Search This Blog

Thursday, July 25, 2013

NINI MAONI YAKO WEWE MDAU KUTOKANA NA HIZI '' HEADLINES ''



HATIMAYE PAPISS CISSE AKUBALI KUVAA JEZI ZENYE NEMBO YA MDHAMINI MPYA BAADA YA KUGOMA KWA WIKI KADHAA SASA


PAPISS CISSE amefikia makubaliano na Newcastle kuvaa jezi mpya za klabu hiyo zilizo na nembo ya mdhamini mpya ambaye biashara yake inaenda kinyume na maadili ya imani ya dini ya mchezaji huyo.
Mchezaji huyo mwenye miaka 28 alikataa kuvaa jezi zenye nembo ya kampuni ya mikopo ya Wonga - kwa sababu kampuni hiyo inatoa mikopo yenye riba - kitu ambacho hakiendani na imani ya dini ya kiislamu.

Alijitoa kwenye ziara ya Newcastle ya kujiandaa na msimu mpya baada ya kusema hana mpango wa kuvaa jezi zenye kupromoti kampuni inayotoa mikopo ya riba lakini baada ya mazungumoz ya muda wa wiki kadhaa sasa jambo hilo limepatiwa ufumbuzi.

Cisse amekuwa akifanya mazoezi peke yake wakati wachezaji wenzake wakiwa nchini Ureno kwenye kambi ya pre season, ingawa sasa anategemewa kujiunga nao mara moja.

Mpaka sasa hakuna taarifa yoyote rasmi kutoka Newcastle kuhusu suala hilo.

VIDEO: HUYU NDIO BENARD - MBRAZILI ANAYEWANIA NA ARSENAL, LIVERPOOL NA TOTTENHAM HOTSPUR - NANI KUSHINDA VITA YA SAINI YAKE?


ANGALIA VIDEO NA TAKWIMU ZAKE



TAKWIMU 

PHOTOS: WACHEZAJI WA TAIFA STARS WAKIWASILI KWENYE HOTELI WALIYOFIKIA JIJINI KAMPALA - LEO WAPUMZIKA KESHO MAZOEZI KUJIANDAA KUICHINJA UGANDA

John Bocco akiwasili katika Hotel waliyofikia jijini Kampala

Wachezaji wa Timu Ya Taifa (Taifa Stars) inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager wakiwsili katika hoteli ya Mt. Zion ambapo wamefikia huku wakijiandaa na mechi ya Jumamosi dhidi ya Uganda Cranes kuwania kufuzu mashindano ya CHAN.

Stars leo wamepumzika na kesho watafanya Mazoezi katika Uwanja wa Mandela uliopo Nambole ambapo mechi ya Jumamosi itapigwa.
Erasto Nyoni


Mrisho Ngassa

Nahodha Juma Kaseja

Kevin Yondani

Aggrey Morris

DAVID MOYES; "MAZUNGUMZO YANAENDELEA KATI YETU NA BARCELONA KUHUSU FABREGAS"


DAVID MOYES amethibitisha kwamba Manchester United bado wapo kwenye mazungumzo na Barcelona juu ya usajili wa Cesc Fabregas.

United wameshatuma ofa mbili kwa ajili ya kiungo wa zamani wa Arsenal kwenye dirisha hili la usajili.

Alipoulizwa kama kuna maendeleo yoyote juu ya usajili wa Fabregas, Moyes alijibu: “Mazungumzo ya mtu yanaendelea.”
Moyes pia alitoa taarifa kwamba Robin van Persie anaendelea vizuri na yupo fiti kucheza mechi ya kesho dhidi ya Cerezo Osaka.

Wakati huo huo pia, kocha huyo wa Scotland amesisitiza anataka kuendelea kuwa na makinda yenye vipaji vikubwa Adnan Januzaj na Jesse Lingard kwenye klabu yake kuliko kuwatoa kwa mkopo. 

Moyes alisema: “Wote wawili wamefanya kazi nzuri. Wamezoea vizuri kucheza kikosi cha kwanza na wametoa mchango mkubwa kwenye timu..
“Nina matumaini kwamba tutaweza kuwa nao wote na kuwapa nafasi ya kucheza msimu ujao lakini wote wawili wanahitaji kuendeleza jitihada zao na kuimarisha viwango vyao.”

