Kocha Jamhuri Kiwhelu akizungumza na EXCLUSIVELY na http://www.shaffihdauda.com/ amesema makocha Milovan Cirkovic wa Simba pamoja na Kim Poulsen wa timu ya Taifa ya vijana ndo makocha pekee wenye uwezo wa kufundisha soka miongoni mwa makocha wazungu waliofanikiwa kufanya kazi hapa nchini.
pamoja na kuwasifia makocha hao Jamhuri maarufu kwa jina la Julio hakusita kumpa sifa za kipekee kocha wa timu ya taifa ya vijana mdenish Kim Poulsen kuwa ndiye kocha bora mzungu miongoni mwa makocha wote wazungu waliowahi kufanya kazi hapa nchini.
Pia Julio ameliomba shirikisho la soka nchni kumtumia Kim Poulsen kama kocha mkuu katika timu ya taifa ya wakubwa ili kuweza kuiwezesha timu ya taifa kupata mafanikio kwa kuwa ni kocha ambaye anaipenda kazi na kuiheshimu na uwezo mkubwa wa kufundisha soka.
Search This Blog
Thursday, May 10, 2012
KUTOKA KUCHEZA PEKUPEKU MPAKA KUJA KUWA MWANASOKA TAJIRI DUNIANI: FAHAMU NJIA ALIZOPITIA YAYA TOURE KUFIKA HAPA ALIPO.
![]() |
| YAYA TOURE AKISUKUMA GOZI HUKU AKIWA PEKUPEKU NCHINI KWAO IVEORY COAST KATIKA KLABU YA ASEC MEMOSAC. |
Yaya Toure aliwasili Ubelgiji akiwa hana chochote bali kipaji chake. Hiyo ndio kumbukumbu waliyokuwa nayo juu ya Toure pale Beveren: hakuwa hata na pea za viatu vya kuchezea soka.
Nyingine ni kwamba hakuwa na tabia ya kuamka mapema asubuhi; alikuwa anakula kama farasi na kunywa kama samaki, soda ya fanta na sio pombe.
Yaya Toure alitua Beveren, mji mdogo uliopo magharibi mwa Antwerp, akiwa tu ndio anafikisha miaka 18, akiwa amelelewa kwa kuongea lugha ya kifaransa katika mitaa ya Abidjan, Ivory Coast. Alikuwa na pesa kidogo sana, pair moja ya viatu na nguo chache.
Lakini pale Flanders, wanasema hata akiwa mdogo, kijana ambaye ameshinda Champions league na Barcelona na ambaye msimu huu amekuwa moyo wa timu ya Manchester City alikuwa mtu ambaye anapenda kuwa yeye kitu ambacho kilimtofautisha na wenzake.
Leo hii Toure anaonekana na kung'ara - moja ya viungo bora kwenye soka, mwenye uzoefu na akiwa tayari kuiongoza Manchester City kushinda taji lake kwanza baada ya miaka 44 jumapili ijayo, ambayo itakuwa ndio siku yake ya kuzaliwa akitimiza miaka 29. Tangu zamani Yaya alionekana kuwa mtu ambaye atakuja kufanikiwa.
Nyingine ni kwamba hakuwa na tabia ya kuamka mapema asubuhi; alikuwa anakula kama farasi na kunywa kama samaki, soda ya fanta na sio pombe.
Yaya Toure alitua Beveren, mji mdogo uliopo magharibi mwa Antwerp, akiwa tu ndio anafikisha miaka 18, akiwa amelelewa kwa kuongea lugha ya kifaransa katika mitaa ya Abidjan, Ivory Coast. Alikuwa na pesa kidogo sana, pair moja ya viatu na nguo chache.
Lakini pale Flanders, wanasema hata akiwa mdogo, kijana ambaye ameshinda Champions league na Barcelona na ambaye msimu huu amekuwa moyo wa timu ya Manchester City alikuwa mtu ambaye anapenda kuwa yeye kitu ambacho kilimtofautisha na wenzake.
Leo hii Toure anaonekana na kung'ara - moja ya viungo bora kwenye soka, mwenye uzoefu na akiwa tayari kuiongoza Manchester City kushinda taji lake kwanza baada ya miaka 44 jumapili ijayo, ambayo itakuwa ndio siku yake ya kuzaliwa akitimiza miaka 29. Tangu zamani Yaya alionekana kuwa mtu ambaye atakuja kufanikiwa.
![]() |
| YAYA ALIYEZUNGUSHIWA KIDUARA ALIPOKUWA UBELGIJI PALE BEVEREN |
"Nilikuwa nawachukua kila siku, Yaya na rafiki zake wawili,' anasema Anour Bou-Sfia, ambaye alicheza na Toure pale Beveren. 'Yaya alikuwa na tabia fulanihivi - alikuwa anajua atakuja kufanikiwa na kuwa bora.
"Mahali walipoishi ndio ilikuwa njia yangu ya kwenda uwanjani na kulikuwa na siku nyingi tu ambazo ilibidi Yaya tuwe tunamuamsha kwenda mazoezini, lakini yeye alikuwa tofauti ukilinganisha na wengine - Yaya alikuwa na akili sana na aliyepevuka. Wengine wote walikuwa na mentallity za kijinga za vijana kutoak afrika ambao ghafla tu walijikuta wapo ulaya. Yaya hakuwa anapenda camera, magazeti, alikuwa na aibu sana. Alikuwa hapendi kutoka kama wenzake. Alikuwa muislamu kamili. Mimi ni mmoroco, ni muislam.
"Muda mwingine tukiwa uwanjani angeweza kufanya vitu ambavyo vilitushangaza wote. Nilicheza nae kwa misimu miwili na nusu lakini kwa muda wote huo nilikuwa bench. Hivyo nilikuwa namuangalia, niliwaleta rafiki zangu kuja tu kumuangalia alikuwa mchezaji mzuri sana.
"Angalia goli la kwanza alilowafunga Newcastle jumapili, alilifanya lionekane rahisi. Angalia nmna alivyofunga. Alishinda Champions league pale Barcelona akicheza pembeni ya Gerard Pique katika safu ya ulinzi. Alilifanya suala lile lionekane rahisi.
"Nafikiri alikuwa kama anaboa muda mwingine alipokuwa akiichezea Barcelona. Ilikuwa rahisi sana. Hata Beveren alikuwa hivyo - kule ufaransa wanamuita nonchalance.
"Yaya hakuwa mtu anayependa kujionyesha. Nilikuwa mtafsiri lugha wao, kuwapeleka supermarket, kuwapeleka kwenda kununua viatu kwa sababu hawakuwa na viatu."
Career ya Yaya Toure ilipitita katika njia ngumu. Alienda Beveren mwaka 2001, ikiwa ni sehemu ya majaribio nchini Ubelgiji - wazo la mchezaji wa zamani wa Ufaransa Jean-Marc Guillou, mtu wa karibu sana na Arsene Wenger.
Guillou amejenga academy nchini Ivoery Coast - ambapo kaka yake Yaya, Kolo Toure ndio alitokea hapo na kwenda moja kwa moja mpaka Arsenal.
Pale KSK Beveren, Guillou aliipata timu ndogo iliyokuwa ikihitaji uwekezaji. Akainunua na msaada kutoka kutoka Arsenal.
Sheria nzuri za Ubelgiji zilikuwa na manufaa kwa Guilloi ambaye sasa kashayapatia maisha. Ada yoyote ya uhamisho kwa wachezaji watakaouzwa kutoka klabu hiyo - ilikuwa inagawanywa pasu kwa pasu. Guillou na Beveren.
![]() |
| YAYA TOURE NDANI YA UZI THE GUNNERS AMBAPO ALIFANYA MAJARIBIO. |
Mwaka 2003, kutokana na uhusiano uliopo kati ya Arsenal na Guillou pamoja Beveren Yaya Toure akapelekwa London kwa majaribio ya muda mfupi. Japokuwa sasa anafananishwa na Patrick Vieira - haikuwa hivyo mwanzoni.
Toure alicheza mechi ya pre-season dhidi ya Barnet lakini dimba la juu. Aidha Toure hakumshawishi au Wenger tayari alikuwa na mbadala wake, kijana kutoka Ivory Coast akarudi Ubelgiji. Wote wawili Wenger na Toure wameshasemakulikuwa na matatizo juu ya passport.
'Labda alikuwa bado hajakaa sawa,' alisema Martin Keown, ambaye bado alikuwa Arsenal kipindi hicho.
