Search This Blog

Friday, August 31, 2012

LIVE - SIKU YA MWISHO YA USAJILI BARANI ULAYA - USAJILI ULIOKAMILIKA NA TETESI


Micheal Essien amethibitishwa kuwa ataungana tena na kocha Jose Mourinho, baada ya Chelsea kuthibitisha kwamba atajiunga na Real Madrid kwa mkopo wa mwaka mmoja.


Yossi Benayoun amekamilisha uhamisho wa kujiunga na West Ham kwa mkopo wa mwaka mmoja.


Javi Garcia akiingia kwenye hosptali ya Bridge water kwa ajili ya kufanya vipimo vya afya baada ya klaby yake ya Benfica kukubaliana ada ya uhamisho na City - £16MILLION

Liverpool wamepigwa bao na Tottenham baada ya Clint Dempsey kujiunga na Spurs dakika za mwisho kutoka Fulham kwa ada ya uhamisho wa £6million.

Stephen Mbia yupo Loftus Road akikamilisha vipimo vya afya kwa ajili ya kujiunga na QPR.

Matija Nastasic amekamilisha uhamisho wake kutoka Fiorentina na kujiunga na Mannchester City, na anakuwa mchezaji wa 3 kujiunga na mabingwa hao wa England kwenye siku ya mwisho ya usajili. Wakati huo huo Javi Garcia anafanya vipimo vya afya kwa ajili ya kukamilisha uhamsiho wake kutoka Benfica kwenda City.


Lassana Diara, mchezaji wa zamani wa Chelsea, Arsenal na Portsmouth, amejiunga na Anzhi Makhachkhala kutoka Real Madrid

Breaking news - Edinson Cavan amesaini mkataba mpya wa kuendelea kuichezea Napoli na kuzima uvumi wa kutaka kujiunga na Chelsea.

Golikipa Hugo Lloris wa Lyon amekamilisha vipimo vya afya na Tottenham na muda mchache na amesaini mkataba wa miaka minne kujiunga klabu hiyo kwa ada ya uhamisho wa £13million.
Nigel De Jong ameondoka rasmi Manchester City na kujiunga na AC Milan kwa ada ya uhamisho ya £3.4million

Gael Kakuta ameenda kwa mkopo Vitesse Arnhem kutokea Chelsea

Ryan Babel mchezaji wa zamani wa Liverpool, amerudi timu yake ya utotoni Ajax akitokea Hoffenheim

Gael Kakuta

Hatimaye Dimitar Berbatov amehamia rasmi Fulham kutoka Manchester United kwa ada ya £5million

Mchezaji wa kimataifa wa Brazil Douglas Maicon amesajiliwa kutoka Inter Milan kwenda Manchester City

Charlie Adam amejiunga na Stoke City City akitokea Liverpool kwa ada ya £4MILLION



Andy Carroll amejiunga na West Ham kwa mkopo wa mwaka mzima

Rafael Van Der Vaart amejiunga na Schalke akitokea Tottenham Hotspur

Pablo Hernandez amejiunga na Swansea City akitokea Valencia ya Spain

Scott Sinclair amekamilisha uhamisho wake kutoka Swansea na kuhamia kwa mabingwa wa England Man City
ION.

Nicklas Bendtner amehama Arsenal na kwenda kujiunga na Juventus ya Italia

HIZI NDIZO SABABU ZINAZOCHANGIA WATU WA MUSOMA KUPENDA SOKA LA NJE KULIKO LA NDANI




Kadri siku zinavyozidi kwenda hapa nchini Tanzania ndivyo ambavyo soka la nyumbani linavyozidi kupoteza mvuto kwa mashabiki ambao wanazidi kutekwa na ushabiki wa soka la kimataifa hasa la barani ulaya.



Kwa takribani siku nne nilizokuwepo hapa Musoma kwa ajili ya tamasha la Fiesta 2012, nimekuwa nikishuhudia namna soka la nje ya nchi lilivyokuwa na kwa mashabiki wa soka katika mkoa huu uliopo kanda ya ziwa.

Katika tembea tembea yangu nimekuwa nikikutana na madaladala mengi sana yakiwa yamebandikwa picha na kuchorwa majina ya wachezaji wa timu za ulaya, kuanzia Barcelona, Chelsea, Man United, Real Madrid mpaka Arsenal na vilabu vingine vikubwa vya ulaya.

Ukiachana na madaladala pia kwenye maduka na salooni za kiume hapa Mara karibia zote zimepewa majina ya wachezaji au timu kubwa za Ulaya.

Nilipojaribu kufanya utafiti ili kujua kwanini mashabiki wa hapa wana mapenzi makubwa na vilabu vya nje kuliko vya ndani ndipo waliponipa sababu zao.

