Search This Blog

Thursday, June 23, 2011

MAN UNITED YATHIBITSHA KUMSAJILI ASHLEY YOUNG


Klabu ya ligi kuu ya Uingereza Manchester United leo wamethibitisha kumsajili winga Ahley Young kutoka Aston Villa kwa mkataba wa miaka mitano, baada ya kufaulu vipimo vya afya jana jioni.


Young anakuwa mchezaji wapili kuthibitishwa kusajiliwa na Man United bada ya Phil Jones wiki iliyopita.




Karibu O.T YOUNG

HIVI NDIVYO ILIVYOKUA KATIKA FAINALI YA COPA LIBERTADORES.



HAPPY BIRTHDAY ZINEDINE YAZID ZIDANE


Miaka 39 iliyopita siku kama ya leo kaskazini mwa jiji la Marseille- France familia ya Smail na Mallika Zidane walifanikiwa kupata mtoto wao wa tano Zinedine Zidane.

Zidane a.k.a Zizou ni moja ya wachezaji bora kabisa kuwahi kutokea katika historia ya mchezo wa soka duniani, takwimu zinadhihirisha juu ya uwezo wa Zidane.

Alianza kucheza la ushindani akiwa katika klabu ya Cannes kuanzia mwaka 1988-1992 akiwa na miaka 17, na alifanikiwa kucheza mechi 61 na kufunga magoli sita pamoja na kuiwezesha timu hiyo kupata nafasi ya 4 kwenye ligi na kwa mara ya kwanza AS Cannes walifanikiwa kucheza UEFA Cup.

Mwaka 1992-1996 alikuwa akiitumikia klabu ya Bordeaux ambapo aliichezea michezo 139 na kufunga mabao 28.Akiwa pamoja na Bixente Lizarazu na Chistopher Dougary ndani kikosi cha Bordeaux walifanikiwa kuipa timu hiyo ubingwa wa Intorto Cup in 1995 na pia kuwa washindi wa pili wa UEFA Cup.Mambo aliyoyafanya akiwa na timu hiyo yalimvutia kocha wa Blackburn Ray Harford kutaka kumsajili Zizou na Dugarry lakini mmiliki wa Blackburn Jack Walker alimwambia unamtak Zidane w NINI WAKATI TAYARI TUNAYE TIM SHERWOOD?

1996 Zizou alihamia Italy na kibibi kizee cha Turin-Juventus kw uhamisho wa paundi million 3.2.Alifnikiwa kushinda ubingwa wa Serie A 1996-1997, 1996 Intercontinental Cup lakini wakapoteza ubingwa wa ulaya baada ya kufungwa na Dortmund.Baada ya hapo alifanikiwa kushinda makombe mengine ya 1997–98 Serie A, ushindi wa pili wa 1998 UEFA champions league na 2000–01 Serie A.

Mwaka 2001 Real Madrid walimsajili kwa uhamisho wa rekodi ya dunia €75 million.Akiwa Madrid alifanikiwa kucheza michezo 155 na kufunga mabao 37.Pia alifanikiwa kushinda ubingwa wa ulaya mwaka 2001-2002, ubingwa wa La Liga 2003.Mwaka 2006 Zizou aliacha majonzi miongoni mwa wapenda soka baada ya kutangazakustaafu soka.

TAKWIMU ZA MICHEZO YA TIMU YA TAIFA

National TeamYearAppsGoalsAssists
France1994220
1995623
19961224
1997810
19981553
1999611
20001344
2001820
2002912
2003733
2004741
2005521
20061031
Total1083123

MAFANIKIO BINAFSI
ANGALIA MAVITU YA ZIDANE

KALI YA LEO: Wamesusa!

haaaa! haaaaa! hiyo mipira ni idadi ya magoli waliyojifunga.

Timu Fulani hivi iitwayo Stade Olympique L’Emryne ya huko Madagascar ilijifunga jumla ya mabao 149 katika mechi ya ligi dhidi ya mabingwa AS Adema mwaka 2002,hawa jamaa walikuwa wakitia mpira kimiani mwao kila baada ya gozi kuwekwa kati kisa wanabishia maamuzi yaliyofanyika katika mechi iliyopita!

Sasa mlikuja uwanjani kufanya nini!

SANCHEZ AKATAA KUPANDA NDEGE KWENDA KUONGEA NA CITY


Alexis Sanchez ameipiga chini Manchester City baada ya kukataa kupanda ndege kwenda kufanya mazungumzo ya kujiunga na Matajiri wa Premier League kwa dili lenye thamani ya £30 million.

Superstar huyo kutoka Chile ambaye kwa sasa yupo katika kambi ya timu ya taifa inayojiandaa na michuano ya Copa America alipewa ruhusa na klabu yake ya Udinese kwenda jijini Manchester kufanya mazungumzo na City baada ya timu hiyo inayomilikiwa na matajiri wa kiarabu kuwashinda Man United na Barcelona.