RONALDINHO AWATHIBITSHIA WABAYA WAKE KWAMBA BADO ANATISHA - AIWEZESHA KLABU YAKE KUWA MABINGWA WA BARA LA AMERIKA YA KUSINI


Kombe la Dunia, Kombe la Mabara, Kombe la Mabingwa wa ulaya, Copa America, Ubingwa wa Serie A na makombe mawili ya La Liga.
Kuna vikombe vichache sana ambavyo Ronaldinho hajashinda bado katika maisha yake ya soka lakini usiku wa jana aliongeza idadi ya makombe makubwa ambayo amewahi kushinda - baada ya kuvaa medali ya kombe la mabingwa wa America ya kusini Copa Liberatadores.


Mbrazili huyo ambaye alijiunga na Atletico Mineiro kiangazi kilichopita na mpaka sasa ameshajishindia tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Brazil - akasaidia klabu yake kushinda ubingwa wa kwanza wa America ya Kusini.

Timu anayochezea Ronaldinho ilifungwa 2-0 katika mechi ya kwanza lakini waliweza kufanya 'comeback' katika mechi ya pili kwa kushinda 2-0 na kusababisha mechi kwenda hatua ya mikwaju ya penati na hatimaye wakashinda 4-2.

Pamoja na kiungo huyo mwenye miaka 33 kushinda makombe mengi na vilabu vyake, pia ana utajiri wa tuzo binafsi akiwa nazo 23 mpaka sasa 

Mshambuliaji alikuwa na wakati mzuri akivichezea vilabu kama FC Barcelona na AC Milan barani ulaya ambapo alishinda navyo ubingwa wa ulaya na makombe ya ndani.

Lakini ubingwa wa Copa Liberatadores ndio kombe kubwa zaidi kwa ngazi ya klabu barani America ya Kusini na kombe hili ni  maalum sana kwa mchezaji huyu bora wa dunia wa zamani 
 
'Hii ndio sababu kwanini nilirudi Brazil,' Ronaldinho alisema. 'Muda mfupi uliopita baadhi yawatu walikuwa wakisema kwamba nimeisha, lakini tumeonyesha hilo jambo sio kweli.'



OFFICIAL: YANGA YAMALIZANA RASMI NA HAMIS KIIZA

Sakata la usajili la mshambuliaji Uganda anayekipiga kwa mabingwa wa ligi kuu ya Tanzania Dar Young African Hamisi Kiiza limefikia tamati rasmi baada ya Yanga na Kiiza kukubaliana kimsingi kuongeza mkataba mpya wa mshambuliaji huyo.

Kwa mujibu wa Hamis Kiiza ambaye nimekutana nae mapema leo ni kwamba anatarajia kusaini mkataba wa miaka miwili kabla hajaondoka kwenda kwao Uganda.
"Tumefikiana na klabu yangu - sasa nitaongeza mkataba na kuendelea kuitumikia klabu ya Yanga msimu ujao. Baada ya kumaliza taratibu zote za kusaini mkataba mpya nitarudi nyumbani Uganda mara moja kabla ya kurudi kuja kujiunga rasmi na wenzangu kwenye pre-season," Kiiza alisema. 

SAKATA LA USAJILI WA SUAREZ: LIVERPOOL YASEMA KWA OFA YA £50M WATAMUUZA SUAREZ - ARSENAL WAGOMA KUONGEZA DAU - MADRID WAKIMNYELEA MTUKUTU SUAREZ


Klabu ya Liverpool imekubali kwamba inaweza kuumuza mshambuliaji wa kiuruguay Luis Suarez endapo tu timu inayomtaka italipa kiasi cha paundi millioni 50 - ambayo ndio thamani ya mshambuliaji huyo kwa mujibu wa Liverpool wenyewe.

Juzi usiku klabu ya Arsenal ilivunja bank na kuamua kutoa ofa ya £40million kwa Liverpool kwa ajili ya kumsaini Luis Suarez lakini majogoo wa jiji wakaipiga chini ofa hiyo na kusisitiza kwamba ikiwa Arsenal wanahitaji saini ya Suarez basi inabidi walipe fedha ambayo ni thamani ya kweli ya mshambuliaji ambayo inatajwa kuwa £50m - kwa mujibu wa kocha wa Liverpool Brendan Rogers.

"Ikiwa Arsenal wanamtaka Suarez, then inabidi walipe fedha ambayo inaendana na thamani ya kweli ya mchezaji."

Lakini huku Rogers akisema hivyo imeripotiwa kwamba Arsenal wanataka mshambuliaji mwenyewe alazimishe kuondoka na kujiunga nao.

Arsenal wanaamini kwamba Suarez ameshaamua kwa dhati kuondoka Anfield ili ajiunge na timu inayocheza soka la ligi ya mabingwa wa ulaya.

