Search This Blog

Monday, August 29, 2011

BARCLAYS PREMIER LEAGUE KWENYE NAMBA


0 – Swansea City ndio timu pekee ambayo bado haijafunga bao kwenye EPL msimu huu.The Swans wametoka sare ya 0-0 dhidi ya Sunderland na Wigan Athletic baada ya kupokea kichapo cha 4-0 kutoka kwa Manchester City katika wiki ya ufunguzi.

3 – Ashley Young na Samir Nasri wote wameshatoa assist 3 katika mechi zao walizocheza kwenye EPL Jumapili.Ni mchezaji mmoja alifanikiwa kufanya hivyo msimu uliopita.

3.33 – Baada ya kufungwa 8-2 na United, Arsenal sasa wamefungwa wastani wa 3.33 wa magoli kwa kila mchezo ndani ya EPL msimu huu.

6 – Jumla ya magoli yaliyofungwa na Edin Dzeko katika Epl, akiwa ndio top scorer.

21 – Kufungwa kwao 0-1 na Everton, Blackburn Rovers walipata attempts on goal 21.

34 – Ilimchukua dakika 34 akitokea benchi Juan Mata kufunga bao katika mchezo wake wa kwanza, Chelsea wakishinda 3-1 dhidi ya Norwich.

115 – Mara ya mwisho Arsenal kuruhusu wavu kutikisika mara nane ilikuwa miaka 115 iliyopita, baada ya kufungwa na Loughborough Town in 1896.

ETO'O AIFUNGIA ANZHI KWENYE MECHI YA KWANZA.






Afunga bao la kwanza kwenye mechi yake ya kwanza...... MONEY WELL SPENT !!!






Aanza mazoezi mara tu baada ya kutua nchini Urusi....... HAKUNA KULALA!!






Hapa alipotua nchini Urusi......

Manchester United 8-2 Arsenal: Kipigo kizito kuliko vyote kwa Wenger kwenye maisha yake ya ukocha.

Timu zilizoanza.
Hakika ulikuwa mchezo wa kushangaza kwa matokeo yalitokea hadi mwisho .
Sir Alex Fergusson alianza na kikosi kile kile ambacho kiliwafunga Tottenham siku ya jumatatu na Danny Welbeck aliendelea kupangwa mbele akiwa na Wayne Rooney.
Arsene Wenger aliwakosa ThomasVermaelen na Bacary Sagna na ukiongeza wachezaji wanaokosekana kwa majeruhi na kufungiwa, hii ilimaanisha kuwa Carl Jekinson alicheza kama beki wa kulia na Johan Djorou alicheza kati na Francis Coquelin alipata nafasi ya kucheza mechi yake ya kwanza akianzia kwenye nafasi ya kiungo.
Mchezo huu ulikuwa kama wa kujifurahisha kwa Man United kwa jinsi walivyokuwa wanatengeneza nafasi na kuutawala. Arsenal walikuwa wameharibika toka mwanzo hadi mwisho huku wakishindwa kutumia wingi waliokuwa nao katikati mwa uwanja ambako walikuwa wamejaza wachezaji wengi kuliko United na pia walionekana kukosa mpangilio kwenye safu ya ulinzi.

Ulinzi/Beki

Unaanzia wapi kuchambua safu mbovu ya ulinzi ya Arsenal? Ni vigumu sana kutazama ubao wa matokeo unaoonyesha mabao 8-2 na kuanza kueleza sehemu moja baada ya nyingine yenye matatizo yaliyosababisha kipigi kama hicho kwa ‘Ze Ganaz’.
Walikuwa hovyo sana kiasi kwamba unaweza kufikiria hawakuwa wamejiaandaa kwa ajili ya kushindana , na utakuwa sahihi ukifikiri kuwa shida ya Arsenal haipo kwenye mbinu za mchezo bali zinaanzia mbali sana zaidi ya uwanjani ambako jumapili ya tarehe 28 /8/ 2011 wamefungwa mabao 8.

Hiyo siyo kusema kuwa hakuna matatizo ya kiufundi ,kwa kuanza tu , Arsenal walikosa umoja hasa pale ambako walikuwa hawana mpira . Baadhi ya wachezaji walionekana wanafanya vyema kazi ya ‘pressing’ yaani kumsukuma adui lakini wengine ni kama walikuwa wamesimama tu . Ulikuwa mchezo mkubwa na mgumu sana kwa kijana mdogo Coquelin ambaye alicheza kama kiungo wa chini akiwa na jukumu la kumkaba “ng’ombe pori” Wayne Rooney.

Cha kushangaza ni kwamba pamoja na kwamba Wayne Rooney alifunga ‘hat-trick’ Coquelin alifanya kazi yake vizuri. Kazi hii nzuri inatokana na ukweli kuwa ‘influence’ ya Wayne Rooney kwenye kipindi cha kwanza ilikuwa ndogo hasa kwenye jukumu la Rooney la kuufungua mchezo kwa wenzake.

Na kingine ni kwamba mabao yote ya Rooney yalitokana na mipira iliyokufa na si kwenye ‘open play’. Uamuzi wa Wenger kumtoa Coquelin wakati Arsenal wakiwa nyuma kwa 3-1 kwenye dakika ya 61 ulionekana kuwa na matokeo mabaya sana kwa Arsenal.
Hilo ndilo jambo pekee ambalo lilienda sawa kwa Arsenal. Tatizo la kushindwa kufanya ‘pressing’ ya maana lilimaanisha kuwa Arsenal walikuwa hawafanyi presha yoyote kwenye mpira hasa kwenye ‘midfield’ pamoja na kwamba walikuwa na mchezaji ( Coquelin) ambaye alikuwa amekaa kwenye ‘midfield’, kwa sababu Aaron Ramsay na Tomas Rosicky wangeweza kumkaba Anderson pamoja na Tom Cleverly.

Hili lilishindikana na Viungo hawa wawili wa United walikuwa wanamiliki mpira watakavyo na walikuwa wakipiga pasi wapendavyo.

Tatizo la pili lilikuwa kwenye mstari wa juu wa ‘defense’ ambao Arsenal walikuwa wanatumia kujilinda , kwa kawaida kukaba kwa mstari huu ni kama kujipiga risasi au kunywa sumu hasa pale inapokosekana presha ya kutosha kwenye mpira – lakini kikubwa ni jinsi wachezaji wanne wa safu ya ‘defense’ ya Arsenal walivyokosa umoja baina yao.


Wachezaji wawili mara zote walisogea juu na wengine wawili walibaki.
Wakati mwingine ilikuwa Ajabu jinsi United walivyopenya kwa urahisi na kufunga – bao la Nani ni mfano mzuri.


Nyakati Nyingine Arsenal wangemuacha beki mmoja akiwa amenasa nyuma ya wenzake na kulazimika kufanya ‘tackling’ ya mtu wa mwisho –Mchezaji aliyetolewa kwa kadi nyekundu Carl Jenkinson alikuwa mfano mzuri wa hili na hata kadi mbili za njano ambazo zilipelekea nyekundu alizipata kwa mtindo huu.

United walicheza soka la kupendeza machoni,na kiwango cha umaliziaji wao kilikuwa bora muda wote , lakini hawakuwa na haja ya kucheza vizuri kufanya maangamizi waliyoyafanya .

