Search This Blog
Wednesday, February 1, 2012
UPANGAJI MATOKEO WAWAPELEKA WACHEZAJI 67 WA ZIMBABWE JELA YA SOKA
Tuesday, January 31, 2012
SIKU YA MWISHO YA USAJILI: USAJILI ULIOKAMILIKA MPAKA SASA
Klabu ya AC Milan imethibitisha imemsajili kwa mkopo Sulley Muntari kwa mkopo kutoka kwa mahasimu wao wakubwa Inter Milan mpaka mwishoni mwa msimu.
- Barcelona wamefikia makubalianao ya kumuachia kiungo wa zamani wa Arsenal Alexander Hleb kutoka katika mkatba aliokuwa nao na klabu hiyo. Hivyo kuanzia sasa Hleb ni mchezaji huru.
MAMA YAKE DROGBA MPISHI WA MASHABIKI IVORY COAST NCHINI GUINEA

YANGA NA ZAMALEK HAWACHEKANI!
WAMISRI KUICHEZESHA STARS FEB 29
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Misri kuchezesha mechi ya kwanza ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za 29 za Kombe la Mataifa ya Afrika kati ya Tanzania na Msumbiji. Waamuzi watakaochezesha mechi hiyo namba 25 itakayochezwa Februari 29 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni Farouk Mohamed atakayekuwa mwamuzi wa kati. Wasaidizi wake ni Ayman Degaish na B.T Abo El Sadat wakati mwamuzi wa akiba ni Ghead Grisha. Kamishna wa mechi hiyo ni Loed Mc Ian wa Afrika Kusini. Mchezo wa marudiano kwa ajili ya fainali hizo zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini utafanyika jijini Maputo baadaye mwaka huu.
NAHODHA TWIGA STARS KUCHEZA UTURUKI

CLOUDS MEDIA GROUP YAIPATIA TWIGA STARS SHILINGI MILIONI MOJA.
Kampuni ya Clouds Media Group imemkabidhi hundi yenye thamani ya Tsh milioni moja ( 1,000,000) mkurugenzi mtendaji wa kampuni Edge Entertainment Ltd bwana Edwin Ngere.
Kampuni hiyo imepewa jukumu na TFF la kukusanya michango ya Twiga Stars.
Shaffih Dauda akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Clouds Media Group Bwana Joseph Kusaga amesema wameamua kutoka kiasi hicho cha pesa ili kiwe kianzio cha kufunguliwa Akaunti maalum ya Twiga Stars ili pesa zinazokusanywa na wadau mbali mbali ziingizwe kwenye iyo akaunti ya Twiga stars.
ZIFAHAMU REKODI ZA FC BARCELONA
**Lionel Messi ndiye mchezaji pekee wa Barcelona kuwahi kushinda tuzo ya Uchezaji bora wa Dunia, Ballon d’Or, Pichichi na Kiatu cha dhahabu katika msimu mmoja. Alifanya hivyo katika msimu wa 2009/10. 



AZAM WAZIDI KUTESA LIGI KUU - WAIADHIBU MORO UNITED CHAMAZI
MCHEZAJI BORA WA DUNIA UPANDE WA WANAWAKE AENDA BARCELONA

Monday, January 30, 2012
MICHEZO MITANO AMBAYO INAWEZA IKAAMUA HATMA YA MANCHESTER CITY MSIMU HUU
Pindi mwezi January utakapoisha hapo kesho, tutakuwa katika kipindi muhimu cha ligi kuu ya England, baada ya kupita kipindi cha Christmas na Mwaka Mpya. 




WOLPER: HUNIAMBII KITU KUHUSU ARSENAL NA YANGA

YANGA IJIFUNZE KUPITIA MCHEZO DHIDI YA ZAMALEK!