Na wanaamini ofa yao ya £40m imefikia fedha ambayo inatakiwa kuvunja mkataba wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 - kitu ambacho kinawapa ruhusa ya kuongea na mchezaji huyo.

Lakini tatizo kubwa kwa Arsenal ni kwamba wanaamini mshambuliaji huyo angependelea zaidi kujiunga na Real Madrid ambayo nayo imeomnyesha nia ya kumhitaji. 

Real Madrid jana walimuuza mshambuliaji wao Gonzalo Higuain kwenda Napoli kwa ada ya uhamisho wa £32 +nyongeza, na hivyo wanaweza kuja kumalizana na Liverpool muda wowote ikiwa wataachana na mpango wa kumsajili Gareth Bale ambaye anaweza kuwagharimu kiasi kisichopungua £70m.

Wednesday, July 24, 2013

VIDEO: BAADA YA KUIONEA KWENYE CHAMPIONS LEAGUE - FC BAYERN MUNICH YAITANDIKA TENA FC BARCELONA KWENYE MECHI YA KUJIANDAA NA MSIMU MPYA

PHOTOS: STARS ILIVYOTUA JIJINI KAMPALA TAYARI KUWAKABILI UGANDA THE CRANES








TAIFA STARS YATUA KAMPALA NA MATUMAINI MAKUBWA

Timu ya Taifa (Taifa Stars) imewasili Uganda jioni hii Jumatano tayari kuikabili Uganda Cranes kwa mechi ya marudiano kutafuta tiketi ya kucheza katika mashindano ya CHAN.
Kikosi hicho chichi nye wachezaji 20, kiliwasili muda mfupi baada ya saa kumi alasiri huku wachezaji na benchi la ufundi wakiwa na matumaini makubwa.
Akiongea mara baada ya kuwasili Kocha wa Timu ya Taifa Kim Poulsen alisema wamejiandaa vizuri wakiwa Mwanza na ana imanikikosi hiki kitabadili matokeo ya awali ambapo Stars ilifungwa 1-0 na Cranes Jijini Dar es Salaam.
Alisema licha ya kuwakosa wachezaji Shomari kapombe na Mwinyi Kazimoto, ana imani na kikosi chake hiki kuwa kitafanya makubwa Kampala.
“Tumekuja kubadilisha mahesabu kwani tumejiandaa vizuri kabisa,” alisema Poulsen.
Wadhamini wa Stars, Kilimanjaro Premium Lager wamewaomba watanzania wasikate tama kwani Stars bado ina nafasi kubwa ya kupindua meza.
“Sisi kama wadhamini bado tuna imani na Stars na tunajua watatuwakilisha vizuri ni vyema watanzania wawe na imani na kuiombea dua timu iibuke na ushindi mnono katika mechi hii ya marudiano,” alisema Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, george Kavishe.
Mechi hii ni gumzo kubwa Jijini Kampala kwani baadhi ya waganda wana hofu kuwa henda wakafungwa nyumbani kwao.
Mechi hii itapigwa katika Uwanja wa Nambole Jijini Kampala JUmamosi hii saa kumi jioni.
Mashindano ya CHAN yanatarajiwa kufanyika Januari mwakani nchini Afrika Kusini.

USHAHIDI WA VIDEO NA PICHA - GONZALO HIGUAIN AKITUA RASMI NCHINI ITALIA NA KULAKIWA NA MAMIA YA WASHABIKI WA NAPOLI

Muda mchache uliopita tuliripoti kwamba mchezaji wa Real Madrid Gonzalo Higuain yupo nchini Italia akifanyiwa vipimo vya afya - sasa tumepata video rasmi inayomuonyesha Higuain akiwasili Italia na akizongwa na mashabiki wa Napoli kwenye uwanja wa Ndege jijini Rome Italia wakati akielekea Napoli kwenda kukamilisha usajili wake wake wa £32M kutoka Real Madrid na kujiunga na klabu hiyo ya Serie A.

PICHA YA SIKU: MARIO BALOTELLI VS ROBERTO MANCINI AU PELLEGRINI VS MICAH RICHARDS

Manuel Pellegrini na Micah Richard leo walikuwa wakitaniana mazoezini asubuhi kwa kusukumana - lakini Balotelli na Mancini walikwazana kweli mazoezini msimu uliopita.