"Kwanza ningependa kuweka wazi kwamba sio kweli watu hapa hawana mapenzi na soka la nyumbani. Watu tunapenda sana mpira hapa Tanzania na tunaushabikia ndio maana naona umekutana na watu kadhaa wenye kuvaa jezi za timu kubwa kama Simba na Yanga japo sio kwa wingi mkubwa," anasema Msafiri Kisase ambaye ni shabiki mkubwa soka la kimataifa.


"Kiukweli hapa Musoma watu wamechoka na ubabaishaji wa viongozi wa soka la Tanzania kuanzia chama mama TFF mpaka vyama mikoa na wilaya. Mambo yanaendeshwa kienyeji sana, hakuna usawa kwenye michezo, hali inayopelekea mkoa huu kukosa hata timu moja kwenye ligi kuu kwa miaka kibao sasa. 

"Kwa hali hii unadhani nani atakuwa na mshawasha wa kushabikia soka la ndani kwa nguvu, wakati mkoa hauna timu za kwenye mashindano makubwa kwa miaka kibao sasa, hata hizo Simba na Yanga ambazo zina mashabiki nchi nzima kuna watu wengine wanazisikia tu kama timu za nchi ya nchi. Zitakuja huku kutoka Dar kwa minajili gani wakati hakuna timu ya kushindana nayo? Viongozi wa mkoa wamelala na TFF nayo imeshindwa kuutawanya mpira katika mkoa, wamebaki kwenye eneo moja tu. Soka litaendeleaje kwa hali hii? Matokeo yake watu wanakuwa wanatekwa zaidi na kushabikia timu za nje ya nchi kwa sababu hakuna timu za ndani za kuwashawishi wawe na mapenzi na soka la hapa." - aliongea Msafiri Kisase 
 









HAMSHA HAMSHA YA FIESTA 2012 MKOANI MUSOMA INAYOFANYIKA LEO

Kila kona ya Musoma leo ni Fiesta tu - Homa imepanda kila mahala, wasanii wameshaningia na muda wowote kutoka sasa intaanza. Bhaaaaaaaasi



Hadi watoto wamepandwa na homa ya Fiesta

Shaffih Dauda nikiwa namashabiki wa Fiesta tukipata picha ya pamoja


Fiesta 2012 - Muonekano mpya Burudani ile ile

SALUM KINJE NA PASCAL OCHIENG WA SIMBA ITC ZAO KUPATIKANA HIVI KARIBUNI YASEMA TFF - HUKU AYOUB WA MTIBWA AKIIPATA YA KWAKE

Shirikisho la Vyama vya Mpira wa Miguu Uganda (FUFA) limetuma Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa ajili ya mchezaji Ayoub Hassan Isiko aliyejiunga na Mtibwa Sugar akitokea timu ya Bull FC ya nchini humo.
ITC hiyo ilitumwa jana (Agosti 30 mwaka huu), hivyo kufanya wachezaji ambao ITC hazijapatikana hadi sasa kubaki wawili tu. Dirisha la usajili wa wachezaji litafungwa rasmi Septemba 4 mwaka huu.
Wachezaji ambao ITC zao bado hazijapatikana ni Salum Kinje na Pascal Ochieng kutoka AFC Leopards ya Kenya waliojiunga na Simba. ITC hizo zinatarajiwa kupatikana wakati wowote kwani tayari Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeshaziomba kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Kenya (FKF) baada ya nyaraka zote zilizokuwa zikitakiwa kupatikana.

MBUYU TWITE AANZA MAZOEZI RASMI YANGA - HUKU SIMBA WAKIMUWEKEA PINGAMIZI TFF





PICHA ZOTE NA GLOBAL PUBLISHER

SIMBA VS AFRICAN LYON - TANZANIA PRISONS KUIKABILI YANGA UFUNGUZI LIGI KUU 2012/13

Michuano ya Ligi Kuu kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kwa msimu wa 2012/2013 itaanza Septemba 15 mwaka huu kwa timu zote 14 kujitupa kwenye viwanja tofauti.
 
Mechi za ufunguzi zitakuwa kati ya Simba vs African Lyon (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam), Polisi Morogoro vs Mtibwa Sugar (Jamhuri, Morogoro), Tanzania Prisons vs Yanga (Sokoine, Mbeya), Mgambo JKT vs Coastal Union (Mkwakwani, Tanga), JKT Ruvu vs Ruvu Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), Kagera Sugar vs Azam (Kaitaba, Bukoba) na Toto Africans vs Oljoro JKT (Kirumba, Mwanza).
 
