Pages

Tuesday, May 29, 2012

KALI YA LEO: BAADA YA KUDUNDWA NA KOCHA WAKE - ADAM LJAJIC AFUNGIWA KWA KUSHINDWA KUIMBA WIMBO WA TAIFA

Chama cha soka cha Serbia kimesema kiungo Adam Ljajic amesimamishwa kuichezea timu ya Taifa kwa kushindwa kuimba wimbo wa Taifa kabla ya mechi dhidi ya Spain.

Ni adhabu kubwa kwa mchezaji ukilinganisha na kosa, lakini ukiwa na kocha aina ya mtu kichaa kama Sinisa Mihajlovic - then adhabu kama hizi inabidi uzizoee tu.

Chama cha soka kimesema Mihajlovic aliamua kumrudisha nyumbani Ljajic kwa sababu alishindwa kufuata masharti na sheria alizoweka kocha wake kwa wachezaji kuimba wimbo wa taifa kabla ya mechi.

Kweli huu sio mwezi mzuri kwa Adam, baada ya kupigwa mangumi na kocha wake wa Fiorentina sasa hivi ametemwa kuichezea timu ta taifa.

No comments:

Post a Comment