KALI YA LEO: CRISTIANO RONALDO AMVUNJA MKONO SHABIKI KWA SHUTI LA UMBALI WA MITA 35

Ouch: Charlie Silverwood Cristiano Ronaldo

Cristiano Ronaldo alimuacha mtoto mdogo shabiki wa klabu ya  Bournemouth akiwa amevunjika mkono kutokana na shuti lake la mita 35 lilotokana na faulo wakati wa wa mchezo wa Real Madrid dhidi ya timu hiyo inayoshiriki ligi ya daraja la kwanza nchini England. 

Charlie Silverwood, 11, alikuwa mmoja ya washabiki waliobahatika kuwepo kwenye uwanja wa Dean Court kuangalia mechi hiyo - alikuwa amekaa siti ya pembezoni mwa goli la Bournemouth wakati nahodha wa Ureno alipokuwa akipiga faulo ya umbali wa mita 35.  
 
Ronaldo akipiga faulo iliyoenda kusababisha kuvunjika mkono kwa Charlie

Baba yake Charlie aliona hatari ya shuti la Ronaldo na akaweza kulikwepa shuti la Ronaldo, lakini akakutwa na uzito wa shuti hilo kwenye mkono wake, na kuacha kiganja chake kikiwa kimevunja mara mbili.  

Pamoja na maumivu makali, Charlie hakutaka kukosa kumuangalia kipenzi chake Ronnie na akaendelea kuangalia mpira mpaka dakika ya 84 ndio akaelekea hospitali, ambapo ndipo alipofahamu uharibifu uliofanywa na shuti la Ronaldo kwenye mkono wake.

Charlie alipigwa X-ray na akatakiwa kufanyiwa uapasuaji kabla ya mkono wake kuwekwa P.O.P ambalo atakaa nalo kwa wiki sita. 

Lakini kuliko kuacha maumivu yake yasimfanye kuweza kuonana na mastaa kama Gonzalo Higuain, Luka Modric na Mesut Ozil alijikaza na kurudi maeneo ya Dorset, kujaribu kuonana na mastaa wake. 

‘Niliumia sana,’ Charlie aliiambia The Sun. ‘Nimewambia marafiki zangu na hawaamini. Ronaldo ndio mchezaji ghali zaidi duniani - na amenivunja mkono wangu.

‘Niliuona mpira ukinijia mbele yangu, Uliupunyua mwamba na kupita na ulikuwa unakuja kwenye uso wangu - hivyo niliamua kuuzuia na mkono. Baba yangu alikuwa karibu na mie na akaukwepa na hivyo wote ukanikumba mie kwa nguvu zote.


Baada ya mchezo huo klabu ya Bournemouth ilimpa jezi iliyosainiwa na wachezaji wa Real Madrid pamoja na mpira.

BASHIRI GARETH BALE ATAICHEZEA TIMU IPI MSIMU UJAO KATI YA MANCHESTER UTD NA REAL MADRID.

Mdau Daniel Petrosa anauliza kitendawili kifuatacho:
  Manchester united wametuma maombi ya kumsajili Gareth Bale kwa kutoa ofa ya paundi milioni 60,wakati Real Madrid asubuhi ya leo wametuma ofa paundi milioni 65. Manchester united wamepanga kumlipa mshahara wa paundi 230,000 kwa wiki huku Madrid wakiwa tayari kumlipa 200,000 kwa juma,. Je ni klabu ipi itafanikiwa kumshawishi Bale?





MAKALA: IDELFONCE AMLIMA: ALICHUKUA FEDHA ZA USAJILI SIMBA, YANGA, MAJIMAJI KISHAAKAINGIA MITINI NA KURUKA ADHABU YA FAT



Amlima (mwenye tshirt ya kijivu) akiwa na mwandishi wa mtandao huu Elius Kambili


JINA la Idfonce Amlima si geni masikioni mwa wadau wengi wa soka hasa waliokuwa wakifuatilia soka katika miaka ya 1990, huyu ni miongoni mwa wachezaji wachache kutoka mikoa ya kusini mwa Tanzania ambao wamepata mafanikio katika soka.
Amlima aling’ara zaidi miaka ya 1990 akiichezea Bandari Mtwara kisha Yanga.
Amlima aliyezaliwa mwaka 1967 mkoani Lindi, kwa sasa anajishughulisha na kazi ya ukocha katika timu ya vijana chini ya miaka 15 ya mkoa wa Mtwara, lakini bado anamudu kucheza soka ingawa si katika hali ya ushindani.
Kama alivyokuwa katika miaka ya 1990, Amlima wakati nazungumza naye mara nyingi anaonekana akitabasamu huku akitikisa mguu wake na kukumbuka vitu alivyowahi kufanya wakati akicheza soka.
Akicheza katika nafasi ya ushambuliaji, Amlima alimudu kucheza kama kiungo mshambuliaji kuanzia katikati na pembeni katika pande zote mbili, lakini anajivunia zaidi uwezo wa kufunga aliokuwa nao wakati wake.