"Kulikuwa na attention kubwa sana juu yake kwa sababu alikuwa mdogo wake Kolo, lakini Yaya hakuwa na mwezi wa mazoezi wa pre-season kama wengine . Labda mwili wake bado haukuwa sawa.
"Lakini pamoja na yoteYaya aliacha gumzo. Yeye na kaka yake ni wakarimu na watu wazuri sana. Na wanapenda mpira - tumekuwa tukisikia kuhusu watoto wa mzee Neville walivyo, ndugu hawa wa Toure nao wapo hivyo hivyo."
Aliporudi Ubelgiji Toure hakukataa tamaa aliendeleza juhudi ya kujifunzana mazoezi na hata tabia zake hazikubadilika.
Ingawa katika mahojiano aliyoyafanya na Dailymail Toure anasema alifanya mambo mengi ya kijinga alipokuwa Beveren lakini hakuna mtu anakumbuka. lakini Danny Stuer mkufunzi wa mazoezi ya viungo anasema tofauti: "Yaya alikuwa mtu wa maadili, tofauti sana, muda wote mkimya na mtu anayependa kufanya kazi. Alikuwa anakuja gym na alikuwa proffessional tangu mwanzo - wengine wote hawakuwa hivyo - kwao gym ilikuwa mchezo mtu.
"Baada ya mechi Yaya hakuwa akitoka kwenda kunywa mabia kama wenzie. Alirudi nyumbani na kubaki kupumzika huku akiangalia TV, hasa soka na soka zaidi."
"Mwanzoni alikuwa akiishi na wenzie lakini wenzake walipokuwa wanatoka usiku na kurudi wamechelewahuanza kumsumbua. Hivyo mwishowe akaomba aishi peke yake, na klabu ikafanikisha hilo.
"Labda alienda kwenye party nyuma ya mgongo wangu kama wengine- lakini kwa kile ninachojua Yaya alikuwa tofauti"
Pale Beveren walikuwa wanajua wachezaji wa kiafrika walikuwa wakienda Liege au Brussels kwa ajili ya kupati.
Baada ya misimu miwili na nusu na mechi 70 akiwa na Beveren, Toure aliuzwa kwa fedha ya ubelgiji millioni 2.
Mahasimuwawili wa Ubelgiji, Anderlecht na Club Bruges, wote walikuwa wakimtaka Toure, lakini sio kwa bei hiyo. Hivyo akiwa na miaka 20, akahamia Ukraine kwenye timu ya daraja ya pili ya Donetsk, Metalurh. Haikuwa sehemu nzuri kwa mtu ambaye alikuwa na ndoto ya kuwa star wa dunia, lakini Toure anasema uhamisho huo ulikuwa mzuri kwake. "Soka ni kazi; nilijifunza hivyo Ukraine."
Baada ya muda kidogo -akahamia Ugiriki na kujiunga na Olympiakos. Club Bruges inaweza kuwa ilikataa kulipa €2m lakini manager wao, mnorway Trond Sollied, ambaye alijiunga na Olympiakos akamsaini Toure na kushinda kombe la Ugiriki. "Niliona almasi, kitu fulani special kwake, alipokuwa pale Beveren," anasema Sollied. "Hakuwa na nguvu alizonazo sasa, au kufunga magoli mengi lakini alikuwa na kitu extra ndani ya timu.
"Kumpata na kumleta Ugiriki ilikuwa ni vizuri. Kimwili alikuwa amepevuka, alikuwa yupo vizuri kuliko alivyokuwa Ukraine. Tulijua hatutoweza kukaa nae sana. Alikuwa na uhakika sana kuhusu alivyo. Nafikiri kaka yake alimsaidia. Walikuwa wakibadilishana uzoefu."
Baada ya kombe la dunia la mwaka 2006, AS Monaco, timu ya zamani ya Wenger, ilimnunua Toure kwa ada ya £4million, ingawakulikuwa na kutokuelewana kidogo kule Donetsk kuhusu mkataba wake.
![]() |
| YAYA TOURE ALIPOKUWA BARCELONA. |
Lakini baada ya msimu mmoja tu nchini Ufaransa, Barcelona wakamsaini. Yaya Toure akaenda Catalunya ambako alipata majina mengi kamavile "Colossus - yaaani sanamu kubwa sana la mtu", wengine wakamuita "Treni " lakini Pep Guardiola alimuelezea Yaya kama "Diesel Player" - inachukua muda muda mrefu kwenda anapopataka lakini hasimami.
Huyu ndio Yaya Toure ambaye ama kwa hakika ndio kiungo bora kabisa katika msimu huu wa Premier League ambayo inaisha Jumapili huku mwenyewe akitimiza miaka 29 siku hiyo.
ZIMBABWE YAFURAHIA KUJIPIMA KWA TWIGA STARS
Timu ya Taifa ya mpira wa miguu kwa wanawake ya Zimbabwe imefurahia kucheza mechi ya kirafiki na Tanzania (Twiga Stars) itakayofanyika Jumamosi (Mei 12 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Kocha Mkuu wa Zimbabwe, Rosemary Mugadza amesema wamefurahi kupata mechi hiyo kwa vile wanaamini Twiga Stars ni kipimo kizuri kwao kabla ya kucheza mechi yao ya mashindano ya Afrika dhidi ya Nigeria.
Amesema anaijua vizuri Twiga Stars, kwani mwaka jana alicheza nayo mara mbili. Mara ya kwanza ilikuwa kwenye nusu fainali ya Kombe la COSAFA ambapo katika mechi hiyo iliyochezwa Julai 5 jijini Harare, Zimbabwe ilishinda kwa penalti 4-2. Mechi ya pili ilikuwa kwenye michezo ya All Africa Games (AAG) iliyofanyika Maputo, Msumbiji ambapo katika mechi yao iliyochezwa Septemba 11 timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2. Mabao ya Twiga Stars yalifungwa na Asha Rashid na Mwanahamisi Shuruwa. Mugadza amesema sababu nyingine iliyowafanya watake kucheza na Twiga Stars ni kwa vile ilishacheza na Nigeria kwenye fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) zilizofanyika Afrika Kusini mwaka 2010.
Twiga Stars ilifungwa na Nigeria mabao 2-1. Kocha huyo amesema hiyo itakuwa mechi ya pili kujipima nguvu kabla ya kuivaa Nigeria. Mwishoni mwa wili iliyopita Zimbabwe ilicheza mechi ya kirafiki jijini Harare dhidi ya Zambia na kushinda mabao 2-1. Zimbabwe ambayo iliwasili jana (Mei 9 mwaka huu) saa 1.30 usiku kwa ndege ya South African Airways (SAA) ina msafara wa watu 28 ambapo kati ya hao 20 ni wachezaji wakati waliobaki ni benchi la ufundi na viongozi wa timu hiyo.Viingilio katika mechi hiyo kati ya Twiga Stars na Zimbabwe itakayochezwa kuanzia saa 10.30 jioni ni sh. 1,000 tu kwa sehemu zote isipokuwa VIP A ambayo ni sh. 10,000 na VIP B ambayo kiingilio chake ni sh. 5,000.
Twiga Stars ilikuwa katika ziara ya mechi za kirafiki katika mikoa ya Dodoma na Mwanza na inatarajia kurejea kesho (Mei 11 mwaka huu) tayari kwa mechi hiyo itakayochezwa na mwamuzi wa kimataifa Judith Gamba. Boniface WamburaOfisa HabariShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Amesema anaijua vizuri Twiga Stars, kwani mwaka jana alicheza nayo mara mbili. Mara ya kwanza ilikuwa kwenye nusu fainali ya Kombe la COSAFA ambapo katika mechi hiyo iliyochezwa Julai 5 jijini Harare, Zimbabwe ilishinda kwa penalti 4-2. Mechi ya pili ilikuwa kwenye michezo ya All Africa Games (AAG) iliyofanyika Maputo, Msumbiji ambapo katika mechi yao iliyochezwa Septemba 11 timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2. Mabao ya Twiga Stars yalifungwa na Asha Rashid na Mwanahamisi Shuruwa. Mugadza amesema sababu nyingine iliyowafanya watake kucheza na Twiga Stars ni kwa vile ilishacheza na Nigeria kwenye fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) zilizofanyika Afrika Kusini mwaka 2010.