Lakini Sanchez baada ya kuambiwa na klabu yake aliwaambia City sio chaguo lake hivyo ajiunge na United au aongee na Barca kujua mipango yao.

Tukio la Sanchez kuikataa City lilitokea katika uwanja wa ndege wa Santiago ambapo waandishi wa habari walikuwa wamekusanyika kuangalia Sanchez akipanda ndege kuelekea England, lakini walikuja kugundua mchezaji amekataa kwenda uwanja wa ndege kuelekea Eastlands.

Sanchez alidhani kuwa anakwenda kuzungumza na mabingwa wa ulaya Barcelona, lakini ofa ya Barca ambayo ilihusishwa kutolewa kwa mchezaji Jeffren ilikataliwa na Udinese ambao waliamua kuichangamkia ofa nzuri ya City.

Kwa sasa usajili wa winga huyo ambaye ameamua kuingilia suala la usajili wake, upo wazi zaidi kwa vilabu vya United na Barca kupigania saini ya mchezaji huyo.

Inasemekana kuwa Barca walikuwa wanataka kutoa £22 million na kutoa mchezaji mmoja kati ya Bjoan Krkicc, Thiago Alcantara na Jeffren ambao wote walikataa kujiunga na Udinese.

Man United ambao wenyewe walitoa ofa ya £27 million cash, sasa wanapewa nafasi kubwa ya kushinda vita ya kumsaini winga huyo kutoka Chile.


Wednesday, June 22, 2011

ON THIS DAY WOZA 2010



Miaka 25 iliyopita siku kama ya leo katika robo fainali ya kombe la dunia 1986 kati ya England vs Argentina, Diego Armando Maradona alifunga bao mkono na mwenyewe alipoulizwa akadai lilikuwa ni bao la mkono wa mungu.Waingereza wakatolewa katika fainali hizo na mpaka leo wananung'unika kuhusu bao la mkono la Diego.









Lakini mwaka jana katika fainali za kombe la dunia lililofanyika Afrika ya Kusini siku kama ya leo ikiwa imepita miaka 24 tangu afunge bao la mkono Diego Maradona alikuwa kwenye benchi la timu ya taifa akiongoza timu ya taifa ya Argentina kuizamisha Greece kwa mabao 2-0.





MDOGO WA MARIGA AKARIBIA KUSAJILIWA CELTIC


Wakala wa kiungo raia wa Kenya Victor Wanyama amethibitisha kuwa klabu ya Celtic ya Uskochi wamekubali kumsajili mchezaji huyo.

Wanyama ambaye ni mdogo wake kiungo wa Inter Milan MacDonald Mariga amekuwa akizivutiwa klabu kadhaa za ulaya, lakini Celtic wanasemekana kuwa karibu na kukamilisha usajili wa mchezaji huyo.

Wanyama mwenye umri miaka 19 kwa sasa anacheza katika klabu ya Ubelgiji Germinal Beerschot, amekuwa akizivutia klabu nyingi kutokana na uwezo mzuri aliouonyesha katika klabu yake. na sasa wakala Ivan Modia amethibitisha kuwa mchezaji huyo anataka kuhamia Scotland.

Wanyama amecheza michezo 11 katika timu ya taifa, na sasa ameshajitengenezea nafasi ya kudumu ndani ya kikosi cha klabu yake, akicheza michezo 30 na akifunga magoli mawili.


HARUNA NIYONZIMA AKABIDHIWA JEZI NAMBA 8.

KIUNGO HARUNA NIYONZIMA 'FABREGAS' ATAWASILI NCHINI HAPO KESHO MISHALE YA SAA KUMI NA MBILI JIONI KWENYE UWANJA WA NDEGE WA MWALIMU JULIUS K NYERERE AKITOKEA NCHINI RWANDA.
KIUNGO HUYO AMEJIUNGA NA YANGA KWA MKATABA WA MIAKA 2 AKITOKEA KLABU YA APR YA NCHINI RWANDA.
.

Haruna NIYONZIMA AKIKABIDHIWA JEZI NAMBA 8 NA MJUMBE WA KAMATI YA MASHINDANO NA USAJILI WA YANGA ABDALLAH BIN KLEYB.





ARUNA NIYONZIMA AKIMWAGA WINO KUJIUNGA RASMI NA YANGA KWA AJILI YA MSIMU UJAO.







MAMBO 10 UNAYOPASWA KUJUA KUHUSU ANDRE VILLAS-BOAS



1:Alizaliwa tarehe 17, 1977 akiitwa Luis Andre Pina Cabral.Anaongea vizuri kabisa lugha ya kiingereza akiwa amefundishwa vizuri lugha hiyo na babu yake.



2: Ameoa na ana watoto wawili, pia Villas-Boas ametoka katika familia yenye historia ya utajiri.



