Search This Blog

Thursday, October 11, 2012

WAYNE ROONEY KUPATA MTOTO WA PILI MWEZI MEI MWAKANI



Coleen Rooney ametangaza kwamba ni mjamzito na anategemea kupata mtoto wa pili.

Mtangazaji wa TV na mumewe, mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney walitangaza kupitia ukurasa wa Twitter kwamba wanatagemea kumuongezea ndugu mtoto wao Kai, ambaye anafikisha miaka mitatu mwezi ujao.

Coleen amasema anategemea kujifungua mwezi May 2013.

Akiandika kwenye ukurasa wake wa Twitter, Coleen alisema: "Watu kadhaa waliotea, hivyo sasa habari zipo nje!! Mimi, Wayne na Kai tuna furaha kwamba tunategemea kupata member mpya katika familia yetu mnamo mwezi May.

"Ni mapema bado lakini tuna furaha kubwa, pia tungependa habari hizizitoke kutoka kwetu sisi kwanza kabla ya mtu yoyote mwingine!"

Baada ya kutangaza habari hizo kwenye Twitter wanandoa hao walipongezwa na watu maarufu mbalimbali wakiwemo marafiki kama Danielle O'Hara, Jude Cisse, Charley Webb na Piers Morgan.

Piers Morgan ambaye ni shabiki mkubwa Arsenal aliandika: "Hongera kwa habari hii nzuri @WayneRooney & @ColeenRoo - na tuombe mtoto apate muonekano wako...."

Rooney na Coleen ambao ni marafiki tangu utotoni walioana nchini Italy mwakak 2008 baada ya kuwa wamechumbiana kwa miaka 5. Walianza mapenzi tangu walipokuwa na miaka 16, wakati Coleen akiwa bado yupo shule.

No comments:

Post a Comment