Search This Blog

Wednesday, October 12, 2011

WAMBURA: TFF NDIO WALIOIUA STARS MICHUANO YA AFRIKA


Mgombea nafasi ya uenyekiti katika chama cha soka cha soka mkoani Mara ambaye amewahi kuwa katibu mkuu wa chama cha soka nchini TFF zamani FAT, Michael Wambura amedai kuwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), linapaswa kubeba lawama kutokana na timu ya soka ya Taifa ‘Taifa Stars’ kushindwa kufuzu fainali za Afrika mwaka 2012.


Wambura alisema TFF haiwezi kukwepa lawama kwani baadhi ya viongozi wao wameshindwa kusimamia vyema majukumu ya timu hiyo badala yake nguvu zao wamezielekeza zaidi kwenye Uchaguzi Mkuu wa shirikisho hilo utakaofanyika mwakani.

“Taifa Stars ilikuwa na nafasi nzuri ya kufuzu kabla hata ya mechi ya Algeria Juni mwaka huu
hapa Dar es Salaam, lakini baadhi ya viongozi mambo yao ni uchaguzi wa TFF utakaofanyika
mwakani.

“Hivi sasa mipango mingi ni kuhusu uchaguzi huo, wanajipanga namna ya kudhibiti watu, wanapanga namna ya kumdhibiti Wambura (yeye), huwezi ukaendesha mpira kwa jinsi hiyo.

“Matokeo yake tulishindwa kuifunga Algeria nyumbani tukatoka sare, Jumapili iliyopita bado
tulikuwa na nafasi lakini ugonjwa wetu ukaendelea, badala ya kuelekeza nguvu kuiua Morocco
unasafiri kwenda Mara kuona namna ya kumzuia Wambura asiwanie uongozi Mara.

“TFF wananisikitisha sana, yaani wakisikia Wambura anataka kuwania uongozi
wanachanganyikiwa kabisa, matokeo yake ndiyo hayo Taifa Stars imekwama, Watanzania hatuna haja ya kumlaumu Poulsen (Jan-Kocha Mkuu wa Taifa Stars), sababu zinajulikana wazi,” alisema.

Alieleza kuwa hata kukosekana kwa mchezaji Nizar Khalfan anayecheza soka nchini Canada ni
kutokana na kuchelewa kutumwa taarifa kwa timu yake ya Vancouver Whitecaps, kwa sababu
mawazo ya watu ni uchaguzi wa mwaka 2012.

“Unaweza ukabeza kauli yangu, lakini ukweli ni kuwa hivi sasa kuna chaguzi za vyama vya
mikoa, sasa baadhi ya viongozi wa TFF mawazo yao ni uchaguzi na kuona mikoani wanaenda
watu gani na kama ni wafuasi wao au la, kama sio wao wanawadhibiti na kuweka wao, hii ni hatari,” alisema Wambura.

Wambura amejitosa kuwania uenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mara
(FAM), ambacho awali ilikuwa kifanye uchaguzi Jumamosi ijayo, lakini umesogezwa mbele na TFF hadi mwezi ujao kutokana na kuelezwa kuwa baadhi ya taratibu za uchaguzi hazikufuatwa.


SINA HOFU NA AJIRA YANGU STARS, KAULI ZA MAXIMO HAZINIPI PRESHA - POULSEN


Baada ya kuambiwa kuwa falsafa zake za kufundisha soka hazifai, kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Jan Poulsen amesema hapati shinikizo lolote kutokana na kauli za
aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Mbrazili Marcio Maximo kwamba yuko tayari kurudi kufundisha Stars.

Maximo alinukuliwa na na vyombo vya habari jana akisema yupo tayari kurudi nchini kuifundisha Taifa Stars, kama Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakimhitaji kufanya hivyo.

Akizungumza Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam jana baada ya Stars kurejea ikitokea Morocco ilikofungwa mabao 3-1 Jumapili na kushindwa kufuzu fainali za Afrika mwakani, alisema hasumbuliwi na kauli hiyo kwani bado ana mkataba wa miaka miwili wa kuifundisha Stars.