Twiga Stars ilifungwa na Nigeria mabao 2-1. Kocha huyo amesema hiyo itakuwa mechi ya pili kujipima nguvu kabla ya kuivaa Nigeria. Mwishoni mwa wili iliyopita Zimbabwe ilicheza mechi ya kirafiki jijini Harare dhidi ya Zambia na kushinda mabao 2-1. Zimbabwe ambayo iliwasili jana (Mei 9 mwaka huu) saa 1.30 usiku kwa ndege ya South African Airways (SAA) ina msafara wa watu 28 ambapo kati ya hao 20 ni wachezaji wakati waliobaki ni benchi la ufundi na viongozi wa timu hiyo.Viingilio katika mechi hiyo kati ya Twiga Stars na Zimbabwe itakayochezwa kuanzia saa 10.30 jioni ni sh. 1,000 tu kwa sehemu zote isipokuwa VIP A ambayo ni sh. 10,000 na VIP B ambayo kiingilio chake ni sh. 5,000.
Twiga Stars ilikuwa katika ziara ya mechi za kirafiki katika mikoa ya Dodoma na Mwanza na inatarajia kurejea kesho (Mei 11 mwaka huu) tayari kwa mechi hiyo itakayochezwa na mwamuzi wa kimataifa Judith Gamba. Boniface WamburaOfisa HabariShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
WACHEZAJI WA MAN UNITED WAGAWA ZAWADI NCHINI KENYA: GARI LILOBEBA MIPIRA 200 LAENDESHWA KUTOKA UINGEREZA MPAKA KENYA
Man United star Nani amezoea kuingiza mipira kwenye nyavu za uwanjani, lakini sasa ameamua kuitumibikiza kwa gari aina ya Van.
![]() |
| Andy Cole na Fortune wakigawa mipira 200 iliyotoka Uingereza na kuletwa nchini Kenya kwa gari. |
![]() |
| Watoto nchini Kenya wakiwa na zawadi ya mipira kutoka kwa wachezaji wa Man United |
Gari hilo liliendeshwa kwa maili 4,395 mpaka kwenye World Hope Community Project nchini Kenya na Dan Magness ambaye ni mchezea mipira wa ustadi.
AIRTEL RISING STARS YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM.
Mashindano ya kuvumbua vipaji maarufu kama Airtel Rising Stars yamezinduliwa rasmi hii leo jijini Dar Es Salaam na Wazir wa Mawasiliano Sayansi na Teknojoria Profesa Makame Mbarawa,
Kwenye uzinduzi huo pia alikuepo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Bwana Sam Elangalloor. Mwakilishi wa TFF kwenye uzinduzi huo alikua ni mkurugenzi wa Mashindano Bwana Saad Kawemba.
Kiungo wa zamani wa Manchester Utd Quinton Fortune akionyesha ujuzi wake wa kuuchezea mpira.
KALI YA LEO: BOBAN ASAFIRI KWENDA SUDAN AKIVAA KANDAMBILI
| Haruna Moshi Boban akiwa ndani ya kandambili uwanja wa taifa jana. |
Kiungo mshambuliaji wa timu ya Simba, Haruna Moshi ‘Boban’ jana alikuwa kivutio kwa mashabiki, wasindikizaji na hata baadhi ya wasafiri waliomuona wakati wakiondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, kuelekea Sudan.
Simba inakwenda Sudan katika mchezo wa marudiano dhidi ya Al Ahli Shendi utakaopigwa Jumapili, huku ikiwa na mtaji wa ushindi wa mabao 3-0, iliyoupata kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Uvaaji wa Boban, ndio uliowavutia watu kumtizama, kutokana na kuvaa kama mtu asiyesafiri.
Boban alikuwa amevaa fulana, suruali ya kimichezo ‘trakisuti’ na kandambili, hivyo kusababisha watu kuvutika kumuangalia, huku baadhi yao wakibaki kujiuliza kuhusu vituko vya nyota huyo ambaye mashabiki humuita Balotteli wa Bongo.
Mchezaji huyo anafananishwa na mshambuliaji mahiri wa Italia, anayekipiga klabu ya Manchester City ya England, ambako mara kwa mara amekuwa akibeba vichwa vya habari katika magazeti ya England na Ulaya kutokana na vituko vyake.
Ukiondoa vituko hivyo vya uvaaji wa Boban, msafara wa watu 25 wakiwamo viongozi watano na wachezaji 20 wa timu hiyo waliondoka chini ya uongozi wa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Hussein Mwamba, majira ya saa 8:00 mchana
SIMBA YAFIKA SALAMA SUDAN
Majira ya saa 6 usiku nilifanikiwa kufanya mawasiliano na mchezaji wa Simba Emmanuel Okwi na ameniambia kwamba timu nzima imefika Salama huko Sudan. Kwa taarifa zaidi endelea kutembelea hapa
SIMBA ILIPOONDOKA KWENDA SUDAN LEO MCHANA
Makamu mwenyekiti wa timu ya Simba Bw. Godifrey Nyange ''Kaburu''akionyesha ishara ya vidole vitanona mchezaji nyota wa timu hiyo Emmanueli Okwi, kwa kuonyesha alama hii huenda walikuwa wakimaanisha ushindi wa magoli 5 walioupata baada ya kuwafunga watani wao timu ya Yanga .hii ilikuwa katika uwanja wa ndege wa mwalimu juliasi Nyerere jijini Dar es salaam wakati timu hiyo ikijianda kuondoka kwenda Sudani kwenye mchezo wao wa marudio na Al Hilal Shandy jumapili ijayo.
Kapteni wa timu ya Simba Juma Kaseja akihojiwa na waandishi wa habari kuhusiana na maandalizi ya timu hiyo.
Makamu mwenyekiti wa timu ya simba Bw;Godifrey Nyange ''Kaburu akiteta jambo na wachezaji wa timu ya Simba.
Wachezaji wa timu ya Simba wakiingia kwenye chumba maalumu tayari kwa kuondoka.
LLOYD NCHUNGA AJIBU MAPIGO: SITOJIUZULU YANGA, PAPIC ATAONDOKA, UONGOZI HAUDAIWI. FAGIO LA CHUMA KUPITA YANGA TISA KUONDOKA. MWAPE NA SHAMTE ALLY KUTOVAA JEZI ZA NJANO NA KIJANI MSIMU UJAO
WAKATI uongozi wa Yanga ukipuuza shinikizo zito la kutakiwa kujiuzulu toka baadhi ya wanachama wa klabu hiyo kwa madai ya kuwa kiini cha kipigo cha aibu toka Simba Jumapili iliyopita, wachezaji tisa timu hiyo wamekalia kuti kavu baada ya mikataba yao kufikia.
Wachezaji hao wako hatarini kutemwa kwa sababu kuna uwezekano mdogo, au usiwapo kabisa kusaini mikataba mipya, taarifa za ndani toka klabu hiyo ya Jangwani zimedai
Ni pamoja na Shamte Ally, Jerry Tegete, Chacha Marwa, Mohamed Mbegu, Abuu Ubwa, Zuberi Ubwa, Kigi Makasi, Shadrack Nsajigwa na Athuman Idd 'Chuji'.
Ni pamoja na Shamte Ally, Jerry Tegete, Chacha Marwa, Mohamed Mbegu, Abuu Ubwa, Zuberi Ubwa, Kigi Makasi, Shadrack Nsajigwa na Athuman Idd 'Chuji'.
Tegete anahusishwa kwenda Simba, wakati Nsajigwa anatuhumiwa kucheza chini ya kiwango katika mechi yao dhidi ya Simba, ambapo alisababisha penalti mbili kati ya tatu na kuwapa mahasimu wao ushindi wa mabao 5-0.
"Wachezaji wengi wamemaliza mikataba yao, wapo baadhi huenda wakaongezewa kama Chuji, lakini wengine watatemwa akiwamo Shamte ambaye hakuna ubishi hatarudi Jangwani msimu ujao," alisema mtoa habari.
Alisema wachezaji Nurdin Bakari, Hamis Kiiza, Kenneth Asamoah bado wana mkataba wa mwaka mmoja, wakati Yaw Berko na Davis Mwape mikataba yao itamalizika Novemba mwaka huu.
Alisema wachezaji Nurdin Bakari, Hamis Kiiza, Kenneth Asamoah bado wana mkataba wa mwaka mmoja, wakati Yaw Berko na Davis Mwape mikataba yao itamalizika Novemba mwaka huu.
"Uongozi umeshaanza kuzungumza na Berko kuangalia uwezekano wa kuongeza mkataba wake, lakini Mwape hatacheza Yanga msimu ujao mara baada ya mkataba wake kumalizika," alisema mpashaji huyo habari.
Jumamosi wiki hii Kamati ya Utendaji itakutana, na moja ya mambo watakayozungumza ni ushiriki wa Ligi Kuu, changamoto zilizokuwepo na kujadili wachezaji watakaochwa na wanaostahili kubaki.