3:Alianza kucheza soka kama kiungo lakini akagundua kuwa hakuwa na uwezo ulijitosheleza kuwa mchezaji wa kucheza mechi za ushindani, Villas-Boas akaamua kujiunga na uhandishi wa habari za michezo lakini akasitisha mpango huo na kuamua kujiunga na mafunzo ya ukocha kupitia Hayati Sir Bobby Robson, rafiki wa bibi yake.Anelezea: "Kipindi Mr.Robson alipokuja Porto kuwa kocha mwaka 1994 alihamia katika jengo letu.Nilikuwa mdogo lakini kwa sababu nilikuwa napenda soka nilienda kwake kumwelezea matamanio yangu.Alipenda jinsi nilivyokuwa na mapenzi na mchezo wa soka hivyo akanisaidia kuweza kuingia katika mafunzo ya ukocha ndani ya chuo cha Lilleshall.Kiukweli nisingeruhusiwa kujiunga pale kwa kuwa sheria zilikuwa haziruhusu vijana wadogo kujiunga na mafunzo.Nilikuwa kocha mdogo kuliko wote pale lakini nilikuwa na nia ya dhati ya kufanikiwa kuwa kocha mzuri."


4: Villas-Boas alikuwa na miaka 21 alipokuwa mkurugenzi wa ufundi wa visiwa vya Virgin nchini Uingereza mwaka 2000, lakini FA walikuwa hawajui.Anasimulia: "Nilikuwa mdogo, lakini hawakutambua.Niliwaambia ukweli kuhusu umri wangu siku ambayo nilikuwa naacha kazi."



5: Kocha Villas-Boas alikuja kuwa kocha msaidizi wa Porto chini ya Jose Mourinho mwaka 2002.Alikuwa ndiye kiongozi wa kitengo cha kuwasoma wapinzani, na baadae wote kwa pamoja na Mourinho wakaamia Chelsea. Mourinho alikuwa akiwaita wasaidizi wake "macho na masikio yake".Alipokuwa Chelsea alipewa jukumu la kuwapa wachezaji DVDs za kuonyesha mchezo wa wapinzani wao kwa kila mechi, akiewalezea wachezaji udhaifu na uimara wa wapinzani wao.

6: Villas-Boas anatajwa kuwa moja ya wasaidizi wa Mourinho waliohusika na ugomvi na Frank Rijkaard mwaka 2005.Andre anasema kuwa alimuona Rijkaard akiongea na refa Frisk kwa mara 3 kipindi cha mapumziko katika mchezo wa kwanza UEFA Champions League february 2005.Mourinho nae alirudia kutoa shutuma hizo za Rijkaard kumshawishi refa kuipendelea Barca hivyo kupelekea kufungiwa kwa Special One katika mechi ya pili dhidi ya Barcelona.



7:Villas-Boas pia alifanya kazi na Mourinho ndani ya Inter Milan, ingawa kwa sasa watu hawa wawili hawaongei kwa sababu ambazo Villas-Boas anazificha lakini anasema: "Tuna itikadi na maono tofauti kuhusu mchezo wa soka.Namuheshimu Mourinho lakini sitaki kufuata mitazamo yake.Nataka kuwa na uhuru wa kufanya kazi nitakavyo bila kujizuia wala kuwa wasiwasi kama anavyofikiria."



8:Villas-Boas aliacha kazi Inter mwezi wa 10, 2009 ili aweze kupata nafasi ya kuwa kocha mkuu kwenye timu ya Academia De Coimbra, iliyokuwa chini ya mkia wa msimamo wa ligi, ikiwa haijashinda mechi yoyote kati ya michezo saba lakini alifanikiwa kuifanya timu hiyo kushika nafasi ya 11 kati ya timu 16 na pia kuingoza kucheza nusu fainali ya kombe la Ureno.Mafanikio haya ndani ya miezi miwili yaliwavutia Sporting Lisbon na wakata kumpa nafasi ya kuwa kocha wao lakini Andre aliamua kurudi Porto.


9: Villas-Boas aliweka rekodi msimu uliopita akiwa Porto, baada ya kuwa ndiyo timu ya kwanza ya bara la ulaya kushinda mara mbili makombe matatu ya kombe la ligi kuu, kombe la FA, na kombe la UEFA cup.Ushindi wa kombe la UEFA cup umemfanya awe kocha umri wa mdogo kuweza kushinda kombe kubwa la barani ulaya.


10: Villas-Boas anapenda kutumia mchezo wa mashambulizi katika mfumo 4-3-3.

KARIBU STAMFORD BRIDGE SPECIAL ONE NO.2

Exclusive interview with Andre Villas-Boas from Chelsea TV.