“Sina presha na alichokisema kocha huyo, zaidi ya yote bado nina mkataba wa miaka miwili wa kuifundisha timu hii na ninachoangalia ni kuiandaa timu kwa ajili ya michuano ya kufuzu fainali za Kombe la Dunia,” alisema Poulsen.

Maximo alikaririwa juzi pamoja na mambo mengine akikosoa utaratibu wa sasa wa kutoinua vijana na badala yake kuita katika timu ya Taifa wachezaji wakongwe kwa sababu tu wanaishi Ughaibuni.

Pia alishangaa kusikia kuwa hivi sasa Mrisho Ngassa anakalishwa benchi katika timu ya Taifa na kuingia baadaye, wakati ni mchezaji mahiri na kusema kuwa kufanya hivyo ni kuua kiwango chake.

Tayari Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema linasubiri ripoti ya kocha huyo ili kujua nini kifanyike kuboresha timu hiyo.

Hata hivyo akizungumza jana kuhusu Stars kushindwa kufuzu fainali hizo, Poulsen alisema, wamefungwa na timu bora yenye wachezaji wengi wanaocheza Ulaya na Ligi Kuu ya England.

Poulsen alisifu kiwango kilichooneshwa na timu yake kwa kudai kuwa wachezaji wake walionesha mchezo mzuri na kujituma muda wote.

Akizungumzia mchezo ujao dhidi ya Chad kuwania kuingia makundi ya mchujo kwa ajili ya michezo ya kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2014, Poulsen alisema atabadilisha kidogo kikosi hicho na kwamba wachache kati ya wachezaji waliopo sasa ndio watakaokosekana.

“Nitawezaje kubadili kikosi chote? Haiwezakani, wengi watakuwepo wachache watakosekana,” alisema Poulsen.

Tuesday, October 11, 2011

DAVID HAYE AASTAFU NDONDI


BONDIA TOKA NCHINI ENGLAND DAVID HAYE ANATARAJIWA KUTANGAZA RASMI UAMUZI WAKE WA KUSTAAFU MCHEZO WA NDONDI .

HAYE ANATARAJIWA KUFANYA HIVYO BAADA YA KUMUARIFU KAMISHNA WA MCHEZO HUO NCHINI KWAKE KUWA HATAENDELEA TENA NA MASUMBWI.

UAMUZI HUU ULIKUWA UNATARAJIWA NA WENGI KWANI HAYE MWENYEWE ALIWAHI KUAHIDI KUWA ASINGEENDELEA NA MCHEZO HUU BAADA YA KUTIMIZA UMRI WA MIAKA 30. HATA HIVYO UAMUZI HUU ULITARAJIWA KUGEUZWA BAADA YA HAYE KUPIGWA NA VLADMIR KLITSCHKO MIEZI MICHACHE ILIYOPITA .

DAVID HAYE AMBAYE ANATIMIZA UMIR WA MIAKA 30 SIKU YA ALHAMIS AMEPIGANA MAPAMBANO YA NDONDI ZA KULIPWA 27 AMBAPO AMEPOTEZA MAWILI .

ANZHI KUTOA OFA YA £200,000 KWA ASHLEY COLE


Baada ya kumfanya Samuel Eto’o kuwa mchezaji tajiri barani Afrika na mchezaji analipwa mshahara mkubwa kuliko mcheza soka yoyote matajiri wapya barani klabu ya Anzhi Makhachkala wanajipanga kuivamia Chelsea na kumsaini Ashley Cole.

The Russian mega-spenders wapo tayari kumpa ofa ya mshahara wa £200,000 kwa wiki Ashley Cole.

Anzhi ambayo inamilikiwa na tajiri wa kirusi Suleyman Kerimov tayri wameshavunja rekodi ya mishahara barani ulaya kumpa Eto’o mkataba ambao unamfanya aweke kibindoni £350,000 kwa wiki.

Sasa Cole, ambaye mkataba wake na Chelsea unakimbilia ukingoni mwishoni mwa msimu ujao ameibuka kama target mpya ya klabu hiyo, na inavyoonekana dili hilo litakuwa majaribu makubwa kwa beki huyo wa kushoto wa England.