Jumamosi wiki hii Kamati ya Utendaji itakutana, na moja ya mambo watakayozungumza ni ushiriki wa Ligi Kuu, changamoto zilizokuwepo na kujadili wachezaji watakaochwa na wanaostahili kubaki.
"Kikubwa kinachoangaliwa ni nidhamu wa wachezaji ndani na nje ya uwanja pamoja na kiwango, na pia kuna wachezaji wengine watahama kwenda timu nyingine haya yote yataangaliwa."
Alisema ajenda nyingine kwenye kikao hicho ni kupanga tarehe ya Mkutano Mkuu wa wanachama pamoja na vuguvugu la mgogoro lililopo ndani ya klabu hiyo.
Alisema ajenda nyingine kwenye kikao hicho ni kupanga tarehe ya Mkutano Mkuu wa wanachama pamoja na vuguvugu la mgogoro lililopo ndani ya klabu hiyo.
Mwenyekiti wa Yanga Llody Nchunga alisema masuala yote yanayohusu usajili wa wachezaji watawekwa wazi wiki ijayo mara baada ya kikao chao cha Kamati ya Utendaji.
Aidha, kuhusu wachezaji wanaodai, Nchunga alisema ni wale waliongezewa mikataba ambao ni Nurdin Bakari na Nadir Haroub.
Aidha, kuhusu wachezaji wanaodai, Nchunga alisema ni wale waliongezewa mikataba ambao ni Nurdin Bakari na Nadir Haroub.
"Wachezaji wanaodai fedha za usajili ni wachache tena waliongezewa mikataba kipindi cha uongozi uliopita na hata hivyo fedha hizo wanatakiwa walipwe msimu ujao kwa kuwa ndiyo watakaoanza kuutumikia," alisema Nchunga na kuwataja wachezaji hao kuwa ni Nurdin na Nadir.
"Nawashangaa wazee wetu wanavyosema wachezaji wanadai Sh127 milioni. Hivi hawa wazee ni wahasibu? Wamepata wapi hesabu hizi, napenda kuwaambia kuwa hatudaiwi kiasi hicho," alisema.
Kuhusu shinikizo la kutakiwa kujiuzulu, Nchunga alisema hawezi kufanya hivyo kwa shinikizo la watu wachache wakati Yanga ni timu ya wanachama.
Kuhusu shinikizo la kutakiwa kujiuzulu, Nchunga alisema hawezi kufanya hivyo kwa shinikizo la watu wachache wakati Yanga ni timu ya wanachama.
"Mimi nilichaguliwa na wananchana wa Yanga, wao ndiyo wanaweza kunitaka nijiuzulu tena kupitia Mkutano Mkuu wa Klabu. Tunaendeshwa na katiba na siyo kelele za vikundi vya watu. Hatima yangu itaamuliwa na Wanayanga, siyo kikundi.
"Kamati ya Utendaji itapanga tarehe ya Mkutano Mkuu, mimi nafuata katiba na wala sing'ang'anii madaraka Yanga. Wale wote wanaotaka mimi na uongozi wangu tujiuzulu, basi waje kwenye mkutano mkuu," alisema bosi huyo.
Alisema utamaduni wa kuondoa madarakani uongozi kwa njia za mkato umepitwa na wakati. "Mambo ya kupinduana yamepitwa na wakati, dhambi hii ya kupinduana haitaishia kwa Nchunga peke yake itawatafuta wengine. Ifike mahali tubadilike tufanye kazi kwa kufuata katiba na siyo mazoea."
Aliongeza: "Wanaona sifai wafuate taratibu na watoe sababu za msingi siyo kwa vile tumepokwa pointi tatu ndiypo wanishinikize nijiuzulu hayo ni makosa ya soka.
Naomba itoshe kusema hivi...wale wote wanaodhani nitajiuzulu nafasi yangu, ni wazi wamepitwa na wakati. Sijiuzulu kwa sababu ya kikundi cha watu wachache, wanachama ndiyo wataamua."
Kuhusu madai ya kocha wa Yanga Kostadin Papic, Nchunga alisema: "Papic tunamuandalia malipo yake ambayo ni mishahara ya miezi miwili na muda wowote atalipwa.
Alikiri uongozi wake kutokuwa na ushirikiano na Papic kwa sababu kocha mwenyewe amekuwa akionyesha dharau mbele ya uongozi kwa kushindwa kuheshimu maagizo anayopewa.
"Sikiliza nikuambie, Papic hatuwezi kuwa naye tena tunamuandalia chake aondoke, kwanza hata wachezaji hawamtaki. Tulishawahi kumuonya kuhusu kutoa mambo ya ndani ya klabu kwenye vyombo vya habari lakini hakuwahi kutekeleza agizo hilo.
"Mechi ya Toto kule Mwanza alichangia kwa kiasi kikubwa tukapoteza mchezo. Kwanza alikataa kwenda na timu, baadaye akataka atumiwe tiketi aende Mwanza akatumiwa kufika tu wachezaji wakakosa raha.
Hata hivyo Nchunga hakutaka kuweka wazi mbadala wa Papic kwa madai kuwa Kamati ya Utendaji ndiyo itakayoamua hatima yake. Hata hivyo kuna taarifa klabu hiyo ipo kwenye mchakato wa kupitia vielelezo vya makocha kutoka Romania na Scotland.
source:mwananchi.co.tz
Wednesday, May 9, 2012
BREAKING NEWS! TBL YAINGIA MKATABA WA MIAKA 5 NA TFF
| Tenga na Mgongolwa wakifurahia |
| Tenga na Mgongolwa |
| Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah kushoto, katikati mama Juliana Yassoda na kulia Robin |
| Wadau wa soka, Msafiri Mgoyi Mjumbe wa TFF, beki wa zamani Taifa Stars na Meneja wa timu hiyo, Leopold Mukebezi, Fred na kocha Joseph Kanakamfumu |
| Mwandishi wa Nipashe Somoe Ng'itu na kocha Jamhuri Kihwelo |
| Makamu wa kwanza wa rais wa TFF, Athumani Nyamlani na Mdau Salim |
MUDA MCHACHE ULIOPITA KAMPUNI YA BIA NCHINI TANZANIA,TBL IMEINGIA MKATABA NA SHIRIKISHO LA MPIRA NCHINI TANZANIA TFF MKATABA WA MIAKA 5 WENYE THAMANI YA DOLA ZA KIMAREKANI MILIONI KUMI.
TANZANIA YAICHAPA LESOTHO 57-13 MICHUANO YA AFRIKA YA NETIBOLI
Mashabiki wakifuatilia mchezo wa ufunguzi.
Wanamuziki wa Bendi ya Mwenge Jazz wakitumbuiza wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Afrika ya Netiboli.
Kikosi cha Taifa Queen's
Mlinzi wa timu ya taifa ya Netiboli Tanzania, ‘Taifa Queens’, Lilian Sylidion (kushoto), akiwania mpira mbele ya wachezaji wa timu ya Lesotho katika mchezo wa ufunguzi wa mashindano ya Afrika uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Taifa Queen's imeshinda 57-13.
PAPISS DEMBA CISSE: NDOTO YANGU NI KUICHEZEA REAL MADRID - NAIPENDA TANGU UTOTONI
Papiss Demba Cisse amekiri kwamba ndoto yake ni kuichezea Real Madrid.
Straika huyo wa Newcastle na Senegal amefunga mabao 13 katika mechi 13 tangu alipokamilisha usajili wa £10million kutoka Freiburg mwezi January mwaka huu.
Lakini mshambuliaji huyo mwenye miaka 26 ameamua kukiri kwamba angependa kujiunga na mabingwa wapya wa La liga ikitokea nafasi ya kufanya hivyo siku moja.
Cisse alisema: "Ndoto yangu ya muda mrefu ni kuichezea klabu kubwa duniani na kushinda ubingwa wa ulaya. Nimekuwa naipenda Real Madrid tangu nilipokuwa mdogo.
Lakini nina furaha kwa sasa nipo Newcastle. Ni klabu kubwa - hata kama sio kama zilizvyo Manchester United au City."
Straika huyo wa Newcastle na Senegal amefunga mabao 13 katika mechi 13 tangu alipokamilisha usajili wa £10million kutoka Freiburg mwezi January mwaka huu.
Lakini mshambuliaji huyo mwenye miaka 26 ameamua kukiri kwamba angependa kujiunga na mabingwa wapya wa La liga ikitokea nafasi ya kufanya hivyo siku moja.