Mzunguko wa kwanza (first round) utamalizika Novemba 11 mwaka huu ambapo kwenye mzunguko huo mechi ya watani wa jadi Yanga na Simba itachezwa Oktoba 3 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
Ligi hiyo itamalizika Mei 18 mwakani kwa mechi kati ya Toto Africans vs Ruvu Shooting (Kirumba), Mgambo JKT vs African Lyon (Mkwakwani), JKT Ruvu vs Mtibwa Sugar (Azam Complex), Tanzania Prisons vs Kagera Sugar (Sokoine), Simba vs Yanga (Uwanja wa Taifa), Oljoro JKT vs Azam (Sheikh Amri Abeid Kaluta) na Polisi Morogoro vs Coastal Union (Jamhuri).
 
Endapo Simba na Azam hazitafanikiwa kuvuka hatua mojawapo ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho, ratiba hiyo itafanyiwa marekebisho.
 
MECHI YA UFUNGUZI WA MSIMU WA LIGI 2012/2013
Mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kuashiria ufunguzi rasmi wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2012/2013 kati ya bingwa mtetezi Simba na makamu bingwa Azam itachezwa Septemba 11 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
WAKATI HUO HUO - SERENGETI BOYS KUJIPIMA KWA ASHANTI
Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) iliyokuwa kambini kujiandaa kwa mechi dhidi ya Kenya itavunja rasmi kambi yake kesho (Jumamosi) kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Ashanti United.
 
Mechi hiyo dhidi ya Ashanti United iliyoko daraja la kwanza itachezwa kuanzia saa 10 jioni Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam kwa kiingilio cha sh. 2,000.
 
Serengeti Boys ilikuwa Septemba 9 mwaka huu icheze na Kenya kwenye mechi ya raundi ya kwanza ya michuano ya Afrika kwa vijana chini ya miaka 17, lakini Kenya ikajitoa ambapo sasa itacheza na Misri katika raundi ya pili. Mechi ya kwanza itachezwa Oktoba 14 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
 
Mwishoni mwa Septemba, Serengeti Boys itarejea tena kambini kujiandaa kuikabili Misri ambapo kabla inatarajia kupata mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya timu itakayotangazwa baadaye

REDONDO, LUHENDE, CHRISTOPHER EDWARD, KIGGY MAKASI, YONDAN WAWEKEWA PINGAMIZI KUCHEZA LIGI KUU

Klabu mbalimbali zimewasilisha pingamizi Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupinga usajili wa wachezaji 17 walioombewa usajili katika timu za Ligi Kuu.
Toto Africans ya Mwanza imewawekea pingamizi wachezaji Enyinna Darlinton aliyeombewa usajili Kagera Sugar, na Mohamed Soud anayekwenda Coastal Union kwa maelezo kuwa bado ina mikataba na wachezaji hao.
Pia Flamingo ya Arusha inapinga usajili wa wachezaji wake Kelvin Friday Iddy katika timu za Azam na Salim Walii (Polisi Mara) kwa vile taratibu za kuwahamisha bado hazijafanywa. Nayo Kagera Sugar inapinga usajili wa beki David Charles Luhende kwenda Yanga kwa vile ada ya uhamisho haijalipwa.
Super Falcon ya Chanjamjawiri, Chakechake, Pemba inapinga wachezaji wake wanne; Edward Christopher Shija, Samir Said Luhava (Simba), Robert Joseph Mkhotya (African Lyon) na Sultan Juma Shija (Coastal Union) kusajiliwa katika timu hizo kwa maelezo taratibu halali za uhamisho hazikufuatwa.
Mchezaji Othman Hassan aliyeombewa usajili Coastal Union anapingwa na Oljoro JKT kwa vile bado ana mkataba na timu hiyo unaomalizika Mei 24, 2013. Nayo Rollingstone Multipurpose Ateclass Foundation ya Arusha inapinga usajili wa Kigi Makassy kutoka Yanga kwenda Simba hadi itakapolipwa fidia ya kumlea mchezaji huyo kwa vile bado hajafikisha umri wa miaka 23.
Azam inapinga usajili wa Ramadhan Chombo ‘Redondo’ kwenda Simba kwa maelezo bado ina mkataba naye unaomalizika Juni 11 mwakani. Nayo Simba inapinga Kelvin Yondani kusajiliwa Yanga kwa maelezo kuwa ina mkataba naye uliosainiwa Desemba 23 mwaka jana.
Vilevile Simba imewasilisha malalamiko ya mchezo usio wa kiungwana katika usajili wa Mbuyu Twite aliyeko Yanga kwa maelezo alisaini mkataba na klabu yao Agosti Mosi mwaka huu mbele yao, viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Rwanda (FERWAFA) na APR ambapo alilipwa dola 30,000 na nyingine 2,000 ikiwa ni fedha ya kujikimu na nauli yake ya kujiunga na klabu hiyo.
Nayo Yanga inapinga Simba kuwaacha wachezaji Dan Mrwanda, Haruna Shamte, Kanu Mbiyavanga na Lino Masombo kwa maelezo walishapatiwa leseni za kucheza Ligi ya Tanzania walizozitumia kwenye mashindano ya Kombe la Kagame. Pia inapinga Ramadhan Chombo ‘Redondo’ kujiunga Simba kwa vile ana leseni ya kuchezea Azam kwa msimu wa 2012/2013.
Pingamizi lingine la Yanga kwa Simba ni kuwa imezidisha idadi ya wachezaji wa kigeni wanaotakiwa kusajiliwa kwa maelezo inao wanane wakati wanaoruhusiwa ni watano. Imewataja wachezaji hao kuwa ni Lino Masombo, Felix Sunzu, Emmanuel Okwi, Mussa Mude, Kanu Mbiyavanga, Pascal Ochieng, Komalmbil Keita na Daniel Akuffor.
Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya TFF chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa inatarajia kukutana Jumapili (Septemba 2 mwaka huu) kupitia pingamizi hizo pamoja na usajili wa wachezaji kwa ujumla kwa 2012/2013.