Kocha mchezaji wa Anzhi Roberto Carlos ameiambia bodi ya wakurugenzi ya timu hiyo kuwa Ashley ndio mtu anayemuhitaji katika kikosi chake kama mrithi wake.

Mbrazil huyo wambaye alikuwa ndio mchezaji mkubwa wa kwanza tajiri Kerimov kumsajili anatarajiwa kustaafu msimu huu mwishoni.

Carlos tayari ameshawataja wachezaji wengine anaowahitaji kuwa ni Nicolas Anelka, Robin Van Persie na Neymar.

REAL MADRID YAMTAKA CHICHARITO KWA £30 MILLION


Real Madrid wamemuweka mshambuliaji wa kimataifa wa Man United Javier Hernandez Chicharito kama mchezaji namba moja katika listi ya wachezaji wapya wanaotakiwa na klabu hiyo.

The Spanish giants wameweka kiasi cha £30 million kwenye meza kwa ajili mchezaji huyo raia wa Mexico, lakini Boss wa United Sir Alex Ferguson yupo desparate kuhakikisha “Little Pea” anabaki Old Trafford.

United wanataka kumpa mkataba mpya wa miaka 5 ambao utaongeza mshahara wa Chicharito mara 3, kwa sasa anapata kiasi cha £25,000.

Lakini Real watakuwa tayari kumpa mshahara mnono mara 6 ya upatao sasa pamoja na kulipa ada ya uhamisho ambayo itakuwa ni mara 5 zaidi ya Manchester United waliyotoa kumsajili kutoka Chivas miezi 18 iliyopita.

HAPPY BIRTHDAY ABDALLAH KING MPUTA KIBADEN


KWA HABARI ZAIDI KUHUSU SIKU YA KUZALIWA KWA KIBADEN SIKILIZA KIPINDI CHA SPORTS EXTRA KUPITIA CLOUDS FM LEO SAA 3 USIKU.

Nashukuru tumetolewa… Sasa Tuondokane na fikra za kutegemea kufuzu kwa miujiza..