Cisse alisema: "Ndoto yangu ya muda mrefu ni kuichezea klabu kubwa duniani na kushinda ubingwa wa ulaya. Nimekuwa naipenda Real Madrid tangu nilipokuwa mdogo.
Lakini nina furaha kwa sasa nipo Newcastle. Ni klabu kubwa - hata kama sio kama zilizvyo Manchester United au City."
BAADA YA KIPIGO KUTOKA MTANI: YANGA SASA YAANZA KUJENGA TIMU - OWEN KASULE WA UGANDA NJIANI KUTUA JANGWANI
Kiungo wa timu ya Taifa ya Uganda ‘The Cranes’, Owen Kasule ametua Dar es Salaam kufanya mazungumzo ya usajili na uongozi wa timu ya Yanga ya Dar es Salaam.
Kasule alifika Dar es Salaam juzi, ambapo jana alifanya mazungumzo ya muda mrefu na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga inayoongozwa na Salum Rupia kuhusiana na
kusajiliwa na timu hiyo kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao.
Habari zilizopatikana ndani ya Yanga jana na kuthibitishwa na Rupia pamoja na Kasule zilieleza kuwa mazungumzo hayo yalikuwa mazuri, lakini kuna mambo ya kimsingi ambayo yaliwakwamisha kufikia mwafaka.
Rupia alikiri kuzungumza na Kasule jana, lakini alisema hawakusaini naye mkataba kwani amewaambia anaenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika timu ya Al Ahly ya Misri na kwamba kama atakwama huko atakuja kusaini Yanga.
Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Usajili alisema, Kasule amewaeleza kuwa ni rafiki wa karibu wa mshambuliaji Hamisi Kiiza wa Yanga na Emmanuel Okwi wa Simba ambao amesoma nao shule Uganda, hivyo wanapomjulisha habari za soka la Tanzania anatamani sana kuja kucheza.
“Ametwambia ana mapenzi sana na Yanga, hivyo naamini atakuja,” alisema Rupia. Okwi na Kiiza ni miongoni mwa wachezaji wa nje waliong’ara kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara iliyomalizika Jumapili.
Kwa upande wake Kasule akizungumza jana akiwa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere kabla ya kurejea kwao, alikiri kuzungumza na Yanga, lakini akisema kuna mambo hawajafikia mwafaka.
“Mazungumzo yetu hayajaisha, nitakujulisha kwa kirefu zaidi, lakini kwa sasa hapana, elewa kwamba tumezungumza na Yanga,” alisema.
Kasule alifika Dar es Salaam juzi, ambapo jana alifanya mazungumzo ya muda mrefu na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga inayoongozwa na Salum Rupia kuhusiana na
kusajiliwa na timu hiyo kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao.
Habari zilizopatikana ndani ya Yanga jana na kuthibitishwa na Rupia pamoja na Kasule zilieleza kuwa mazungumzo hayo yalikuwa mazuri, lakini kuna mambo ya kimsingi ambayo yaliwakwamisha kufikia mwafaka.
Rupia alikiri kuzungumza na Kasule jana, lakini alisema hawakusaini naye mkataba kwani amewaambia anaenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika timu ya Al Ahly ya Misri na kwamba kama atakwama huko atakuja kusaini Yanga.
Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Usajili alisema, Kasule amewaeleza kuwa ni rafiki wa karibu wa mshambuliaji Hamisi Kiiza wa Yanga na Emmanuel Okwi wa Simba ambao amesoma nao shule Uganda, hivyo wanapomjulisha habari za soka la Tanzania anatamani sana kuja kucheza.
“Ametwambia ana mapenzi sana na Yanga, hivyo naamini atakuja,” alisema Rupia. Okwi na Kiiza ni miongoni mwa wachezaji wa nje waliong’ara kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara iliyomalizika Jumapili.
Kwa upande wake Kasule akizungumza jana akiwa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere kabla ya kurejea kwao, alikiri kuzungumza na Yanga, lakini akisema kuna mambo hawajafikia mwafaka.
“Mazungumzo yetu hayajaisha, nitakujulisha kwa kirefu zaidi, lakini kwa sasa hapana, elewa kwamba tumezungumza na Yanga,” alisema.
TAARIFA KUTOKA TFF!
VITUO LIGI YA TAIFA VYAPANGWA
Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imepanga vituo vitatu vya Ligi ya Taifa inayoshirikisha mabingwa wa mikoa kwa ajili ya ligi hiyo itakayoanza Mei 26 mwaka huu.
Kundi A lenye mabingwa wa mikoa ya Iringa (Kurugenzi Mufindi), Lindi (Lindi SC), Mbeya (Tenende FC), Morogoro (Mkamba Rangers), Mtwara (Ndanda SC), Pwani (Super Star), Rukwa (Mpanda Stars) na Ruvuma (Mighty Elephant) zitacheza mechi zake mjini Mtwara.
Mji wa Kigoma utakuwa mwenyeji wa mabingwa wa mikoa ya Dodoma (CDA), Kagera (Bandari FC), Kigoma (JKT Kanembwa), Mwanza (Pamba SC), Shinyanga (Mwadui SC), Singida (Aston Villa) na Tabora (Majimaji).
Kundi C lenye mabingwa wa mikoa ya Arusha (Flamingo SC), Dar es Salaam (Ashanti United ya Ilala, Red Coast ya Kinondoni na Tessema FC ya Temeke), Kilimanjaro (Forest FC), Manyara (Nangwa VTC), Mara (Polisi Mara) na Tanga (Korogwe United) watachezea mechi zao mkoani Mara.
Mwisho wa kuwasilisha fomu za usajili ni Mei 15 mwaka huu wakati kipindi cha pingamizi ni kuanzia Mei 16 hadi 22 mwaka huu. Mei 23 mwaka huu Kamati ya Mashindano ya TFF itakutana kupitia usajili huo. Wachezaji wanaosajiliwa ni wale wale waliochezea timu hizo katika ligi ya mkoa.
Mei 14 mwaka huu ni mwisho kwa mikoa yenye pingamizi kwa mabingwa wao kuwa wameshashughulikia rufani husika. Kamati ya Mashindano imeagiza kuwa kwa mikoa itakayoshindwa kufanya hivyo mpaka baada ya tarehe hiyo mabingwa wao hawatashiriki ligi hiyo.
Timu tano zitapanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza msimu ujao. Mshindi wa kwanza kutoka kila kundi na washindwa wawili bora (best losers) kutoka kundi A na C ambayo yana timu nane kila moja.
LIUNDA KUSIMAMIA MECHI LESOTHO
Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua Leslie Liunda wa Tanzania kuwa Kamishna wa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia 2014 Kanda ya Afrika kati ya Lesotho na Sudan itakayochezwa jijini Maseru.
Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili itachezwa kati ya Juni 1 na 3 mwaka huu. Lesotho na Sudan ziko kundi D pamoja na Ghana na Zambia.
Naye Hafidhi Ally ameteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuwa Kamishna wa mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Dynamos FC ya Zimbabwe na Esperance Sportive ya Tunisia.
Mechi hiyo ya marudiano hatua ya 16 bora itachezwa Mei 13 mwaka huu kwenye Uwanja wa Rufaro jijini Harare. Esperance Sportive ilishinda mechi ya kwanza kwa mabao 6-0.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Powered by Sorecson : Creation de site internet
WAZEE WA YANGA WATOBOA UKWELI KUHUSU 5-0 ZA SIMBA: DENI LA PAPIC NA WACHEZAJI ZAIDI YA MILIONI 75 NDIO CHANZO KIKUBWA CHA KIPIGO DHIDI YA SIMBA.
Takribani zaidi ya masaa 48 baada ya klabu bingwa ya Tanzania bara na mwakilishi pekee wa Afrika mashariki na kati katika michuano ya kimataifa - Simba Sports Club kuifanyia mauaji ya kutisha mahasimu wao wa jadi klabu bingwa ya Afrika mashariki na kati Dar Young African kwa kuitandika bao tano kwa nunge - leo hii wazee wa klabu ya Yanga chini ya uongozi wa Ibrahimu Akilimali umeamua kuweka wazi sababu kuu zilizochangia mno kupokea kipigo kutoka kwa mnyama.
Akizungumza leo hii katika mkutano wa waandishi wa habari Mzee Akilimali kwanza kabisa alikana madai ya uongozi wa Mwanasheria Lloyd Nchunga kwamba wazee hao waliihujumu klabu hiyo katika mchezo, pia akimuonya Nchunga asithubutu kumfukuza mchezaji hata mmoja kwa madai ya kuhusika kuihujumu Yanga.
