Search This Blog

Friday, July 5, 2013

DOGO ALIYETANDIKWA NA HAZARD AUZA KOTI LAKE ALILOKUWA AMEVAA WAKATI WA MECHI YA CHELSEA VS SWANSEA - ILI KUSAIDIA WAGONJWA WA KANSA

Wote tunamkumbuka yule kijana muokota mipira aliyepigwa na Eden Hazard msimu uliopita katika mechi ya nusu fainali ya kombe la ligi kati ya Chelsea dhidi ya Swansea - kijana yule sasa ameamua kulipiga mnada koti alilovaa siku ile wakati akipokea kipigo kutoka kwa Hazard.

Charlie Morgan, ambaye aliukalia mpira uliotoka nje wakati Chelsea wakitafuta ushindi wa kuweza kuwapeleka fainali, Hazard alipoenda kuufuata ule mpira dogo akawa bado ameukali ndipo winga huyo wa Mbelgiji alimpopiga teke katika kuujaribu kuuchukua mpira huo. Hazard alitolewa kwa kadi nyekundu kwa kosa hilo. Lakini baadae wawili hao walikutana na kumalizana kistaarabu na mchezaji huyo wa Chelsea alisaini koti alilokuwa amevaa kijana Charlie Morgan muokota mipira.
 

Sasa ikiwa imepita miezi kadhaa tangu tukio hilo litokee - kijana Charlie ameamua kulipiga mnada koti lake lilosainiwa na Hazard kwenye mtandao wa Ebay - na mapato yatakayopatikana yataenda kusaidia wagonjwa wa kansa.


No comments:

Post a Comment