikuwa ndio mchezaji wa kwanza kupewa nafasi ya kuzungumza kwenye mkutano wa waandishi wa habari mara tu baada ya timu kuingia kambini, na kama washambuliaji Helder Postiga na Hugo Almeida watashindwa kuonyesha uwezo, Oliveira atakuwa ndio mchezaji washabiki watakayetaka kumuona akichukua nafasi ya kuongoza mashambulizi. Ingawa kwa sasa ataanzia benchi.
Je Ronaldo atamfunika Eusebio?
Ikiwa Ureno watashinda taji la Euro 2012, au kukaribia kufanya hivyo, Cristiano Ronaldo anaweza akaondoa ukungu uliopo kuhusu nani hasa ni mchezaji bora wa muda wote wa Ureno. Kwa sasa, Eusebio bado anaaminika na wengi kama ndio mchezaji bora wa historia ya soka la Ureno, lakini Ronaldo anakaribia tena sana. Ikiwa mchezaji huyu wa Real Madrid ataisadia Ureno kushinda taji la ulaya (ambayo haijawahi kushinda kombe la ulaya wa World Cup) ubishi utakuwa umeisha.
MBINU
Bento anapenda kutumia mfumo wa 4-3-3, lakini timu yake inashambulia zaidi kuliko ilivyokuwa chini ya Queiroz, huku beki wa kushoto Fabio Coentrao akipanda mbele na kushambulia kwa kasi akimruhusu Ronaldo kuingia ndani zaidi. Moutinho na Meireles wakicheza kwa mtindo wa box mpaka box, huku Veloso au labda Custodio wakicheza kama kiungo mlinzi, hivyo kwa mchezo wa kwanza, atleast, Postiga atapata nafasi.
Ingawa ndio kocha mwenye umri mdogo zaidi kwenye Euro akiwa na miaka 42, Bento ameonyesha kwamba hana uoga katika kufanya maamuzi makubwa: ameshamtimua kwenye timu ya taifa Ricardo Carvalho na Jose Bosingwa, huku akipunguza presha kwa Cristiano Ronaldo kwa kumfanya acheze huru kama mshambuliaji kivuli. Jambo hilo liliisaidia Ureno sana kwenye mchezo wa play off dhidi ya Bosnia and Herzegovina.
Bento na Ronaldo walikuwa ni wachezaji wa timu moja pale Sporting Lisbon, na sapoti kubwa aliyoionyesha Ronaldo kwa Bento wakati wa sakata la Carvalho, limeukomaza uhusiano wa wawili hao.
Bento amekuwa na mahusiano mazuri na sana na wachezaji kuliko ilivyokuwa kwa Carlos Queiroz, na ushindi wa 4-0 dhidi ya Spain mwezi November 2010 uliongeza kujiamini ndani ya kikosi. Hilo linadhihirishwa na mfumo wa ongezeko la bonasi wachezaji wa Ureno walivyokubaliana na shirikisho: hawatopata kiasi chochote cha fedha kama watashindwa kuvuka kwenye hatua ya makundi, na kiasi cha kwanza watakipata ikiwa tu watafanikiwa kufika hatua ya robo fainali.
Huku wakiwa na timu mojawapo inayopewa nafasi ya juu kubeba taji Ujerumani, wakipewa nafasi ya kuongoza kundi lao, labda itabidi Ureno wawafunge Denmark na Uholanzi kuweza kufika kwenye hatua ya robo fainali. Ikiwa Ronaldo atacheza kwa mafanikio japo nnusu kama ilivyo kwa Real Madrid basi lolote linawezekana.
WACHEZAJI MUHIMU
Cristiano Ronaldo
Hakuna ubishi wala swali kama Ronaldo ni mchezaji bora wa bara la ulaya, lakini siku zote imekuwa ni vigumu kwake kuileta form yake ya kwenye klabu katika timu ya taifa. Wakati Bento alipopewa ukocha alimrudisha kucheza nafasi yake kutoka pembeni, na kumuondolea mzigo wa kuwa kufunga magoli. Lakini ukiangalia rekodi yake ya kutupia nyavuni katika msimu na Real Madrid, michuano hii ndio nafasi nyingine ya Ronaldo kuweza kuirudisha tuzo ya mchezaji bora wa dunia inayomilikiwa na Lionel Messi.