Wakati ilipotoka ratiba iliyoonyesha kuwa Yanga watacheza na Zamalek kwenye hatua za awali za michuano ya Ligi ya mabingwa barani afrika watu wengi kwa haraka waliamiani kuwa mwanzo wa mwisho wa yanga umewadia . Ukitazama historia ya timu za Tanzania dhidi ya timu za kaskazini mwa Afrika unapata sababu ya kwanza ya kuona jinsi Yanga walivyo na kazi kubwa ya kufanya lakini ukiangalia rekodi ya Yanga kama klabu katika michezo yao dhidi ya Klabu za Uarabuni hapo ndio kabisa unaona kiza mbele kwani katika mara chache ambazo klabu za Tanzania zimeonyesha kujitutumua mbele ya timu toka Uarabuni Simba ndio imekuwa ikifanya hivyo na si Yanga.
Hii haimaanishi kuwa Yanga wanapaswa kukata tama moja kwa moja kwani ndio hali halisi ya ushindani wa soka mahali kokote pale hata barani ulaya kwa mtu yoyote anayepangwa kucheza na Barcelona anaona kama UEFA imemuonea kwani asilimia 90 ya matarajio ni kipigo .
Kitu kimoja ambacho klabu za Tanzania zimekuwa zikizembea ni kuchukulia changamoto ya kufanya vibaya kama chachu ya kujipanga na kufanya vizuri siku za mbeleni kwa sababu pale unapofungwa haimaanishi kuwa mchezo wa soka ndio umefikia mwisho , mbele kuna michezo mingine ambayo kama kweli umejifunza kupitia makosa ya nyuma lazima utafanya vizuri .
Zamalek ni moja ya timu tano bora za miaka yote barani Afrika , hivi majuzi tu klabu hii imetimiza miaka mia moja na sehemu walikofika inaendana ama unaweza kusema inaakisi umri waliofikia katika miaka yote hiyo kwani klabu hii imewekeza kwenye soka na ndio maani imefika hapa ilikofika.
Kwa ufupi tu Historia ya Zamalek ilianzia mwaka 1911 ambapo mwanasheria raia wa Ubelgiji aliamua kuanzisha timu ya mpira wa miguu aliyoipa jina la Kasr El-Nile Club . Klabu hii wakati ilipoanzishwa ilikuwa na tofauti na klabu nyingine kwani yenyewe haikuwa na matabaka ambayo yangemzuia mtu kujiunga nayo , kwa kifupi ilikuwa klabu ya kila mtu.
Katika historia yake Zamalek imewahi kutwaa mataji 11 ya ubingwa wa Ligi ya Misri pamoja na mataji 11 ya Kombe la Misri au Egyptian Cup. Kwa upande wa mataji ya kimataifa Zamalek imetwaa ubingwa wa klabu bingwa ya Afrika mara tano pamoja na ubingwa wa kombe la washindi barani afrika mara moja huku wakiwa na mataji matatu ya Caf Super cup.
Hata hivyo hali haijawa nzuri sana kwa Zamalek kwenye miaka ya hivi karibuni kwani hawajatwaa ubingwa wa ligi ya Misri kwa miaka saba sasa huu wa 2012 ukiwa wa nane na mara ya mwisho walionja ladha ya ubingwa huo mwaka 2004. Mwezi uliopita tu bodi ya uongozi wa Zamalek ilisitisha kazi ya Hossam Hassan kama kocha baada ya miaka miwili isiyokuwa na mafanikio na nafasi yake ikachukuliwa na gwiji wa klabu hii pamoja na timu ya taifa ya Misri Hassan Shehata ambaye ndiye amepewa jukumu la kumaliza ukame wa Zamalek kwenye soka la nyumbani na la kimataifa.
Msimu huu ulioisha safari ya Zamalek kwenye klabu bingwa ya Afrika iliishia kwenye hatua za awali kabisa mikononi mwa Club Africain ya Tunisia .
Tangu Shehata aingie kwenye benchi la Zamalek hali inaonekana kubadilika na wachezaji wanacheza kwa furaha tofauti na kipindi cha Hossam ambapo klabu hii ilikuwa inaoenekana kukosa muelekeo . Kwenye ligi Zamalek wana rekodi ya kushinda michezo minne kati ya mitano iliyopita wa mwisho ukiwa Alhamis iliyopita ambapo vijana wa Shehata waliifunga El Dakley 2-1.
Shehata amewarudisha washambuliaji mahiri wa timu ya taifa ya Misri ambao kwa muda waliwahi kucheza Zamalek Amr Zaki pamoja na Ahmed Hossam Mido ambao walikuwa barani ulaya kwa vipindi tofauti .Ukiwaacha hao , Zamalek pia inao wakali kama Razak Omotoyosi ambaye anatoka Benin pamoja na mtu ambaye wengi wanamtazama kama mchezaji bora wa misri katika miaka mitano iliyopita lakini hajawahi kupewa nafasi kwenye timu ya taifa Mahmoud El Razak Shikabala .
Hakuna anayeweza kusema kuwa Yanga watafungwa kirahisi na Zamalek kwani huenda rekodi ya mwaka 2003 ikajirudia na Zamalek ikatolewa na timu toka Tanzania lakini kinachobaki kama ukweli kwa Yanga ni kimoja tu kuichukulia michezo miwili dhidi ya Zamalek kama kozi muhimu ya mafunzo ya jinsi ya kuendesha soka kisasa na kuachana na mambo ya kizamani ambayo yanarudisha soka nyuma.
MAXIMO APATA TIMU.