Pasi nyingi zilitembea kwa United kuliko kwenye mchezo uliopita dhidi ya Spurs na hata kwenye mchezo wa ngao ya jamii.
Baadhi ya magoli (mfano la Ji sung park na la Welbeck) yalikuja kwa sababu ya Arsenal kuruhusu muda mrefu na nafasi kubwa kwa wachezaji wa United kuanzisha na kumaliza’move’.


Mabao matatu ya Rooney yalikuja kwa jinsi Arsenal walivyokuwa wanatoa faulo nyingi kwa jinsi walivyokuwa wanajitupa kwa wachezaji wa United wakijaribu kuwakata kasi wakiwa kwenye ‘move’.

Mabao ya Young yalikuwa mazuri lakini kama yangekuwa ndiyo mabao pekee tungekaa hapa na kuhoji kwanini mchezaji anayetumia mguu wa kulia anayecheza upande wa kushoto alipewa nafasi ya kuingia ndani na kuhamishia mpira kwenye mguu wake wenye nguvu (wa kulia) na kufunga kirahisi . Karibu kila kitu kilikwenda hovyo kwa Arsenal.

Makosa ya msingi.

Kitu cha kushangaza kwenye ubao uliopo hapo chini ni kwamba sehemu za msingi kabisa ambazo mtu yoyote aliyewahi kucheza hata mechi moja tu ya mpira angeweza kukifanya kwa Arsenal zilikuwa hovyo.

Arsenal walichezewa kila mahali. United walifanya ‘tackling’ zenye mafanikio kwa asilimia 64% na Arsenal walifanya ‘tackling’ kwa asilimia 45 % tu.
Mfano mwingine ni kwamba pamoja na mpira kuwepo kwenye eneo la mita 18 la Arsenal , United waliweza kuzuia mashuti 6 na Arsenal walizuia 8 tu.

Kufanya ‘tackling’ na kuzuia mashuti si kitu kigumu au cha ajabu ambacho kinahitaji kufundishwa naMalaika toka Mbinguni ili kieleweke, sawa siyo mchezo wa Arsenal lakini pale unapokuwa unamiliki mpira kwa asilimia chache ni vizurri kuwa na mabeki ambao takwimu zao za ‘tackling’ na kuzuia mashuti ni nzuri.

Unapokuwa na timu ambayo haisimamishi mstari wa ‘off-side’ , ambayo haimiliki mpira na inawapa wapinzani mwanya wa kucheza ni lazima ufungwe na ndicho kilichotokea kwa Arsenal.

Mwisho.

Sehemu ya mchezo huu kwa maneno rahisi ni kwamba Arsenal hawakuwa na wachezaji waliokuwa ‘fit’ kuikabili timu kama Manchester United .
Hii ni kwa sababu ya kukosa uzoefu na wengine walikuwa wachezaji wasiojengwa kwa ajili ya michezo kama hii.


Laureant Koscielny alimaliza akiwa na asilimia 100% kwenye umaliziaji wa pasi zake. Lakini bado alikuwa anakamatwa sana eneo la juu la uwanja mahali ambako kwa hali ya kawaida beki hapaswi kuwa kwenye eneo kama hilo.
Carl Jenkinson alikuwa mchezaji bora kwa Arsenal kwa muda aliokuwa uwanjani na ndiyo maana Arsenal walikuwa nyuma kwa mabao macheche alipokuwa uwanjani lakini Tsunami ikawaangukia alipotoka na hata aliweza kutoa ‘assist’ moja lakini bado hakuweza kufanya ‘tackling’ hata moja .

Ramsay na Rosicky ni watengenezaji na si waharibifu na kwa mchezo wa leo Arsenal walikuwa wanahitaji mtengenzaji mmoja na muuaji mmoja ili ‘kubalance’ hesabu za midfield na kuwatumia wachezaji hawa ni lazima uumiliki mchezo lakini Arsenal hakuwa na umiliki wa mchezo huu.

United bado wanaendelea na mwanzo wao mzuri kwenye ligi japo hata wao lazima watakuwa wameshangazwa na jinsi mchezo huu ulivyokuwa rahisi kwao . Mfumo wao wa 4-4-2 ambapo washambuliaji wawili walikuwa wanashuka mpaka ndani unawapa nafsi ya kutengeneza’runs’ za kuelekea mbele na wanashambulia kwa pande tofauti za uwanja na si upande mmoja kama zamani na walikuwa hatari sana kwa sababu hii.

Sunday, August 28, 2011

Tottenham 1-5 Manchester City: Dzeko afunga manne huku City wakitawala kila idara.


Timu zilizoanza.
Manchester City kwa mara nyingine wameonyesha ‘perfomance’ ya hatari ambayo imewapa matokeo ya asilimia 100% kwenye msimu wao .


Harry Redknapp alilazimika kuwatumia Niko Kranjcar na Luka Modric katikati ya uwanja huku Peter Crouch akisimama peke yake mbele.
Kwa upande wake Roberto Mancini alimpa Samir Nasri mechi yake ya kwanza kama mchezaji wa Man City akichukua nafasi ya James Milner huku Nigel De Jong akikosekana kutokana na kuwa majeruhi.
City walitawala kila idara ya uwanja kwenye mchezo huu mwanzo hadi mwisho na hata matokeo yalionyesha hivyo.

City wanatawala kipindi cha kwanza.

Kipindi cha kwanza kilianza taratibu mithili ya mchezo uliowahi kuanza kwa wachezaji na mashabiki .
Ulikuwa mchezo ambao ulionekana kama mchafu kwa upande mmoja na hilo lilidhihirika kwa kadi za mapema zilitoka kwa pande zote mbili na pale ulipotulia City walishika hatamu na kutawala.
Huku timu zote zikionekana kucheza mchezo unaofanana kimfumo , ufanano huu ulionekana kwa jinsi walivyokuwa wanawatumia wachezaji wa pembeni, Spurs walikuwa na mawinga tena wa kizamani ambao walikuwa wanatambaa na chaki wakiwakabili mabeki wa pembeni na wachezaji wa Pembeni wa City Samir Nasri na David Silva walicheza pembeni lakini mara nyingi sana waliingia ndani kuomba na kutoa mipira na walichangia kujenga ‘move’ nyingi sana za timu yao.

Wakati mwingine inaweza kuwa tatizo unapochezesha mawinga wenye kawaida ya kuingia ndani kwa kuwa wanakuwa na mchezo unaotabirika huku wakiwa wanaufinya uwanja na wakati mwingine pia inapunguza eneo la uwanja ambalo linatumika kwa muda mrefu huku mabeki wa pembeni wakipata nafasi kubwa ya kupandisha timu.
Hili halikuonekana kwenye mchezo kwa kuwa Spurs walikosa kiungo mkabaji , sit u kiungo bali hawakuwa na mchezaji yoyote wa eneo la kati mwenye asili ya ulinzi . Tom Huddlestone alikuwa fit lakini alikuwepo bench na wakati Modric na Kranjcar walikuwa wazuri kwenye umiliki waliacha nafasi kubwa sana nyuma yao.
City waliwatumia Nasri na Silva , wote walisogea kwenye nafasi iliyoachwa wazi na wachezaji hawa wawili wa Spurs toka Croatia na waliidhuru Spurs tangu mwanzoni kwa nafasi ambazo City walianza kuzipata mfano kwenye dakika ya 7 kwa Silva na wakati Aguero alipokuwa anshuka mpaka katikati mwa uwanja Spurs walipata tabu sana .
Nasri hakuwa anaingia ndani mara kwa mara . Nasri alikaa eneo la kushoto wa uwanja lakini alicheza tofauti kidogo na alivyokuwa akicheza wakati yuko Arsenal, mara nyingi alikuwa akikimbia mpaka kwenye mstari na kupiga krosi , wakati mwingine akibadilisha miguu.

