Search This Blog

Monday, June 27, 2011

HAPPY BIRTHDAY RAUL GONZALEZ BLANCO

Siku kama ya leo June 27, mjini Madrid Hispania Raúl González Blanco alizaliwa moja ya washambuliaji hatari kuwahi kutokea kwenye soka alizaliwa.
Raul ambaye kwa sasa ni mchezaji klabu ya kijerumani Schalke 04 ametumia muda mwingi wa maisha yake kuitumikia klabu ya Real Madrid kuanzia mwaka 1994 mpaka 2010, amefanikiwa kuwa mfungaji bora wa muda wote, akishinda kombe la klabu bingwa ya ulaya mara 3, pia akiwa ndio mfungaji bora wa mashidano wa michuano hiyo ya ulaya.
Aliondoka Real Madrid baada ya kuwasili kwa Jose Mourinho akiwa ameifungia timu hiyo mabao 323 katika mechi 741.
Pia Raul anshika nafasi ya pili nyuma ya David Villa kwa kufunga mabao mengi ndani ya historia ya timu za taifa za Spain akiwa amefunga mabao 44.
Raul atakumbukwa pia kwa ushangiliaji wake wa kubusu pete ya ndoa ikiwa ni ishara ya kuithamini ndoa yake na mkewe Mamen Sanz ambaye ameaa nae watoto wanne wa kiume, mapacha Hector na Mateo, Hugo, na Jorge ambaye amempa jina la mtu anayempaenda na kumhusudu sana Jorge Valdano, na mmoja ya kike aitwaye Maria.


HIZI NI REKODI ZA KAMA MCHEZAJI

No comments:

Post a Comment