Kwanza ningependa kuwapongeza Taifa Stars kwa kazi nzuri waliyoifanya.Kiwango cha soka cha timu ya taifa kinaonekana kimeongezeka na hiyo inaonekana sana kwenye baadhi ya matokeo ya timu yetu.
Tumetoka kule ambako tangu mechi ya kwanza tunajua ni miujiza pekee itakayoweza kutupeleka kwenye fainali za kombe la mataifa ya bara la Afrika, na sasa tupo pale ambapo katika mechi ya mwisho tunaamini miujiza pekee ndio inayoweza kutupeleka kwenye AFCON.
Huu ni mwaka wa nne au watano ambao tumekwama kwa kutegemea miujiza ya mechi ya mwisho.
Ingawa kama Mtanzania ningefurahi miujiza itupelekee kwenye AFCON, kwa upande mwingine nashukuru kwamba hatukufanikiwa maana naamini hiyo ingetupa mtizamo ambao sio wa ukweli.
Kutolewa kwetu ni changamoto kwa Taifa letu kuachana na kutegemea miujiza itufikishe mbali. Kutokana na hilo inabidi tujijenge kwa kuweka mipango ambayo itatuwezesha kuwa na uwezo wetu binafsi pasipokutegemea miujiza ili kumpa Mtanzania imani ya kwenda CAN au kwenda kwenye fainali za Kombe La Dunia bila kutegemea miujiza ya mwanzoni au mwishoni.
Tukiangalia kalenda yetu ya taifa kwa miaka mitano ijayo
2012 – Tumekosa AFCON
2013 – Tulikuwa na nafasi ndogo ya kwenda CAN kutokana na mfumo wa kuingia
2014 – Tuna nafasi ndogo sana ya kwenda kombe la dunia kutokana na kundi tulilopangiwa.
2015 – Hakuna AFCON
2017 – AFCON ipo
2018 – Kombe la Dunia
Draw ya kufuzu fainali za kombe la dunia mwaka 2014 ilivyotoka tulipiga yowe la ndani,maana tulijua kufika Brazil ilibidi tupitie njia ndefu inayokutana na miamba kama Ivory Coast.
Kama kawaida yetu,wanahabari na wadau walirudia tena kusema “huwezi jua, mpira ni wa duara na unadunda kwa hiyo lolote linaweza kutokea na tukapita”. Hapo tunarudia tena kusubiria miujiza kabla hata ya kucheza mechi yetu ya kwanza.
Kwa imani yangu kutokana na mpira wetu ulivyo kwa sasa mashindano ya karibu ambayo tunaweza kuondokana na mategemeo ya kufuzu kwa miujiza ni yale ya CAN 2017 huko Libya lakini ambayo ni ya uhakika zaidi ni fainali za kufuzu AFCON 2019 na kama ni kufuzu fainali za kombe la dunia ni za mwaka 2022.
Tuna kama miaka 5 ya kujiandaa kwenda Libya bila kutegemea miujiza. Kwa hiyo la maana kabla ya yote ni kwa taifa kukubali kwamba tusijipe imani ya kucheza mashindano yoyote makubwa kwa miaka 5 ijayo.
Kutimiza hayo inabidi tufanye maamuzi magumu sana kwa siku hizi za mbeleni. Maamuzi magumu yanalipa lakini yanahitaji uvumilivu, na uvumilivu uanze kwa yule shabiki wa kawaida wa mpira mpaka kwa wale wanaotuwezesha kwa hali na mali.
Kwanza ninawashukuru wachezaji wa sasa wa Timu ya taifa, sanasana wale waliotupa miaka yao mingi sana kulitumikia taifa letu. Jasho lenu na nguvu yenu tumezitambua na mmetusogeza mbele hilo tunalitambua.
Lakini Ukweli ni kwamba ukiangalia kiwango kilichooneshwa kwenye mchezo dhidi ya Morocco utangundua , kiwango chetu kilikuwa chini sana kulinganisha na cha wenzetu Moroccou,Pale ndipo uwezo wetu ulipokomea.
Ili kulenga huo mwaka 2017, inabidi tuistaafishe timu yetu ya sasa Inabidi pia tuwashukuru na kuwaaga wachezaji wasasa wa Taifa Stars. Tuunde timu mpya ya vijana (U-23) timu ambayo itashiriki katika mashindano ya kufuzu World Cup 2014 na CAN 2013.
Hivyo basi naamini si timu itakayotupeleka CAN kwa uwezo wao lakini ni timu itayojenga misingi ili sasa wale wa chini yao tuwakuze na kuwalea ili kuhakikisha wanafikia kwenye level ya kutupeleka tunapotaka kwa miaka mingine mingi ijayo.
Hatuna jinsi inabidi tuanzie chini kabisa, tujenge mfumo mpya wa kucheza soka ikiwa ni pamoja na mfumo wa kuibua vipaji na kutengeneza vijana wapya hasa timu timu yetu ya U-17, tujenge na kuimarisha mashindano ya soka la watoto, kuanzia mashuleni sana sana ( Hii ni topic tofauti na ina muda wake ).
La maana sana ni kwanza tukubaliane kufanya maamuzi magumu ya kutoa kabisa tegemeo la kwenda South Africa 2013 au Brazil 2014. Tukikubaliana hilo inamaanisha taifa litakuwa tayari kutekeleza mikakati ya kujenga mpira wetu kuanzia chini.

MAXIMO APONDA FALSAFA ZA POULSEN, BADO ANAIPENDA TZ


Kocha Mkuu wa zamani wa timu ya Taifa, Taifa Stars, Marcio Maximo, yupo tayari kurejea Tanzania, kuifundisha timu hiyo iwapo atatakiwa na uongozi wa juu wa nchi.

“Mimi sina tatizo na kama Rais Kikwete (Jakaya) au Pinda (Waziri Mkuu Mizengo), watasema nirudi, nitafanya hivyo bila matatizo kwani ninaipenda Tanzania na nilishiriki kikamilifu kuiunda timu ya Taifa,” alisema Maximo Jumamosi.

Akizungumza wakati wa mkutano wake na ujumbe wa Waziri Mkuu unaofanya ziara nchini hapa, Maximo alisema ingawa anafanya mazungumzo na timu ya hapa ambayo hakutaka kuitaja, lakini mapenzi yake makubwa yako kwa Taifa Stars.