Mabao mawili ya City yalipikwa na Nasri ambaye pia ‘ ali-link’ vizuri sana na Gael Clichy ambaye wamezoeana tangu Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa.

Kipindi cha Pili.

Redknap alijaribu kumiliki mchezo hasa eneo la kati ambako alimuingiza Tom Huddlestone ambaye kwa upande wake alifanya kazi nzuri ya kuwalinda mabeki wanne ,City waliendelea kuwa timu bora na Dzeko alitupia bao linguine na kumaliza Hat-trick yake na Aguero alifunga bao safi ambalo kwa mara nyingine lilipikwa na Nasri.
Tatizo kubwa la Tottenham lilikuwa jinsi City walivyoziona na kutumia nafasi nyingi zilioachwa wazi na Spurs .Spurs Walilazimika kumtoa Modric na kumuingiza Jake Livemore ambapo kidogo mchezo ulianza kurudi kwa Spurs lakini ilipunguza mashambulizi ambayo kwa sasa yalikuwa yanaongozwa na Jermaine Defoe ambaye mara nyingi alikuwa akijipia nafasi mwenyewe .
Kiukweli mchezo ulimalizwa na bao la Dzeko la dakika ya 55 na kipindi cha pili hakikuwa na ladha yoyote . Dzeko alicheza vizuri sana , alionekana kuwa kwenye kiwango bora kabisa na akiwa anajiamini vibaya.


Muda wote wa mchezo alikuwa anaongoza mashambulizi ya City ambayo yalionekana kuleta hatari kwa Spurs na alikuwa na majaribio (goal attempts) 10 kwenye mchezo wote.
















Mwisho
Ulikuwa mchezo ‘excellent’ kwa City ambao waliwatumia vyema wachezaji watatu wabunifu kwenye timu yao.Mtu aliyefaidika na wachezaji hawa alikuwa Edin Dzeko ambaye kwa kutabiri ana nafasi kubwa sana ya kuwa mfungaji bora wa City na wa ligi kwa ujumla kutokana na ‘service’ anayopata.
Mipira ilipenya kwenye defence ya wapinzani , kulikuwa na krosi na pasi nyingine za aina nyingi sana . Kiukweli City wana silaha nyingi za maangamizi kwenye sehemu ya ushambuliaji.
Tottenham walikuwa kirahisi sana na kurahisisha kazi ya City na pia wachezaji wabunifu wa Spurs walishindwa kuja mchezoni.

FINAL SCORE: MANCHESTER UTD 8-2 ARSENAL.

93'
FULL TIME Arsenal's misery is over, Wenger shakes Fergie's hand and Rooney wanders off with the match ball. Quite simply, a rout, an embarrassment, a roasting, a hammering, a devastating day for Arsenal. What a game.
93'
Six without a win for Arsenal in the Premier League now. Only two wins in 14 games in total.
93'
Park blazes over from Evra's cross! My word, it could have been nine.
92'
Giggs runs down the left, finds young and he bends a shot into the top corner from 17 yards. Brilliant goal.
92'
GOAL Young with a stunner!
91'
Arshavin fires wide from Oxlade-Chamberlain's cross.
90'
Three minutes added...
89'
What on earth will Wenger say after this?
88'
Nearly eight as Hernandez fails to connect with Smalling's cross
87'
Twitter reckons the last time Arsenal conceded seven was in 1927.
86'
Ramsey's run to the edge of the box ends with a shot that arcs narrowly past the post.
85'
Giggs' ball over the top finds Young offside.
84'
Double change for Arsenal as Van Persie and Walcott depart for Chamakh and Lansbury.
81'
Szczesny goes the wrong way and Rooney has a treble. Misery upon misery for Arsenal.
81'
GOAL Rooney hat-trick!
80'
MAN UTD PENALTY Theo clips Evra and this could be seven.
78'
This time Rooney's free kick falls the wrong side of the post.
76'
Another yellow for Jenkinson after bumping Chicarito bearing down on goal and the youngster walks.
75'
Arshavin wants a penalty for falling over, basically.
74'
Jenkinson does well to get down the right and cross, Jones clears but Jenkinson nods it back in and RVP smashes it home from seven yards.
74'
GOAL Van Persie!
73'
Arsenal's fans have their heads in their hands in the stands. This is a mortifying day for their club.
72'
Koscielny gets a free header but can't find the target.
71'
This is hugely embarrassing for Wenger. How long can Arsenal afford this to go on?
70'
Park collects the ball inside the area and has all the time in the world to pick his spot past Szczesny. This is just awful for Arsenal.
70'
GOAL Park gets in on the act!
70'
Rooney has nearly scored the goal of the weekend - a chip from 30 yards that dips over Szczesny and cannons back off the post. Supreme.
69'
If United wanted to they could probably hit seven or eight.
68'
Nani trots off after scoring and Ji-Sung Park is on. Giggs also comes on in place of Anderson.
67'
It's a battering. So much room for Rooney to pick out Nani, played onside by Traore, and he dinks it over the keeper. Arsenal a shambles at the back.
67'
GOAL Nani!
65'
Rooney is now Man Utd's top scorer in the Premier League era.
64'
A free kick masterclass from Rooney, who gives Szczesny the eyes, then drills it in the opposite corner. Superb.
64'
GOAL Rooney!
63'
Djourou hauls Rooney down as he went for a Hernandez ball and is booked.
63'
Man Utd enjoying 61% possession in the second half.
62'
Coquelin goes off and Oxlade-Chamberlain is on for his Premier League debut.
60'
Hernandez wastes a good chance to cross from inside the area. United growing large again as Young goes close before squaring for Nani who misses his kick.
59'
Nani gets to the byline and centres but Djourou clears.
58'
The away contingent must have been singing "We love you Arsenal," for about 15 minutes straight now.
57'
Cracking one-two with Hernandez and Cleverley puts the England midfielder through but his effort lacks pace and Szczesny saves.
56'
Better from Arsenal but they have to take these chances.
55'
What a chance for Arshavin. He is found by Ramsey, gets beyond Jones and gets into the area before dragging a shot wide from nine yards. Got a nick too so its a corner.
54'
Still a ridiculously open game. Expect more goals.
53'
Rosicky clips a ball into Van Persie and his volley is well saved by De Gea. He could have brought it down as he had plenty of time.
52'
Rooney's first time cross is cut out by Djourou after good work from Nani.
51'
Walcott takes a blow to head as the Arsenal fans get behind their team.
50'
Nani bursts beyond Traore but tries an audacious chip when he had numbers in support. Greedy.
49'
Young has taken a blow on the knee after Jenkinson fell over and caught him.
48'
But as is the way, United create the first opportunity, Young testing Szczesny with a low shot then clipping thr rebound wide of goal.
47'
A decent start to the half from Arsenal, but no cutting edge yet.
46'
We begin again.....

Hard to know what Wenger can do to turn things around in the second half given the lack of resources he's faced with. His side were so open in that half it was untrue.


I wonder if they still trust in him after that first half?


