Search This Blog

Thursday, May 2, 2013

TAKWIMU: BARCA VS BAYERN - MAN UNITED NDIO ILIKUWA TIMU YA MWISHO KUITOA BARCA KWENYE UCL BILA NYAVU ZA KUGUSWA - BAYERN WAWEKA REKODI KUFUZU KUCHEZA FAINALI KWA USHINDI WA MABAO MENGI


Takwimu ziliuzunguka ushindi 7-0 wa FC Bayern Munich dhidi ya Barcelona katika hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa wa ulaya

* Bayern wameweza kufuzu kwenda fainali kwa jumla ya ushindi mkubwa kuliko wowote kuwahi kutokea kwenye historia ya ligi ya mabingwa wa ulaya.

* Kiungo wa Bayern Munich Thomas Mueller amefunga mabao nane na kutoa assists mbili katika ligi ya mabingwa wa ulaya msimu huu

Barcelona walikuwa hawajafungwa katika michezo 12 ya Champions League kwenye uwanja wao wa nyumbani - mara ya mwisho walifungwa 2-1 na Rubin Kazan mwezi October 2009.

* Mara ya mwisho Barcelona kufungwa katika mechi zote mbili za hatua ya mtoano kwenye ligi ya mabingwa wa ulaya ilikuwa ni mwaka 1987, wakifungwa na klabu kutoka Scotland ya Dundee United.

* Manchester United ndio ilikuwa klabu ya mwisho kuizuia FC Barcelona kutokufunga bao katika nusu fainali ya klabu bingwa ya ulaya - mwaka 2008. Mechi ya kwanza Nou Camp walitoka sare 0-0, mechi ya pili Old Trafford Scholes akafunga bao pekee la mchezo na kuwatoa Barca.

*Barcelona wameshindwa kufunga goli katika kipindi cha kwanza katika mechi nne zilizopita.

* Wachezaji wa Barca Victor Valdes na Xavi wameweza kuifikia rekodi ya Edwin Van Der Sar ya kucheza mechi nyingi za nusu fainali ya UEFA Champions league. Mechi 14.

No comments:

Post a Comment