Luis Nani
Atakuwa na jukumu muhimu katika kikosi cha Ureno: winga mwenye kila sifa ambaye sifa yake kubwa ni pale anapokutana na vita ya one against one na mabeki huku akiweza kufunga kwa mashuti ya mbali tena akipiga kwa miguu yote miwili. Hii itakuwa ni advantage kwake kwamba attention yote itakuwa kwa Ronaldo jambo litakalomfanya acheze bila presha. Baada ya kukosa kombe la dunia kutokana na majeruhi wakati wa mazoezi, Nani sasa yupo na hamu ya kuonyesha kwamba yeye ni mchezaji bora pia.
Pepe
Katika hali ya kutokuwepo kwa Carvalho, safu ya ulinzi ya Ureno inaonekana itakuwa na taabu kidogo, hasa ukizingatia Pepe na patna wake Bruno Alves wamekuwa wakijikuta wakipata kadi za mara kwa mara hata pale ambapo wanaweza kuziepuka. Pepe ndio kiongozi mpya wa safu ya ulinzi, na form yake itakuwa muhimu katika kuhakikisha nyavu za Ureno haziguswi na wapinzani wao wenye washambuliaji hatari.
MASWALI
Je Bento anaweza akaleta mshtuko?
Kocha huyu atayari anajua watu gani wa kuwapanga kwenye safu ya ulinzi na ushambuliaji, lakini nafasi pekee ambayo inamtia mawazo ni kiungo cha ulinzi. Joao Moutinho na Raul Meireles tayari wana nafasi kubwa ya kuanza, lakini Bento na uamuzi wa kufanya kwa kiungo anayecheza chini zaidi. Miguel Veloso amecheza kidogo sana akiwa na Genoa msimu huu huku kiungo aliye kwenye form wa Braga Custodio, hajawahi kuichezea timu ya taifa ingawa yupo kwenye kikosi kwa sasa. Kiungo halisi mkabaji atakayebaki nyuma na kuwaruhusu Moutinho na Meireles wacheze kwa mtindo wa box to box.
Lini Nelson Oliveira atapata nafasi?
Mshambuliaji wa Benfica anaweza akawa na miaka 20 na kucheza mechi moja tu, lakini Oliveira ndio jina kwenye mdomo wa kila mtu. Alikuwa ndio mchezaji wa kwanza kupewa nafasi ya kuzungumza kwenye mkutano wa waandishi wa habari mara tu baada ya timu kuingia kambini, na kama washambuliaji Helder Postiga na Hugo Almeida watashindwa kuonyesha uwezo, Oliveira atakuwa ndio mchezaji washabiki watakayetaka kumuona akichukua nafasi ya kuongoza mashambulizi. Ingawa kwa sasa ataanzia benchi.
Je Ronaldo atamfunika Eusebio?
Ikiwa Ureno watashinda taji la Euro 2012, au kukaribia kufanya hivyo, Cristiano Ronaldo anaweza akaondoa ukungu uliopo kuhusu nani hasa ni mchezaji bora wa muda wote wa Ureno. Kwa sasa, Eusebio bado anaaminika na wengi kama ndio mchezaji bora wa historia ya soka la Ureno, lakini Ronaldo anakaribia tena sana. Ikiwa mchezaji huyu wa Real Madrid ataisadia Ureno kushinda taji la ulaya (ambayo haijawahi kushinda kombe la ulaya wa World Cup) ubishi utakuwa umeisha.
MBINU
Bento anapenda kutumia mfumo wa 4-3-3, lakini timu yake inashambulia zaidi kuliko ilivyokuwa chini ya Queiroz, huku beki wa kushoto Fabio Coentrao akipanda mbele na kushambulia kwa kasi akimruhusu Ronaldo kuingia ndani zaidi. Moutinho na Meireles wakicheza kwa mtindo wa box mpaka box, huku Veloso au labda Custodio wakicheza kama kiungo mlinzi, hivyo kwa mchezo wa kwanza, atleast, Postiga atapata nafasi.
BREAKING NEWS: ALLY MAYAY NA AARON NYANDA WACHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA UONGOZI YANGA
Taarifa rasmi nilizozipata kutoka makao makuu ya klabu ya Yanga, ni kwamba wachezaji wawili wa zamani wa klabu hiyo Ally Mayay na Aaron Nyanda wameamua kuchukua fomu za kugombea ujumbe wa kamati ya utendaji katika uchaguzi unaokuja ndani timu hiyo.