SAFARI YAKE YA SOKA 

Amlima alianza kucheza soka la kueleweka katika klabu ya Halmashauri ya Lindi mwaka 1985 kisha baada ya miaka minne akajiunga na timu iliyokuwa ikimilikiwa na Mamlaka ya Bandari mkoani Mtwara maarufu kama Bandari Mtwara mwaka 1989.
Amlima aliichezea Bandari hadi mwaka 1994, japokuwa kuna wakati alikuwa akiondoka na kurejea klabuni katika harakati za kuboresha maisha yake.
Wakati anajiunga na Bandari Mtwara, Amlima aliikuta timu hiyo ikiwa daraja la pili lakini kwa kushirikiana na wenzake aliweza kuipandisha hadi daraja la kwanza mwaka 1990.
Ikumbukwe kwamba, wakati huo hakukuwa na Ligi Kuu hivyo daraja la juu katika soka ilikuwa ni daraja la kwanza.

AITWA TIMU YA TAIFA KUTOKA DARAJA LA PILI 

Mwaka 1990 wakati akishiriki Ligi Daraja la Pili Ngazi ya Taifa, Amlima aliitwa katika kikosi cha timu ya taifa sambamba na wachezaji wengine wa timu za daraja la kwanza wakiwemo wakina Hussein Masha.
Hii inaweza kuwa historia kwa Amlima kwani tofauti na sasa ambapo kikosi cha timu ya taifa huitwa vijana ili kupata uzoefu hata kama hawana timu za ligi kuu, Amlima alijiunga na timu akitokea daraja la pili na kupata nafasi moja kwa moja.
“Nakumbuka kocha alikuwa Mzee Masour Magram na Paul West, hawa waliniamini na kunipa nafasi kikosini japokuwa mwanzo sikuamini kama ni mimi nacheza timu ya taifa,” anasema Amlima huku akicheka akionyesha kukumbuka jambo hilo.

‘ASAJILI’ TIMU TATU ZA SIMBA, YANGA NA MAJIMAJI LAKINI AKWEPA ADHABU YA FAT
 

Unaweza ukashangaa lakini ndiyo ukweli wenyewe, Amlima wakati aking’ara na Bandari Mtwara hasa katika ufungaji wa mabao, mwaka 1992 klabu za Simba, Yanga na Majimaji ziliona uwezo wake na kumuwania kumsajili.
Kwa kuwa Amlima alikuwa anahitaji sana fedha, alifanya  makubaliano ya usajili na klabu zote hizo tatu, ambapo Simba na Yanga zote kwa pamoja zilikubali kisha zikamlipa Sh. 1,000,000 (Milioni Moja),ili zimsajili.
“Majimaji niliwaonea huruma kwa ni timu ya kutoka kwetu kusini (Songea), hivyo nikakubaliana nao wanipe Sh. 600,000 (Laki Sita) ili nijiunge nao, nikazichukua hizo fedha, halafu nikakaa kimya,” anasema Amlima.
Amlima anasema alichukua fedha hizo na kuanza kuzitumia lakini ndani ya kichwa chake alijua wazi kwamba hana mpango wa kuchezea hata timu moja katika msimu unaofuata.
“Nakumbuka nilipochukua fedha ya Simba, moja kwa moja nikaenda Kariakoo na kununua bati 60 ambazo hadi leo zinazuia nyumba yangu isiingize maji ndani na hizo nyingine za Yanga na Majimaji nikajihimarisha katika mambo mengine,” anasema Amlima.
Amlima anasema, msimu wa ligi ilipoanza, aliichezea Bandari Mtwara na kuziacha Simba, Yanga na Majimaji katika mataa na hata Chama cha Soka Tanzania (FAT), kilimuhidhinisha kucheza Bandari.
“Hata Simba, Yanga na Majimaji zilipolalamika kuhusu jambo hilo, FAT haikuwasikiliza na mimi nikachezea Bandari kama kawaida,” anasema Amlima.

USIKOSE KUSOMA SEHEMU YA PILI YA MAKALA HII ILI UJUE NI KWA VIPI AMLIMA ALIWAZIDI UJANJA SIMBA, YANGA NA MAJIMAJI     


BREAKING NEWS: GONZALO HIGUAIN NA PEPE REINA WANAFANYIWA VIPIMO VYA AFYA NAPOLI SSC

Inaonekana Arsenal imepoteza nafasi ya kumsajili mshambuliaji wa kiargentina Gonzalo Higuain ambaye imemuwania kwa muda mrefu baada ya mshambuliaji kukaribia kujiunga na klabu ya Napoli ya Italia.

