Search This Blog

Saturday, March 8, 2014

KWANINI KIWANGO CHA OSCAR KIMESHUKA KATIKA SIKU ZA HIVI KARIBUNI?

Oscar alianza msimu huu akiwa kwenye form nzuri, kiungo mchezeshaji huyo wa kibrazil alifunga mabao 5 katika mechi zake 12 za kwanza premier league na akawa chaguo la kwanza la Jose Mourinho. Mourinho alijenga kikosi chake kumzunguka Oscar, huku Oscar akicheza kama namba 10 anayekaba kuanzia juu, akitafuta kufunga au kutoa assists. Lakini katika miezi ya karibuni kiwango cha Oscar kinaonekana kupungua. 

Kushuka kiwango
Pamoja na kufunga mabao 5 katika michezo 12 ya kwanza ya msimu wa EPL, Oscar ameweza kufunga bao 1 tu katika michezo 14 iliyofuatia na huku kiwango chake katika eneo la kushambulia kikiwa chini. Takwimu zinaonyesha kupiga mipira iliyolenga goli kumeshuka kwa 44%. Mchoro wa hapo unaonyesha takwimu za mchezo wake jinsi zilivyoshuka.


Kama tunavyoona uwezo wake wa kufunga ulivyoshuka kwa kiasi kikubwa. Kutisha kwake kwenye kushambulia kumepungua na amekuwa hatengenezi nafasi nyingi za kufunga pia, amejaribu kutengeneza nafasi 36 katika michezo 26. Willian ambaye amecheza mechi 18 pekee ametengeneza nafasi 39, wakati Eden Hazard ametengeneza nafasi 77. 
Kwa mchezaji anayecheza kwenye nafasi yake tulitegemea makubwa zaidi, hata kama Oscar anafanya kazi kubwa bila na mpira katika pressing.
Oscar hata hivyo anafanya kazi, katika kukaba na kupora mipira. Lakini, Oscar alishindwa kufanya tackling hata moja dhidi ya Fulham na taratibu amekuwa akishindwa kulifanyia kazi hili zoezi, ingawa mpaka sasa ameweza kufanikiwa kwa 59% ya tackling zote alizojaribu. 

Nini tatizo?
Tatizo hili lilianza pale Mourinho alipowaelekeza vijana wake kucheza kwa kukaba zaidi, Hii ilikuja baada ya michezo kadhaa ambayo Chelsea walikuwa wakiruhusu magoli mengi na kisha wakapoteza mechi ya Capital One waliyotolewa na Sunderland. Tangu wakati huo Chelsea wamekuwa wakicheza kwa kukaba zaidi huku watatu wa kushambulia wakilazimika kurudi kukaba zaidi..
Oscar amekuwa akicheza no. 10, Willian kulia pembeni na Hazard kushoto pembeni, wakati kumekuwepo na mabadilishano, Oscar amekuwa akirudi kucheza chinizaidi na hivyo kupelekea mchango wake katika kushambulia uwe mdogo. Dhidi ya Fulham alikuwa akicheza zaidi katika kiungo cha juu, na sio katika eneo ambalo no. 10 hucheza 
oscar4
Oscar alicheza chini sana kuliko kawaida. Katika mchezo huu hakufanikiwa kufanya tackling hata moja, na alijaribu mara tano kufanya hivyo, kitu ambacho hakiridhishi. Huu ulikuwa mchezo mgumu kwa Oscar, alitengeneza nafasi moja tu. Mwishowe alitolewa kwenye dakika 77. 
Tatizo jingine ni uchovu. Oscar ni mchezaji ambaye hufanya kazi sana na mfumo wa Chelsea unamlazimu kucheza kwa namna hiyo. Akirudi nyuma kukaba pamoja kunyang'anya mipira jambo ambalo linamchosha mno kijana huyo mwenye miaka 22. Oscar ameshacheza mechi nyingi sana katika misimu miwili ndani ya Chelsea, mpaka sasa tayari ameshacheza mechi 101, hapo bila kutaja namba ya michezo ya kimataifa anayoichezea Brazil tangu ajiunge na Chelsea. Ndio maana haishangazi kuona akiwa amechoka na Mourinho labda hajampumzisha vya kutosha, hivyo Mourinho anahitaji kumpa mapumziko kiasi ili aweze kupata matunda mazuri kutoka kwa mchezaji huyo kwa mara nyingine tena.  

Hitimisho
Ni vizuri kutambua kwamba Oscar ana umri wa miaka 22 na ataendelea kukua kuimarika kuwa na kiwango kizuri. Amefunga mabao 6 msimu huu, hata kama hivi sasa anakabiriwa na ukame wa mabao. Msimu uliopita aliweza kufunga mabao manne tu kwenye ligi hivyo unaweza kuona amefanya vizuri kuliko msimu uliopita kwenye kufunga. Mfumo wa Mourinho katika kukaba zaidi unamaanisha Oscar anafanya kazi nyingi zaidi kuliko msimu uliopita, jambo ambalo linamkaba mwenyewe katika kufanya vizuri kwenye kushambulia. Anachohitaji sasa ni kufanyiwa rotation na Mourinho na hapo ndipo tutamuona yule Oscar tuliyemzoea. 

No comments:

Post a Comment