Danny Welbeck celebrates his opener.
45'
HALF TIME A dominant half from United and nothing but pain for Arsenal. It could have been 1-1 after Arsenal were awarded a penalty but within a minute it was 2-0. Walcott's goal has given the Gunners a ray of hope though.
45'
A slice of hope for Arsenal as Rosicky finds Walcott and his shot goes through De Gea's legs.
45'
GOAL Walcott!
45'
Rooney shoots from the half way line after spotting Szczesny off his line. Good effort too - the keeper catches it under his bar.
44'
A nightmare half for Wenger and perhaps it all hinged on that penalty miss. Score that, get back to 1-1 and it might have inspired the Gunners on.
43'
Szczesny claims Anderson's corner.
42'
Ramsey has a chance to score immediately but loses his footing in the box.
41'
Szczesny got a hand to it but couldn't keep it out and this could get ugly very quickly for Arsenal.
41'
GOAL Rooney floats the free kick into the top corner!
40'
Jenkinson is lucky not to be walking after bringing down Young who was about to go in on goal. Perhaps the cover from Koscielny saved him.
39'
Nani bends a free kick two yards over the bar Djourou fouled Young.
38'
Might that substitution disrupt Man Utd's flow a little?
37'
Just before Welbeck's hammy went, Arshavin went in late on Young and should have picked up a second yellow. Webb let play run on and didn't come back and book him.
36'
Hernandez comes on for Welbeck, who limps down the tunnel.
35'
Welbeck has pulled up - his hamstring has gone. Poor lad.
34'
"Sacked in the morning," United's fans sing.
33'
Walcott, the penalty aside, has been very disappointing.
32'
Cleverley gets in behind this time but Koscielny gets a foot on his pull back.
32'
Already 13 attempts on target in the match.
31'
Great ball to the back post from Rooney as Arsenal are stretched again but Welbeck is stretching and can't get it on target.
30'
Smashing double save from De Gea as he keeps out Arshavin''s drive and then Van Persie's follow up. And Old Trafford sings his name.
29'
Wow, what a minute of football!
28'
What a cruel game it can be - Young picks up Traore's clearance and curls a superb shot into the top corner. Game over.
28'
GOAL Young! What a goal!
28'
A huge confidence boost for De Gea but Van Persie's effort was woeful - lacking in power and too close to the keeper. Arsenal's big chance has gone.
27'
Saved by De Gea! Terrible penalty.
26'
A tug from Evans as Walcott got in front of him inside the area and the Gunners have a great chance to level.
25'
ARSENAL PENALTY
24'
A great chance for Smalling to make it 2-0 as Rooney finds him, he turns outside Traore but pulls his shot well wide.
24'
That could open the floodgates.
23'
A shake of the head from Wenger. That was terrible from Djourou. Clever from Anderson and good from Welbeck.
22'
A cute dink over the top from Anderson and Welbeck fights off Djourou to nod past Szczesny. Such a simple goal. Awful defending.
22'
GOAL Welbeck!
21'
Acres of space for Evra run into as Walcott went AWOL but Traore clears.
21'
Some space for Walcott to take Evans on but he tries a clip across the face and Van Persie was nowhere near it.
20'
Good defending from Traore - matching Nani for pace after Smalling pass round the back.
19'
Cleverley has some blood running from a cut near his eye after being caught by Rosicky's elbow. Unintentional.
18'
Rosicky has a pop from distance, perhaps wanting to test De Gea's confidence, but it is deflected for a corner.
17'
Good counter attack from Arsenal and a lovely cross from Van Persie but only Walcott was in the box and he attacked the near post.
16'
Nani teases Arshavin before skipping round him and winning a corner.
15'
A yellow for Arshavin as he left his studs in on Jones. A painful one for the defender.
13'
Arsenal inviting pressure on themselves by giving possession away cheaply.
12'
Nani rattles a ball into the area and Welbeck nods over under pressure from Koscielny.
11'
A reasonable start from Arsenal. Not looking water tight but bright enough going forward.
10'
Coquelin does well to get in front of Young as he tried to latch onto a neat pass from Welbeck.
9'
Walcott's first involvement is poor, offering up the ball to Evra.
8'
Rooney feeds Young nicely but he fails to lay it off before Djourou closes him down.
7'
Welbeck bursts through the middle and is found by Young but his left foot effort lacks conviction and spirals wide.
6'
Arshavin tries to release Van Persie, who had run beyond Evans, but the defender cuts the pass off.
5'
Promising move from Arsenal as Arshavin finds Traore but Jones nods his cross clear.
4'
Powerful effort on target from Rooney but Szczesny is right behind it.
3'
First break from United as Nani slots in Smalling and his cutback is fired wide by Cleverley, who was on the stretch.
2'
De Gea spreading balls around as Man Utd spray it along their backline.
1'
Welbeck charges down a Szczesny clearance as United lay down a marker early on.
1'
KICK OFF

Some interesting names on Arsenal's bench: Fabianski, Oxlade-Chamberlain, Chamakh, Lansbury, Miquel, Ozyakup, Sunu. Oguzhan Ozyakup doesn't even have his own Wikipedia page.

Arsenal hand Francis Coquelin his Premier League debut - quite some ask - while Bacary Sagna is struck down with a virus. Jenkinson and Traore are full backs. Arshavin starts.

The home side are unchanged from their defeat of Spurs on Monday - its already looking like a settled side.

Good afternoon all and welcome to live coverage of Manchester United's clash with Arsenal

Saturday, August 27, 2011

WACHEZAJI WANNE WA KUKIPA UBORA KIKOSI CHA ARSENAL


Arsene Wenger amefanikiwa kuiwezesha timu yake kupata nafasi ya kushiriki klabu ya ulaya msimu huu.

Sasa ufuatao ni muda muafaka ambao utaamua hatma ya Gunners msimu huu na nini wat-achive kwa msimu wote wa 2011-2012.

Akifanyiwa mahojiano ya TV baada ya ushindi dhidi ya Udinese, nahodha mpya wa Arsenal aliweka wazi kuwa anataka timu yake kufungua akaunti na kuleta wachezaji wa ukweli kuimarisha kikosi kabla halijafungwa dirisha la usajili.

Ni usajili mzuri pekee utakaotoa taswira ya Gunners msimu huu whether itagombea nafasi ya nne kwenye ligi au itagombea makombe makubwa yakiwemo Premier league.

Gunners walikuwa na bajeti ya kutosha hata kabla ya kuuzwa Cesc Fabregas na Samir Nasri, ushamisho ambao umeleta zaidi ya £60m kwenye akaunti ya klabu hiyo huku wakitarajiwa kuzidi kutunisha mfuko kwa mapato makubwa ya kushiriki Champions League.

Hivyo, Arsene Wenger hana tena visingizio.Wengi wa mashabiki wa Gunners bado wanataka kuona mzee Wenger anaijenga upya Arsenal na kufanikiwa, lakini inabidi awashawishi kwamba mataji makubwa yapo njiani.

Sio tu mashabiki, pia itawashawishi watu kama Van Persie na Bacary Sagna kwamba Arsenal bado shauku na hamu ya mafanikio kwa kutaka kunyakua makombe.Hivi ndivyo Wenger anavyohitaji na atapata line up na kikosi kitakuwa imara zaidi ifikapo September 1.

Wachezaji wote hapa chini wamekuwa katika rada ya Arsenal na wengine Wenger ameshajaribu kutuma ofa though hajafanikiwa bado, ama kwa hakika wataibadilisha Gunners.

1: YANN M’VILA – (£22m)

Wenger amaeshatuma ofa mbili kwa ajili ya kiungo huyu wa Rennes, na bid mpya ya Arsenal ya £20m inaonyesha wapo serious na biashara hii.