'MSITARAJIE MAMBO YOTE TOKA KWA MTU MMOJA , TEGEMEENI MAFANIKIO TOKA KWA KUNDI LA WATU WATAKAOFANYA KAZI KWA PAMOJA , WATU WOTE KUWA PAMOJA , MASHABIKI KUWA PAMOJA NA TIMU, WATU KUFURAHI KUTOKANA NA KUWA NA USHIRIKIANO WA PAMOJA NA MAWASILIANO MAPYA NA UONGOZI MPYA ULIOPO. NA HILI NDILO LA MAANA NA LA MSINGI , SIO UJIO WANGU AMBAO UNAJALISHA.


KINACHOJALISHA NI MAFANIKO YA MUENDELEZO YA TIMU HII NA TUJATIBU KUYAREJEA YALE MAZURI AMBAYO TUMEYAFIKIA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA SITA NA YALE TUNAYOWEZA KUYAFIKIA PIA KATIKA MIAKA SITA IJAYO, HAKUNA UBISHI KUWA CHANGAMOTO NILIYO NAYO NI KUENDELEZA USHINDI , NIMEKUWA AINA YA MTU AMBAYE ANA NJAA YA USHINDI NA HILO NITALIENDELEZA HAPA CHELSEA.' -Andre Villas Boas

ASHLEY YOUNG AFANYIWA VIPIMO MAN UNITED


Winga wa Aston Villa Ashley Young ameonekana akiingia katika Hospitali ya Bridgewater jioni kwenda kufanyiwa vipimo vya afya kwa ajili kukamilisha uhamisho wa kuelekea Manchester United.

Winga huyo atatumia muda wa masaa mawili kufanya vipimo hivyo halafu atakwenda kusaini mkataba wa miaka 4 wenye thamani ya paundi 100000 kwa wiki.



Villas Boas atafanikiwa kuzitimiza ndoto za Abramovich?

ANDRE VILLAS BOAS-KOCHA MPYA WA CHELSEA

Hongereni sana Mashabiki wa Chelsea kwa kuajiriwa Andres Villa Boas kama kocha wenu mpya akija kurithi nafasi ya muitaliano Carlo Ancelotti .
Kwa kutazama rekodi ya Andres Villas Boas mashabiki wa Chelsea wana kila sababu ya kuwa na furaha kwa sababu kuu mbili . Nazo ni rekodi ya Villas Boas ambayo ameipata kwa haraka.


Andres Villas Boas ameweza kutwaa kombe La Ligi ya UEFA Europa , kombe la chama cha soka cha Ureno, pamoja na ligi kuu ya nchini Ureno.Hayo yote ameyafanya ndani ya misimu miwili tena akiwa na bajeti ndogo sana ambayo kwa kawaida haitoshi kusaidia timu kufanikiwa katika ulimwengu wa leo . Sababu kuu ya pili ni ukweli kuwa Andres Villas Boas ni mtu ambaye kiukweli anaujua mchezo wa soka na zaidi ya hilo anaifahamu vyema Chelsea kwani aliwahi kukaa kwenye benchi la ufundi la Chelsea chini ya Jose Mourinho hivyo ujio wake hautakuwa wa taabu sana na kuna uwezekano mkubwa kuwa anaweza asihitaji muda sana kuzoea mazingira ya Stamford Bridge pamoja na falsafa na mtindo wa timu ya Chelsea .

Tukitazama upande wa pili hapo ndio kuna utata zaidi . Labda turejee nyuma zaidi na kujiuliza kwanini aliyekuwa kocha wa Chelsea kabla ya ujio wa Villas Boas alifanya nini kibaya hadi kufukuzwa kazi . Carlo Ancelotti ni kocha aliyejijengea jina na heshima kubwa ulimwenguni kote . Heshima aliyonayo Ancelotti ni kutokana na kazi kubwa aliyoifanya akiwa na timu za Juvetus na AC Milan ambapo alitwaa mataji mengi ya ndani na nje ya nchi yake Italia . Kwenye msimu wake wa kwanza nchini England Carlo Ancelotti aliweza kulirejesha taji ambalo Chelsea ililipoteza kwa misimu mitatu taji la ligi kuu ya England , pamoja na hilo alifanikiwa kutwaa taji la kombe la FA.

Kitu ambacho Chelsea ya Roman Abramovich imeona kama kosa la jinai ambalo limemgharimu Ancelotti ajira yake ni kutotwaa taji la Ligi ya mabingwa barani Ulaya ambalo Roman Abramovich analitaka kwa udi na uvumba .Swali la kujiuliza ni moja , kwanini Chelsea imeukosa Ufalme wa ulaya ??? Kunaweza kukawa na majibu mengi kutoka kwa watu wenye mitazamo tofauti lakini nadhani jibu ambalo wote tutakubaliana nalo ni ukweli kwamba Chelsea walipokutana na Manchester United walizidiwa na timu ambayo ilikuwa bora zaidi yao.