Kwa mujibu wa mtandao wa Sky News ni kwamba hivi sasa nchini Italia mshambuliaji Gonzalo Higuain na kipa wa Liverpool Pepe Reina ambaye nae alihusishwa na Arsenal huko nyuma wapo kwenye vipimo vya afya vya kujiunga na klabu ya Napoli.

Real Madrid na Napoli zimekubalina ada ya uhamisho wa Higuain kuwa kiasi cha £32million na kukubaliana na mchezaji mwenyewe mkataba wa miaka mitano kwa mshahara wa paundi 140,000 kwa wiki.

HATIMAYE JOSEPH OWINO KURUDI MSIMBAZI BAADA YA KURUDI KWENYE KIWANGO CHAKE

Beki wa URA ya Uganda Joseph Owino anategemea kujiunga na timu ya Simba ambayo alikuwa akiichezea misimu mitatu iliyopita kabla ya kujiunga na Azam kutoka Mbagala Jijini Dar-es-salaam.

Beki huyo alirejea kwao Uganda baada ya kupata majeraha na kushindwa kucheza katika timu za Simba na Azam akiwa kwenye kiwango chake kama alivyokuwa akicheza kabla ya kuumia.

Baada ya kurudi Uganda Owino alitibiwa na kupona vizuri kisha kujiunga na URA ambayo amekuwa mpaka sasa. Viongozi wa benchi la ufundi la Simba Kocha Abdallah King Kibaden, msaidizi wake Julio ana meneja Moses Basena wote waliridhishwa na kiwango cha Owino na hivyo kupeleka maombi kwa uongozi kumsajili mchezaji huyo. 

Viongozi wa Simba sasa wapo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha dili hilo na kumrudisha Owino msimbazi, sehemu ambayo aliichezea kwa mafanikio makubwa sana alipojiunga na timu miaka kadhaa iliyopita.

MAKALA: JOSE MOURINHO LAZIMA AMFANYE JUAN MATA KUWA NDIO 'MOYO' WA KIKOSI CHAKE CHA CHELSEA


Jose Mourinho anaweza kuwa ametingwa na tamaa yake ya kutaka kumsajili Wayne Rooney, lakini mreno huyo inabidi kwa haraka ahakikishe kwamba mchezaji bora wa Chelsea msimu uliopita Juan Mata ndio msingi mkuu wa wa Chelsea kwenye msimu wa  Chelsea.
Lakini kwa kushangaza mhispania huyo katika kipindi hiki cha kiangazi hatma yake imekuwa kwenye utata. Pamoja na kuwa na msimu mzuri wa 2012-2013 kwa kushinda Europa League, Mata amekuwa akihusishwa na kutokuwa kwenye mipango ya muda mrefu ya Mourinho.

Kama ilivyoripotiwa na na The Daily Telegraph huko nyuma mwezi June, kiungo huyo alilazimika kukanusha taarifa kwamba ni mtu ambaye yupo tu - yaani wa zaida ndani ya kikosi cha Mourinho.

Mourinho ilibidi azikanushe kwa nguvu taarifa za namna hiyo kabla hata hazijaanza kupata nguvu. Wakati Chelsea wakiwa wametuma ofa rasmi ya millioni 25, na ttarifa za Mata kuongezwa kwenye dili - hatimaye boss huyo wa zamani wa Real Madrid akaongea na kukanusha taarifa hizo.

Huku mwandishi mwandamizi wa The Daily Mail's David Kent akiripoti kwamba Mata ni mtu anayetakiwa na na Arsenal, sasa ni muda muafaka wa Mourinho kumhakikishia mchezaji wake umuhimu wake na namna alivyo na thamani ndani ya klabu hiyo.

Uwekezaji wa Chelsea wa wachezaji vijana uliofanywa hivi karibuni kwa kuongezwa kwa wachezaji kama Andre Schurrle na Marco van Ginkel unathibitisha kwamba huu ni msimu wa kuelekea kwenye mabadiliko. Ni wakati wa kiangazi ambao Mourinho anajenga msingi kwa ajili ya mafanikio ya baadae kwa kujenga kikosi akitakacho.