DONE DEAL: MANCHESTER UNITED YATHIBITISHA KUMSAINI KAGAWA - VIMEBAKI VIPIMO NA KIBALI
Manchester United wamethibitisha kukamilisha usajili wa mchezaji bora wa ligi kuu ya Ujerumani Shinji Kagawa, aliyekuwa akiichezea Dortmund ambao ndio mabingwa wa Bundesliga.
Kiungo huyo mwenye miaka 23, atajiunga rasmi na United kwa ada ya £12million mwezi ujao baada ya kufaulu vipimo vya afya pamoja na kupata kibali cha kufanya kazi Uingereza.
Taarifa iliyotolewa na United kupitia website yao: "Tuna furaha ya kuwatangazia kwamba tumekubaliana kimsingi na Borrussi Dortmund na Shinji Kagawa kuhamia kwenye klabu yetu.
"Dili litakamilika baada ya mchezaji kufaulu vipimo vya afya na kupata kibali cha kufanya kazi UK.
"Vitu hivi tunategemea vitakamilika ndani ya mwezi ujao."
Mchezaji wa United Rio Ferdinand alifurahishwa sana usajili wa Kagawa na akaandika kwenye ukarasa wake wa Twitter: "Karibu Manchester United Shinji Kagawa. Muda wa kupata mafanikio ni sasa kaka.!"
Kiungo huyo mwenye miaka 23, atajiunga rasmi na United kwa ada ya £12million mwezi ujao baada ya kufaulu vipimo vya afya pamoja na kupata kibali cha kufanya kazi Uingereza.
Taarifa iliyotolewa na United kupitia website yao: "Tuna furaha ya kuwatangazia kwamba tumekubaliana kimsingi na Borrussi Dortmund na Shinji Kagawa kuhamia kwenye klabu yetu.
"Dili litakamilika baada ya mchezaji kufaulu vipimo vya afya na kupata kibali cha kufanya kazi UK.
"Vitu hivi tunategemea vitakamilika ndani ya mwezi ujao."
Mchezaji wa United Rio Ferdinand alifurahishwa sana usajili wa Kagawa na akaandika kwenye ukarasa wake wa Twitter: "Karibu Manchester United Shinji Kagawa. Muda wa kupata mafanikio ni sasa kaka.!"
Kili Taifa Stars yarejea kutoka Ivory Coast
· Poulsen asema nguvu zote sasa zimeelekezwa katika mechi ya Gambia
TIMU ya Taifa-Kilimanajro Taifa Stars jana imerejea nyumbani ikitokea Ivory Coast ambako ilicheza mechi yake ya kwanza ya kufuzu kucheza kombe la dunia ambapo ilishindwa na mwenyeji wake kwa magoli mawili bila.
Ndege iliyowabeba wachezaji 23 wakiongozwa na kocha Kim Poulsen, benchi la ufundi, viongozi mbalimbali wa TFF na waandishi wa habari ilitua katika Uwanja wa KImataifa wa Julius Nyerere saa moja na nusu asubuhi ikitokea Nairobi baada ya kuondoka Ivory Coast saa nne za usiku saa za frika Mashariki.
Wachezaji hao walipokewa na viongozi mbalimbali wa TFF akiwemo Katibu Mkuu Angetile Osiah.
Mara baada ya kuwasili Kocha Kim Poulsen alisema baada ya matokeo ya mechi yao na Ivory Coast, sasa hivi timu yake imeelekeza nguvu zote katika mchezo wa Gambia utakaochezwa Jumapili Jijini Dar es Salaam.
“Matokeo hayakuwa mazuri kwetu ila vijana walicheza vizuri na tunatumai tutafanya vizuri katika mechi ijao dhidi ya Gambia,” alisema..
Alipoulizwa kuhusu timu kuchelewa kurudi alisema wamekuwa wakifanya mazoezi nchini Ivory Coast kila siku tangu tmu iondoke Dar es salaam Alhamisi iliyopita.
Huku akiwashukuru wadhamini wapya wa Timu ya taifa, TBL kupitia bia yake ya Kilimanjaro Premium Lager, Poulsen alisema mapokezi nchini Ivory Coast yalikuwa mazuri na wachezaji walionesha nidhammu ya hali ya juu ndani na nje ya uwanja.
“Tulicheza vizuri lakini wenzetu wana uzoefu na wana kikosi kizuri kwa hivyo wanatuzidi lakini tunajitahidi ili tuweze kucheza vizuri zaidi kila tunapoingia uwanjani.