Kusema kweli huwezi kujilaumu sana unapofungwa na timu kama Manchester United tena kwa mikwaju ya penalti , na zaidi ya hapo inapokuja ligi ya mabingwa kuna timu ambazo ubora wake huwezi kuufananisha wala kuupima . Mfano mzuri ni jinsi Manchester United walivyosasambuliwa na Barcelona kwenye fainali ya ligi hiyo ya mabingwa tena kwa mara ya pili wakirejea yale waliyoyashuhudia mwaka juzi mjini Rome . Kama Roman Abramovich angekuwa mmiliki wa United ina maana Sir Alex Fergusson angekuwa hana ajira ?

Kabla ya Ancelotti alikuwepo Avram Grant ambaye kama isingelikuwa mvua kubwa iliyonyesha na kumfanya John Terry ateleze na kukosa penati ya muhimu pengine angeendelea kuwa kocha kwani Chelsea walicheza vizuri usiku ule na bahati haikuwa yao kwani United walicheza vizuri mwanzo tu na baada ya hapo Chelsea walikamata usukani na kusawazisha bao la Cristiano Ronaldo mpaka mchezo kufikia hatua ya penati .

Bado kwa Abramovich suala la bahati mbaya halina nafasi na Grant aliondolewa na kazi yake akapewa Felipe Scolari ambaye hakukaa zaidi ya miezi sita , na kabla yake Chelsea waliwahi kuwa na mtu ambaye leo hii dunia nzima inamtambua kama kocha bora kabisa kwenye mchezo wa soka na rekodi yake ni ushahidi tosha juu ya ubora wake Jose Felix Mourinho . Alichokuwa anahitaji Mourinho ni muda na kuungwa mkono kwenye soka la wachezaji na sidhani kama Mourinho angepewa misimu mitano Chelsea angeshindwa kuwafanya wawe mabingwa wa Ulaya . Mbona alifanya hivyo ndani ya misimu miwili tu akiwa Inter ?

Maelezo hayo yote yanaonyesha kuwa tatizo lililopo Chelsea si kwa makocha bali ni mmiliki mwenyewe . Tangu kabla ya mourinho alikuwepo Claudio Ranieri na mpaka leo hii Chelsea imekuwa na makocha sita na katika hao wote zimetumika fedha kiasi cha paundi million 50 kuwaajiri na kuwafukuza tu, jiulize swali moja je fedha hizi angepewa kocha mmoja kununua wachezaji Chelsea ingekuwa wapi?


Tatizo kubwa ni Roman Abramovich , mmiliki asiye mvumilivu ambaye kama angeweza kumpa Mourinho miaka mitano kuna kila ushahidi kwamba si Barcelona , si Real Madrid wala Ac Milan au Manchester United ambao wangesimama mbele ya Chelsea kunako michuano ya ulaya . Makocha wote ambao wamepita Chelsea ukiacha Claudio Ranieri pekee ni washindi na ni watu ambao uwezo wao umedhihirika kwa wapenda soka wote , ni vipi waonekane vimeo Chelsea peke yake ?Jiulize kuwa kama usiku ule uliojaa mvua pale Moscow kwenye benchi la Chelsea kwenye uwanja wa Luzhniki angekuwepo Jose Mourinho na si Avrama Grant je matokeo yangekuwa kama yalivyokuwa kwa United kutawazwa mabingwa wa Ulaya, tazama rekodi ya Mourinho alipokuwa England dhidi ya Alex Fergusson na utapata jibu.


Andres Villas Boas anakuja Chelsea akiwa na heshima kubwa aliyojijengea mapema . Lakini atambue fika kuwa Abramovich ni kinyonga anayebadilika matokeo yanapokuwa mabaya na hatosita kushusha panga kwenye shingo ya kocha pasipo kumpa muda wa kuijenga timu , zaidi ya hapo ni mtu anayependa kuingilia majukumu ya kocha hasa linapokuja suala la usajili wa wachezaji . Kama kwa vikwazo vyote hivyo Andres Villas Boas atafanikiwa kumpa Roman ndoto yake ambayo ni ubingwa wa ulaya atakuwa ameandika ukurasa mpya si tu kwake binafsi kama kocha bali hata kwa makocha wa Chelsea chini ya mrusi Roman Abramovich .


Imeandaliwa na GEOFREY LEA

MICHUANO YA UMISSETA TAIFA : NYANDA ZA JUU YATOA KIPIGO


TIMU ya netiboli ya kanda za nyanda za juu imeweza kuitandika timu ya kanda ya kati kwa mabao 27-18 katika mashindano ya Umoja wa michezo na sanaa kwa shule z sekondari Taanzania (UMISSETA) ngazi ya Taifa kwenye uwanja wa shirika la elimu Kibaha.