M’Vila ambaye ni mfaransa ana nguvu, ufundi na uwezo mkubwa wa kuweza kucheza kama kiungo mkabaji mbele ya mabeki, kitu ambacho kitampa Wenger option ya kumruhusu Jack Wilshare asogee mbele.

Wilshare anaweza kuwa ndio future ya timu ya taifa ya England katika eneo la kiungo, pia ana uwezo na nafasi ya hata kuja kumzidi Cesc Fabregas.M’Vila anabakia ndio chaguo sahihi kwa upande wa kiungo cha Arsenal – ikiwa Rennes watakubali kumuuza.

EDEN HAZARD (£25M)


Wenger amekuwa akimfuatilia mshambuliaji huyu wa klabu ya Lille raia wa Ubelgiji kwa zaidi ya miaka miwili.Hazard ni mchezaji ambaye ni versatile yaani ana machaguo mengi ya kucheza dimbani, ni mchezaji anayewindwa na almost vilabu vikubwa vyote na kama Arsenal wakimpata atawasaidia sana.

Lille wanatambua kwamba Arsenal wanamuhitaji Hazard, lakini hawataki kumuuza ingawa inawezekana kufanyika biashara kwa kiasi ambacho hakitokuwa chini ya £25m.

Arsenal tayari walishajaribu kumsajili, lakini waligonga ukuta ingawa bado wanaweza kutuma ofa nzuri ambayo itakuwa ngumu kwa mchezaji na klabu kukataa.Mchezaji mwezie wa Lille, Gervinho tayari ameshaanza kuilipa fadhila Gunners.

3: PHIL JAGIELKA NA LEIGHTON BAINES (£30M)


Gary Cahill ni mdogo zaidi na mzuri kuliko Jagielka lakini Wenger anamtaka Jagielka na Arsenal hawataki kulipa £17m kwa ajili ya mchezaji huyo wa Bolton.

Jagielka anapapenda sana Goodson Park na amezoeana na wachezaji wenzake, hivyo kumfanya acheze vizuri itabidi Leighton Baines nae ajiunge na Gunners.

Arsenal pia wamekuwa wakimfuatilia sana Baines tangu msimu uliopita na sasa wakiwa na beki wa kushoto ambaye anaandamwa na majeruhi akiwa bado mchanga Kieran Gibbs, wanahitaji guality player kama Baines kuisadia ngome dhaifu ya timu yao.

Hii ndio dream timu ya Arsenal ambayo inaweza kuwashawishi na kuwafanya mashabiki kurudisha imani iliyoanza kupotea kwa timu yao.

Pia usajili wa wachezaji hawa utakuwa upo katika mipaka ya matumzi ya Arsenal baada ya kupata fedha walizowauzia Fabregas na Nasri zinzofikia £60m, za Gael Clichy £7m na zile ambazo Wenger alipewa kwa ajili ya usajili msimu £35m bila kusahau mapato yanayofikia £25m kwenye Champions League.

INTERVIEW YA KWANZA YA NASRI AKIWA NDANI YA UZI WA CITY

Friday, August 26, 2011

MGOMO WA WACHEZAJI SASA WAHAMIA SERIE A

Huku Ulimwengu ukiwa na kumbukumbu ya mgomo uliotokea nchini Hispania ambao ndiyo kwanza umeisha mgomo mwingine umeibuka nchini Italia.
Michezo ambayo ilikuwa imepangwa kuanza mwishoni mwa wiki hii kwa siku za Jumamosi na Jumapili italazimika kusubiri matokeo ya mikutano itakayofanyika baina ya Viongozi wa Umoja wa vilabe nchini Italia (AFE) , mikutano ambayo itaamua hatma ya ligi hiyo baada ya ule uliofanyika siku ya Ijumaa huko Milan kushindwa kufika muafaka.

Kikubwa kinachozuia ligi ni kile kile kilichosababisha mgomo nchini Hispania,Kampuni inayoongoza ligi imetoa fungu dogo la mishahara ya wachezaji ambalo halijakamilika . Kesi kubwa inayosimamiwa na wachezaji ni usalama na uhakika wa malipo yao ilhali Serie A imesimamia kwenye fungu ambalo ni sawa na mshahara wa muda .

Pamoja na hilo wanachohofia wachezaji ni yale yanayotokea kwa timu ndogo pale zinaposhuka daraja ambapo wengi hujikuta wakidai mishahara kwa timu zao kwani mara nyingi kushuka daraja mara nyingi huambatana na hasara kibiashara ambapo timu nyingi hujikuta zikifirisika hadi kuhitaji usimamizi wa kibiashara kwa lugha ya kitaalamu ‘Financial Administration’.

Moja ya mambo yanayofanya hali kama hii ya Kampuni zinazoendesha ligi barani ulaya kama La Liga na Serie A kuwa katika wakati mgumu kibiashara ni tabia ya wenye timu kukopa fedha nyingi benki fedha ambazo wakati mwingine hushindikana kulipwa hali inayopelekea vilabu kuuzwa kwa wamiliki wenye fedha , vilabu vikubwa kama Inter Milan na vingine vya Italia vimekuwa kwenye wakati mgumu kibiashara ambapo vimeshindwa kurejesha fedha vyenyewe huku vikitegemea fedha toka kwenye mifuko ya wamiliki wa timu ambao wanafanya biashara nyingine zinazosapoti timu zao.
Timu za Italia pia zinakosa fedha nyingi kutokana na kushindwa kumiliki viwanja ambapo vinalazimika kulipa fedha kwa manispaa ambazo zinamiliki viwanja , mifano ni Inter Milan na Ac Milan ambazo zinatumia uwanja unaomilikiwa na manispaa ya jiji la Milano na As Roma na SS Lazio zinazotumia uwanja wa Stadio Olimpiki unaomilikiwa na manispaa ya jiji la Roma.

Wamiliki wa timu kina Silvio Berlusconi na Massimo Moratti wamekuwa wakitumia biashara zao za vyombo vya habari kwa Berlusconi na Mafuta kwa Morati kusapoti timu zao huku zikishindwa kutengeneza fedha zenyewe .

TWIGA STARS KWENDA MAPUTO

Timu ya Taifa ya wanawake ya mpira wa miguu (Twigs Stars) inatarajia kuondoka Agosti 31 mwaka huu kwenda Maputo, Msumbiji kwenye michezo ya All Africa Games itakayofanyika nchini humo kuanzia Septemba 3-18 mwaka huu.

Twiga Stars katika msafara wake itakuwa na jumla ya watu 20 ambapo kati yao 16 ni wachezaji na wanne ni viongozi wakiwemo Kocha Mkuu Charles Boniface na msaidizi wake Nasra Mohamed.

Mechi ya kwanza ya Twiga Stars itakuwa Septembe 5 mwaka huu dhidi ya Ghana wakati ya pili dhidi ya Afrika Kusini itachezwa Septemba 8 mwaka huu. Twiga Stars itacheza mechi yake ya mwisho katika hatua ya makundi Septemba 11 mwaka huu dhidi ya Zimbabwe.

ALGERIA KUWASILI SEPTEMBA MOSI
Algeria ‘Desert Warriors’ inatarajia kuwasili nchini Septemba Mosi mwaka huu saa 1 jioni kwa ndege ya kukodi ikiwa na msafara wa watu 50 ambapo kati yao 25 ni wachezaji. Timu hiyo itafikia kwenye hoteli ya Golden Tulip.