Mata inabidi katikati ya moyo wa kundi hili. Tangu ajiunge na Chelsea mnamo mwaka 2011, kiungo huyu mbunifu ameendelea kuwa mchezaji muhimu sana katika timu. Msimu uliopita tuliona umuhimu wake kwa Chelsea, alikuwa ndio moyo wa timu iliyoongozwa na Roberto Di Matteo na Rafa Benitez. Ndio daraja la zama mbili za Chelsea; mtu ambaye ataunganisha kikosi cha wachezaji wa zamani na wapya na kuunda kikosi cha mfanikio cha Jose Mourinho.

Kama ilivyooneshwa na Whoscored.com, alikuwa kiungo muhimu wa Chelsea katika mashindano yote msimu uliopita. Mata alifunga mabao 12 na kutoa assists 12 wakati klabu hiyo ikigombania nafasi ya 3 katika premier league. Mabao muhimu kwenye mechi kubwa dhidi ya Tottenham Hotspur, Arsenal, Manchester United na Everton yaliwasaidia Chelsea kukusanya pointi muhimu msimu uliopita.

Pia goli moja la Mata na assits tano alizotoa kwenye mechi nane za Europa League ziliisakisaida kikosi cha Roman Abramovich kushinda ubingwa wake wa kwanza wa Europa League mara baada ya kushinda champions league msimu uliopita. Goli lake na assits mbili katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Steaua Bucharesti uliisadia The Blues kuingia robo fainali kwa ushindi wa jumala wa mabao 3-2. Assist yake kwenye mchezo wa robo fainali pia ukaivusha Chelsea dhidi ya Rubin Kazan lakini kama haikutosha Mata aliifadhi balaa kwenye mchezo uliofuatia.

Mchezaji huyo wa zamani wa Valencia alitoa pas mbili za mwisho katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Benfica katika fainali ya kombe la Europa.

Namna klabu inavyoendelea, umuhimu wake utaendelea kukua. Sio tu kwamba Mata ni muhimu kwenye mapngo wa maendeleo wa klabu bali pia ni mfuasi wa mpango huo, na pia bado hajafikia kiwango chake cha juu kabisa. Mourinho inabidi ampe msingi wa kukiboresha kiwango chake zaidi kwa faida ya timu, akikijenga kikosi chake cha mbele kwa kumzunguka Mhispania huyo.

Wachezaji wengi wanakuja na kupita katika milango ya Stamford Bridge, lakini huku Mourinho akiwa anaingia katika zama zake za pili kama kocha wa Chelsea, ni muhimu kwamba maendeleo ya Mata yawe moja ya vipaumbele vyake vikubwa. Klabu hiyo ya kiingereza ina gwiji wa baadae mikononi mwake.

Tuesday, July 23, 2013

PAMOJA NA KUCHUKUA UBINGWA - BAYERN YAPOTEZWA KWENYE KUINGIZA FEDHA NYINGI NA JUVE KWENYE LIGI YA MABINGWA - MAN UNITED YAONGOZA ENGLAND,


Juventus wanaweza wakawa wametolewa kwenye robo fainali lakini ndio timu iliyopata mapato makubwa kutoka kwenye michuano ya ubingwa wa ulaya msimu uliopita.

Bayern Munich iliwafunga wapinzani wao wa Ujerumani Borussia Dortmund 2-1 katika fainali ya mabingwa wa ulaya katika uwanja wa Wembley mwezi Mei, lakini hakuna yoyote katika timu hizo zilizocheza fainali ambayo imeifikia Juventus kimapato.

Mabingwa wa Italia wameingiza kiasi cha €65.3 million kutoka kwenye ligi ya mabingwa msimu uliopita, €10 million zaidi kuliko Bayern Munich.
Dortmund wamefuatia kwa kutengeneza kiasi cha €54.2 million.
Vilabu 32 vilivyoshiriki katika hatua ya makundi vimegawana kiasi cha €904.6 million, kwa mujibu wa Uefa.
Tofauti kubwa iliyopo baina ya miamba iliyocheza fainali na Juve ilikuwa ni haki za matangazo ya TV, kwa wataliano wa Turin wakiingiza kiasi cha €44.8 million kupitia haki za matangazo ya TV, ukilinganisha na €19.1 million walichoingiza Bayern.

AC Milan, ambao waliweza kuingia raundi ya pili tu, wenyewe waliingiza kiasi cha €51.4 million mbele ya miamba ya Hispania Real Madrid (48.4m) na Barcelona (45.5m) miamba ya Ufaransa  Paris Saint-Germain (44.7m).
Pamoja na kufanya vibaya kwenye michuano hiyo lakini pia timu za England safari hii zimeshuka sana kwenye kuingiza fedha nyingi - mabingwa wa nchi hiyo Manchester United ndio wamewaongoza wenzao kwa kuingiza €35.6 million.
Timu ambayo imeingiza fedha kidogo kabisa ilikuwa ni Dynamo Zagreb waliingiza kiasi cha €10.5 million.