Katika mchezo mwingine wa netiboli timu ya kanda ya Dar es Salaam, nayo iliweza kutoka kidedea baada ya kuifunga kanda ya magharibi kwa mabao 37-21, wakati knda ya kaskazini masharini ikiibuka na ushindi baada ya kuitandika kanda ya nyanda za juu kusini kwa mabao 41-18.

Mbali na mchezo huo ulipingwa mchezo mwingine wa kikapu kwa upande wavulana kanda ya ziwa iliweza kuichapa timu ya kanda ya Dar es Salaam kwa vikapu 48-39,huku kanda ya kaskazini magharibi ikaitandika kanda ya magharibi kwa vikapu 20-0 na kanda ya kaskazini mashariki ikiondoka na ushindi kwa kuichapa kanda ya mashariki kwa vikapu 49-48.

Kwa upande wa wasichana mchezo wa kikapu timu ya kanda ya mashariki iliweza kutoka kufua mbele baada ya kuifunga kanda ya kusini kwa vikapu 36-6, huku kanda ya kaskazini mashariki ikitoka na ushindi baada ya kuichpa kanda ya nyanda za juu kusini kwa vikapu 47-27,na kanda ya kaskazini magharibi ikaichapa kanda ya ziwa kwa vikapu 26-18.

Katika mchezo wa soka timu ya wavulana ya kanda ya magharibi iliweza kuichapa timu ya kanda ya ziwa magharibi kwa mabao 3-1, wakati timu ya kanda ya nyanda za juu ikiiibuka na ushindi baada ya kuitandika kanada ya kati kwa bao 2-0.

Katika mchezo wa soka upande wa wasichana timu ya kanda ya mashariki iliweza kuibuka kidedea baada ya kuwachabanga majirani zao timu ya kanda ya kaskazini mashariki kwa bao 2-0.Katika mchezo wa wavu wavulana timu ya kaskazini magharibi iliweza kuifunga kanda ya Zanzibar kwa seti 3-0, huku timu ya kanda ya mashariki nayo iliweza kushinda kwa seti 3-0 dhidi ya kanda ya nyanda za juu kusini.


imetayarishwa na Victor Masangu,Pwani

BREAKING NEWS! ANDRE VILLAS-BOAS KOCHA MPYA WA CHELSEA.



KAGAME CASTLE CUP 2011-FIXTURE

June 25 – July 9, 2011 in Tanzania
Group ‘A’:
[Dar es Salaam]
Simba (Tanzania)
Vital ‘O (Burundi)
Etincelles (Rwanda)
Ocean View Boys (Zanzibar)
Group ‘B’:
[Dar es Salaam]
Young Africans (Tanzania}
El Mereikh (Sudan)
Bunamwaya (Uganda)
Elman (Somalia)
Group ‘C’:
[Morogoro]
APR (Rwanda)
St George (Ethiopia)
Ulinzi Stars (Kenya)
Ports (Djibouti)

(Qualification: Group ‘A’, 1st and 2nd; Group ‘B’, 1st and 2nd; Group ‘C’, 1st and 2nd. Plus overall best two teams from any of the groups, go through to the quarter finals)

FIXTURES:-
Saturday June 25:
1. Etincelles [Rwanda] v Ocean View Boys [Zanzibar], Gp ‘A’, Dar es Salaam, 2pm
2. Simba [Tanzania] v Vital’ O [Burundi], Gp ‘B’, Dar es Salaam, 4pm
3. APR [Rwanda] v Ports [Djibouti], Gp ‘C’, Morogoro, 4pm
Sunday June 26:
4. Young Africans [Tanzania] v El Mereikh [Sudan], Gp ‘B’, Dar es Salaam, 4pm
Monday June 27:
5. Bunamwaya [Uganda] v Elman [Somalia], Gp ‘B’, Dar es Salaam, 4pm
6. Ulinzi Stars [Kenya] v St George [Ethiopia], Gp ‘C’, Morogoro, 4pm
Tuesday June 28:
7. Etincelles v Vital’ O, Gp ‘A’, Dar es Salaam, 2pm
8. Ocean View Boys v Simba, Gp ‘B’ Dar es Salaam, 4pm
Wednesday June 29:
9. El Mereikh v Elman, Gp ‘B’, Dar es Salaam, 2pm
10. Bunamwaya v Young Africans, Gp ‘B’, Dar es Salaam, 4pm
11. Ulinzi Stars v APR, Gp ‘C’, Morogoro, 4pm
Thursday June 30:
12. St George v Ports, Gp ‘C’, Morogoro, 4pm
Friday July 1:
13. Vital’ O v Ocean View Boys, Gp ‘A’, Dar es Salaam, 2pm
14. El Mereikh v Bunamwaya, Gp ‘B’, Dar es Salaam, 4pm
15. Ports v Ulinzi Stars, Gp ‘C’, Morogoro, 2pm
Sat July 2:
16. Etincelles v Simba, Gp ‘A’, Dar es Salaam, 2pm
17. APR v St George, Gp ‘C’, Morogoro, 4pm
18. Elman v Young Africans, Gp ‘B’, Dar es Salaam, 4pm
Sun July 3:
REST DAY
QUARTER FINALS
(All knock-out stage matches at National Stadium, Dar es Salaam)
Mon July 4:
19. B2 v C2* “live” on SuperSport 9
20. A1 v Best Qualifier 1* “live” on SuperSport 9
Tue, July 5:
21. C1 v A2* “live” on SuperSport 9
22. B1 v Best Qualifier 2* “live” on SuperSport 9
SEMI FINALS
Wed July 6:
23. Winner 19 v Winner 20* “live” on SuperSport 9
Thur July 7:
24. Winner 21 v Winner 22* “live” on SuperSport 9
Fri July 8:
REST DAY
Sat July 9:
Bronze medal:
25. Loser 23 v Loser 24* “live” on SuperSport 9
26. FINAL: Winner 23 v Winner 24* “live” on SuperSport 9