Mechi kati ya Taifa Stars na Algeria itachezwa Septemba 3 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili. Pambano hilo ni la mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea na Gabon. Katika mechi ya kwanza iliyochezwa Algiers timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1.

Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Nicholas Musonye kutoka Kenya wakati waamuzi ambao wote wanatoka Mauritania ni Ali Lemghaifry, Mohamed Hamada, Hassane el Dian a Pene Cheikh Mamadou.

LIGI KUU YA VODACOM
Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea tena kesho kwa mechi moja kati ya African Lyon na Toto Africans itakayochezwa Uwanja wa Chamazi ulioko Mbande, Dar es Salaam.

LEO NILIPATA UGENI OFISINI KWANGU


MAPAMBANO YA BONDIA MTANZANIA ROGERS MTAGWA !





ALLY KIBA: NILIACHA KUCHEZA SOKA KUTOKANA NA UBABAISHAJI ULIOJAA BONGO




Mwanamuziki wa Bongo flava Ally Kiba ambaye ni mmoja wa wasanii wenye uwezo na kipaji kikubwa cha kucheza soka amefanya mahojiano na blog kuelezea sababu zilizomfanya achague muziki kama kazi badala ya soka.



“Mwanzoni muziki haukuwa na nafasi kubwa kama soka katika maisha yangu, lakini kutokana na ubabaishaji uliopo kwenye medani ya soka la Tanzania, ilipotokea nafasi ya kutengeneza fedha katika muziki then nikaamua kuachana na soka la ushindani na kujikita katika tasnia ya muziki.”
Ally Kiba ambaye mwaka jana alipata nafasi ya kuimba na gwiji la muziki duniani R.Kelly anasema bado anacheza soka kipindi anapopata nafasi “Soka ni mchezo ambao upo moyoni hivyo sijautupa kabisa, bado nacheza mpira kipindi ninapokuwa huru na majukumu yangu ya muziki.”
Je Kiba ni mshabiki wa timu gani ndani na nje ya Bongo?





“Mimi ni shabiki mkubwa wa Dar Young Africans kwa Tanzania, naizimia mno timu ya watoto wa Jangwani na mchezaji aliyenifanya niipende sana ni enzi zile za Edibily Jonas Lunyamila akiwa sambamba na Mohamed Hussein Mmachinga.Kwa upande wa nje ya Tanzania naipenda klabu ya Liverpool.”



NANI ALIKUWA MWENYEJI WA MCHEZO HUU ?

Aisee wadau hivi hii mechi ilichezwa kwenye nchi gani ?
Ebu tazameni 'BRANDING' ya uwanja kwa umakini maana muonekano wa uwanja huu umenifanya mwenzenu nishindwe kuelewa nani alikuwa mwenyeji siku ile ya mchezo wa TANZANIA na BRAZIL, Msaada tafadhali kwenye tuta!!


,


HUYU ndiye Mbwana Samatta!!

Anayefunga bao la kwanza ni MBWANA SAMATTA
























SAMATTA NI MWENYE JEZI NAMBA 26









HAPA ANAFUNGA BAO KWA KICHWA






HAPA ANATOA PASI MBILI ZA MABAO

Thursday, August 25, 2011

The draw for the 2011-12 Champions League group stage


GROUP A
Bayern Munich
Villarreal
Manchester City
Napoli

GROUP B
Inter Milan
CSKA Moscow
Lille
Trabzonspor

GROUP C
Manchester United
Benfica
Basle
Otelul Galati

GROUP D
Real Madrid
Lyon
Ajax
Dinamo Zagreb

GROUP E
Chelsea
Valencia
Bayer Leverkusen
Genk

GROUP F
Arsenal
Marseille
Olympiakos
Borussia Dortmund

GROUP G
Porto
Shakhtar Donetsk
Zenit St Petersburg
APOEL

GROUP H
Barcelona
AC Milan
BATE
Viktoria Plzen








MAANDALIZI YA DROO YA UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
















HII NDIYO NGOZI ITAKAYOTUMIWA KWENYE FAINALI YA CHAMPIONS LEAGUE MSIMU HUU


























USIWE MWEPESI KUZIAMINI KAULI ZA WANASOKA - SOMA HIZI

ADRIAN MUTU

JULY: Adrian Mutu anajiunga na Casena baada ya kuisha kwa kifungo chake cha miezi tisa kwa kosa la kutumia drugs. “Kutokana na yaliyonipata, sasa naweza kuwa mfano bora kwa wachezaji wenzangu.Nitawaonyesha kuwa sasa nimekuwa mwanaume bora.”

AUGUST: Mutu afungiwa maisha kuichezea Romania kwa kosa la kukutwa amelewa usiku wa kuamkia mechi ya kirafiki.

NIGER REO-COKER

MAY: “Nimekuwa nikitakiwa na timu za ulaya zinazoshiriki kwenye Champions League.Mimi ni mcheza soka mwenye hamu ya kucheza katika ngazi ya juu.Mimi sio nacheza soka ili kujionyesha tu, nipo serious kuhusu professional yangu na nini nataka ku-achieve kwenye maisha.”

JULY: Reo-Coker ajiunga na Bolton timu ambayo haichezi Champions League.

KELVIN NOLAN


JUNE: “Pindi mtoto wangu wa kike akiwa anajigamba na kumwambia kila mtu “Baba yangu ni nahodha wa Newcastle” na hapo ndipo nagundua ni namna gani timu hii inamaanisha kwenye maisha yangu.Kweli kutoka chini ya uvungu wa moyo wangu napenda kuichezea klabu hii.”

JUNE 15-2011 – Nolan ajiunga na timu inayocheza ligi ya daraja la kwanza West Ham.

GAEL CLICHY


JULY 2009 – “Naamini kama wewe ni mchezaji ambaye unafikiria pekee kuhusu fedha basi utaishia kuichezea Manchester City.

JULY 2011 – Glichy ajiunga na Manchester City

SAMIR NASRI

APRIL- 21/2010: “Nafikiri Arsenal kama klabu ina mafanikio na ni sehemu nzuri kuliko klabu nyingine zinazotumia mamilioni ya paundi kujenga timu zao ili kupata mafanikio”

AUGUST 2011: Samir Nasri agoma kusaini mkataba mpya na Arsenal, na ajiunga na Manchester City kwa gharama ya £24m na mshahara wa £185,000 kwa wiki.

VICTOR COSTA AREJESHWA STARS


Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen leo (Agosti 25 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 23 kwa ajili ya mechi ya mchujo dhidi ya Algeria ‘Desert Warriors’ kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea na Gabon.
Wachezaji walioitwa ni makipa Shabani Dihile (JKT Ruvu Stars), Juma Kaseja (Simba) na Shabani Kado (Yanga). Mabeki wa pembeni ni nahodha Shadrack Nsajigwa (Yanga), Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya) na Amir Maftah (Simba). Mabeki wa kati ni Aggrey Morris (Azam), Juma Nyoso (Simba) na Victor Costa (Simba).

Viungo wakabaji ni Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Nurdin Bakari (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Juma Seif (Yanga) na Jabir Aziz (Azam). Viungo washambuliaji ni Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada), Mrisho Ngassa (Azam) na Salum Machaku (Simba).

Washambuliaji ni Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Ramadhan Chombo (Azam), Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam), Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden) na John Bocco (Azam).