“Najua Tenga (Leodegar-Rais wa TFF), hana uwezo wa kuniita kwa sasa kwa sababu ana mkataba na kocha mwingine (Jan Poulsen), lakini kama Kikwete au Pinda watasema, bila shaka nitatekeleza,” alisema Maximo huku akijawa na furaha kubwa kukutana na Watanzania jijini hapa.

Hata hivyo, alikosoa utaratibu wa sasa wa kutoinua vijana na badala yake kuita katika timu ya Taifa wachezaji wakongwe kwa sababu tu wanaishi Ughaibuni.

“Angalia hivi sasa mnaacha wachezaji vijana ambao wanahitaji kunyanyuliwa na badala yake mnaingiza wachezaji wenye umri mkubwa (anatoa mfano) ambao wana miaka miwili tu ya kucheza soka,” alisema kocha huyo.

Alishangaa kusikia kuwa hivi sasa Mrisho Ngassa anakalishwa benchi katika timu ya Taifa na kuingia baadaye, wakati ni mchezaji mahiri na kusema kuwa kufanya hivyo ni kuua kiwango chake.

“Tunapaswa kuangalia uwezo wa vijana wadogo na kuwainua, angalia mimi ndiye niliyemuibua Mbwana Samatta na kumuingiza Taifa Stars… angalia sasa, anacheza soka la kulipwa nje ya nchi, hayo ni matunda ya kuibua vijana,” alitamba.

Alisema si vibaya kubadilisha wachezaji, lakini ni mbaya kukiuka filosofia ya soka, ambayo inataka soka kuanzia kwa vijana wadogo na kuwakuza kivipaji.

ZANZIBAR NA NDOTO ZA KUSHIRIKI CHAN

Kikiwa bado na ndoto za kupata uanachama wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), kimeomba kushiriki michuano ya Mataifa ya Afrika kwa nyota wa ndani (CHAN).

Akizungumza jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, msemaji wa ZFA, Munir Zakaria, alisema mbali ya kuomba ushiriki huo CAF, pia wametuma maombi ya ushiriki wa michuano ya Nile Basin inayoandaliwa na Chama cha Soka cha Misri.

Zakaria alisema licha ya fainali za Mataifa ya Afrika (CAN), Tanzania kuwa ni moja, lakini wameamua kuomba CHAN kwa kuwa ni michuano ya ndani.

“Tumemtuma Tenga (Rais wa TFF), kuwasilisha maombi yetu CAF na tunasubiri atupe majibu,” alisema msemaji huyo.

Michuano ya CHAN uhuhusisha nyota wanaocheza ligi za ndani tu ambapo Tanzania ‘Taifa Stars’ ilifanikiwa kufuzu fainali za kwanza zilizofanyika nchini Ivory Coast.

Kuhusiana na Nile Basin, Zakaria alisema wamevutiwa na unono wa zawadi katika michuano hiyo hivyo kuamua kuomba kushiriki baada ya kuchelewa kufanya hivyo mwaka jana.

T.F.F YAOGOPA KUMTIMUA KAZI POULSEN


Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF), limesema haliwezi kumfukuza kazi Kocha Mkuu wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’, Jan Poulsen baada ya kikosi hicho kutolewa kwenye michuano ya kufuzu fainali za Afrika mwakani, kwani ni gharama kubwa kufanya hivyo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema wameyakubali matokeo ya kutolewa kwa Stars na kikubwa sasa wanasubiri ripoti ya kocha huyo.

“TFF tunasema wazi kwamba tumekubali matokeo yote ya uwanjani na kikubwa sasa tunasubiri ripoti ya benchi la ufundi likiongozwa na kocha kwa ajili ya kuangalia nini cha kuifanyia timu yetu,” alisema.

Angetile alisema wataipitia ripoti ya kocha huyo na kuangalia kipi ambacho amekieleza na wao kama TFF kwa kupitia Kamati ya Ufundi watakaa na kujadiliana na nini kifanyike.