KALI YA LEO!!

Kuna mwamuzi mmoja huko Uingereza katika mji mdogo wa Andover alijipa mwenyewe kadi nyekundu baada ya kumchapa makonde mchezaji katikati ya mchezo wa kirafiki. hii ilitokea mwaka 1998.
Hii sasa ndio fair play!







hii nayo kiboko!!!

COUNTDOWN YA KAGAME CASTLE CUP: LUNYAMILA ALIYATEKA MASHINDANO YA MWAKA 1993

Edibily Lunyamila akichanja mbuga

Lunyamila amekuja , yupo kikosini? Hayo ndiyo yalikua maswali toka kwa Waganda pindi timu yoyote iwe ya Taifa au klabu toka Tanzania ilipokua ikienda nchini humo kwenye miaka ya tisini.
Edibily Lunyamila ni mmoja wa wachezaji magwiji wa mashindano haya ya ngazi ya vilabu kwenye ukanda huu wa CECAFA.

yanga waliwacharaza bila huruma SC Villa goli 2-1 katika uwanja wa nakivubo kwenye mechi ya fainali ya kombe lililokuwa na msisimko kipindi hicho la klabu bingwa afrika mashariki na kati na kupelekea serikali ya tanzania kutuma ndege mpaka katika uwanja wa ndege wa entebe kwenda kuwachukua waheshimiwa waliolitoa taifa kimasomaso.
hivyo kuweka adabu kwa waganda ambao hawawezi kuisahau yanga maishani mwao.

Lunyamila akiwa na swahiba wake Mohamed Hussein 'Chinga'

katika mechi hiyo mnamo dakika ya 81 beki mahili wa villa na timu ya taifa ya uganda marehemu Paul Hasule alivua jezi na kutoka nje kwa kile ambacho mwenyewe alikiri kuwa ameshindwa kumkaba winga wa yanga edibily lunyamila, lakini alilazimishwa na kocha wake kumaliza mechi kutokana na aibu iliyokuwa inawakabili.

kutokea hapo waganda walitekwa akili kutokana na kabumbu safi lililoonyeshwa na yanga na kupelekea daladala nyingi nchini humo kuandikwa majina kama "lunyamila trans" "kizota trans" au hata wengine walifuta majina ya salon zao na kuandika "gagarino hair salon" na mpaka leo hii waganda wakisikia timu kutoka tanzania inakwenda huko wanauliza "je ni yanga?".

‘’ Makali yangu kwa Waganda hasa yalianzia Kwenye mchezo wa nusu fainali dhidi ya Express ambapo nilimbuluza sana beki George Ssemogerere na tukafanikiwa kuwafunga mabao 3-1,yaliyofungwa na ‘Chinga’ mawili na ‘ kizota’ baada ya hapo waganda hawakuamini kama nilikua na uwezo wa kumtia njaa kiasi kile Ssemogerere,kwenye mechi ya fainali dhidi ya Villa nahodha wao Paul Hasule ( Marehemu ) alikua na jukumu la kuzuia makali yangu lakini naye alishindwa kwani nilimtesa sana mapaka kuna wakati chenga yangu ilimfanya kukaa chini baada ya kukatika nyonga na huo ndio ulikua mwisho wake wa kucheza soka,tulifanikiwa kuwafunga Villa mabao 2-1 mimi nikifunga bao la pili na la ushindi’’- LUNYAMILA.