EDO KUMWEMBE
KOCHA wa zamani wa Taifa Stars, Mbrazili Marcio Maximo, hatimaye amepata timu ya Ligi Kuu nchini mwake, baada ya kukabidhiwa kikosi cha E.C Democrata cheye maskani yake Jimbo la Minas Gerais.
Akizungumza na Mwanaspoti kutoka Rio de Janeiro anakoishi, Maximo alisema ameanza kazi ya kuifundisha timu hiyo tangu Novemba 2011 baada ya kumaliza kozi mbalimbali za mwendelezo za ukocha.
Ndiyo, klabu yangu mpya ni E.C Democrata inayoshiriki Ligi Kuu lakini katika Jimbo la Minas Gerais. Hapa Brazil kila jimbo lina ligi yake inayochezwa kwa miezi minne kabla ya kupata timu zinazokwenda kucheza Ligi Kuu ya ujumla, alisema Maximo aliyezaliwa jijini Rio de Jeneiro Aprili 29, 1962.
Niko hapa nafanya kazi na kila kitu kinakwenda safi. Nawatakia kila la kheri Watanzania na kamwe siwezi kuwasahau.
E.C Democrata ilianzishwa mwaka 1932 kufuatia ugomvi wa mashabiki wa klabu ya Flamengo ambapo baadhi yao walienda kuunda timu hiyo.
Inatumia uwanja wa nyumbani wa Mamudao ambao una uwezo wa kuchukua mashabiki 15,000.
Maximo aliteuliwa kuwa kocha wa Taifa Stars Juni 29, 2006 na akaondoka Juni 2010 baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kushindwa kumwongezea mkataba mwingine kutokana na mgawanyiko wa kihisia miongoni mwa mashabiki dhidi ya uwezo wa kocha huyo.
Kocha Zamalek ajiuzulu ghafla
KOCHA wa makipa wa Zamalek itakayocheza na Yanga Februari 18 kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, Ahmed Soliman, amejiuzulu ghafla Jumatatu iliyopita, klabu yake imethibitisha na Yanga wameshtukia dili wakacheka wakidai ni danganya toto.
Soliman, ambaye ni swahiba wa kocha mkuu Hassan Shehata, imeripotiwa kwamba amejiuzulu kutokana na sababu binafsi ingawa kipa namba moja, Abdel Wahed El-Sayed, ameeleza kukerwa na jambo hilo.
Nafasi ya kocha huyo imezibwa na Ayman Taher ambaye ni mchezaji wa zamani wa Zamalek.
Habari zaidi zinasema Soliman ameachia ngazi kutokana na kutoelewana na bodi ya sasa kuhusiana na masilahi yake, lakini amekuwa mzito kuweka mambo hadharani kila anapoulizwa sababu za kuondoka.
Kocha msaidizi wa Yanga, Fred Minziro aliposikia habari za kujiuzulu kwa Soliman alionyesha kushangaa.
Sisi tunakomaa tu na mipango yetu ya ndani ya uwanja kuhakikisha mambo yanakaa sawa wala hatuhangaiki na hao jamaa, wana mbinu nyingi sana na safari hii tutawadhibiti tu, japokuwa najua kuna baadhi ya watu wana wasiwasi, sisi tunajua tunachokifanya ndiyo maana tunajiandaa na kwa kila hali.
Timu bado haijakaa sawa lakini tutapambana, muda uliobaki tukizidi kuwa makini unatosha. Tumewasisitiza wachezaji kwamba huu si wakati wa kufanya mzaha wala uzembe, haya ni maisha yao wafanye kazi na wasikilize kile wanachoambiwa na kukitekeleza.
Tatizo la baadhi ya wachezaji wetu ni wazembe na uwajibikaji ni mdogo ndiyo maana unasikia malalamiko ya hapa na pale na hata timu inapoteza mchezo kutokana na uzembe.
Hivi sasa hatukitaki mambo hayo na sisi makocha tutakuwa wakali. Wachezaji wengine wanajitolea kwa nguvu zote lakini wengine wanaona kawaida tu.
Hakuna mambo mapya na makubwa kiasi hicho kama yanavyokuzwa, hizo fomesheni ni matamshi tu lakini timu inabadilisha staili ya uchezaji kila dakika kutokana na aina ya timu tunayocheza nayo na tunataka nini.
Mambo mengine hayahitaji kocha, yanahitaji akili za kawaida tu na juhudi za mchezaji husika. Ndani ya wiki chache mambo yatakaa vizuri.
Yanga inacheza na JKT Ruvu leo Jumamosi saa 12.00 jioni kwenye Uwanja wa Taifa.
Katika hatua nyingine, kocha msaidizi wa Zamalek, Ismail Youssef, amemlaumu beki Hazem Emam kwa kujibizana na mashabiki waliokuwa wakimzomea mazoezini juzi Alhamisi jioni
UNAMKUMBUKA HUYU ?
SHIBOLI APELEKA MSIBA MANUNGU, AITUNGUA MTIBWA SUGAR.