CHEMSHA BONGO: HAWA NI AKINA NANI?????


Thursday, August 30, 2012

HUYU NDIO MCHEZAJI BORA WA BARA LA ULAYA - AWAPOTEZA MESSI NA RONALDO

BREAKING NEWS: CRISTIANO RONALDO ANARUDI MANCHESTER..... KUFANYA NINI??

Mshambuliaji wa kimataifa wa Ureno na Real Madrid Cristiano Ronaldo atarudi kwa mara nyingine kwenye jiji la Manchester baada ya kuondoka takribani miaka mitatu iliyopita.

Ronaldo ambaye alikaa kwenye jiji la Manchester kwa misimu mitano akiwa anaichezea klabu ya Manchester United kabla ya kuuzwa kwenda Real Madrid, atarudi kwenye jiji hilo kwa ajili ya kucheza mechi ya Champions league dhidi ya Mabingwa wa England Manchester City. Madrid wamepangwa kundi D, wakiwa  na City, Ajax, na Dortmund.

Haya ndio makundi yote ya Champions league msimu wa 2012-13


Group A

Team Pld W D L GF GA GD Pts
Portugal Porto 0 0 0 0 0 0 0 0
Ukraine Dynamo Kyiv 0 0 0 0 0 0 0 0
France Paris Saint-Germain 0 0 0 0 0 0 0 0
Croatia Dinamo Zagreb 0 0 0 0 0 0 0 0

Group B

Team Pld W D L GF GA GD Pts
England Arsenal 0 0 0 0 0 0 0 0
Germany Schalke 04 0 0 0 0 0 0 0 0
Greece Olympiacos 0 0 0 0 0 0 0 0
France Montpellier 0 0 0 0 0 0 0 0

Group C

Team Pld W D L GF GA GD Pts
Italy Milan 0 0 0 0 0 0 0 0
Russia Zenit St. Petersburg 0 0 0 0 0 0 0 0
Belgium Anderlecht 0 0 0 0 0 0 0 0
Spain Málaga 0 0 0 0 0 0 0 0

Group D

Team Pld W D L GF GA GD Pts
Spain Real Madrid 0 0 0 0 0 0 0 0
England Manchester City 0 0 0 0 0 0 0 0
Netherlands Ajax 0 0 0 0 0 0 0 0
Germany Borussia Dortmund 0 0 0 0 0 0 0 0

Group E

Team Pld W D L GF GA GD Pts
England Chelsea 0 0 0 0 0 0 0 0
Ukraine Shakhtar Donetsk 0 0 0 0 0 0 0 0
Italy Juventus 0 0 0 0 0 0 0 0
Denmark Nordsjælland 0 0 0 0 0 0 0 0

Group F

Team Pld W D L GF GA GD Pts
Germany Bayern Munich 0 0 0 0 0 0 0 0
Spain Valencia 0 0 0 0 0 0 0 0
France Lille 0 0 0 0 0 0 0 0
Belarus BATE Borisov 0 0 0 0 0 0 0 0

Group G

Team Pld W D L GF GA GD Pts
Spain Barcelona 0 0 0 0 0 0 0 0
Portugal Benfica 0 0 0 0 0 0 0 0
Russia Spartak Moscow 0 0 0 0 0 0 0 0
Scotland Celtic 0 0 0 0 0 0 0 0

Group H

Team Pld W D L GF GA GD Pts
England Manchester United 0 0 0 0 0 0 0 0
Portugal Braga 0 0 0 0 0 0 0 0
Turkey Galatasaray 0 0 0 0 0 0 0 0
Romania CFR Cluj 0 0 0 0 0 0 0 0