HIKI NI KIKOSI CHA YANGA KILICHOCHUKUA UBINGWA MWAKA 1993 JIJINI KAMPALA.

yanga katika mechi hiyo iliwakilishwa na:
1) Steven Nemes/Rifat Said ( Marehemu )
2) Mwanamtwa Kihwelu
3) Keneth Mkapa
4) Willy Mtendamema
5) Issa Athuman ( Marehemu )
6) Method Mogella ( Marehemu )
7) Zamoyoni Mogella
8) Steven Mussa/Hamis Thobias ‘gagarino’ (wote ni Marehemu )
9) Said Mwamba ‘kizota’ ( Marehemu )
10) Mohamed Husein ’Chinga’
11) Edibily Jonas Lunyamila

pia yanga walikuwa na bunduki nje kwenye benchi kama willy martin, rifat said, aboubakar salum "sure boy" david mwakalebela "MP" na wengine wengi ambao walikuwa ni miiba kwa waganda.






TFF KUPELEKWA MAHAKAMANI!

WAKATI timu zinazotarajia kushiriki katika michuano ya Klabu Bingwa afrika Mashariki na Kati zinatarajiwa kuwasili leo, Shirikisho la Kandanda Nchini, TFF bado halijalipa deni la hoteli za Tansoma na Tanso la sh. Milioni 35.
Deni hilo linatokana na TFF kuandaa mashindano ya Chalenji yaliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana na sasa ni miezi saba tokea kumalizika kwa mashindano hayo.
Meneja Mwendeshaji wa hotel ya Tansoma (Paradise Express), Mohamed Hussein alisema kuwa jumla ya timu tatu, Sudan, Rwanda na Ivory Coast zilikaa katika hotel hiyo pamoja na watu wawili walioteuliwa na TFF kwa ajili ya kuzisimamia timu hizo.
Hussein alisema kuwa baada ya kulipa kiasi cha fedha, hotel hilo ambayo ilitoa punguzo la nusu bei kwa kila chumba bila kujali hadhi ya vyumba kwani hata chumba cha dola 135 kiliuzwa kwa dola 60.
“Vyumba vyetu vinaanzia dola 90 kwa chumba kimoja wakati chumba chenye vitanda viwili kinauzwa dola 105 na kile cha ‘suit’ dola 135, kwa vile lengo letu ni kusaidia mashindano kufanyika, vyote tuliuza kwa bei moja, yaani dola 60, hata hivyo hatulipwa mpaka sasa,” alisema Hussein.
Alisema kuwa TFF walitanguliza kulipa dola 25,000 kabla na kubaki dola 14, 629 ambazo wanazisotea mpaka sasa.
Mbali ya deni la hotel ya Tansoma, Hussein alisema kuwa vile vile wanawadai TFF sh. Milioni 13 zikiwa gharama za waamuzi kulala katika hotel yao ya Tanso ya Karikoo iliyokuwa inatumiwa na waamuzi na baadhi ya makocha wa timu.
Alisema kuwa gharama zima ya kulala katika hotel hiyo ni Sh. Million 18.7 TFF ilitanguliza sh. Million 5.6 na tangu walipe kabla ya huduma hiyo kufanyika, mpaka leo hawajalipa.
“Inatuvunja nguvu kibiashara, hatuwezi kuendelea hivyo maana tangu tuanze kufuatilia ni miezi mingi sana sasa, fikiria hii ni biashara gani tunafanya, inatuweka katika hali ngumu,” alisema Hussein.
Alisema kuwa waliwasiliana na Kayuni (Sunday) ambaye wakati huo alikuwa kaimu Katibu Mkuu, lakini mpaka sasa bado mambo magumu pamoja na kupewa majibu ya matumaini.
“Tuliwasiliana na katibu wa sasa, Angetile Osiah, lakini bado mambo ni magumu mbali ya kumpigia Rais wa TFF, Leodegar Tenga ili kupata fedha zetu, bado tukambiwa tusubiri,” alisema.
Alisema kuwa kutokana na hali kuwa mbaya kwetu, tuliwasiliana na wakili wetu, kampuni ya Marando, Mnyele & Co. Advocates na kuwapelekea barua Mei 31huku tukitoa sku saba tulipwe, lakini mpaka sasa kimya.
“Tunafanya mpango wa kuchukua hatua za kisheria, pamoja na kwenda mahakamani, suluhu la suala hili ni kulipwa fedha zetu,” alisema.
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alithibitisha sakata hilo na kusema kuwa watalipa deni hilo bila tatizo.
“Tansoma ni wadau wetu, vile vile tunampango wa kuweka timu hizi kwa ajili ya michuano ya Kagame, tutawalipa, kudaiwa ni jambo la kawaida kwa taasisi yoyote duniani,” alisema Osiah.


Mwandishi:Majuto Omary

Tuesday, June 21, 2011

UZI MPYA WA TOTENHAM HOTSPURS MSIMU UJAO

Picha ambayo mashabiki wengi wa Spurs wanaisubiri kwa hamu, ya Luka Modric akivaa jezi mpya yao msimu ujao na si ile ya Chelsea au Man utd.
Je Gareth Bale na Luka Modric watacheza pamoja next season???