Mzee Akilimali pia amesema Nchunga na uongozi wake ndio watu wa kulaumiwa kwa klabu hiyo kupokea kipigo cha aibu kutoka kwa watani wao, huku akitoa sababu zifuatazo.
1: MAANDALIZI
Timu ya Yanga iliingia kambini siku tatu kabla ya mchezo dhidi ya Simba huku wachezaji wakiwa hawana morali yoyote kutokana na kuwa walikuwa wakidai malimbikizo ya mishahara na bonasi za mechi za msimu mzima.
2: KOCHA PAPIC NA MADAI YA MIL. 24
Kwa muda mrefu kocha mkuu wa Yanga amekuwa akiudai uongozi wa Yanga shilingi milioni 24 za malimbikizo ya mshahara wake, hali iliyopelekea Mserbia huyo kutokuweza kuishi vizuri nchini na kupelekea kutokuwa na maelewano mazuri ya uongozi hivyo mwishowe kukosa kabisa utulivu wa akili wa kuweza kuitumika klabu kuelekea katika crucial moment ya msimu-hasa katika mechi ya marejeano na watani wao jadi.
3: MADAI YA BONASI ZA SHILINGI 70,000 KWA KILA MCHEZAJI KWA MECHI - MSIMU MZIMA. (JUMLA YA PESA ZA BONASI ZA MSIMU MZIMA NI 52,780,000)
Uongozi wa Yanga umejiwekea utaratibu wa kutoa bonasi ya shilingi 70,000 kwa kila mchezaji kila baada ya mechi. Lakini katika hali ya kushangaza ndani ya kipindi chote cha Ligi kuu ya Tanzania bara uongozi wa bwana Lloyd Nchunga haukuwalipa hata shilingi ya bonasi za mechi zote za msimu wachezaji kama walivyokubaliana. Na pale alipoulizwa alikuwa akitoa ahadi tu.Kutokana na deni hili na kushindwa kutimiza ahadi Lloyd hakuwa hata akienda kuangalia kambi inaendaje wala kuwatia hamasa wachezaji kuelekea mchezo dhidi ya mahasimu wao wa jadi. Kiukweli hali ya kambi ilikuwa mbaya kifedha na kuwafanya wachezaji wa Yanga kutokuwa katika hali nzuri ya kiakili kuweza kuvaana na wapinzani wao bila kuambulia matokeo ya namna ile. Ilifikia hatua mpaka wachezaji wakaamua kwamba kabla ya mechi walipwe pesa zao au hawatoenda uwanjani kucheza na Simba - kitu ambacho kama wangekifanya wangeweza kushushwa daraja kama adhabu. Lakini wale wale watu ambao Bwana Lloyd amekuwa akiwatuhumu kwamba wanawarubuni wachezaji na pesa zao chafu ndio waliokuja kuokoa jahazi na kutoa kiasi cha shilingi 300,000 kwa kila mchezaji, ja,bo ambalo liliwafanya wachezaji kuingia uwanjani kucheza japo kwa shingo upande.
Sasa mchezaji akiwa kwenye hali waliyokuwa nayo wachezaji hawa halikuwa jambo la ajabu kuona wakiwa katika morali ya chini na kucheza ovyo kwenye mechi dhidi ya Simba." -Alisema Mzee Akilimali.
MASWALI
Ikiwa tuhuma hizi zilizotolewa na wazee wa Yanga ni kweli. Je ni wapi zilipokuwa zinaenda fedha nyingi zinazotolewa na mdhamini wa klabu hiyo Bia ya Kilimanjaro kila mwezi kwa madhumuni ya kulipa mishahara ya wachezaji, kocha na staffs wengine? Papic anadai mshahara wake.
Yanga ina chanzo kikubwa cha kukusanya mapato ya mlangoni tofauti na timu nyingi kwenye ligi kuu. Je yale mapato yote waliyokuwa wakiyakusanya ama kuyapata kutokana na viingilio vya mashabiki yamekwenda wapi kiasi cha kufikia kushindwa kuwalipa bonasi wachezaji?
Kwa undani zaidi wa stori hii sikiliza taarifa kutoka kwa wazee wa Yanga.
Akizungumza leo hii katika mkutano wa waandishi wa habari Mzee Akilimali kwanza kabisa alikana madai ya uongozi wa Mwanasheria Lloyd Nchunga kwamba wazee hao waliihujumu klabu hiyo katika mchezo, pia akimuonya Nchunga asithubutu kumfukuza mchezaji hata mmoja kwa madai ya kuhusika kuihujumu Yanga.
Mzee Akilimali pia amesema Nchunga na uongozi wake ndio watu wa kulaumiwa kwa klabu hiyo kupokea kipigo cha aibu kutoka kwa watani wao, huku akitoa sababu zifuatazo.
1: MAANDALIZI
Timu ya Yanga iliingia kambini siku tatu kabla ya mchezo dhidi ya Simba huku wachezaji wakiwa hawana morali yoyote kutokana na kuwa walikuwa wakidai malimbikizo ya mishahara na bonasi za mechi za msimu mzima.
2: KOCHA PAPIC NA MADAI YA MIL. 24
Kwa muda mrefu kocha mkuu wa Yanga amekuwa akiudai uongozi wa Yanga shilingi milioni 24 za malimbikizo ya mshahara wake, hali iliyopelekea Mserbia huyo kutokuweza kuishi vizuri nchini na kupelekea kutokuwa na maelewano mazuri ya uongozi hivyo mwishowe kukosa kabisa utulivu wa akili wa kuweza kuitumika klabu kuelekea katika crucial moment ya msimu-hasa katika mechi ya marejeano na watani wao jadi.
3: MADAI YA BONASI ZA SHILINGI 70,000 KWA KILA MCHEZAJI KWA MECHI - MSIMU MZIMA. (JUMLA YA PESA ZA BONASI ZA MSIMU MZIMA NI 52,780,000)
Uongozi wa Yanga umejiwekea utaratibu wa kutoa bonasi ya shilingi 70,000 kwa kila mchezaji kila baada ya mechi. Lakini katika hali ya kushangaza ndani ya kipindi chote cha Ligi kuu ya Tanzania bara uongozi wa bwana Lloyd Nchunga haukuwalipa hata shilingi ya bonasi za mechi zote za msimu wachezaji kama walivyokubaliana. Na pale alipoulizwa alikuwa akitoa ahadi tu.Kutokana na deni hili na kushindwa kutimiza ahadi Lloyd hakuwa hata akienda kuangalia kambi inaendaje wala kuwatia hamasa wachezaji kuelekea mchezo dhidi ya mahasimu wao wa jadi. Kiukweli hali ya kambi ilikuwa mbaya kifedha na kuwafanya wachezaji wa Yanga kutokuwa katika hali nzuri ya kiakili kuweza kuvaana na wapinzani wao bila kuambulia matokeo ya namna ile. Ilifikia hatua mpaka wachezaji wakaamua kwamba kabla ya mechi walipwe pesa zao au hawatoenda uwanjani kucheza na Simba - kitu ambacho kama wangekifanya wangeweza kushushwa daraja kama adhabu. Lakini wale wale watu ambao Bwana Lloyd amekuwa akiwatuhumu kwamba wanawarubuni wachezaji na pesa zao chafu ndio waliokuja kuokoa jahazi na kutoa kiasi cha shilingi 300,000 kwa kila mchezaji, ja,bo ambalo liliwafanya wachezaji kuingia uwanjani kucheza japo kwa shingo upande.
Sasa mchezaji akiwa kwenye hali waliyokuwa nayo wachezaji hawa halikuwa jambo la ajabu kuona wakiwa katika morali ya chini na kucheza ovyo kwenye mechi dhidi ya Simba." -Alisema Mzee Akilimali.
MASWALI
Ikiwa tuhuma hizi zilizotolewa na wazee wa Yanga ni kweli. Je ni wapi zilipokuwa zinaenda fedha nyingi zinazotolewa na mdhamini wa klabu hiyo Bia ya Kilimanjaro kila mwezi kwa madhumuni ya kulipa mishahara ya wachezaji, kocha na staffs wengine? Papic anadai mshahara wake.
Yanga ina chanzo kikubwa cha kukusanya mapato ya mlangoni tofauti na timu nyingi kwenye ligi kuu. Je yale mapato yote waliyokuwa wakiyakusanya ama kuyapata kutokana na viingilio vya mashabiki yamekwenda wapi kiasi cha kufikia kushindwa kuwalipa bonasi wachezaji?
Kwa undani zaidi wa stori hii sikiliza taarifa kutoka kwa wazee wa Yanga.