Naye nahodha wa Timu ya Kilimanjaro Taifa Stars, Juma Kaseja, alisema mechi yao dhidi ya The Elephants ilikuwa ngumu lakini wachezaji walijitahidi kucheza vizuri.
Alisema anaamini watapata matokeo mazuri katika mchezo dhidi ya Gambia utakaopigwa katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam siku ya Jumapili.
Hii ilikuwa ni mechi ya kwanza ya Taifa Stars ya mchujo wa kufuzu kucheza katika mashindano ya kimataifa tangu ipate mdhamini mpya-Kilimanjaro Premium Lager na pia tangu timu hii itangazwe na kocha Poulsen.
Tayari watanzania mbalimbali waishio ndani na nje ya Tanzania wametoa maoni yao kuhusiana na ttimu hii na kwa mujibu wa wengi, timu hii inaonesha matumaini makubwa.
Watu mbalimbali nchini Ivory Coast wakiwemo wachezaji nyota kama Didier Drogba, Solomon Kalou, Yaya Tourre na wengine walistaajabishwa sana na kiwango cha hali ya juu kilichoonesha na Taifa Stars.
TIMU ya Taifa-Kilimanajro Taifa Stars jana imerejea nyumbani ikitokea Ivory Coast ambako ilicheza mechi yake ya kwanza ya kufuzu kucheza kombe la dunia ambapo ilishindwa na mwenyeji wake kwa magoli mawili bila.
Ndege iliyowabeba wachezaji 23 wakiongozwa na kocha Kim Poulsen, benchi la ufundi, viongozi mbalimbali wa TFF na waandishi wa habari ilitua katika Uwanja wa KImataifa wa Julius Nyerere saa moja na nusu asubuhi ikitokea Nairobi baada ya kuondoka Ivory Coast saa nne za usiku saa za frika Mashariki.
Wachezaji hao walipokewa na viongozi mbalimbali wa TFF akiwemo Katibu Mkuu Angetile Osiah.
Mara baada ya kuwasili Kocha Kim Poulsen alisema baada ya matokeo ya mechi yao na Ivory Coast, sasa hivi timu yake imeelekeza nguvu zote katika mchezo wa Gambia utakaochezwa Jumapili Jijini Dar es Salaam.
“Matokeo hayakuwa mazuri kwetu ila vijana walicheza vizuri na tunatumai tutafanya vizuri katika mechi ijao dhidi ya Gambia,” alisema..
Alipoulizwa kuhusu timu kuchelewa kurudi alisema wamekuwa wakifanya mazoezi nchini Ivory Coast kila siku tangu tmu iondoke Dar es salaam Alhamisi iliyopita.
Huku akiwashukuru wadhamini wapya wa Timu ya taifa, TBL kupitia bia yake ya Kilimanjaro Premium Lager, Poulsen alisema mapokezi nchini Ivory Coast yalikuwa mazuri na wachezaji walionesha nidhammu ya hali ya juu ndani na nje ya uwanja.
“Tulicheza vizuri lakini wenzetu wana uzoefu na wana kikosi kizuri kwa hivyo wanatuzidi lakini tunajitahidi ili tuweze kucheza vizuri zaidi kila tunapoingia uwanjani.
Naye nahodha wa Timu ya Kilimanjaro Taifa Stars, Juma Kaseja, alisema mechi yao dhidi ya The Elephants ilikuwa ngumu lakini wachezaji walijitahidi kucheza vizuri.
Alisema anaamini watapata matokeo mazuri katika mchezo dhidi ya Gambia utakaopigwa katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam siku ya Jumapili.
Hii ilikuwa ni mechi ya kwanza ya Taifa Stars ya mchujo wa kufuzu kucheza katika mashindano ya kimataifa tangu ipate mdhamini mpya-Kilimanjaro Premium Lager na pia tangu timu hii itangazwe na kocha Poulsen.
Tayari watanzania mbalimbali waishio ndani na nje ya Tanzania wametoa maoni yao kuhusiana na ttimu hii na kwa mujibu wa wengi, timu hii inaonesha matumaini makubwa.
Watu mbalimbali nchini Ivory Coast wakiwemo wachezaji nyota kama Didier Drogba, Solomon Kalou, Yaya Tourre na wengine walistaajabishwa sana na kiwango cha hali ya juu kilichoonesha na Taifa Stars.
Subscribe to:
Posts (Atom)
_02_(t)%5B1%5D.jpg)
