“TFF haiwezi kusema inamfukuza kocha kwa sababu tumeshindwa kufuzu, tunachosubiria ni ripoti yake baada ya michuano hiyo.

“Tutaangalia nini tulichokubaliana naye kwenye mkataba na kipi kimefanyika na nini ambacho hakijafanyika na kwa sababu zipi.

“Ripoti hiyo ndiyo itakayotoa mwanga na ni jambo la kawaida kwa mwalimu kutoa ripoti yake kila baada ya michuano.

Katika ripoti hiyo, kocha ataainisha kile alichokiona na mipango yake, kwani pengine sisi TFF ndiyo tulioshindwa kutimiza baadhi ya vipengele na kusababisha timu kufanya vibaya.

“Hivyo baada ya ripoti yake tutajua nini cha kufanya, lakini kwa sasa hatuwezi kusema tutamfukuza kocha, kwani kukatisha mkataba ni gharama kubwa,” alisema Angetile.

Wadau mbalimbali nchini wamekuwa wakihoji uwezo wa kocha huyo, huku wakitoa maoni kwamba TFF ikatishe mkataba wake.

Monday, October 10, 2011

MOROCCO VS TANZANIA HIGHLITES



MATCH REPORT: MOROCCO 3-1 TANZANIA

Wenyeji Morocco ndiyo walioanza kupata bao dakika ya 19 mfungaji akiwa Marouane Chamakh kwa mpira wa kichwa ambao ulidunda kabla ya kumpita kipa Juma Kaseja wa Taifa Stars. Abdi Kassim aliisawazishia Stars dakika ya 40 kwa shuti la nguvu- umbali wa meta 35 lililomshinda kipa Nadir Lamyaghri kufuatia pasi ya Idrisa Rajab.

Mabao mengine ya Morocco ambayo imepata tiketi ya kucheza fainali za AFCON zitakazochezwa mwakani katika nchi za Equatorial Guinea na Gabon yalifungwa dakika ya 68 na Adel Taarabt. Mbark alifuta matumaini ya Stars kupata sare katika mechi hiyo kwa bao lake la tatu alilifunga dakika ya 90 kwa shuti la chini akiwa ndani ya eneo la hatari.
Mwamuzi Bakary Gassema kutoka Gambia aliwaonya kwa kadi za njano Idrisa Rajab, Juma Nyoso, Dan Mrwanda na Mohamed Rajab wa Stars wakati kwa upande wa Morocoo aliyeoneshwa kadi ya njano alikuwa nahodha wa timu hiyo Houcine Kharja.

Akizungumza baada ya pambano hilo, Kocha wa Taifa Stars, Jan Poulsen aliwataka wachezaji wake wasikate tamaa kutokana na matokeo hayo kwa vile walicheza na timu bora kuliko wao. Alisema hivi sasa wanatakiwa kuelekeza akili kwenye mechi mbili zilizo mbele yao dhidi ya Chad. Mechi hizo za mchujo kwa ajili ya kuingia hatua ya makundi ya mchujo Kanda ya Afrika kwa ajili ya fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Brazil mwaka 2014 zitachezwa Novemba 11 mwaka huu jijini Ndjamena na Novemba 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Stars; Juma Kaseja, Erasto Nyoni/Nassoro Cholo, Idrisa Rajab, Juma Nyoso, Aggrey Morris, Shabani Nditi, Dan Mrwanda, Henry Joseph, Mbwana Samata/John Bocco, Abdi Kassim na Mohamed Rajab/Mrisho Ngasa.

Morocco; Nadir Lamyaghri, Michael Basser, Abdelhamid El Kaoutari, Badri El Kaddouri, Mehdi Benatia, Younes Belhanda, Houcine Kharja, Mbark Boussoufa, Adel Taarabt/Youssef El Arabi, Marouane Chamakh/Said Fettah na Oussama Assaidi/Karim Al Ahmadi.

Taifa Stars inatarajiwa kurejea Dar es Salaam saa 2.30 asubuhi Oktoba 11 mwaka huu kwa ndege ya Qatar Airways.