Tuesday, May 8, 2012
SIMBA KWENDA SUDAN NA NDEGE YA KUKODI
BAADA ya kumaliza Ligi Kuu bara kwa kishindo, Simba sasa inajipanga kwa safari ya kwenda Sudan kwa ajili ya mechi ya michuano ya kimataifa, na imepanga kuondoka kesho kwa ndege ya kukodi.
Simba iliifunga Yanga mabao 5-0 juzi katika mechi ya mwisho ya Ligi hiyo na hivyo kunogesha furaha za kutwaa ubingwa ilioutwaa tangu Ijumaa iliyopita.
Akizungumza Dar es Salaam jana, makamu mwenyekiti wa Simba Godfrey Nyange ‘Kaburu’ alisema kuwa timu yao itaondoka kesho kwa ndege ya kukodi kuelekea Sudan kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa Kombe la shirikisho dhidi ya Al Ahly Shandy ya huko.
Katika mechi ya kwanza ya raundi ya tatu ya michuano hiyo iliyochezwa Uwanja wa Taifa takriban wiki moja iliyopita, Simba ilishinda kwa mabao 3-0 na hivyo kuhitaji sare ama ushindi wa aina yoyote kwenye mechi hiyo ili kufuzu kwa hatua inayofuata.
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage amesema kuwa mafanikio ya
timu yao msimu huu yanatokana na ushirikiano mzuri kati ya uongozi wa sasa, uongozi uliopita na marafiki wa klabu hiyo ‘Friends of Simba’.
Rage akizungumza baada ya ushindi wa juzi dhidi ya Yanga, alisema kuwa mshikamano
uliokuwepo ndani ya klabu hiyo kwa sasa ndio siri ya mafanikio ya timu yao.
Alisema kuwa siku zote panapokosekana mshikamano madhubuti miongoni mwa wanachama wa klabu hiyo lazima timu yao inakuwa haifanyi vizuri, lakini kwa sasa kwa kuwa wako pamoja ndio maana mafanikio yanaonekana
Simba iliifunga Yanga mabao 5-0 juzi katika mechi ya mwisho ya Ligi hiyo na hivyo kunogesha furaha za kutwaa ubingwa ilioutwaa tangu Ijumaa iliyopita.
Akizungumza Dar es Salaam jana, makamu mwenyekiti wa Simba Godfrey Nyange ‘Kaburu’ alisema kuwa timu yao itaondoka kesho kwa ndege ya kukodi kuelekea Sudan kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa Kombe la shirikisho dhidi ya Al Ahly Shandy ya huko.
Katika mechi ya kwanza ya raundi ya tatu ya michuano hiyo iliyochezwa Uwanja wa Taifa takriban wiki moja iliyopita, Simba ilishinda kwa mabao 3-0 na hivyo kuhitaji sare ama ushindi wa aina yoyote kwenye mechi hiyo ili kufuzu kwa hatua inayofuata.
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage amesema kuwa mafanikio ya
timu yao msimu huu yanatokana na ushirikiano mzuri kati ya uongozi wa sasa, uongozi uliopita na marafiki wa klabu hiyo ‘Friends of Simba’.
Rage akizungumza baada ya ushindi wa juzi dhidi ya Yanga, alisema kuwa mshikamano
uliokuwepo ndani ya klabu hiyo kwa sasa ndio siri ya mafanikio ya timu yao.
Alisema kuwa siku zote panapokosekana mshikamano madhubuti miongoni mwa wanachama wa klabu hiyo lazima timu yao inakuwa haifanyi vizuri, lakini kwa sasa kwa kuwa wako pamoja ndio maana mafanikio yanaonekana
ANGALIA NAMNA DIDIER ZAKORA ALIVYOMLIPIZIA MCHEZAJI ALIYEMTOLEA MATUSI YA KIBAGUZI
Kiungo wa kimataifa wa Ivory Coast anayeichezea klabu ya Trabzonspor Didier Zakora amefanya kitendo ambacho kimetafsiriwa kama kulipiza kisasi - kwa mchezaji kiungo wa Fenerbahce Emre Belozoglu - ambaye alimtuhumu kumtolea maneno ya kibaguzi Zakora mwanzoni mwa msimu.
Kutokea kipindi hicho kumekuwepo hakuna dalili yoyote ya kupatana kwa wawili hao kwa upande wa Zakora - ambaye nae juzi aliamua kulipa kisasi kwa namna ile ile lakini kwa ubaya zaidi.
Hii hapa ni video inayomuonyesha Zakora akikataa kushikana mikono na Emre, huku wachezaji wenzie wa Trabzonspor wakimchezea kindava zaidi Emre wakisaidiana na Didier mwenyewe.
Haki imetendeka? Nani anajua. Inaonekana kwamba Zakora alipata kadi ya njano tu kwa undava aliokuwa akimchezea Emre; labda tu-assume kwamba refa ameamua kuangalia matukio ya kabla ya mchezo baina ya wachezaji hao.
Kutokea kipindi hicho kumekuwepo hakuna dalili yoyote ya kupatana kwa wawili hao kwa upande wa Zakora - ambaye nae juzi aliamua kulipa kisasi kwa namna ile ile lakini kwa ubaya zaidi.
Hii hapa ni video inayomuonyesha Zakora akikataa kushikana mikono na Emre, huku wachezaji wenzie wa Trabzonspor wakimchezea kindava zaidi Emre wakisaidiana na Didier mwenyewe.
Haki imetendeka? Nani anajua. Inaonekana kwamba Zakora alipata kadi ya njano tu kwa undava aliokuwa akimchezea Emre; labda tu-assume kwamba refa ameamua kuangalia matukio ya kabla ya mchezo baina ya wachezaji hao.
JERRY TEGETE AVALISHWA JEZI NA MASHABIKI WA SIMBA.
Mshambuliaji wa Yanga Jerry Tegete alivishwa jezi na mashabiki kwenye uwanja wa Taifa mara tu baada ya mchezo dhidi ya Yanga na Simba kumalizika.
JE HII INAASHIRIA NINI ?
EURO 2012 COUNTDOWN: CARLES PUYOL KUIKOSA MICHUANO YA EURO
Kocha wa timu ya taifa ya Hispania Vicente Del Bosque amepokea taarifa mbaya kwamba katika kuelekea kwenye michuano ya EURO 2012 hatoweza kupata huduma za nahodha wake Carles Puyol kutokana na beki huyo kupata majeraha ya goti.
Puyol, 34, alicheza dakika zote 90 katika mechi kati ya Barcelona na Espanyol - lakini akapata maumivu makubwa ya goti baada ya mchezo.
Alifanya vipimo leo asubuhi ili kuweza kujua undani ya maumivu na majeraha yake - na Barcelona wametangaza kupitia website yao kwamba Puyol atafanyiwa upasuaji.
Puyol atapitiwa na visu jumamosi ijayo, na atakuwa nje ya dimba kwa takribani wiki sita.
Puyol, 34, alicheza dakika zote 90 katika mechi kati ya Barcelona na Espanyol - lakini akapata maumivu makubwa ya goti baada ya mchezo.
Alifanya vipimo leo asubuhi ili kuweza kujua undani ya maumivu na majeraha yake - na Barcelona wametangaza kupitia website yao kwamba Puyol atafanyiwa upasuaji.
Puyol atapitiwa na visu jumamosi ijayo, na atakuwa nje ya dimba kwa takribani wiki sita.
KOCHA WA AZAM FC: STEWART HALL ASEMA RUSHWA NDIO KIKWAZO CHA MAENDELEO YA SOKA TANZANIA
KOCHA wa Azam, Stewart Hall amelia na wadau wa Simba na Yanga wanavyoipiga vita timu yake, ambayo imeibuka kuwa kigogo cha Ligi Kuu Tanzania Bara.
Akizungumza na Mwanaposti katika mahojiano maalumu, Hall anasema anashangazwa na mashabiki hasa wa Simba na Yanga kwa kuijengea chuki timu yake kutokana na kutishia ubabe wao.
Hall anaonya kuwa tabia ya wadau wa Simba na Yanga wanaotaka kuona ligi ya Tanzania ikitawaliwa na timu mbili zao tu kitu ambacho si sahihi kwa maendeleo ya soka.
"Timu hizi zimekuwepo kwa miaka mingi sana lakini nashangaa zimeshindwa kusaidia kukuza soka la Tanzania.
"Ninachokiona katika soka la Tanzania kinanisikitisha na kinachonikera zaidi wameingia watu makini wa Azam, ambao wameingiza fedha lakini wanapigwa vita," anasema Hall, ambaye ni raia wa Uingereza.