Timu itaingia kambini Jumapili (Agosti 28 mwaka huu) mchana na jioni itaanza mazoezi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume. Mechi dhidi ya Algeria itachezwa Septemba 3 mwaka huu kuanzia saa 10.00 jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Coastal Union yapokea msaada wa vifaa vya 2 milioni kutoka kwa Bawazir

Mdau Mohamed Bawazir akimkabidhi jezi mwenyekiti wa Coastal Union Ahmed Aurora


Pia Viongozi hao walikabidhiwa Mipira

Na Burhani Yakub,Tanga.
KLABU ya Coastal Union ya Jijini hapa imepokea msaada wa vifaa vyamichezo vyenye thamani y ash 2 milioni kutoka kwa mdau wa michezonchini Mohamed Bawazir ikiwa ni mchango wake wa kuiwezesha kushirikivyema ligi kuu vodacom.
Vifaa hivyo ni jezi,mipira,beeps soks jezi za walinda mlango kwa ajili ya wachezaji pamoja na vifaa vya uhamasishaji vya kutumiwa na mashabiki ambavyo ni vuvuzela na tambara la hamasa. Makabidhiano ya vifaa hivyo yalifanyika jana asubuhi katika hoteli ya Tanga Beach Resort ambapo clabu ya Coastal iliwakilishwa wapenzi wake wakiongozwa na Mwenyekiti wao,Ahmed Aurora na Makamu mwenyekiti Steven Mguto.
Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo,Bawazir alisema lengo ni kutoa hamasa kwa wadau wengine kujitolea kuisaidia Coastal Union inayokabiliwa na michuano ya Ligi kuu Vodacom pamoja na kuendelezamichezo kwa ujumla katika mkoa wa Tanga.
“Nimeamua kuongoza njia ili wadau wengine wajitokeze kusaidia kuhuisha michezo katika mkoa wa Tanga ambayo ilikuwa ikiwika katika miaka ya nyuma kwenye michezo mbalimbali”alisema Bawazir.
Mdau huyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Darworld Links Ltd ya jijini Dar es salaam,alisema kuna kila haja kwa wadau wa Tanga walioko maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi kujitokeza kusaidia. Vifaa vilivyokabidhiwa ni sare jozi moja,seti mbili za sare za walinda mlango ,soks pea 20,jezi za mazoezi jozi 30,mipira mitatu aina ya jabulani,bendera na tambara kubwa la hamasa.
Mwenyekiti wa klabu hiyo,Aurora alimshukuru mdau huyo kwa mchango wake mkubwa ambapo alisema vifaa hivyo vitawasaidia wachezaji pamoja mashabiki wakati wa michuano yote inayoikabili timu hiyo.
“Bawazir amekuwa mdau wa kwanza kuisaidia klabu yetu ukiacha wadhaminiwakuu,tangu tumechaguliwa tumekuta Coastal haina vifaa wala chochote hii ni hatua kubwa kwetu”alisema Aurora.

EMMANUEL PETIT NA KIKOSI CHAKE BORA


GOALKEEPER-FABIAN BARTHEZ

Alicheza football katika namna ya tofauti sana na ndio kitu kilichomfanya aokoe michomo mingi.Fabian pia alikuwa umbo zuri linalomfaa golikipa.

BEKI WA KULIA – LILIAN THURAM

Mchezaji mwenzangu wa zamani ndani ya timu ya taifa na Monaco.Moja ya mabeki wazuri niliwahi kucheza nao.Thuram alikuwa na kila kitu ipasavyo kwa mlinzi wa kulia navyo.

BEKI WA KATI – FRANZ BECKENBEUER

Gentleman wa kweli wa soka, ambaye alikuwa na uwezo wa kucheza mahali popote katika uwanja kwa sababu alikuwa na ujuzi mkubwa na alijua namna ya kuusoma mchezo vizuri.

BEKI WA KATI – TONY ADAMS

Alikuwa ni chuma kwenye ulinzi wa timu.Wote tunajua alikuwa na matatizo yake, lakini alirudi na imara zaidi.Kiongozi wa wanaume, sio wachezaji wengi walikuwa na uwezo kumpita.

BEKI WA KUSHOTO – PAOLO MALDINI

Rekodi zake zinaongea zenyewe, kwa upande wa ubora na kucheza kwa muda mrefu, Alikuwa mgumu sana kumpita hivyo ni vigumu kumuacha nje ya kikosi changu.

KIUNGO WA KATI/MKABAJI – ROY KEANE

Alikuwa mzuri kwa pande zote kuanzia nguvu mpaka akili ya mchezo.Nilikuwa nafurahi sana kuchuana nae kipindi tulipokutana Arsenal na Manchester United-ilikuwa ni vita, lakini nilikuwa namuangalia kama mfano bora.

KIUNGO WA KATI/MSHAMBULAJI – STEVEN GERRARD

Moja ya viungo bora katika ulimwengu wa soka.Mchezaji anayeweza kufanya kila kitu: kupasia, kukaba, ku-dribble, kukimbia na kupiga mashuti makali yenye kulenga target.Pia napenda ukarimu wake,Kwangu mimi hii ni ishara ukubwa uliotukuka.

WINGA WA KULIA – PELE

Kitu ambacho watu muda mwingine wanasahau kugundua kuwa Pele alikuwa anacheza aina ya mchezo ambao sisi tumeucheza miaka hii ya karibuni katika namna ya kucheza kwa nguvu na kujitolea.Alicheza mchezo ambao zaidi miaka 30 baadae tulicheza sisi.Proffesional wa ukweli na mwenye uwezo mkubwa kucheza soka, fundi.

NYUMA YA MSHAMBULIAJI – DIEGO MARADONA

Ukicheza dhidi ya Maradona huwezi kujua nini kitakupata.Moja ya wachezaji bora wa muda wote.Alikuwa na akili mno katika timu yoyote aliyocheza.Jeshi la mtu mmoja lenye kubadili matokeo muda wowote.Alizaliwa na zawadi ya kipaji.

WINGA WA KUSHOTO – HRISTO STOICHKOV

Mchezaji ambaye alikuwa na uwezo wa kubadilisha mwelekeo wa mchezo muda wowote atakapopata nafasi, alikuwa hatabiriki.Alikuwa na mguu wa kushoto uliobarikiwa, kiukweli nilikuwa namtamani sana uwezo wake.

MSHAMBULIAJI WA KATI – ERIC CANTONA

Kitu ambacho hakijasemwa kuhusu Eric Cantona? Mchezaji mwenye utukufu, na mtu ambaye alifungua milango kwa wachezaji wengi wa kifaransa nchini England.King Eric mwenye rekodi nzuri ya kimataifa pia.

MAKOCHA –ARSENE WENGER NA SIR ALEX FERGUSON

Ndio, imebidi waungane.Wemawahi kuwa na upinzani mkubwa lakini wanaheshimiana sana, kwa sababu naamni wanafanana katika kutaka mafanikio kwenye soka.Wote wanafahamu mahitaji ya kuwa katika level ya juu.Wana umuhimu mkubwa kwa mchezaji mmoja mmoja, kwangu mimi wale wote ni vyuma vya soka.

SUBSTITUTES

MICHEAL PLATIN – Shujaa kwa watu wote wa Ufaransa na alikuwa hashikiki katika miaka 80, mpaka alipoibuka Maradona.

ZINEDINE ZIDANE – Mrithi asilia wa Platini, mchezaji bora wa kizazi chake.