MTIBWA WAPIGISHWA KWATA NA JKT RUVU


JKT Ruvu imeichapa Mtibwa Sugar mabao 3-2 katika mechi ya Ligi Kuu ya Tanzania iliyochezwa kwenye uwanja wa Azam, Chamazi jijini Dar es Salaam.Kwa ushindi huo klabu ya JKT Ruvu imefikisha pointi 15 kama ilizonazo klabu za Mtibwa Sugar na Azam.

Mtibwa ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya tisa lililofungwa na Vicent Barnabas aliyeunganisha krosi ya Issa Rashid.JKT Ruvu walisawazisha bao hilo katika dakika yabaada ya Mtibwa kujifunga wenyewe wakizembea kuondoa mpira wa kona.

JKT Ruvu pia waliongeza bao la pili kupitia kwa Rajab Chau aliyepokea mpira wa faulo ndogo uliopigwa na Emmanuel Linjechele.Timu hizo mpaka zinaenda mapumziko JKT Ruvu ilikuwa ikiongoza kwa mabao 2-1, lakini katika kipindi cha kwanza timu zote zilicheza kwa kushambuliana.

Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko ya wachezaji, lakini mabadilko hayo yalionekana kuwasaidia zaidi JKT Ruvu kwa sababu walipata penati katika dakika ya 85 ambayo ilifungwa na Stanley Nkomola na kuandika bao la tatu.

Penati hiyo ilipatikana baada ya Hussein Bunu kudondoshwa na Salvatory Ntebe katika eneo la hatari na mwamuzi Amon Paul wa Mara aliamuru ipigwe penati.Slavatory Ntebe aliipatia Mtibwa bao la pili katika dakika ya 89 baada ya kupiga shuti kali lililomshinda kipa wa JKT, Hamis Seif.

Ligi Kuu itaendelea tena Oktoba 14 kwa Yanga kucheza na Kagera Sugar, halafu Oktoba 15 JKT Ruvu itacheza na Azam, pia Oktoba 16 Simba itacheza na African Lyon.

VIGOGO WATUPWA NJE KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA 2012

GROUP A

TeamPldWDLGFGAGDPts
Mali631296+310
Cape Verde631277010
Zimbabwe622275+28
Liberia6123712−55

Group B

TeamPldWDLGFGAGDPts
Guinea6420135+814
Nigeria6321125+711
Ethiopia6213813−57
Madagascar6015414−101

Group C

TeamPldWDLGFGAGDPts
Zambia6411112+913
Libya633061+512
Mozambique621346−27
Comoros6015214−121

Group D

TeamPldWDLGFGAGDPts
Morocco632182+611
Central African Republic62225508
Algeria622258−38
Tanzania612369−35

Group E

TeamPldWDLGFGAGDPts
Senegal6510162+1416
Cameroon6321125+711
Congo DR62131011−17
Mauritius6006222−200

Group F

TeamPldWDLGFGAGDPts
Burkina Faso4310123+910
Gambia411256−14
Namibia4103311−83

Mauritania ilijitoa kwenye 2012 AFCON Qualification kabla ya mechi yoyote kuchezwa kwenye kundi hili.

Group G

TeamPldWDLGFGAGDPts
Niger630368–29
South Africa623142+29
Sierra Leone62315509
Egypt61235505

Group H

TeamPldWDLGFGAGDPts
Côte d'Ivoire6600194+1518
Rwanda6204515−106
Burundi612379−25
Benin6123811−35

Group I

TeamPldWDLGFGAGDPts
Ghana6510131+1216
Sudan641183+513
Congo6204510−56
Swaziland6006214−120

Group J

TeamPldWDLGFGAGDPts
Angola640275+212
Uganda632162+411
Kenya62224408
Guinea-Bissau610528−63

Group K

TeamPldWDLGFGAGDPts
Botswana852173+417
Tunisia8422146+814
Malawi8260138+512
Togo8134610−46
Chad8035720−133

BEST LOSERS GROUP

GrpTeamPldWDLGFGAGDPts
C Libya422020+28
I Sudan421132+17
A Cape Verde421134–17
B Nigeria412185+35
G South Africa412132+15
J Uganda412132+15
E Cameroon41214405
D Central African Republic41212205
F Gambia411256–14
H Rwanda4103412–83

[edit]