Anasema Watanzania wanapaswa kuruhusu ushindani na kutolea mfano Ligi Kuu Scotland inavyoshindaniwa na timu mbili tu za Rangers na Celtic na kufanya soka la sehemu hiyo kuwa chini.
Ligi Kuu Tanzania Bara
Hall anasema anafurahia timu yake kushika nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwa miaka chache tangu kuanzishwa kwake.
Anaeleza ni kitu kizuri kuona timu yake iliyoanzishwa mwaka 2004, imeipiku Yanga iliyoasisiwa katika miaka ya 1930.
Azam safari hii imenyakua nafasi ya pili na mwakani itashiriki katika mashindano ya Kombe la Shirikisho.
Hall anaonya Watanzania wanapaswa kubadilika kama kweli wanataka soka la nchi hii ibadilike.
Anasema kuwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linatakiwa kuwa makini katika kuendesha katika ligi hiyo.
Analalamikia vitendo vya rushwa kwenye ligi hiyo na viwango duni vya uchezeshaji miongoni mwa waamuzi.
Hall anaeleza kuwa anashangaa kuona rushwa na upangaji matokeo vinakubalika kama sehemu ya soka la Tanzania.
"Ni hatari kwa soka la nchi yenu kama mtakubali masuala ya upangaji matokeo," anasema Hall, ambaye timu yake ililazimika kurudiana na Mtibwa kwenye mzunguko wa pili baada ya mechi ya kwanza kukatizwa kutokana na makosa ya mwamuzi Rashid Msangi.
Pia mechi za Yanga na Polisi Dodoma zilimalizika kwa waamuzi kupigwa kutokana na timu hizo kudai mwamuzi alikuwa anaibeba Azam.
Kocha huyo anakanusha vikali madai hayo na kudai kuwa watu wanaionea wivu tu timu yake kutokana na kuwa na fedha nyingi.
Hall anasema TFF kwa kushirikiana na wadau wa soka la Tanzania wanapaswa kupiga vita kwa nguvu zote masuala ya rushwa.
Anatahadharisha ni ndoto kwa timu za Tanzania kufanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa kama wadau wa soka watakumbatia rushwa kama sehemu ya soka la Tanzania.
Anasema wapangaji matokeo wanapaswa kuchukua hatua kali kama Marseille ya Ufaransa ilivyoadhibiwa mwaka 1993 baada ya kubainika ilikuwa inanunua baadhi ya mechi za Ligi Kuu Ufaransa au ile kashfa ya upangaji matokeo ya Italia iliyokuja kujulikana kwa jina la Calciopoli.
Anaonyesha kuwa ubaya wa timu kununua mechi unasababisha Tanzania kuwakilishwa na timu dhaifu kwenye michuano ya Afrika.
"Bwana mwandishi jiulize, timu gani ya Tanzania imetwaa kutwaa taji la Afrika? Jibu linafahamika na ni wazi kuwa linasababishwa na rushwa ndani ya Ligi Kuu," anaeleza Hall, ambaye amewahi kuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Birmingham.
Hall, hata hivyo, anadai anategemea ushindani mkali zaidi msimu ujao kwenye Ligi Kuu kwani ameona timu kama Mtibwa na Coastal Union ziko juu.
Mashabiki wa Simba na Yanga
Hall anaeleza pia mashabiki wa Simba na Yanga kwa kiasi kikubwa nao wanachangia kwa kiasi kikubwa kuvuruga soka la Tanzania.
Anasema mashabiki hao wanaweka presha kubwa kwa wachezaji na viongozi wa soka kuhakikisha timu zao zinashinda.
Hall anatolea mfano vurugu za mechi ya Yanga na Azam kuwa zilichangiwa zaidi na viongozi na mashabiki wa Yanga kuwapa shinikizo wachezaji wao kushinda.
"Unajua tulikuwa tumeifunga Yanga mara kadhaa, sasa safari hii wakaona hapana wanapaswa kushinda kwa njia zozote. Basi baada ya kuona mambo hayaendi vizuri wakampiga mwamuzi," anasema Hall, ambaye pia ni Mshauri wa Ufundi wa timu ya Zanzibar.
Hall anasema anaelewa mashabiki wa soka wa Tanzania wamegawanyika kushabikia timu hizo lakini amesema zinapaswa kubadilika.
Anaeleza mashabiki wa timu hizo wanapaswa kuhakikisha timu zao zinaendeshwa kisasa zaidi ndani na nje ya uwanja badala ya kuendekeza siasa za nje ya uwanja.
Hall anaeleza kutokana na presha na wingi wa mashabiki wa Simba na Yanga kumefanya wababaike wanapochezesha mechi za baina ya timu hizo.
Pia ameponda mashabiki hao kwa kukosa uzalendo na kuzishabikia timu za kigeni zinapokuja kucheza Tanzania.
"Nimefundisha soka katika nchi mbalimbali duniani lakini sijawahi kuona timu ya kigeni inashabikiwa," anasema Hall.
Katika miaka ya karibuni, imekuwa kitu cha kawaida kwa mashabiki wa Simba na Yanga kushangilia timu za kigeni zinapocheza na mahasimu wao.
Hall anasema ameshangazwa kuwa tabia hiyo imeingia katika timu ya taifa.
"Mashabiki wa Simba na Yanga wanaua soka lenu kwani wameingiza siasa zao kwenye timu ya taifa," anaeleza Hall, ambaye alikuwa anazungumzia vituko vya Kombe la Chalenji mwaka jana wakati mashabiki wa Yanga walipokuwa wanaizomea timu ya Bara kutokana na kuwa na wachezaji wachache wa Yanga.
Pia anatolea mfano jinsi mashabiki hao walivyokuwa wanamsakama mshambuliaji wake John Boko na kumfanya ajitoe kwenye kikosi cha timu ya taifa.
"Boko ni mchezaji mdogo sana lakini ameacha kuchezea Stars kutokana na kujengewa chuki na mashabiki hawa. Watu hawa wanaua soka la Tanzania," anaeleza Hall.
Pia anaeleza kuwa mashabiki hao wamejenga chuki kubwa dhidi ya timu yake kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na matajiri wa timu hiyo.
Azam imejenga uwanja na hosteli ya wachezaji na ina mfumo mzuri wa timu kuanzia watoto wenye umri wa miaka 12.
Pia wachezaji wa timu hiyo wanaangaliwa vizuri kwa kulipwa mishahara na marupurupu kwa wakati.
"Mimi nilitegemea kuwa mashabiki hawa wangetuunga mkono na kushinikiza viongozi wao kubadilika na kuendesha timu zao vizuri lakini badala yake wanatupiga vita," anaeleza Hall kwa mshangao.
Hall anatoa mwito kwa wadau wa soka la Tanzania kuiangalia Azam kama kioo cha soka la Tanzania badala ya kuichukulia kama adui.
Maendeleo ya Azam
Hall anaeleza kuwa anasema licha ya changamoto za waamuzi lakini anapongeza timu yake kwa kushika nafasi ya pili nyuma ya Simba iliyotwaa ubingwa.
Amesema amefurahia kuona malengo yao yametimia msimu kwani walikuwa wanataka kuvunja ubabe wa Simba na Yanga kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara.
"Lengo letu kubwa lilikuwa kushika nafasi mbili za juu, kitu ambacho tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa.
"Sasa msimu ujao tunataka kupigania ubingwa jambo ambalo ninaamini tuna ubavu nalo," aliongeza Hall, ambaye amewahi kuzifundisha timu za taifa za St.Vincent, Grenada na Pune ya India.
Hall anafichua kuwa timu hiyo imeandaa programu ya miaka 10 yenye lengo la kuifanya timu hiyo kuwa miongoni mwa timu kubwa Afrika.
"Tunataka tufikie hatua kutoa upinzani kwa timu kama TP Mazembe au Al-Ahly ya Misri," anaongeza Hall.
Amesema kuwa anasikitishwa na kuona timu yake inapigwa vita na wadau wa soka.
Hall anasema kutokana na haya yanayowakuta Azam yatafanya watu wengine wenye fedha kuogopa kuingiza fedha zao kwenye soka.
"Unajua kuna watu wanaangalia tunayofanya sasa watu wenye fedha zao wakishuhudia jinsi Azam inavyonyanyasika basi hawatataka kushiriki katika mchezo huu," anasema Hall, ambaye anaongeza fedha ni muhimu kwa maendeleo ya soka.
www.mwanaspoti.co.tz
Subscribe to:
Posts (Atom)
