KAMA ILIVYOKUWA KWA KAKA, RONALDO NA MODRIC - GAZETI LA MARCA LARIPOTI KWAMBA BALE ATAJIUNGA RASMI NA REAL MADRID MSIMU HUU

Pamoja na mwenyekiti wa klabu ya Tottenham Danie Levy na kocha Andre Villas-Boas kusema mara kwa mara kwamba Gareth Bale hatouzwa kwenda popote msimu huu - lakini leo hii gazeti la kihispania la Marca kimeripoti kwenye ukurasa wake wa mbele kwamba Gareth Bale ameshakubaliana kimsingi na Real Madrid kuhamia kwenye klabu hiyo.

Marca wameripoti kwamba Real wamempa ofa ya mkataba wa miaka sita Bale na mshahara wa £8.5million kwa mwaka.
 
Marca pia imesema kwamba Bale ameiambia rasmi klabu yake kwamba anataka kwenda Santiago Bernabeu. 

Gazeti hili lenye maskani yake jijini Madrid lina uhusiano wa karibu na klabu ya Real Madrid, na siku zote usajili mkubwa wa klabu hiyo umekuwa ukiripotiwa kwanza na gazeti hilo.

Inaaminika mara tu Marca wanapoandika habari ya Madrid kufanikisha usajili wa mchezaji yoyote na kumuweka kwenye ukurasa mbele wa gazeti hilo basi amini kifuatacho ni kukamilika kwa usajili huo. Ni mara chache sana gazeti hilo huandika habari sio za kweli.

Usajili wa wachezaji kama Luka Modric, Cristiano Ronaldo na  Kaka - wote ulianza kuandikwa kwanza kwenye gazeti la MARCA na mwishowe kweli wachezaji hao walisajiliwa na klabu hiyo
Waliandika kuhusu kusajliwa kwa Modric na kweli ilitokea

Ronaldo pia walimuweka kwenye ukurasa wa mbele na kweli Madrid walivunja rekodi na kumsaini Ronnie

Pia walifanya hivyo kwenye usajili wa Kaka

Je Spurs wataweza kuvunja rekodi ya MARCA kuripoti usajili wa wachezaji na kweli usajili huo ukafanikiwa?Muda utaongea........

BREAKING NEWS! BEKI WA BLACK LEOPARDS VINCENT MABUSELA ATUA NCHINI KUJIUNGA NA SIMBA


Ikiwa zimebakia siku chache kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili kwa vilabu vya ligi kuu nchini,Timu ya Simba imempokea beki raia wa Afrika ya kusini Vincent Mabusela kwa kwa ajili ya kujiunga na timu hiyo kwa msimu ujao.
Beki huyo ambaye anatokea klabu ya Black Leopards ambayo imeshuka  daraja msimu uliopita katika Ligi kuu nchini humo,amepokewa jioni hii katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mjumbe wa Kamati ya utendaji ya Klabu ya Simba Daniel Manembe.

HUYU NDIO KOCHA MPYA WA FC BARCELONA - SOMA WASIFU WAKE NA MAFANIKIO YAKE KAMA KOCHA NA MCHEZAJI

FC Barcelona imefikia makubaliano rasmi kumsaini Gerardo Martino kuwa kocha mkuu wa timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili, kwa mujibu wa mtandao rasmi wa FC Barcelona.
  
Kilichobakia kwenye makubaliano hayo ni kusaini mkataba baada pande zote mbili kukubalina kila kitu.

Ratiba rasmi ya kuwasili kwake Nou Camp, utiaji saini wa mkataba na kutambulishwa rasmi itatangazwa msaa kadha yajayo. 

Gerardo ambaye anajulikana kamaTata’, alizaliwa jijini Rosario (Argentina) November 20, 1962. Ana uzoefu mkubwa wa soka la America ya Kusini, kwanza kama mchezaji na baada kama kocha, kazi yake ya mwisho ilikuwa kuiongoza klabu ya Newell's Old Boys, ambao alishinda nao ubingwa wa mwaka huu.

Gerardo Martino anakuwa kocha wa nne raia wa Argentina kuifundisha FC Barcelona baada ya Roque Olsen, Helenio Herrera na César Luis Menotti.

WASIFU WA KOCHA GERARDO MARTINO TATA