FRANCO BERESI – Alifanya ubeki uonekane rahisi.

GIANFRANCO ZOLA – Uwezo wa juu, kuburudisha ndio sifa zake, moja ya wachezaji wa kigeni kucheza katika ligi ya England.

DENNIS BERGKAMP – Genius wa soka aliyekuwa akifurahia mno kucheza soka kwa sababu muda wote wa mchezo angefanikiwa kupata nafasi ya kupata mpira.

FRANK RIJKAARD – Muda wote alicheza kwenye standars ya juu, katika kiungo na ulinzi huku akiwapa moyo wachezaji wenzie kucheza achezavyo.

PETER SCHMEICHEL – Uwepo wake golini ulikuwa unawatisha washambuliaji kutokana na ukubwa wa mwili wake na uwezo wa kudaka.Golikipa bora niliyewahi kucheza dhidi yake nchini England.

OFA YA ARSENAL KUMCHUKUA KAKA KWA MKOPO YAKATALIWA


Ofa ya Arsenal kumchukua kiungo wa Real Madrid Ricardo Kaka imekataliwa.

Manager Arsene Wenger alijaribu kumsaini kwa haraka Kaka ili kuwashusha presha washabiki baada ya kuondoka kwa Nasri aliyejiunga na Manchester City, ambaye alimfuatia Cesc Fabregas aliyerudi Barcelona.

Lakini ofa yake ya kumsaini kwa mkopo Mbrazil huyo ambaye ni mchezaji bora wa dunia mwaka 2007 ilikataliwa.

Wenger sasa itabidi aamue kumsaini Kaka ambaye kocha wa Real Madrid Jose Mourinho anasemekana kutomuhitaji katika kikosi chake.

Real Madrid wanataka kuondokana na gharama ya kulipa mshahara mkubwa wa Kaka (£153,000) na watahitaji kiasi kisichopungua £20m kama ada ya uhamisho.

Kumsajili Kaka, 29, itakuwa ni kinyume na sera za usajili za Wenger, ingawa mchezaji atarudisha imani ya mashabiki kwa timu yao.

Wakati huo huo matajiri wapya wa Europa Paris Saint German na klabu ya Sao Paulo zimeonyesha nia kumuhitaji Kaka.

HAYA WADAU WENYE UWEZO WA KUUSIMAMIA HUO MZIGO FANYENI FASTA.





NASRI NA JUAN MATA WATAMBULISHWA NA VILABU VYAO VIPYA

JUAN MANUEL MATA AKITAMBULISHWA NA KLABU YAKE MPYA YA CHELSEA

SAMIR NASRI AKITAMBULISHWA NA TIMU YAKE MPYA YA MANCHESTER CITY KATIKA UWANJA WA ETIHAD STADIUM.

UDINESE 1-2 ARSENAL.

Champions League Qualification

Finished Rubin Kazan 1 - 1 Lyon
Finished Benfica 3 - 1 Twente
Finished Sturm Graz 0 - 2 BATE Borisov
Finished Udinese 1 - 2 Arsenal
Finished Viktoria Plzen 2 - 1 FC Copenhagen

England: Carling Cup

Bristol City 0 - 1 Swindon
Finished Exeter 1 - 3 Liverpool
Finished Peterborough 0 - 2 Middlesbrough
Finished West Ham 1 - 2 Aldershot
Finished Blackburn 3 - 1 Sheffield Wednesday
Finished Bolton 2 - 1 Macclesfield
Finished Everton 3 - 1 Sheffield United




Wednesday, August 24, 2011

MATCH LIVE CENTER: FINAL SCORES: SIMBA 1:0 COASTAL UNION, YANGA 1: 1 MORO UTD.

MPAMBANO WA LIGI KUU YA VODACOM BAINA YA COASTAL UNION NA SIMBA UTAANZA MUDA SI MREFU TOKA HIVI SASA
BLOG YAKO ITAKUWA INAKUPATIA MATOKEO YA MICHEZO MBALI MBALI INAYOPIGWA HII LEO KWENYE VIWANJA MBALI MBALI

VIKOSI.
SIMBA:
1. JUMA KASEJA
2. SAID NASSOR ' CHOLLO '
3. AMIR MAFTAH
4. JUMA NYOSO
5. VICTOR COSTA
6. JERRY SANTO
7. ULIMBOKA MWAKINGWE
8. PATRICK MAFISANGO
9. GERVAIS KAGO
10. EMMANUEL OKWI
11. HARUNA MOSHI

RESERVES

WILBERT WILLIAM
OBADIA MUNGUSA
JUMA JABU
SHIJJA MKINA
AMRI KIEMBA
SALUM MACHAKU

COASTAL UNION
1. OMAR HAMIS
2.MBWANA HAMIS
3. SOUD ABDI
4. JAMAL MACHELENGA
5. SALUM OMAR
6. SABRI MAKAME
7. FRANCIS BUSUNGU
8. MWINYI ABDULRAHMAN
9. HASSAN SALUM
10.RASHID MANDAWA
11. SALIM GILLA

RESERVES
FAROUK RAMADHAN
SHAFI KALUANI
VICTOR MGOME
DANIEL LYANGA
OMAR MALIGWA
KIBABU CHANDIGA
RAMADHANI NYUMBI.

KIKOSI CHA YANGA VS MORO UTD.

1. SHABANI KADO
2. SHADRACK NSAJIGWA

3.OSCAR JOSHUA
4. BAKAR MBEGU
5. CHACHA MARWA
6. JUMA SEIF
7. GODFREY TAITA
8. HARUNA NIYONZIMA
9. PIUS KISAMBALE ( GODFREY BONNY DK 54 )
10. HAMIS KIIZA
11. NURDIN BAKAR

RESERVES

SAID MOHAMED
ABUU UBWA
ZUBERI UBWA
JULIUS MROPE
RASHID GUMBO
SHAMTE ALLY.







DK 1: GAME IMEANZA MKWAKWANI







DK 2: ULIMBOKA ANAPIGA KROSI MABEKI WA COASTAL WANAOKOA.






DK 4: COASTAL U WANAPATA KONA MBILI PACHA ILA VICTOR COSTA ANAOKOA.







DK 5: KAGO ANAFUNGA BAO LAKINI MWAMUZI ANASEMA NI OFFSIDE.







DK 8: SIMBA WANAPATA FAULO KARIBU NA LANGO LA COAST,MAFISANGO ANAPIGA NJE.







DK 9: COAST WANAPATA KONA SIMBA WANAOKOA.









MATOKEO YA VPL:





COASTAL UNION 0:1 SIMBA -FT


mfungaji: mafisango






KAGERA SUGAR 1:1 VILLA SQUARD - FT





Wafungaji: Felix Bwanya dk 28-kagera, Zuber Dadi dk 90-villa


Sunday Frank (red card)-Kagera






POLISI 2:2 JKT RUVU - FT


wafungaji:Hamad Kambangwa na Brighton Mponji-polisi


Chau Rajab na Jimmy Shoji-JKT

YANGA 1:1 MORO UTD - FT


Wafungaji: Niyonzima-Yanga, Jerome Lembele ( Moro )
Juma Seif ( amepewa kadi nyekundu )




TOTO AFRICANS 1:0 RUVU SHOOTING-FT


mfungaji:Emanuel Swita ( penalty )

JKT Oljoro 1:0 MTIBWA SUGAR-FT
mfungaji:Aziz Roshuwa sec 50