Timu ya wakata miwa wa Manungu Turiani – Mtibwa Sugar wamendelea kufanya vibaya katika hatua ya pili ya ligi kuu Tanzania bara baada ya kuchapwa na Coastal Union ya Tanga.
Mtibwa Sugar wamepoteza mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa Manungu ukiwa ni mchezo wa pili kwa Mtibwa Sugar kupoteza katika uwanja huo wa Manungu.
Goli hilo la Coastal Union lilifungwa na Mshambuliaji wa Simba aliyopo Coastal kwa mkopo akitokea Kagera Sugar Ahmed Shiboli.
MSIMAMO WA VPL.
Kwenye Mabano Idadi ya Mechi Zilizochezwa.
1. Simba SC (14) 31
2. Yanga (15) 31
3. JKT Oljoro (14) 26
4. Azam FC (14) 26
5. Mtibwa Sugar (15) 22
6. Kagera Sugar (15) 20
7. JKT Ruvu (15) 17
8. Ruvu Shooting (15) 17
9. Moro United (14) 15
10. African Lyon (14) 14
11. Coastal Union (15) 14
12. Toto Africa (15) 13
13. Polisi Dodoma (14) 12
14. Villa Squad
(15) 10
Sunday, January 29, 2012
TWIGA STARS YAITANDIKA NAMIBIA MABAO 5-1
Timu ya Taifa ya Wanawake ya Soka Twiga Stars wamewasambaratisha Namibia kwa jumla ya magoli 7 kwa 2 na sasa wanawangoja kati ya Misri ama Ethiopia ambapo mchezo wa kwanza Misri walishinda goli 4-2.
Katika mchezo wa leo ambapo Twiga Stars wameibuka na ushindi wa goli 5-2 katika uwanja wa Taifa huku wa Namibia wakienda huku wakimkumbuka mshambuliaji alivaa jezi namba 8 Mwanahamisi Omary, kwanamna alivyokuwa wanawaenyesha mabeki wa timu hiyo.
Twiga Stars walianza kuandika goli la kwanza katika dakika ya 22 kupitia kwa Mshambuliaji Hatari na mwenye kasi Mwanahamisi Omar.
Goli hilo halikukaa sana kwani katika dakika ya 30 Albert Dakisi aliisawazishia goli hilo kwa mpira wa kona na yeye kuiunga kwa kichwa na mpira kutinga moja kwa moja nyavuni. Na kupelekea timu kwenda mapumziko wakiwa sare ya goli 1-1.
Katika kipindi Cha pili Mwanahamisi Omari aliyekuwa ana ama kila upande alimpa pasi murua Asha Rashidi katika dakika ya 47, ambapo Asha akufanya ajizi na kuundumbukiza mpira wavuni.
Baada ya goli hilo Namibia walikuja juu huku ukuta wa Twiga ukifanya makosa ya hapa na pale lakini Namibia walishindwa kuyatumia mpaka katika dakika 72, ambapo mpira ulidundishwa chini na mwamunzi ndani ya eneo la hatari ya Twiga stars baada ya Mwanahamisi Omary kuwa chini, wakati Twiga wakitegemea Namibia wangecheza fair play kwa kutoa mpira nnje mambo yalikuwa tofauti, kwani alitoa pasi ya goli huyo mchezaji wa Namibia na kuipatia goli la 2 Namibia.
Mwanahamisi Omari aliendeleza usumbufu wake safari hii akitokea kushoto, upande uliokuwa dhaifu kwa Namibia hii leo, kwa kuwalamba chenga mabeki wa Namibia na Kipa wake lakini mpira wake ulizuiwa na mlinzi na kumkuta Eto'o Mlenzi na kuifungia Twiga goli la 3 katika dakika ya 84.
Goli hilo liliwafanya Twiga kucheza soka safi na dakika ya 88 Asha Rashidi aliipatia Twiga Stars goli la 4 na la 5 likifungwa na Mwanahamisi Omari katika dakika 90 na mchezo kumalizika kwa Twiga kushinda goli 5-2.
Kwa ushindi huo Twiga Stars imeitoa Namibia kwa jumla ya goli 7-2 hivyo wanangoja mshindi kati ya Misri na Ethiopia. Na endapo wakishinda mchezo huo utakao chezwa mei watakuwa wamefuzu kwa mara ya pili mfululizo katika michuano ya 8 ya mataifa ya Africa itakayo fanyika Equaterial Guinea hapo november mwaka huu.























